Bomoa bomoa Iringa ni hujuma dhidi ya Rais Samia au ni udhaifu wa CCM Iringa

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,305
33,924
Jana tarehe 13/06/2023 Saa kumi jioni Mkuu wa MKoa wa Iringa anatoa Masaa 48 kwa wafanyabiashara wasio maeneo rasmi ya Biashara waondoke kwa hiyari yao ama wataondolewa kwa nguvu baada ya muda huo kupita.

Masaa 12 baadae (saa kumi usiku) vyombo vya dola vinaongoza bomoa bomoa eneo la Magari mabovu. Jee kauli ya Mkuu wa Mkoa kutoa masaa 48 ilibatilishwa na nani au nini kilitokea mpaka hayo masaa 48 kupungua mpaka kubaki 12?

Tarehe 02/06/2023 Meya wa Manispaa Iringa anamwagiza Kaimu Mkurugenzi kukaa na wafanyabiashara wa Magari Mabovu kuangalia jinsi watakavyoondoka eneo hilo. Siku nne baadae 06//06/2023 Manispaa inabomoa baadhi ya sehemu za kufanyia biashara. Kwa nini Meya aliagiza Mkurugenzi akae na wafanyabiashara wa Magari Mabovu halafu Ghafla Mkurugenzi anaamua eneo hilo libomolewe?

Tarehe 06/06/2023 Wafanyabiashara wanakwenda ofisi za CCM kulalamika kubomolewa eneo lao bila ya kufuatwa kwa utaratibu, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Iringa Mjini anaigiza serikali yake isimamishe kwa muda zoezi la ubomoaji mpaka ijulikane wanaobomolewa wanakwenda wapi.

Siku tisa baadae serikali inavunja maeneo ya biashara ya wafanyabiashara walioahidiwa na CCM kwamba hayatavunjwa. CCM iliwatapeli wafanyabiashara wale huku ikijua kwamba serikali kumbe haiisikilizi CCM?

CCM inawezaje kujiita chama tawala kama haiwezi kuitawala serikali inayoongoza Iringa??
 
unatetea ujinga.
Watu wamekusanyana huko vijijini wameacha ardhi yenye rutuba na kuja kupanga mifudu barabarani wewe unatetea?
Huu sasa ndiyo ujinga wenyewe, wewe unadhani kwamba kila mtu kazaliwa kijijini na nani kakwambia bado tunatumia watu kama nyenzo kwenye kilimo??

Upumbavu huu wa kudhani kila mtu anatakiwa kuwa mkulima ni ujima uliokuzwa na watawala wetu kwenye kukwepa jukumu lao la kuzalisha ajira.

Kama kilimo ndiyo suluhu kwa wafanyabiashara wadogo mbona watawala wanaingiza mabilioni ya shilingi kwa hilo kundi ambalo wewe unataka "lirudi"" mbona wakulima walioko huko vijijini hawaendelezwi??

Halafu waliobomolewa siyo hao unasema "wamekusanyana"bali ni wafanyabiashara wa muda mrefu sana. Halafu badala ya kuwaza ni kwa nini watu wanakimbia vijijini wewe unaona kama wanapendelewa kuwepo mjini.
 
Jana tarehe 13/06/2023 Saa kumi jioni Mkuu wa MKoa wa Iringa anatoa Masaa 48 kwa wafanyabiashara wasio maeneo rasmi ya Biashara waondoke kwa hiyari yao ama wataondolewa kwa nguvu baada ya muda huo kupita.

Masaa 12 baadae (saa kumi usiku) vyombo vya dola vinaongoza bomoa bomoa eneo la Magari mabovu. Jee kauli ya Mkuu wa Mkoa kutoa masaa 48 ilibatilishwa na nani au nini kilitokea mpaka hayo masaa 48 kupungua mpaka kubaki 12?

Tarehe 02/06/2023 Meya wa Manispaa Iringa anamwagiza Kaimu Mkurugenzi kukaa na wafanyabiashara wa Magari Mabovu kuangalia jinsi watakavyoondoka eneo hilo. Siku nne baadae 06//06/2023 Manispaa inabomoa baadhi ya sehemu za kufanyia biashara. Kwa nini Meya aliagiza Mkurugenzi akae na wafanyabiashara wa Magari Mabovu halafu Ghafla Mkurugenzi anaamua eneo hilo libomolewe?

