Bongo ukiwa na PhD lazima uchukiwe

Bongo ukiwa na PhD lazima uchukiwe

Wabongo wanataka mwenye PhD awe na mawazo kama yake wa darasa la saba.

Yaani wanataka wafanane mawazo, bila hivyo mara ni msaliti, mara PhD fake au elimu haija msaidia.

Mtu unalazimisha wa PhD awe na mtazamo kama wako wa darasa la 7.
Baadhi ya KIWADU ndo hawa kutwa kupost picha safarini mgombani na kuonyesha nyama choma mtandaoni. Inferiority!
 
PhD holder akichumia tumbo kuna shida gani? Mnataka mje kumcheka baadae?
 
Hii imekaaje? Yaani ukimbie umande mwenyewe wakati mwenzako kakomaa mpaka kapata PhD halafu unanuna?

Tuache ghilba na chuki dhidi ya wasomi wetu. Kama hatukupata nafasi ya kusoma mpaka PhD tusiendekeze chuki itazidi kutuumiza sisi Kiwango Duni (KIWADU).
Hakuna anaechukiwa Bali lazima ulinganishe kuwa PHD na Yale anayofanya yanalingana ???????

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi naamini kuwa mtu mwenye PhD anauwezo mkubwa kwa kuchambua mambo, kulingana na elimu yake inapaswa awe ni mtu wa kuleta zaidi majawabu yenye tija na ndio maana mnapokuwa kwenye mikutano/ mikusanyiko na wakishajua kuwa wapo watu wa level hiyo ya elimu huwa wanapewa attention ya kiwango kinachostahili kwa sababu inaaminika wanaweza kuleta mchango chanya. Lakini kama unayohiyo PhD halafu hoja zako haziakisi elimu yako ndipo hapo watu wanakuwa na mashaka na wewe.

Niliwahi kwenda nchi mmoja kwenye mafunzo ya muda mfupi (wiki mbili), wawezeshaji walikuwa vizuri sana kwenye uwasilishaji wa mada na hata nje ya mafunzo hayo katika uzungumzaji wao unakuwa na shauku ya kujua huyu mtu ana elimu gani.
Katika kuwafatilia nikagundua wote walikuwa ni PhD holders, lakini haukuna mahali walijitambulisha kwamba mimi ni Dr......, nilifanya kazi ya ku-google majina yao ndo nikapata salutation zao. Nikapata cha kujifunza kwamba tekeleza wajibu wako kwa kiwango chako halafu waache watu wawe na shauku ya kukufahamu wewe ni nani, sio kujikweza mimi nina PhD (" ndo unasikia watu wanasema eti naye Dr.)

Mwisho, PhD ni elimu kubwa sana, tuitendee haki inayostahili.
 
Nilipataga scholarship ya kusoma PhD sasa kuna mzee mmoja Professor nikaenda kumweleza hiyo habari na kumtaka ushauri. Alichoniambia ni kwamba kwa nafasi uliyonayo ambayo hata PhD holders wanaitamani usipoteze muda kwenda kusoma Zaidi, elimu uliyonayo inakutosha usiende kujaza maelimu halafu ukakutana na matarajio tofauti ukawa frustrated. Nilichukua ushauri wake sikwenda na sijutii .

Wengi wa PhD holders walitegemea kupata matokeo makubwa kimadaraka na kifedha na baada ya kukutana na utofauti wanaishia kudata tu. Kuna mmoja aliingia kujenga fensi mpk ndani ya eneo langu sehemu Fulani nilikuwa nimepanunua nimepaacha. Siku niliyoenda akaniletea nyodo wakati mpk huko kwenye hati halali kabisa. Nilichukua Tingatinga nikabomoa mchana kweupe baada ya kujiridhisha kuwa kavamia. Jamaa alipaniki kaenda polisi mie nikaenda kwa wakili wangu na watu wa Ardhi. Kufika pale anasema unajua mie ni Dokta, nikamwambie kajambe ukanye, kama ungekuwa na akili usingeshindwa kusoma Ramani ya kiwanja
Tulimshtaki na alitulipa Fidia
 
Nilipataga scholarship ya kusoma PhD sasa kuna mzee mmoja Professor nikaenda kumweleza hiyo habari na kumtaka ushauri. Alichoniambia ni kwamba kwa nafasi uliyonayo ambayo hata PhD holders wanaitamani usipoteze muda kwenda kusoma Zaidi, elimu uliyonayo inakutosha usiende kujaza maelimu halafu ukakutana na matarajio tofauti ukawa frustrated. Nilichukua ushauri wake sikwenda na sijutii .

Wengi wa PhD holders walitegemea kupata matokeo makubwa kimadaraka na kifedha na baada ya kukutana na utofauti wanaishia kudata tu. Kuna mmoja aliingia kujenga fensi mpk ndani ya eneo langu sehemu Fulani nilikuwa nimepanunua nimepaacha. Siku niliyoenda akaniletea nyodo wakati mpk huko kwenye hati halali kabisa. Nilichukua Tingatinga nikabomoa mchana kweupe baada ya kujiridhisha kuwa kavamia. Jamaa alipaniki kaenda polisi mie nikaenda kwa wakili wangu na watu wa Ardhi. Kufika pale anasema unajua mie ni Dokta, nikamwambie kajambe ukanye, kama ungekuwa na akili usingeshindwa kusoma Ramani ya kiwanja
Tulimshtaki na alitulipa Fidia


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Very true,ukiangalia wasomi wa nje wenye phd hutafuta matatizo ya jamii na kuyasolve wakati huku wanatumia hizo phd kuwatishia watu.
Nitawaona wa maana sasa hivi wakiingia maabara na kutuletea dawa ya corona.
Unachokizungumzia sijawahi kukiona. Nilichokiona ni wenye hizo PhD wengi wao hawajui kutangamana na binadamu wenzao ndani ya jamii.

Mara nyingi kwa sehemu ya elimu waliyoipata huwa wanawadharau wale wengine ambao hawajapata sehemu ya elimu kama waliyopata wao. Wanakuwa na viburi na dharau.

Matokeo yake yanakuwa huo uzi uliyouleta wewe. Hawachukiwi kwa sababu ya elimu yao, wanachukiwa kwa sababu ya mienendo yao ya kutangamana na watu ndani ya jamii.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom