Bodaboda hawana Haki

Bodaboda hawana Haki

Ajali ni ajali tu mkuu tho sometimes bodaboda wanajisabibishi vifo wenyewe kizembe...... sjui ni bangi au nini??
 
Mkuu
Ukiwa unapanda haya mabus ya mwendokasi kila siku, na ukawa unakaa pale mbele kabisa na dereva, utakubaliana na mimi kabisa kuwa bodaboda ni wapumbavu.

Na mbaya zaidi huwa wanajiaminisha kwamba hawezi kupatwa na hatari..
Gari ishatoka kasi, anaenda kujichomeka anavyopenda.

Mwendokasi huwa wanajitahidi mno kuwakwepa,
Muda mwingine hadi hupelekea gari lililobeba mamia ya watu kuyumba, kwa sababu ya mtu Moja aliyeamua kujitoa ufahamu na kukatiza bila mpangilio.


Kama mna ndugu zenu bodaboda na mnawapenda, tafadhali washaurini washikilie akili zao, badala ya kuziweka mfukoni.


Mwendokasi ina mapungufu mengi mno ila siyo kwa upande wa uendeshaji wa madereva .
Madereva wake wapo makini sana..
Laiti wangekuwa rafu kama wa daladala, ama wangekuwa na akili kama za bodaboda
Akiyanani kungekuwa na mamia ya misiba kila siku.
Sent from my TECNO CG6 using JamiiForums mobile app
Mwendokasi vituo vipo karibu karibu sama,pia barabarq zetu zebra kila mahari,ndio maana watu wanagongwa
 
Sio DIT kabisa ni nyuma kidogo pale kwenye mataa ambapo kuna barabara ya kwenda Lumumba kama sijakosea.. Muda mwingine madereva wa mwendokasi wanadharau mataa.

Kama ni hapo basi kweli bodaboda kwa asilimia 99 ndiye aliyejimiksi....

Huwa wanagongwa sana kwenye hayo mataa hasa wale wanaotoka Morogoro Road kukatiza kuelekea Lumumba Road...

Maderava wa pikipiki huwa hawana subira na wengi ni weupe sana wa sheria za barabarani...
 
Mi kinachonipa hasira ni madereva wa magari wanapowapigia honi waendesha pikipiki wapishwe ili wapite. Wakati hivyo vyombo vyote vina hadhi sawa barabarani.

Gari na pikipiki havina hadhi sawa barabarani tafadhali mkuu, ingawa vyote ni vyombo vya moto...

Kisheria mtu wa pikipiki anapaswa aendeshe upande wa kushoto wa barabara na sio katikati au kulia mwa barabara...

Kuna sheria ya mwendokai pia, "dereva azingatie ukomo wa mwendo (speed limit) na wakati wote asizidi mwendo wa kilometa hamsini kwa saa (50kph)"...

Sasa katika haya mawili, kwa nini usipigiwe honi na gari ambalo kwa kawaida speed limit kwenye maeneo huru ni 80kph?
 
Leo asubuhi pametokea ajali maeneo ya DIT iliyohusisha basi la Mwendokasi na Pikipiki maarufu Bodaboda sina details za kutosha kuhusu madhara yaliyotokea kwa maana ya majeruhi au kama kuna kifo chochote lakini so far ni ajali mbaya maana time niliyokuwa napita basi la Mwendokasi lilikuwa linapigwa jeki na Pikipiki inatolewa chini ya uvungu mwa basi.

Kila mtu baada ya kuona mazingira yale alikuwa anatoa lawama kwa dereva bodaboda bila hata ya kuwa na picha halisi ya kile kilichotokea mpaka kusababisha ajali.

It's like ajali yoyote itakayohusisha bodaboda basi lawama zote atatupiwa bodaboda huu ni uonevu wa kiwango cha juu sio bodaboda wote hawaobey sheria za barabarani na sio kila dereva wa gari yupo perfect asilimia mia.

Tuheshimu Bodaboda nao ni Binadamu licha ya kuwa na mapungufu yao lakini still wana mema yao kama walivyo Binadamu wengine as long unajua kuendesha Pikipiki inabidi uwe mstari wa mbele kutetea bodaboda maana siku unaweza kuwa kwenye mizunguko yako ukapata mushikeli waka kuhukumu kama wanavyowahukumu bodaboda.
Boda wanavunja sana Sheria ! Na wanakera sana. Wameshazuiwa kutumia Barabara za Mwendo kasi muda tu awasikii! Uwezi risk maisha ya watu zaidi ya 100 waliopo kwenye bus kwa ajili ya mpumbavu mmoja- unakula kichwa tu hii ndo dawa- ajali ya jana ni miongoni mwa makumi ya ajali za Boda na Bus za mwendo kasi. Inatakiwa bodas wapewe mafunzo ya Driving na pia ije kuwa boda akipata ajali ya kutokana na uzembe afutiwe leseni milele hapo ndo watakuja kuwa na adabu
 
kuna muda natamani wizara husika, ama sekta husika zingewapeleka boda boda kujifunza Kigali Rwanda. Kila dereva na abiria lazima avae helmet, na ni wasafiri wawili tuu (dereva na abiria) kwa boda boda

Pia, madereva wa magari akikutwa amelewa ni jela siku 5/7 na fine juu. Wengi hupaki magari na kutumia usafiri wa uma kwenda kwenye burudani
Kwamba Mwendokasi dereva alikuwa kalewa?

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Mwache huyo anaongea, binafsi npo napambania afya hapa wiki ya pili siendi kazini kisa kichaa Moja alikua anaendesha gari Kwa speed kubwa na hayupo site yake kubalance mambo ikabidi aforce kupenya akaniparamia
Mkuu pole sana
 
Back
Top Bottom