Bomoabomoa itakavyoyumbisha taasisi za kifedha

Bomoabomoa itakavyoyumbisha taasisi za kifedha

Ukitaka kumuu mbwa mpe jina baya. wemeitwa "wavamizi wa hifadhi ya barabara" na wavamizi wakiondolewa hakuna fidia!

Hiyo hifadhi ya meta 121 kila upande ni barabara za namna gani zitajengwa? Labda wahandisi wa barabara watuelimishe!

Na hata kama zitajengwa ni karibuni au miaka 50 ijayo?
 
Halafu ukiangali kwa undani ni kama dhuluma fulani hivi. Hawa watu wanaoambiwa hawakuwa pale kihalali, ni wao walikuwa wanalipa kodi, wanakata leseni za biashara na kulipa tozo mbali mbali za kibiashara na wengine Kampuni zao zimesajiliwa Brela kwa kutumia eneo hilo hilo ambalo leo wanaambiwa hawako kihalali. Ina maana serikali ilikuwa inajishughulisha na wafanyabiashara haramu?
Serikali haina Mfumo wa kutunza kumbukumbu za kutosha za kila mtanzania na mazingira yanayomzunguka hivyo ni ngumu idara zake kugundua kasoro kutoka idara nyingine. Kwa mfano mtuhumiwa anaweza kuwa na kesi zaidi ya moja kwenye mahakama tofauti bila Hakimu wa mahakama moja kujua. Halikadhalika mtanzania anaweza kuwa na passport zaidi ya moja kwa majina tofauti. Haya yote hayawezekani kwenye nchi zenye Mfumo mzuri wa kidigitali wa kumbukumbu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maendeleo hayaji bila bomoa bomoa. Si nyumba tu, hata misingi ya utu inabidi ibomolewe. Hujaona watu wa jinsia moja wanaoana, tena cha ajabu wengine ni wachungaji wa kondoo wanaoana na kondoo zao.

Misingi ya utu inabomolewa na kanisa linabariki kwa kuwa wameendelea itakuwa serikali kubomoa nyumba kupisha highways? Fikiri.
Halafu hawa wameuziwa viwanja na watu waliofidiwa tayari

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali haina Mfumo wa kutunza kumbukumbu za kutosha za kila mtanzania na mazingira yanayomzunguka hivyo ni ngumu idara zake kugundua kasoro kutoka idara nyingine. Kwa mfano mtuhumiwa anaweza kuwa na kesi zaidi ya moja kwenye mahakama tofauti bila Hakimu wa mahakama moja kujua. Halikadhalika mtanzania anaweza kuwa na passport zaidi ya moja kwa majina tofauti. Haya yote hayawezekani kwenye nchi zenye Mfumo mzuri wa kidigitali wa kumbukumbu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nyumba moja inaweza kutumika kama dhamana mikopo zaidi ya mmoja

Sent using Jamii Forums mobile app
 
bima hailipi deni kisa retrenchment...ndio maana mafao ya mfanyakaz ndio yanakatwa kama ana mkopo....

mimi niliondoka nmb baada ya kupata kazi nyingine.. so inawezekana taratibu zimebadilika ila mpaka naacha kazi benk bima hailipi nje ya hizo sababu tatu nilizotoa





Ombwe Hilo... Je retrenchment?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
bima hailipi deni kisa retrenchment...ndio maana mafao ya mfanyakaz ndio yanakatwa kama ana mkopo....

mimi niliondoka nmb baada ya kupata kazi nyingine.. so inawezekana taratibu zimebadilika ila mpaka naacha kazi benk bima hailipi nje ya hizo sababu tatu nilizotoa
Ni tatizo kubwa mifumo ya kibenk ya tz bado inamkandamiza mteja. Ilibidi bima ya mkopo ikave kila kitu ambacho kitasababisha mteja ashindwe kulipa deni beyond his or her power.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jana nilipokuwa naangalia kwenye mitandao ya kijamii niliona picha mbali mbali za bomoabomoa ya nyumba inayoendelea Dar es salaam. Pamoja na huzuni, hasira, navilio vilivyokuwa vimetawala zoezi hilo, mimi kwa mtizamo wangu nimeona kwamba zoezi lenyewe litaziathiri sana taasisi za kifedha na uchumi wa nchi kwa ujumla.

Kati ya nyumba zilizobomolewa miongoni mwake kuna nyumba ambazo ziliwekwa dhamana kwa mikopo pia kuna nyumba ambazo zilitumika kama ni anwani za wakopaji. Na kwenye maeneo hayo pia kuna nyumba zilizokuwa zinatumika kama nyumba za biashara zilizotathiminiwa kupata kigezo cha kukopeshwa.

Nyumba za aina hiyo zinapobomolewa zinaleta sintofahamu kubwa sana kwa taasisi za kifedha. Kwa mfano nyumba iliyowekwa dhamana na mkopaji imebomolewa na nyumba iliyotumika kama anwani ya mkopaji nayo imebolewa, na eneo ilikokuwa inafanyika biashara iliyokopeshwa nayo imebomolewa. Hapa taasisi ya kifedha iliyokopesha inawezaje kulipwa?

