Bodi ya Maziwa Tanzania ya nini?

Bodi ya Maziwa Tanzania ya nini?

Halafu, hebu tazama upatikanaji wa maziwa Tanzania. Kenya hadi kijijini unanunua maziwa fresh kila siku. Tanzania kuona maziwa hata mji mkuu wa Wilaya taabu!
 
Mie kwangu naona iko sahihi. Kwanza tofautisha kati ya vitu vya muhimu na vitu vya muhimu zaidi. Mfano mtoto mdogo akizaliwa afu kwa bahati mbaya mama akafaliki huwa nalishwa nyama au dagaa? Hapo ndipo utajua kuwa maziwa ni kitu cha muhimu. Nakumbuka kuwa hasa watoto wanapotumia maziwa kwa wingi huwa na afya bora na uelewa mkubwa darasani
Bodi ya pamba, bodi ya korosho, bodi ya sukari, .......
 
Naongezea list ya Mabidi:
Bodi ya Mikopo
Bodi ya kulipa madeni
Bodi ya Bomoabomoa
Bodi ya bonde la M/mbazi
 
BODI YA MATOFALI na BODI YA SIMENTI zianzishwe kusimamia bei za matofali na saruji, tunanyonywa sana
 
Bodi ya maziwa ndo mpango mzima. Yaan full Maziwa na safari za ulaya wenyewe wanaita "BENCHMARKING"
 
Bodi hii iimarishwe tena wateuliwe Mabrigedia Majenerali ndo waiongoze hii bodi. Tunahitaji Maziwa kuliko hata maji. Asanteni
 
Jaribu kutafuta umuhimu wa maziwa kwa afya ndo utajua kwanin kuna bodi ya mazima!
acha ujinga kwa hiyo tuwe na bodi ya samaki, bodi ya mchicha,bodi ya nyama, bodi ya vitunguu, bodi ya nyanya kwa vyote hivyo vina kazi kubwa mwilini?
 
Bodi ya MAJIPU iundwe haraka maana majipu yameongezeka likiwemo la yule Mrombo wa TANESCO ajira yake ipo shakani sana. Naye sasa anaruka ruka kama Pop corn kwenye kikaango kila siku Press Conference. Chezeya NGOSHA wewe!
 
Hizi ni baadhi za bodi/taasisi ambazo lazima zijipambanue kwa ufanisi wao ili ZISIVUNJILIWE mbali
1. Tanzania Tourist Board (TTB), Wamefanikiwa nini mpaka sasa?
2. Tanzania Industrial Research & Development Organization (TIRDO) vs Centre for Agriculture Mechanisation & Rural Technology (CARMATEC), Binafsi naona hawa jamaa ni kama hawapo kabisaaa, zaidi ya kupokea mishahara na Trip za nje, kama tu Power Tiller (enzi za Kilimo kwanza) tuliagiza toka nje hawa wanafanya nini jamanii?
3. National Housing & Building Research Agency (NHBRHA) vs National Housing Corporation (NHC)??? Taasisi mbili zenye kazi almost zinazofanana!!!
4............................................................................................
Halafu tunafikir eti wafanyakazi wa kigeni ndo jipu la kutumbua kumbe tulipaswa kuanza kutumbua hiz taasisi Lukuki ambazo ni kama mfu vile.
 
Itaundwa hadi bodi ya mbilimbi, watu wanajitafutia ulaji!
 
Mie kwangu naona iko sahihi. Kwanza tofautisha kati ya vitu vya muhimu na vitu vya muhimu zaidi. Mfano mtoto mdogo akizaliwa afu kwa bahati mbaya mama akafaliki huwa nalishwa nyama au dagaa? Hapo ndipo utajua kuwa maziwa ni kitu cha muhimu. Nakumbuka kuwa hasa watoto wanapotumia maziwa kwa wingi huwa na afya bora na uelewa mkubwa darasani
NDUGU YANGU MTOTO MDOGO ALIYEZALIWA HAPEWI MAZIWA HAYA TUNAYOZUNGUMZIA, KAMA MGENI NA MAMBO HAYA BORA UNYAMAZE
 
Mie kwangu naona iko sahihi. Kwanza tofautisha kati ya vitu vya muhimu na vitu vya muhimu zaidi. Mfano mtoto mdogo akizaliwa afu kwa bahati mbaya mama akafaliki huwa nalishwa nyama au dagaa? Hapo ndipo utajua kuwa maziwa ni kitu cha muhimu. Nakumbuka kuwa hasa watoto wanapotumia maziwa kwa wingi huwa na afya bora na uelewa mkubwa darasani
Kwa hiyo kwa kuwa mahaba ni muhimu kwa afya ya binadamu basi nashauri iundwe BODI YA MAHABA
 
Kuna bodi nyingi sana. Kuna hadi bodi ya chumvi, sukari, kama hivyo maziwa, mchele, unga, mafuta, yani ni nyingi sana.
 
Nimestushwa na kukutana na gari STL pembeni imeandikwa BODI YA MAZIWA daah! hivi kweli tumefikia hatua ya kuunda BODI MAALUM Kwa ajili ya MAZIWA (naamini wanamaanisha haya maziwa ya KUNYWA kupitia mdomoni) hapo hapo tuna TANZANIA FOOD AND NUTRITION CENTRE (TFNC) nao wanapata bajet nenee!!

Mgao wa magari ya kutosha bila kusahau safari za nje ya nchi. Hapo hapo tuna TANZANIA FOOD & DRUGS AUTHORITY (TFDA) nao vile vile tiripu za nje kama kawa, VX za kutosha. Jamani tuoneeni huruma sisi walipa kodi maskini. TUMEROGWA??

Bodi ya maziwa ipo kwa mujibu wa sharia kama zilivyo bodi nyingine katika wizara ya kilimo na mifugo na imeundwa tangu mwaka 2004. Bodi ya maziwa ni taasisi muhimu inabidi kuimarishwa zaidi kwani kulingana na majukumu yake ya kusimamia sharia ya maziwa, kuendeleza tasnia ya maziwa na kulinda afya ya watumiaji maziwa.

Kwa ufupi kazi za bodi ya maziwa ni

· Kuendeleza Sekta ya maziwa Tanzania

· Kudhibiti uingizaji wa maziwa na bidhaa zake toka nje ya nchi ili kulinda wazalishaji masoko ya wazalishaji wa ndani

· Kuwaunganisha wadau wa maziwa nchini

· Kuhamasisha unywaji, uzalishaji na usindikaji wa maziwa Tanzania

· Kushawisi uwekezaji katika sekta ya maziwa

TFDA kwa upande mwingine kazi yake katika upande wa maziwa ni kulinda afya ya mlaji kama ilivyo kwa bidhaa nyingine ambazo sio za maziwa.

TFNC kazi yake kubwa ni kufanya utafiti katika maswala yanayohusu chakula na lishe kwa ujumla
 
Back
Top Bottom