Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 25,828
- 50,508
- Thread starter
- #81
Sijui ni kwa nini watu wanajitia upofu kwa kujifanya hata wao wanaishi kwenye maeneo yaliyopimwa. Tanzania nzima ni asilimia chini ya kumi ya ardhi ndiyo imepimwa. Na uhalali wa kuwa kwenye ardhi si kuwa na "Title deed" bali ni kuwa kihalali kwenye eneo husika.
Hivi vijijini ni wangapi wana hizo "title deeds" ambazo watu wanauliza kama watu wa Kimara walikuwa nazo, na jee kutokuwa na "title deeds" kunafanya nyumba yako kuwa "Condemned" na serikali? Jee kuaharamishwa kwa leo huko mbele ya safari kutakuwa halali?
Hawa watu waliobomolewa leo walikuwa hawalipi kodi za serikali, jee mipango miji walipoweka Namba kwenye nyumba hizo walikuwa wanawalaghai wamiliki wake? Watu wa mitaa hiyo walipowekewa serikali za mitaaa na mitaa yao ilitambulikaje na Serikali kuu na tume ya Uchaguzi kama walikuwa pale kiharamu? Miaka yote hiyo na shughuli zote hizo zilizokuwa zinatambuliwa na serikali ilikuwa ni danganya toto?
Hivi vijijini ni wangapi wana hizo "title deeds" ambazo watu wanauliza kama watu wa Kimara walikuwa nazo, na jee kutokuwa na "title deeds" kunafanya nyumba yako kuwa "Condemned" na serikali? Jee kuaharamishwa kwa leo huko mbele ya safari kutakuwa halali?
Hawa watu waliobomolewa leo walikuwa hawalipi kodi za serikali, jee mipango miji walipoweka Namba kwenye nyumba hizo walikuwa wanawalaghai wamiliki wake? Watu wa mitaa hiyo walipowekewa serikali za mitaaa na mitaa yao ilitambulikaje na Serikali kuu na tume ya Uchaguzi kama walikuwa pale kiharamu? Miaka yote hiyo na shughuli zote hizo zilizokuwa zinatambuliwa na serikali ilikuwa ni danganya toto?