Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Baadhi ya wanachama wa Umoja wa Waendeshaji Bajaji, Bodaboda na Wajasiriamali Jijini Dar es Salaam wametangaza kutoshiriki maandamano yaliyoitishwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), yaliyopangwa kufanyika Aprili 24, 2025, kuelekea Mahakama ya Kisutu, ambako kesi ya Mwenyekiti wa chama hicho, Tundu Lissu, inatarajiwa kusikilizwa.
Akizungumza katika mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Ilala, Makamu Mwenyekiti wa Wajasiriamali Wadogo nchini, Steven Lusinde, amesema wanachama wao wameamua kutumia siku hiyo kwa shughuli za kiuchumi badala ya kushiriki maandamano.
"Hatuko tayari kupoteza muda kwenye maandamano. Tunajitambua na tunathamini kazi zetu za kila siku ambazo zinatuletea riziki na maendeleo," amesema Lusinde.
Lusinde ameongeza kuwa wanapinga vitendo vya uchochezi, na badala yake wanahamasisha amani na utulivu. Pia amekumbusha kauli ya zamani ya mmoja wa viongozi wa CHADEMA aliyewahi kudharau kazi ya bodaboda kwa kusema ni 'kazi ya laana, jambo ambalo bado halijapokewa vizuri na wahusika.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Shirikisho la Maofisa Wasafirishaji nchini, Said Kagomba, amethibitisha kuwa wamepata taarifa za maandamano kupitia vyombo vya habari, lakini hawatashiriki. Ametoa wito kwa Jeshi la Polisi kuhakikisha amani inadumishwa.
Akizungumza katika mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Ilala, Makamu Mwenyekiti wa Wajasiriamali Wadogo nchini, Steven Lusinde, amesema wanachama wao wameamua kutumia siku hiyo kwa shughuli za kiuchumi badala ya kushiriki maandamano.
"Hatuko tayari kupoteza muda kwenye maandamano. Tunajitambua na tunathamini kazi zetu za kila siku ambazo zinatuletea riziki na maendeleo," amesema Lusinde.
Lusinde ameongeza kuwa wanapinga vitendo vya uchochezi, na badala yake wanahamasisha amani na utulivu. Pia amekumbusha kauli ya zamani ya mmoja wa viongozi wa CHADEMA aliyewahi kudharau kazi ya bodaboda kwa kusema ni 'kazi ya laana, jambo ambalo bado halijapokewa vizuri na wahusika.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Shirikisho la Maofisa Wasafirishaji nchini, Said Kagomba, amethibitisha kuwa wamepata taarifa za maandamano kupitia vyombo vya habari, lakini hawatashiriki. Ametoa wito kwa Jeshi la Polisi kuhakikisha amani inadumishwa.