Halafu eneo lote linalobomolewa, serikali imewahi kujua ni biashara ya thamani kiasi gani ilikuwa inafanyika kwenye eneo hilo? Leo wote waliokuwa wanawazuia bidhaa wafanyabiashra wa eneo hilo wamepoteza wateja na waliokuwa wateja nao wamepoteza mitaji. Ni kwa kiasi gani biashara iliyopootezwa kwenye eneo hilo italeta athari kwenye uchumi wa Dar es salaam na Taifa kwa ujumla?

Wafanyakazi wa serikali ambao watakuwa wanashughulika na matokeo ya ubomoaji huo,ni kwa kiasi gani watashusha ufanisi wao kazini na pia wanawezaje kuhimili makato ya mikopo yao waliyokopa ili kuendeshea shughuli za kujiongezea kipato kwenye maeneo nyumba zilikobomolewa?
Napata shida kuelewa Serikali za Wanyonge zinakuwaje hapa Duniani
 
hizi ni sop za karibu dunia nzima... benki yeyote duniani haipo kwa ajili ya kumsaidia mtu au maskini... benki inafanya biashara inawaza faida yao tu....

ukiruhusu bima ifute mkopo wa retrenchment mtu anaweza acha kazi ili afutiwe mkopo.. au akafanya kosa makusudi ili apunguzwe kazini sababu anajua atasamehewa mkopo wake... maana makato yanatesa sana.....


Ni tatizo kubwa mifumo ya kibenk ya tz bado inamkandamiza mteja. Ilibidi bima ya mkopo ikave kila kitu ambacho kitasababisha mteja ashindwe kulipa deni beyond his or her power.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hizi ni sop za karibu dunia nzima... benki yeyote duniani haipo kwa ajili ya kumsaidia mtu au maskini... benki inafanya biashara inawaza faida yao tu....

ukiruhusu bima ifute mkopo wa retrenchment mtu anaweza acha kazi ili afutiwe mkopo.. au akafanya kosa makusudi ili apunguzwe kazini sababu anajua atasamehewa mkopo wake... maana makato yanatesa sana.....
Sio kweli retrenchment maana yake ni kuondolewa kazini bila kosa yaani kupunguzwa kazi. Lkn bado kuna nchi zinazomcover hata mkopaji aliyefukuzwa kazi kwa uzembe au makusudi kwa sab tayari hawezi kulipa deni lkn akipata kazi nyingine anaendelea kulipa. Mtu hawezi kufanya kosa makusudi kwa ajili ya kukwepa kulipa deni kwa sab kazi inamsaidia kukidhi gharama zingine labda afanye hivyo akiwa na alternative option.

Ni kweli bank wanajijali zaidi lkn mamlaka lazima ziwe mbele kuwabana kuwatetea wananchi wake kitu ambacho serikali haikifanyi kwa ukamilifu wake hivyo watanzania kuendelea kufanywa ng'ombe wa Maziwa watakamuliwa mpk damu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna hata mtu mmoja ambaye anazembea isipokuwa serikali ndiyo inazembea. Tanzania watu wanajenga nyumba kwa fedha zao binafsi na si kwa kutegemea fedha za serikali. kwa mantiki hiyo kunakobomolewa leo zama hizo yalikuwa ni mashamba tu ya watu binafsi ambao waliuza maeneo hayo kwa wengine. Serikali ina wajibu wa kupima Ardhi lakini ni kwa nini mpaka sasa Ardhi waliyopima haifiki hata asilimia 20?

Pili eneo linalobomolewa sasa halikuwa sehemu ya hifadhi ya barabara kwani hapo mwanzo hifadhi ya barabara haikuwa na sheria inayotumika hivi sasa. Kwa maana nyingine sheria ilitungwa wakati tayari watu wako pale na hapo wanasthaili kufikiriwa.

Nina miaka 19 nafuatilia kiwanja changu kipimwena hakipimwi halafu baaadaye anatokea mtu anasema nimejenga kiholela! FaizaFoxy hiyo Kariakoo yenu ulipimwa enzi za Mkoloni. Hivi wale ndugu zako wa Vingunguti kiembe mbuzi na kule Tandale kwa mtogole maeneo yao yamepimwa na kupangwa?
Eneo la maendeleo si lazima liwe hifadhi ya barabara. Kumbuka hilo.
 
Maendeleo hayaji bila bomoa bomoa. Si nyumba tu, hata misingi ya utu inabidi ibomolewe. Hujaona watu wa jinsia moja wanaoana, tena cha ajabu wengine ni wachungaji wa kondoo wanaoana na kondoo zao.

Misingi ya utu inabomolewa na kanisa linabariki kwa kuwa wameendelea itakuwa serikali kubomoa nyumba kupisha highways? Fikiri.
Na yule shehe punga wa moro mbona umemsahau

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom