BabaMorgan kwa picha ya haraka unaweza kuwatetea bodaboda na kuwalaumu wanaowalaumu bodaboda hasa kwenye hizi ajali za barabarani.. Lakini bodaboda ni pasua kichwa hasa japo sio wote
Tunacholaumu wengi wetu ni matokeo na sio chanzo ama asili ya tatizo
Maono kimo cha mbilikimo ya mamlaka ya kisiasa ndio asili kuu. Ili kupunguza kelele za ajira wakaamua kuruhusu biashara huria ya pikipiki kama aina ya usafiri wa haraka bila maandalizi ya kutosha na bila kujali viwango vya chombo husika
Mwendelezo wa tatizo ni pale kijana asiye na mafunzo kamili na sahihi kukabidhiwa chombo cha moto kwa ajili ya biashara ya kubeba binadamu
Huyu kijana hana mafunzo kamili na sahihi ya kuendesha chombo cha moto, sheria na kanuni za barabarani, usalama wake na wa wengine, elimu ya uchumi nk.. Na hii yote inasababishwa na uwezo wa kifedha,, mafunzo ya udereva yanahitaji hela na kijana hana
Rushwa na ufisadi
Ili kijana athibitishwe ni dereva na amefuzu mafunzo ya udereva na kufaulu anahitaji nyaraka zinazothibitisha hilo.!! Leseni.. Kuipata leseni kwa kufuata utaratibu wa kisheria kunachukua muda na ni gharama
Kupitia vishoka na watendaji wa mamlaka ya mapato na jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani wasiojali usalama wa raia na mali zao kijana anapata leseni chap kwa haraka na kwa bei poa
Kuna ukiukwaji mkubwa sana kwenye kupata leseni za udereva
Sasa kijana ana leseni na ana chombo cha moto anaanza biashara bila kufahamu walau kanuni moja tu ya kupita makutano ya barabara penye taa nyekundu
Majumuisho haya ya wanasiasa, watendaji wa serikali wasio waaminifu na vijana wasio na ajira matokeo yake ndio haya ya ajali zisizokoma, zinazoteketeza nguvu kazi ya taifa na kuleta uhujumu mkubwa wa uchumi kupitia vifaa tiba, vilema, uharibu wa vyombo na vifo
Sent using
Jamii Forums mobile app