Bila kuvunja ukimya, UKIMWI utalimaliza Taifa

Bila kuvunja ukimya, UKIMWI utalimaliza Taifa

Juliana anapita na wengi kwa kasi sana, tuchukue tahadhari.
 
Virus kufubaa na kuzuia maambukizi connection yake
Ukinywa dawa na kufanikiwa kufubuza virusi huwezi kuwaambukiza wengine. Kiingereza wanaita undetectable status ni hali ambayo virus vibavotembea kwenye damu vimeshauliwa na ARV’s.
 
Kwakweli ipite maana leo tu manzi nayofukizia imeniambia tukapime kwanza eet siwezi kukupea
😀😀😀 pole aisee. Kama kile kipimo cha macho kakikataa hamna namna itabidi uende kupima tu.
 
Tatizo hichi siyo kipaumbele chao , wameshayatamia madaraka wamesahau raia wanateketea kwa hili gonjwa.

Muhimu ni kuwa na nidhamu katika maisha yako ya ndoa.
 
Bila kuvunja ukimya na sasa watu wenye maambukizi kutambulika na kuweka sera madhubuti basi Taifa lita angamia lote.

Jamani ipo shida kubwa sana sana. Watu wanasambaza huu ugonjwa na wengine wana pesa. Wanasambaza kwa vijana na vijana wanasambaziana.

Siri ni kubwa sana na Taifa lina angamia. Vijana wana angamia na wazee pia nani atapona nani atakuwa na uchungu kwa Taifa?
Nilikuwa naangalia vzr date ya hii post nilidhani ni ya 2012 kumbe ya 2020, nani alikuambia kuwa ukimwi bado ni tishio mpk leo?
 
Wengi wanajidanganya kwamba eti dawa imepatikana, wanasema heri ukimwi kuliko Ebola au corona maana ukimwi unaweza kutumia dawa uka survive hata miaka 20 wakati Ebola na corona week mbili tu umekatika,


Kiukweli ukimwi unaua watu wengi sana sana , jamani dawa zina mwisho wake wa nguvu, zinafika mahali zinaishiwa nguvu kabisa, nimeshuhudia watu wengi sana wanaotumia dawa wakiondoka baada ya dawa kushindwa kazi kabisa, ndugu zangu chonde chonde wapendwa tuwe makini jamani Ukimwi bado upo na una ua wandugu!
Ingekuwa ukimwi una sifa hizo ulizozitaja basi leo hii pasingekuwapo mtu Tanzania hii, ni kwamba huo ugonjwa upo ila watu walishapewa tahadhari kuanzia wazee mpk watoto wadogo wanajua jinsi ya kuepuka so kilichobaki ni nature tu.
 
Tatizo hichi siyo kipaumbele chao , wameshayatamia madaraka wamesahau raia wanateketea kwa hili gonjwa.

Muhimu ni kuwa na nidhamu katika maisha yako ya ndoa.
Serikali imeshakupa elimu namna ya kujikinga. Unataka ije ikupige kufuli kwenye nyeti ndio utambue inachukua hatua na kulipa kipaombele hili janga. Mambo mengine ni uzembe wa wananchi yakiwapata wanalaumu serikali.

Mfano serikali imetengeneza mitaro ya kuondoa maji, mnafagia na kugeuza mitaro madampo ya taka na siku mafuriko yakiwapiga mnalaumu serikali haizibui mitaro. Nyambafu, kufeni kwa uzembe wenu.
 
Nilikuwa naangalia vzr date ya hii post nilidhani ni ya 2012 kumbe ya 2020, nani alikuambia kuwa ukimwi bado ni tishio mpk leo?
Ndugu bila kuchukua tahadhali huu ugonjwa ni tisho, sio kwa taifa bali kwa mtu husika. Kwanza jiulize kumeza madawa kila siku na kuzorota kwa kinga ya mwili.

2020 Tanzania ina wagonjwa 1,600,000. Hii inakaribia kabisa nguvu kazi iliyompigia kura TUNDU.
 
Serikali imeshakupa elimu namna ya kujikinga. Unataka ije ikupige kufuli kwenye nyeti ndio utambue inachukua hatua na kulipa kipaombele hili janga. Mambo mengine ni uzembe wa wananchi yakiwapata wanalaumu serikali.

Mfano serikali imetengeneza mitaro ya kuondoa maji, mnafagia na kugeuza mitaro madampo ya taka na siku mafuriko yakiwapiga mnalaumu serikali haizibui mitaro. Nyambafu, kufeni kwa uzembe wenu.

Nyambafu Mama yako.
 
Back
Top Bottom