Bodi ya Maziwa Tanzania ya nini?

Bodi ya Maziwa Tanzania ya nini?

Tuseme kazi za bodi ya maziwa haziwez kufanywa na TFDA au TFNC? kwa minajili ile ile ya kubana matumiz ya serikali?
 
Tuseme kazi za bodi ya maziwa haziwez kufanywa na TFDA au TFNC? kwa minajili ile ile ya kubana matumiz ya serikali?

ili kazi za bodi ya maziwa zifanywe na TFNC au TFDA hapo inabidi sheria za kuunda hizo taasisi zibadilishwe na pengine lengo la kuunda bodi ya Maziwa lisifikiwe kama ilivyo kusudiwa
 
asante ndugu snail sasa utashangaa wabunge wa upinzani hawataliona hili kwa miaka 5 inayokuja wao watahangaika na ishu za kipuuz mule ndani
 
Hii bodi inahakikisha kila mtu anapata walau kikombe kimoja cha maziwa kwa siku..
mkuu wewe umewahi kupata hicho kikombe cha maziwa kutoka bodi ya maziwa?..

au huku kwetu Tanganyika, hawafiki
 
1. Bodi ya NAFAKA & MAZAO MCHANGANYIKO;
2. Bodi ya KAHAWA (Wafanyakazi, Magari-Mapya mfano; v8, Toyota Double Cabin, ofisi, SAFARI za kujifunza nje ya nchi etc.)
3. Bodi ya KOROSHO (Wafanyakazi, Magari-Mapya, ofisi, SAFARI za kujifunza nje ya nchi.
4. Bodi ya PAMBA (Wafanyakazi, Magari-Mapya, SAFARI za kujifunza nje ya nchi.
5. Bodi ya PARETO
6. Bodi ya UTALII, Tanzania Tourist Board.
7. Bodi ya Mfuko wa Barabara Tanzania.
8. Bodi ya Mikopo Elimu ya Juu
9. Bodi ya Mishahara & Maslahi
Je UFANISI upo?
 
mkuu wewe umewahi kupata hicho kikombe cha maziwa kutoka bodi ya maziwa?..

au huku kwetu Tanganyika, hawafiki

ha ha ha, unatakiwa ununue mkuu! bodi inakuhakikishia upatikanaji wa maziwa nchi nzima tu!
 
Nimestushwa na kukutana na gari STL pembeni imeandikwa BODI YA MAZIWA daah! hivi kweli tumefikia hatua ya kuunda BODI MAALUM Kwa ajili ya MAZIWA (naamini wanamaanisha haya maziwa ya KUNYWA kupitia mdomoni) hapo hapo tuna TANZANIA FOOD AND NUTRITION CENTRE (TFNC) nao wanapata bajet nenee!!

Mgao wa magari ya kutosha bila kusahau safari za nje ya nchi. Hapo hapo tuna TANZANIA FOOD & DRUGS AUTHORITY (TFDA) nao vile vile tiripu za nje kama kawa, VX za kutosha. Jamani tuoneeni huruma sisi walipa kodi maskini. TUMEROGWA??
Umuhimu wa Bodi ya Maziwa upo, sema tatizo haifanyi kazi inayotakiwa. Kumbuka TZ tuna ng'ombe milioni 23 lakini tuna-process kiasi kidogo sana cha maziwa. Dairy industry iko chini sana. Hivyo kama bodi hiyo ingekuwa inafanya kazi vizuri hata tusingeona maziwa kutoka Kenya, uganda, S.Africa hata S. America
 
ni aibu kwa nchi kama hii kutegemea maziwa toka Kenya amabayo robo tatu ni ARID & SEMI-ARID LAND (ASAL) tena maziwa yameundiwa na bodi na wanaapata bajeti toka serikalini na magari ya kifahari (V8), posho za kumwaga na TRIPS za nje za kutosha.
 
ni aibu kwa nchi kama hii kutegemea maziwa toka Kenya amabayo robo tatu ni ARID & SEMI-ARID LAND (ASAL) tena maziwa yameundiwa na bodi na wanaapata bajeti toka serikalini na magari ya kifahari (V8), posho za kumwaga na TRIPS za nje za kutosha.

Una uhakika na unachokisema mkuu? hebu katembelee bodi halafu uhesabu hizo V8 unazozisema, Bodi ya maziwa nje ya nchi wanaenda kufanya nini? ungesema vijijini ningekuelewa! usikurupuke
 
Bodi ya maziwa imeundwa na wadau husika kama vile wafugaji, wasindikaji, wachuuzi, wakusanyaji na wauzaji wa maziwa ambao wameiunda baada ya kuona umuhimu wa Tanzania kuzalisha maziwa kwa wingi, kutatua changamoto zilizopo kwenye sekta ya maziwa na kukuza uzalishaji wa maziwa nchini. Nakushauri utembelee website yao kwa ufahamu zaidi

Ukiwa unakunywa maziwa utajua umuhimu wa hii bodi kusaidia wafugaji vijijin kuzalisha maziwa kwa wingi, ikiwemo kuwapa elimu juu ya ufugaji bora, madawa, malisho n.k ili kupambana na soko la nje
 
Mdau ameongea vizuri kusema tuna ng'ombe wengi uzalishaji ni mdogo, hii ni changamoto ambayo bodi ya maziwa inatakiwa kuiona na kuifanyia kazi lakini hii itategemea pia serikali kuiwezesha bodi hii ili kusaidia wafugaji vijijini kuzalisha maziwa kwa wingi kwa kuwapa vitendea kazi vya kutosha na elimu ya kutosha kwa wafugaji wengi
 
Mdau ameongea vizuri kusema tuna ng'ombe wengi uzalishaji ni mdogo, hii ni changamoto ambayo bodi ya maziwa inatakiwa kuiona na kuifanyia kazi lakini hii itategemea pia serikali kuiwezesha bodi hii ili kusaidia wafugaji vijijini kuzalisha maziwa kwa wingi kwa kuwapa vitendea kazi vya kutosha na elimu ya kutosha kwa wafugaji wengi

100 Madame Mkuu!!!
 
Bodi ya maziwa ipo kwa mujibu wa sharia kama zilivyo bodi nyingine katika wizara ya kilimo na mifugo na imeundwa tangu mwaka 2004. Bodi ya maziwa ni taasisi muhimu inabidi kuimarishwa zaidi kwani kulingana na majukumu yake ya kusimamia sharia ya maziwa, kuendeleza tasnia ya maziwa na kulinda afya ya watumiaji maziwa.

Kwa ufupi kazi za bodi ya maziwa ni

· Kuendeleza Sekta ya maziwa Tanzania

· Kudhibiti uingizaji wa maziwa na bidhaa zake toka nje ya nchi ili kulinda wazalishaji masoko ya wazalishaji wa ndani

· Kuwaunganisha wadau wa maziwa nchini

· Kuhamasisha unywaji, uzalishaji na usindikaji wa maziwa Tanzania

· Kushawisi uwekezaji katika sekta ya maziwa

TFDA kwa upande mwingine kazi yake katika upande wa maziwa ni kulinda afya ya mlaji kama ilivyo kwa bidhaa nyingine ambazo sio za maziwa.

TFNC kazi yake kubwa ni kufanya utafiti katika maswala yanayohusu chakula na lishe kwa ujumla
 
Headmistress, acha hasira (huenda unanufaika na uwepo Bodi Mufilsi ya Maziwa) unachoshangaa ni nini? Bodi ya Maziwa kuwa na V8? kwenda nje ya nchi (kabla ya katazo?) hebu tuliza akili acha mihemko. Ni ukweli bodi hii haijafanya inavyopaswa kufanya ndo maana tunahoji uwepo wake, sis ndo walipaji kodi so tuna haki ya kuhoji jinsi kodi yetu inavyoteketezwa kwenye kuendesha bodi hizi Mufilisi.
Tujiandae na Wiki ya Kitaifa ya Maziwa mwezi wa Mei. Asante
 
Back
Top Bottom