Bongo ukiwa na PhD lazima uchukiwe

Bongo ukiwa na PhD lazima uchukiwe

Tatizo siyo wivu na PhD za watu, tatizo ni matukio yanayofanywa na baadhi ya wasomi hao mfano;

-Bungeni wakati wa hoja za maana jitu limelala halafu linakurupuka na kugonga meza kwamba linaunga mkono hoja.

-PhD holder katumbuliwa ukuu wa mkoa analia akidai kuwa yeye yatima na anategemewa.

-Kwenye nafasi za siasa wakiwamo na PhD holders hushauri watoto wa wakulima wakajiajiri wakiwa na shahada lakini wao wameng'ang'ania hizo nafasi huku wakiweka mzingira kwa watoto wao kuzirithi.

-PhD holder kama Mwakyembe kule Ujerumani ambako aliipata PhD kwa kuandika Tethys inayotaka serikali tatu tena aliitetea kwa hoja nzito hadi ma prof wa kijerumani wakamkubali lakini kwenye bunge la katiba aliitupilia mbali hadi Tundu Lissu aliingia na kitabu cha Mwakyembe mle bungeni lakini jamaa akafumba macho kama hakuandika yeye.

-PhD holder tena mchana kweupe hataki takwimu za wagonjwa na Vifo vinavyotokana na COVID-19 zisitolewe hadharani na hoja hii IKAMKOSHA SANA PhD mwingine na kugawa uteuzi wa uwaziri siku chache baadae.

-Kamati na tume nyingi zinazoundwa tena zikiongozwa na ma PhD na ma Prof wabobezi zinakuja na findings zisizo na kichwa wala miguu na zenye maelekezo eg 'The makinikia Professorial Rubish hadi tukaaminishwa sisi ni Donner kantri.

Kwa kifupi ni kwamba kuna utopolo mwingi sana unaofanywa na PhD holders hasa wakihamia chama fulani au wakipewa madaraka hadi inafika wakati Mbunge MUSUKUMA au KIBAJAJI ambao hawa ni la saba Graduates wanaweza jenga hoja kuliko wasomi hawa na kinachopunguza uwezo wao kwa kila nyanja ni kwamba wanafikiria kwa kutumia tumbo yaani wanawaza teuzi na si vinginevyo.
 
Tanzania inahitaji watu wenye akili na maarifa mengi kwa ajili ya ujenzi wa Taifa lao na siyo hayo Ma PhD! Huwezi kumpima mtu uwezo wake wa akili eti kwa sababu ana digrii au la! Huko ni kukengeuka na kujitoa ufahamu.

Huenda ile sumu aliyowekewa Mheshimiwa wakati ule wa utawala wa awamu ya nne mpaka akanyonyoka nywele, haijawahi kumuacha salama. Tuendelee kumvumilia na kumsamehe.
Mbaya zaidi akanyamaza kimya kama siyo yeye na hii ni baada ya kupewa kacheo Jamani njaa hizi zinafuta hata PhD
 
Wabongo bado wajamaa Sana. Hawataki kuona mtu kafanikiwa mwenyewe
 
Kuna mkuu wa mkoa wa Moro(PHD) ya mambo ya food security wkt Magu anaingia alitengua uteuzi wake jamaa likaanza kulia lia eti ooh eti hata yohana alimezwa kwny tumbo la samaki sijui nini nisamehe baba.Matunda ya PHD hayo

PHD-Permanent Head Damage
😃😃 mtu ana phd but hajui nini cha kufanya😂😂
 
Hii imekaaje? Yaani ukimbie umande mwenyewe wakati mwenzako kakomaa mpaka kapata PhD halafu unanuna?

Tuache ghilba na chuki dhidi ya wasomi wetu. Kama hatukupata nafasi ya kusoma mpaka PhD tusiendekeze chuki itazidi kutuumiza sisi Kiwango Duni (KIWADU).
PhD fake zimejaaa bongo
 
Back
Top Bottom