Binti Mariam

Binti Mariam

mentor toa kabila, ingawa kwa uelewa wangu makabila yanaruhusu kuoa sehemu na familia moja!! hivyo wewe utaoa huyo mary wako na itakuwa bomba sana kwa koo zote mbili yako na ya Mary. Unajipa hofu tu, au kama unataka kutengeneza Movie!!!!(kamwone Ndauka na Ray) Hii wala siyo kitu cha kuomba ushauri. after next month wewe peleka posa, Mary siyo ndugu yako hivyo wewe oa, watu wanaoa binam!!
 
Dah, ngoja nimtafute Paloma aniambie although ninachojua mimi na wewe wote ni walutheri na wote ni waimbaji ila all ni all nitamuuliza Paloma.

Ila Mentor usimuache Mary bana lol! Najaribu kuvaa viatu vyake hata havinitoshi lol!

Halafu ram, mimi na wewe tuna kitu kimoja very common hujajua tu! Hebu muulize dada Paloma atakuambia...kila nkiona post yako...




besame mucho bestiii...
 
Last edited by a moderator:
Dah, ngoja nimtafute Paloma aniambie although ninachojua mimi na wewe wote ni walutheri na wote ni waimbaji ila all ni all nitamuuliza Paloma.

Ila Mentor usimuache Mary bana lol! Najaribu kuvaa viatu vyake hata havinitoshi lol!

I will take your advice kwa sasa nangojea mawazo ya wazazi...

Duh hilo la Ulutheri sikuwa nalifahamu though..kutokana na 'kitu' kinachotufanya tuwe common one could guess that!


ha Mentor kumbe we schoolmet wangu?ukute tulikuwa darasa moja


Haha..hisabati ulifundishwa na mwalimu Msaki? yule anayetumia mkono wa kushoto? Usiombe siku akikuchapa atoe saa....

Au Sayansi kilimo ulifundishwa na mwalimu Mboya???

Na Kiingereza je darasa la tatu na nne? Mwalimu Kasa...alikuwa ananiita 'my singer' akiingia tu darasani akanikuta nimepiga magoti mbele (kisa kusumbua darasani) ataniambia nisimame halafu niimbe wimbo nikakae..dah! dem good old days.."one man and his dog, in a little house..."



Sioni tatizo..hamhusiani damu wala maji.

@madameX, undugu ulishaundwa na kaka yangu au? wewe ni mchaga?
 
Ungekua unampenda kwa dhati, usingeandika hta hii thredi. Ungefanya uamuzi mwenyewe wa kumuoa hata kama ungetishiwa kung'olewa kucha.
 
Mwl Msaki nasikia sijui kawa mlokole kwenye mambo y akuombe?just hearsay.Da long tena nata ka kufuata cheti changu nije kuomba kazi PCB hahhaha.
Ile njia ya kwenda kibo tokea moshi arusha hosp imekwisha2 yani utafikiri moshi hakuishiwatu zile nyumba zimekuwa kama za makumbusho.huyo upendo usikute baba ke ananziwa na B?Am just try to speculate.

Mary msahau bwana time is a good healer.Usidanganywe kuoa nyumba moja kwa kichaga hizo ni" mbaka"kuichi mbaka?
 
Ungekua unampenda kwa dhati, usingeandika hta hii thredi. Ungefanya uamuzi mwenyewe wa kumuoa hata kama ungetishiwa kung'olewa kucha.

@kakaJambazi, wahenga walisema, "It takes more than love for two people to be together." Ukilielewa hilo hutokimbilia kuwa na mtu eti kisa tu unampenda...


Mwl Msaki nasikia sijui kawa mlokole kwenye mambo y akuombe?just hearsay.Da long tena nata ka kufuata cheti changu nije kuomba kazi PCB hahhaha.
Ile njia ya kwenda kibo tokea moshi arusha hosp imekwisha2 yani utafikiri moshi hakuishiwatu zile nyumba zimekuwa kama za makumbusho.huyo upendo usikute baba ke ananziwa na B?Am just try to speculate.

Mary msahau bwana time is a good healer.Usidanganywe kuoa nyumba moja kwa kichaga hizo ni" mbaka"kuichi mbaka?

Hahah..eti kawa mlokole? sipati picha.

