Bodaboda hawana Haki

Bodaboda hawana Haki

Leo asubuhi pametokea ajali maeneo ya DIT iliyohusisha basi la Mwendokasi na Pikipiki maarufu Bodaboda sina details za kutosha kuhusu madhara yaliyotokea kwa maana ya majeruhi au kama kuna kifo chochote lakini so far ni ajali mbaya maana time niliyokuwa napita basi la Mwendokasi lilikuwa linapigwa jeki na Pikipiki inatolewa chini ya uvungu mwa basi.

Kila mtu baada ya kuona mazingira yale alikuwa anatoa lawama kwa dereva bodaboda bila hata ya kuwa na picha halisi ya kile kilichotokea mpaka kusababisha ajali..

It's like ajali yoyote itakayohusisha bodaboda basi lawama zote atatupiwa bodaboda huu ni uonevu wa kiwango cha juu sio bodaboda wote hawaobey sheria za barabarani na sio kila dereva wa gari yupo perfect asilimia mia.

Tuheshimu Bodaboda nao ni Binadamu licha ya kuwa na mapungufu yao lakini still wana mema yao kama walivyo Binadamu wengine as long unajua kuendesha Pikipiki inabidi uwe mstari wa mbele kutetea bodaboda maana siku unaweza kuwa kwenye mizunguko yako ukapata mushikeli waka kuhukumu kama wanavyowahukumu bodaboda.
BabaMorgan kwa picha ya haraka unaweza kuwatetea bodaboda na kuwalaumu wanaowalaumu bodaboda hasa kwenye hizi ajali za barabarani.. Lakini bodaboda ni pasua kichwa hasa japo sio wote

Tunacholaumu wengi wetu ni matokeo na sio chanzo ama asili ya tatizo
Maono kimo cha mbilikimo ya mamlaka ya kisiasa ndio asili kuu. Ili kupunguza kelele za ajira wakaamua kuruhusu biashara huria ya pikipiki kama aina ya usafiri wa haraka bila maandalizi ya kutosha na bila kujali viwango vya chombo husika

Mwendelezo wa tatizo ni pale kijana asiye na mafunzo kamili na sahihi kukabidhiwa chombo cha moto kwa ajili ya biashara ya kubeba binadamu

Huyu kijana hana mafunzo kamili na sahihi ya kuendesha chombo cha moto, sheria na kanuni za barabarani, usalama wake na wa wengine, elimu ya uchumi nk.. Na hii yote inasababishwa na uwezo wa kifedha,, mafunzo ya udereva yanahitaji hela na kijana hana

Rushwa na ufisadi
Ili kijana athibitishwe ni dereva na amefuzu mafunzo ya udereva na kufaulu anahitaji nyaraka zinazothibitisha hilo.!! Leseni.. Kuipata leseni kwa kufuata utaratibu wa kisheria kunachukua muda na ni gharama
Kupitia vishoka na watendaji wa mamlaka ya mapato na jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani wasiojali usalama wa raia na mali zao kijana anapata leseni chap kwa haraka na kwa bei poa
Kuna ukiukwaji mkubwa sana kwenye kupata leseni za udereva

Sasa kijana ana leseni na ana chombo cha moto anaanza biashara bila kufahamu walau kanuni moja tu ya kupita makutano ya barabara penye taa nyekundu

Majumuisho haya ya wanasiasa, watendaji wa serikali wasio waaminifu na vijana wasio na ajira matokeo yake ndio haya ya ajali zisizokoma, zinazoteketeza nguvu kazi ya taifa na kuleta uhujumu mkubwa wa uchumi kupitia vifaa tiba, vilema, uharibu wa vyombo na vifo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hawa boda boda wa dar wana haraka sana kuna siku nimetoroka chuo mkoani nikaenda dar lengo nifike kariakoo nikashuka ubungo nikabageini na boda boda anifikishe apo napotaka kwenda kwa haraka zake akaingia kwe bara bara ya mwendo kasi atujatembea ata mita 500 bus la mwendokas linakuja nyuma mungu tu alisaidia akapata kisehemu cha kuchepukia kama sio ivo ilikua tayar maj yashazid unga
🤣🤣🤣
 
hawa boda boda wa dar wana haraka sana kuna siku nimetoroka chuo mkoani nikaenda dar lengo nifike kariakoo nikashuka ubungo nikabageini na boda boda anifikishe apo napotaka kwenda kwa haraka zake akaingia kwe bara bara ya mwendo kasi atujatembea ata mita 500 bus la mwendokas linakuja nyuma mungu tu alisaidia akapata kisehemu cha kuchepukia kama sio ivo ilikua tayar maj yashazid unga
Kama ulimwambia akukimbize chap Kariakoo ulitegemea nini? Ndio maana wanashauri na wewe kama abiria kuchukua tahadhari unapoona dereva wako anakiuka sheria
 
Leo asubuhi pametokea ajali maeneo ya DIT iliyohusisha basi la Mwendokasi na Pikipiki maarufu Bodaboda sina details za kutosha kuhusu madhara yaliyotokea kwa maana ya majeruhi au kama kuna kifo chochote lakini so far ni ajali mbaya maana time niliyokuwa napita basi la Mwendokasi lilikuwa linapigwa jeki na Pikipiki inatolewa chini ya uvungu mwa basi.

Kila mtu baada ya kuona mazingira yale alikuwa anatoa lawama kwa dereva bodaboda bila hata ya kuwa na picha halisi ya kile kilichotokea mpaka kusababisha ajali.

It's like ajali yoyote itakayohusisha bodaboda basi lawama zote atatupiwa bodaboda huu ni uonevu wa kiwango cha juu sio bodaboda wote hawaobey sheria za barabarani na sio kila dereva wa gari yupo perfect asilimia mia.

Tuheshimu Bodaboda nao ni Binadamu licha ya kuwa na mapungufu yao lakini still wana mema yao kama walivyo Binadamu wengine as long unajua kuendesha Pikipiki inabidi uwe mstari wa mbele kutetea bodaboda maana siku unaweza kuwa kwenye mizunguko yako ukapata mushikeli waka kuhukumu kama wanavyowahukumu bodaboda.
Baba mogani siku ukiendesha gari ndio utajuwa hawa jamaa ni washenzi kiasi gani.



Sent from my vivo 1938 using JamiiForums mobile app
 
BabaMorgan kwa picha ya haraka unaweza kuwatetea bodaboda na kuwalaumu wanaowalaumu bodaboda hasa kwenye hizi ajali za barabarani.. Lakini bodaboda ni pasua kichwa hasa japo sio wote

Tunacholaumu wengi wetu ni matokeo na sio chanzo ama asili ya tatizo
Maono kimo cha mbilikimo ya mamlaka ya kisiasa ndio asili kuu. Ili kupunguza kelele za ajira wakaamua kuruhusu biashara huria ya pikipiki kama aina ya usafiri wa haraka bila maandalizi ya kutosha na bila kujali viwango vya chombo husika

Mwendelezo wa tatizo ni pale kijana asiye na mafunzo kamili na sahihi kukabidhiwa chombo cha moto kwa ajili ya biashara ya kubeba binadamu

Huyu kijana hana mafunzo kamili na sahihi ya kuendesha chombo cha moto, sheria na kanuni za barabarani, usalama wake na wa wengine, elimu ya uchumi nk.. Na hii yote inasababishwa na uwezo wa kifedha,, mafunzo ya udereva yanahitaji hela na kijana hana

Rushwa na ufisadi
Ili kijana athibitishwe ni dereva na amefuzu mafunzo ya udereva na kufaulu anahitaji nyaraka zinazothibitisha hilo.!! Leseni.. Kuipata leseni kwa kufuata utaratibu wa kisheria kunachukua muda na ni gharama
Kupitia vishoka na watendaji wa mamlaka ya mapato na jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani wasiojali usalama wa raia na mali zao kijana anapata leseni chap kwa haraka na kwa bei poa
Kuna ukiukwaji mkubwa sana kwenye kupata leseni za udereva

Sasa kijana ana leseni na ana chombo cha moto anaanza biashara bila kufahamu walau kanuni moja tu ya kupita makutano ya barabara penye taa nyekundu

Majumuisho haya ya wanasiasa, watendaji wa serikali wasio waaminifu na vijana wasio na ajira matokeo yake ndio haya ya ajali zisizokoma, zinazoteketeza nguvu kazi ya taifa na kuleta uhujumu mkubwa wa uchumi kupitia vifaa tiba, vilema, uharibu wa vyombo na vifo

Sent using Jamii Forums mobile app
Nakubaliana na wewe mkuu.. je kila panapotokea ajali inayohusisha bodaboda mwenye makosa anakuwa bodaboda peke yake??

Hizi lawama inabidi ziende na kwa watumiaji wengine wa barabara kama madereva kwa vile wao sio victim ndio maana tunawaona bodaboda kama wanamakosa.
 
Nakubaliana na wewe mkuu.. je kila panapotokea ajali inayohusisha bodaboda mwenye makosa anakuwa bodaboda peke yake??

Hizi lawama inabidi ziende na kwa watumiaji wengine wa barabara kama madereva kwa vile wao sio victim ndio maana tunawaona bodaboda kama wanamakosa.
Sio zote lakini asilimia 90 ni bodaboda

Sent using Jamii Forums mobile app
 
japo sijajua sababu wala kupata maelezo ya ajali but mimi kama mtu wa uchunguzi nakuja na majibu haya

kutokana na experience nliyonayo na hilo eneo, ajali ipo hivi
basi litakuwa linatokea fire uelekeo kisutu na boda alikuwa anatokea fire kukunja lumumba, kivyovyote boda anamakosa, kwani angle yake ya kuona kinachokuja nyuma ni ndogo mno.
 
Usimuonee huruma bodaboda hata kidogo, ajali ya jana iliyoua abiria 2 wa Noah Morogoro, sababu ni Bodaboda
huko vijijini wanagonga sana watu na kuwauwa afu wewe unawaonea huruma, wacha wafe. unakuta Boda anapita sehemu kuna vilabu wazee wanapumzika au kuna watoto na maspidi kama linaenda wapi sijui ! wacha wafe
 
Mi kinachonipa hasira ni madereva wa magari wanapowapigia honi waendesha pikipiki wapishwe ili wapite. Wakati hivyo vyombo vyote vina hadhi sawa barabarani.

Ni kweli vina hadhi sawa ila hata gari kama Haina mwendo sana inakaa upande kupisha wanaenda Kasi wapite.

Unakuta boda boda anaendesha taratibu mbele Yako, barabara Pana, na hajali kabisa kama Yuko peke yake barabara nzima. Hapo kinachotakiwa aendeshe upande urakaoruhusu gari kupita bila kusumbuana.
 
Leo asubuhi pametokea ajali maeneo ya DIT iliyohusisha basi la Mwendokasi na Pikipiki maarufu Bodaboda sina details za kutosha kuhusu madhara yaliyotokea kwa maana ya majeruhi au kama kuna kifo chochote lakini so far ni ajali mbaya maana time niliyokuwa napita basi la Mwendokasi lilikuwa linapigwa jeki na Pikipiki inatolewa chini ya uvungu mwa basi.

Kila mtu baada ya kuona mazingira yale alikuwa anatoa lawama kwa dereva bodaboda bila hata ya kuwa na picha halisi ya kile kilichotokea mpaka kusababisha ajali.

It's like ajali yoyote itakayohusisha bodaboda basi lawama zote atatupiwa bodaboda huu ni uonevu wa kiwango cha juu sio bodaboda wote hawaobey sheria za barabarani na sio kila dereva wa gari yupo perfect asilimia mia.

Tuheshimu Bodaboda nao ni Binadamu licha ya kuwa na mapungufu yao lakini still wana mema yao kama walivyo Binadamu wengine as long unajua kuendesha Pikipiki inabidi uwe mstari wa mbele kutetea bodaboda maana siku unaweza kuwa kwenye mizunguko yako ukapata mushikeli waka kuhukumu kama wanavyowahukumu bodaboda.
Huko chini ya basi iliiona na gari ndogo ikiwa imekandamizwa? Kama hakuna jiulize kwanini gari zilisimama bodaboda akaingia.
 
Leo asubuhi pametokea ajali maeneo ya DIT iliyohusisha basi la Mwendokasi na Pikipiki maarufu Bodaboda sina details za kutosha kuhusu madhara yaliyotokea kwa maana ya majeruhi au kama kuna kifo chochote lakini so far ni ajali mbaya maana time niliyokuwa napita basi la Mwendokasi lilikuwa linapigwa jeki na Pikipiki inatolewa chini ya uvungu mwa basi.

Kila mtu baada ya kuona mazingira yale alikuwa anatoa lawama kwa dereva bodaboda bila hata ya kuwa na picha halisi ya kile kilichotokea mpaka kusababisha ajali.

It's like ajali yoyote itakayohusisha bodaboda basi lawama zote atatupiwa bodaboda huu ni uonevu wa kiwango cha juu sio bodaboda wote hawaobey sheria za barabarani na sio kila dereva wa gari yupo perfect asilimia mia.

Tuheshimu Bodaboda nao ni Binadamu licha ya kuwa na mapungufu yao lakini still wana mema yao kama walivyo Binadamu wengine as long unajua kuendesha Pikipiki inabidi uwe mstari wa mbele kutetea bodaboda maana siku unaweza kuwa kwenye mizunguko yako ukapata mushikeli waka kuhukumu kama wanavyowahukumu bodaboda.
Kwanza kabisa kwa clip iliyorushwa nitoe pole kwa huyo boda boda kama bado ni mzima Mungu ampe nafuu apone haraka ila kama vinginevyo basi naoumba Mungu amjalie pumziko jema.
Nikirudi kwenye mada , siyo kwamba boda boda hawana haki, ila matendo yao ndiyo yanayopelekea siku zote kuonekana wanamakosa. Asilimia kubwa sana ya ajali unakuta makosa ni wao.
Kwanza asilimia kubwa unakuta wamshepata kilevi, viatu wanavyovaa haviendani na usalama wao unavaa makubazi huku unaendesha boda. Haya sheria sasa hawazifati kabisa unakuta mara wanapita gari mbele yao na mwendo kasi upande wa kushoto na mara hapo hapo wanahamia upande wa kulia mbele kidogo ya gari walilopita. Ukaaji wao unakuta wanakaa tako moja nje ya kiti yaani upande na jinsi wanavyoshika uskani wa piki piki unaogopa. Kibaya zaidi wao muda wote wapo na haraka tu. Kuna madau anasema kuwapigia honi ni sawa unakuta wamekaa katikati ya barabara na hawataki kupisha gari ipite unategemea nini asipigiwe honi? kama taratibu pikipiki ukiwa mwendo mdogo kaa kushoto ili chombo kingine kiweze pita kwa urahisi.
Pita magomeni wakati wa foleni unakuta njia ni nyembamba wanalazimisha kupita tena wengine wanakuwa na mamizigo na kusababisha uharibifu wa magari yaliyopo kwenye foleni. Kwenye taa hawataki kabisa kusubiri muda wa kupita.
Unakuta wakati mwingine wapo kituoni wakiona mteja upande wa pili kama nyumbu wanakurupuka hata piki piki 4 bila hata kuangalia barabara kugombea mteja 1.
Gari nyingi Dar es Salaam ukikuta kugongwa au mikwaruzo asilimia kubwa ni sababu ya boda boda.
 
Leo asubuhi pametokea ajali maeneo ya DIT iliyohusisha basi la Mwendokasi na Pikipiki maarufu Bodaboda sina details za kutosha kuhusu madhara yaliyotokea kwa maana ya majeruhi au kama kuna kifo chochote lakini so far ni ajali mbaya maana time niliyokuwa napita basi la Mwendokasi lilikuwa linapigwa jeki na Pikipiki inatolewa chini ya uvungu mwa basi.

Kila mtu baada ya kuona mazingira yale alikuwa anatoa lawama kwa dereva bodaboda bila hata ya kuwa na picha halisi ya kile kilichotokea mpaka kusababisha ajali.

It's like ajali yoyote itakayohusisha bodaboda basi lawama zote atatupiwa bodaboda huu ni uonevu wa kiwango cha juu sio bodaboda wote hawaobey sheria za barabarani na sio kila dereva wa gari yupo perfect asilimia mia.

Tuheshimu Bodaboda nao ni Binadamu licha ya kuwa na mapungufu yao lakini still wana mema yao kama walivyo Binadamu wengine as long unajua kuendesha Pikipiki inabidi uwe mstari wa mbele kutetea bodaboda maana siku unaweza kuwa kwenye mizunguko yako ukapata mushikeli waka kuhukumu kama wanavyowahukumu bodaboda.
Boda boda wanakufa sana kwa ujinga wao na kiburi.
Waliomba wenyewe kuingia mjini kati, ati wafanye biashara.
Fuata sheria basi-hakuna!
Sasa huyo slikiwa anafanya nini njia ya mwendokasi?
Wacha wasagwe, asiyefundishika sheria za barabarani, tairi halali yake
 
Bodaboda wanayohaki ila wao ndiyo hawapendi kutumia haki yao. Wanahaki ya kusubiri taa ziwaruhusu kupita ila wao hawasubiri.
Wanahaki ya kuruhusu watu wapite kwenye vivuko vya waenda kwa miguu ila wao hawarusu. Wanahaki ya kulipita gari kwa upande wa kulia (single lane) ila wao upita popote.
Wanahaki ya kupunguza mwendo kwenye maeneo hatarishi ila wao upiga honi tu.
Kimsingi bodaboda wanahaki zote kama watumiaji wengine wa vyombo vya moto ila wao ndiyo hawazingatii haki zao
 
Back
Top Bottom