Tarehe 06/06/2023 Wafanyabiashara wanakwenda ofisi za CCM kulalamika kubomolewa eneo lao bila ya kufuatwa kwa utaratibu, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Iringa Mjini anaigiza serikali yake isimamishe kwa muda zoezi la ubomoaji mpaka ijulikane wanaobomolewa wanakwenda wapi.

Siku tisa baadae serikali inavunja maeneo ya biashara ya wafanyabiashara walioahidiwa na CCM kwamba hayatavunjwa. CCM iliwatapeli wafanyabiashara wale huku ikijua kwamba serikali kumbe haiisikilizi CCM?

CCM inawezaje kujiita chama tawala kama haiwezi kuitawala serikali inayoongoza Iringa??
CCM haina wataalamu wa mipangomiji, serikali ziko mbili kikatiba, kwanza serikali kuu na pili serikali za mitaa hizi mbili zina tarehe zake za kuchaguliwa.
 
Acha siasa

Barabara si sehemu ya biashara
Nani kakwambia palipovunjwa ni barabarani. Haya kama ni barabarani uliwalipisha vitambulisho vyao Ujasiriamali ili iweje??

Jua barabara kisheria inaweza kugeuzwa Parking maana barabara siyo lami bali ni sehemu iliyoamriwa kupita magari kisheria na inawezekana kutunga kanuni ya kubadili matumizi yake kwa muda.

Yaani nawezaje kutetea wauzaji vitu barabarani. Acha kukaririshwa!!

Halafu utekelezaji wowote unapokuwa unatekelezwa ""Biased"unatengeneza "double standard" kwa watu. Kama kubomolewa ni lazima mji mzima maeneo yanayofanana kwa matumizi ya barabara ni lazima yabomolewe. Wao wanabagua sehemu za kubomoa, KWA NINI??
 
CCM haina wataalamu wa mipangomiji, serikali ziko mbili kikatiba, kwanza serikali kuu na pili serikali za mitaa hizi mbili zina tarehe zake za kuchaguliwa.
Yap na hii ndiyo hoja. Unatakaje nyumba na mitaa iliyojengwa kuanzia mwaka 1930 ifanane na nyumba zinazotakiwa kuwepo mwaka 2023 bila ya kuzibomoa za zamani??

Mji wa kale watu anaishi kwa usasa na idadi ya watu wameongezeka halafu mtu anataka sheria zilizotungwa baada ya nyumba hizo kujengwa ndiyo zitumiwe kuendeleshea miji ya kale.

Ni kama kutaka mji Mkongwe Zanzibar kuwa na barabara za laini mbili.
 
Jana tarehe 13/06/2023 Saa kumi jioni Mkuu wa MKoa wa Iringa anatoa Masaa 48 kwa wafanyabiashara wasio maeneo rasmi ya Biashara waondoke kwa hiyari yao ama wataondolewa kwa nguvu baada ya muda huo kupita.

Masaa 12 baadae (saa kumi usiku) vyombo vya dola vinaongoza bomoa bomoa eneo la Magari mabovu. Jee kauli ya Mkuu wa Mkoa kutoa masaa 48 ilibatilishwa na nani au nini kilitokea mpaka hayo masaa 48 kupungua mpaka kubaki 12?

Tarehe 02/06/2023 Meya wa Manispaa Iringa anamwagiza Kaimu Mkurugenzi kukaa na wafanyabiashara wa Magari Mabovu kuangalia jinsi watakavyoondoka eneo hilo. Siku nne baadae 06//06/2023 Manispaa inabomoa baadhi ya sehemu za kufanyia biashara. Kwa nini Meya aliagiza Mkurugenzi akae na wafanyabiashara wa Magari Mabovu halafu Ghafla Mkurugenzi anaamua eneo hilo libomolewe?

Tarehe 06/06/2023 Wafanyabiashara wanakwenda ofisi za CCM kulalamika kubomolewa eneo lao bila ya kufuatwa kwa utaratibu, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Iringa Mjini anaigiza serikali yake isimamishe kwa muda zoezi la ubomoaji mpaka ijulikane wanaobomolewa wanakwenda wapi.

Siku tisa baadae serikali inavunja maeneo ya biashara ya wafanyabiashara walioahidiwa na CCM kwamba hayatavunjwa. CCM iliwatapeli wafanyabiashara wale huku ikijua kwamba serikali kumbe haiisikilizi CCM?

CCM inawezaje kujiita chama tawala kama haiwezi kuitawala serikali inayoongoza Iringa??
CCM ndiyo Serikali yenyewe
 
Back
Top Bottom