Cheti cha darasa la saba wakitakiani? Hata sijui kama bado vipo aisee...Halafu hiyo njia imekua kamsitu tu...watu wpo dar wanakusanya hela. sijui wanangojea nani aje aendeleze mji ndo wao waje kuishi!??? kama pale exactly opposite na kibo primary...dah mpaka panasikitisha!

Halafu waliniuzije walipobadilisha jinaaaa!??? sipapendi tenaaa...

:focus: Sikutajii aisee..unaweza ukanifahamu na mimi!!!
 
Paloma, Mentor aliniambia nikuuulize kwamba, mimi na mentor tuna kitu ambacho ni common, hebu niambia dada ni nini hicho, plz!

what?!?!?!!
pole sana!!! kweli mapenzi yamekuchanganya!!! hebu tulia kwanza!!!
 
POLE SANA...ILA NILIWAHI KUSIKIA KUWA INAWEZEKANA KABISA MKAOA SEHEMU MOJA NA KAKA YAKO...SIJUI KWENYE MILA YENU
 
Mi ninaye fahamu hilo,,mi lilinitokea nikaamua kuowa tu na Leo tunaishi ,,Hapo uamuzi ni kwenu,,Sometime unatikiwa uwe wrong kwenye chaguzi sahihi,Ukiamgalia kwamba wewe hutakuwa wa kwanza,duniani nilipiga mimba nikasema bahati mbaya kwa ndugu lakini Leo ndio mke sahihi wa maisha yangu na tunapendana,, na Leo siishi maisha yangu ya zamani yaani leaving my dream life,,coz we know each other since ,,Childhood,, mpaka Leo 30+,,,
 
Kwa ushauri wangu,ww mchukue mary hyo kwa sababu ni family moja na sio kwamba mmeshea mke.
 
Sahau kabisa about Mary, mbona wanawake wapo wengi? Kwanza sidhani kama huyo Mary mnapendana naye kikweli, nashangaa eti tangu utotoni mnafahamiana/marafiki? Sasa ndo umekomaa na unaweza kufanya maamuzi na chaguo sahihi kabisa.
 
Binti Mariamu

Weekend hii kwangu ilikuwa ya tafakuri nyingi zisizo na majibu na msongo mkubwa wa mawazo. Ilikuwa weekend yenye kuumiza na ya kujiuliza sana juu ya mustakabali wa maisha yangu ya mahusiano.

Nilienda kwenye send off ya mchumba wa kaka yangu.

Kwanza nitangulize samahani kwa dada zangu wapenzi gfsonwin, AshaDii na Paloma na shostito zangu mimisa na BelindaJacob kwa kutowahi kuwasimulia jambo hili lililokuwa linanitesa moyoni kwa muda mrefu..huenda wangenipa ushauri wa kunifaa…

Moshi, Kilimanjaro 1994


Baba alikuwa amehamishiwa mkoa wa Kilimanjaro kama Mkuu wa Polisi Wilaya ya Moshi Mjini. Mwaka huo huo alikuja Afisa Mifugo mpya wa Wilaya. Tulikuwa tukiishi karibu maeneo ya Shanty Town. Afisa mifugo huyu alikuwa na watoto watatu. Wa kwanza ni binti mkubwa (dada Pendo), wa pili ni binti mwingine mrembo zaidi (Mary) na mdogo wao wa kiume (Michael).

Nilikuwa naingia darasa la nne.

Dada Pendo alikuwa anaingia darasa la sita na Mary ndo alikuja kuanza darasa la Kwanza wakati Michael alikuwa bado mdogo kuanza shule ya msingi hivyo yeye alienda shule ya awali ya St. Margeth maeneo ya kule kule shanty town.
Pendo, Mimi na Mary tulienda shule moja ya Kibo primary enzi hizo mwalimu mkuu ni mama Nkya.

Tulipatana sana na Mary kwani licha ya kucheza pamoja nlikuwa nikimfundisha sana hesabu. Na kwa vile tulikuwa majirani basi tulishirikiana kwa mambo mengi…hadi nilipomaliza shule ya msingi tulikuwa na urafiki mkubwa sana.

Sekondari nilipangiwa Kibaha na hata huko bado niliendelea kuwasiliana na Mary. Tuliwasiliana zaidi kama marafiki na kwa kipindi kile hakuna kati yetu aliyekuwa akiwaza mapenzi (atleast kwangu sikuwa nikiwaza kabisa).

Dada yake na ndugu wengine walifahamu jinsi tulivyokuwa tunapatana na Mary mpaka hadi wazazi wake wakawa wanatuita wachumba.

Mary ni binti aliyelelewa vizuri kwao. Nashindwa kuamua nimeliona hilo zaidi kwake kwa kuwa tu tulikuwa majirani au ni kweli ni mmoja wa mabinti waliofunzwa wakafundika.

Mary ameniona at my best and worst moments..na katika nyakati zote hizo bado tuliendelea kuwa marafiki.

Nakumbuka utotoni nilikuwa nikitoroka nyumbani kwenda kucheza mpira uwanja wa Ushirika. Siku moja nilirudi usiku baba akanichapa nje ya nyumba yetu huku Mary akiniona. Of course pamoja na kuona aibu sikuacha kutoroka, ila siku mbili baadaye nilirudi nyumbani jioni. Mary aliponiona tu akanikimbilia akanipeleka kwao nkanawa miguu halafu kama nusu saa hivi nikatoka nje na yeye akaniaga kwa nguvu ili wajue nlikuwa kwao namfundisha…

December, 2009

Baada ya kumaliza chuo tuliendelea sana kuwasiliana na Mary. Wakati huu mawasiliano yetu yalibadilika kwenda more personal. Kwa bahati nzuri she was as single as I was. Tukawa tunawasiliana sana..calls. sms na safari za mara kwa mara kwenda Arusha ambako ndiko aliko kwa sasa.

Ghafla mwaka 2010..

Mary akanitext kuniambia kuwa kuna kitu kinaendelea kwa dada yake. Kwanza dada yake alimuambia kuwa amepata boyfriend ila hata yeye mwenyewe Mary atakuwa anamfahamu sana tu. Hakuhisi chochote hadi aliponitumia ujumbe huo mfupi. Alikuwa ni kaka yangu.

Sijui ni lini walianza mahusiano yao lakini kwa vyovyote vile walijua mimi na Mary tulikuwa more than friends. Ni mara nyingi nilikuwa namuambia bro naenda Arusha kumsalimia Mary. Kwani yeye alidhani nilikuwa naenda kucheza naye karata? Au kuruka kamba? <machungu> Ndiyo sikumuambia exactly uhusiano wetu ulipofika ila ni kwa sababu haukuwa muda muafaka.

Kaka yangu akanizunguka akaenda kumchumbia dada Pendo.

Nakumbuka Mwaka juzi nilipoenda tena Arusha Mary alitaka nimpe mimba tu lolote na liwe alimradi tu tuvunje mipango yao. Alinisisitiza sana ila nilimkatalia…how I wish I just did it <majuto>.

Muda ulienda haraka mara tukaitwa utambulisho wa shemeji yetu kama familia.

Ilikuwa kama miaka ile tulipokuwa tunaishi wote Moshi. With the exception ya mimi, watu wote walikuwa na furaha sana. Nilishindwa kujua kwa nini kaka yangu aliamua kunifitini vile <usaliti>.

Ghafla tukaenda kupeleka posa kwa kina Mary…mtoto mchanganyiko wa Kisukuma na Mnyakyusa..yaani mchangamfu ila adabu tele. Acha tu!!!!! <machungu>

I wish ningemkubalia Mary wazo lake kipindi kile..sasa Mary ni shemeji yangu.

Mary, kwa yeyote atakayekuja kukuoa..am sure amepata mke mwema. Sijaona binti mwenye nidhamu kama wewe. Mcheshi na mwenye kupenda watu.

Jumamosi hii ndiyo tulikuwa Morogoro, walipo wazazi wa Mary, kwenye send off party ya binti yao, dada Pendo, ambaye mwisho wa mwezi ujao atakuwa officially shemeji yangu and hence make Mary officially out of bounds for me.

Ndo nimerudi kutoka Morogoro jana..na sasa nipo kazini,


Wasalaam wapendwa,
Mentor.

Kaoe acha ushamba wasukuma nyie vipi?? Hakuna zuio la mtu kumuoa shemeji yake! Kikwetu shemeji yako ata kama siyo kuoa ukiomba mzigo huwezi nyimwa. Oa acha umami wa kisukuma.
 
Back
Top Bottom