Bila kuvunja ukimya, UKIMWI utalimaliza Taifa

Bila kuvunja ukimya, UKIMWI utalimaliza Taifa

Na hayo madonge yanasumbua kama una kinga dhaifu utaumwa kila leo uombe uwe na group zuri la damu hapo hutasumbuka maana nina mtu wa karibu hapa kila siku mgonjwa hata sielewi nifanyaje nae
 
ukimwi bado upo, tuache ngono, tuache michepuko ya nje baki na mke wako uliye muoa, hutopata ukimwi.
kwa asilimia 99 ukimwi unaambukizwa kwa ngono.
sema baki na mke au mume wako.maana hapa hujawa gender sensitive.Inasemekana Wanawake ndiyo wanaoongoza kwa kutouogopa UKIMWI.wanaaume ni waoga balaa.na huwa wana hofu sana wakistukia kuna tabia hatarishi wamefanya
 
sema baki na mke au mume wako.maana hapa hujawa gender sensitive.Inasemekana Wanawake ndiyo wanaoongoza kwa kutouogopa UKIMWI.wanaaume ni waoga balaa.na huwa wana hofu sana wakistukia kuna tabia hatarishi wamefanya
Wanawake ni wengi vile ukienda clinic na mimba ni lazima upimwe na nyie wanaume kwenda hospital ni binde ipitishwe Sheria kupima iwe lazima
 
Elimu izidi kutolewa, hasa kutokukubali kushiriki ngono bila kupima. Hii itasaidia kwa asilimia kadhaa kupunguza maambukizi
 
Tiba za asili zipo na zinaua virus japo Wazungu wanaamini Virusi hawafi. Nimeshuhudia watu kadhaa.
Ingekua vizuri kama watu watakua na uelewa wa kupima damu kila mara hata kama wanatumia dawa za asili. ARV zimefanyiwa majaribio ya kisayansi na kuna ushahidi kuwa zinafubaza virusi lakini wengi wanaacha kutumia ARV wakitumia dawa za kienyeji matokeo yake bado hayajafanyiwa utafiti wa kisayansi.
 
Acha tuishe, wapumbavu sisi acha tuishe tu kije kizazi kinachojitambua
 
Hii December mosi ipite tu maana kila ikikaribia ni tafarani tu. Kila aina ya story utaisikia

NB: Ukimwi upo lakini
Kwakweli ipite maana leo tu manzi nayofukizia imeniambia tukapime kwanza eet siwezi kukupea
 
Wengi wanajidanganya kwamba eti dawa imepatikana, wanasema heri ukimwi kuliko Ebola au corona maana ukimwi unaweza kutumia dawa uka survive hata miaka 20 wakati Ebola na corona week mbili tu umekatika,


Kiukweli ukimwi unaua watu wengi sana sana , jamani dawa zina mwisho wake wa nguvu, zinafika mahali zinaishiwa nguvu kabisa, nimeshuhudia watu wengi sana wanaotumia dawa wakiondoka baada ya dawa kushindwa kazi kabisa, ndugu zangu chonde chonde wapendwa tuwe makini jamani Ukimwi bado upo na una ua wandugu!

Umeshuhudia watu wengi sana????[emoji276]
 
Back
Top Bottom