Hongera FF.
Ila jamani, FF ni mgumu kiasi cha hata kushukuru? Manake simuoni ati, au sijapitia posts zote?
Dina huyu FF hua full time hapa JF... leo sijui nini, I really
hope inahusiana na kuboresha ndoa and she will be back....
Faiza, nakupa hongera za dhati kabisa, nimejaribu sana kukupigia simu sijakupata, kwa bahati nzuri "Gozi" lako likanipigia alfajiri ya leo na kunieleza kuwa kakunyang'anya simu yako na kaizima. I wonder why.
Nikikupa pongezi peke yako itakuwa simtendei haki "shemeji" yangu, Gozi lako, nampa pongezi sana kwa kuidumisha ndoa hii kwa miaka hii yote. Najua kakustahamilia sana, au niseme mmestahamiliana? Nawapa pongezi za dhati.
Jamani wana JF, wakati FF ananiita mimi "Anko" huwa anakosea, mimi si "Anko" wake bali ni "cousin" wake kwa mama, yaani ni mtoto wa mama mkubwa na mdogo, ingawa nimemzidi kidogo tu kwa umri (tumecheza pamoja utotoni) lakini amezoea kuniita anko baada ya kuwa tu watu wazima na nephews wamekuwa wengi kiasi cha kusahaulika jina langu na kuwa ni ama "anko" au mjomba kwa wengi wanaonifahamu, inanshangaza kuwa hata "bi mdogo" (mke wangu wa pili) huniita anko.
Nimeongea hayo, kwa kutaka tu kuwafahamisha kuwa FF namjuwa, sana sana tena sana.
FF, kwa anaemjuwa, ni easy going, fun loving, with a big smile always. Anaependa sana ndugu zake na marafiki zake, yupo tayari kuwatetea awajuao hata kama wana makosa, she will never betray you! Ni mwanamke straight forward hatafuni maneno na siku zote husema, "nichukie kwa ukweli wangu, usinipende kwa uongo wangu".
Katika kukua kwetu jijini Dar. FaizaFoxy, mitaa ya kariakoo (ya late 60's na early 70's) ni maarufu sana kiasi anatisha kufatana nae. Umaarufu wake una kuja mara mbili, kwanza kazaliwa, kasoma na kukulia hapo Kariakoo, pili kaolewa na mtu maarufu sana pale Kariakoo na Dar au Tanzania kwa ujumla, kutokana na shughuli zake, ni mtoto wa Kariakoo tuliye kuwa nae pia.
Kwa miaka mingi tulipoteana na FF baada ya yeye kuolewa na kwenda kuishi nje ya Tanzania kwa muda mrefu sana, ukimuuliza mwenyewe kwanini mliamua kukaa nje miaka yote hiyo? mwenyewe hujibu "tulimkimbia" Nyerere na siasa zake za kukandamizana. Lakini najua ni stihizai zake tu, kama kuna mtu alikuwa akimpenda Nyerere tulivyokuwa tunakua basi sijamuona zaidi ya FF. Sijui kwa nini baada ya kurudi Tanzania akawa hapatani na Nyerere.
FF ni mkimya sana na huwa haongei mengi, mimi nashangaa hapa JF kawa ni mmoja wa "wapayukaji" na saa zingine huwa ananikera, lakini naweza kukisia ni kwa nini. Ntamuachia mwenyewe.
Nna mengi ya kuongelea kuhusu FF lakini itakuwa si vyema nikamsemea, pengine mwenyewe hatopenda kusemewa yake.
Hongera Faiza, Hongera G.
Psss. Hiyo nick ya Foxy, alipewa na kakaetu mkubwa (mungu amrehem), toka utotoni na imeshika mpaka leo, ingawa sana ilikuwa kwa kifamilia tu tunayoijua, nashangaa kukuta anaitumia humu JF, muulizeni mwenyewe ina maanisha nini.
mimi miezi mitatu tu ya ndoa, mke nimefukuza karudi kwao
Hongera Asha kwa kufikia uzee!!!
Maini hayazeeki lakini!!
Zomba... What an insight on FF.... Thank you.... I feel i know her mo'
And sasa i understand our last VM disagreement imetoka wapi....
Pamoja Saaana.
ADI
Nikisikiaga jina Foxy basi namkumbuka Pam Grier.
kwa kauli hizo juu inaonesha wewe ni
FF.
Hongera jaman FF!
wifi nilikuambia natamani lile jukwaa la FF aliloliota! yaani siku hizi ukiongelea 2nd anniversary watu wanakuona like ana alien! it is a sad one, nadhani analysis ya tatizo inabidi ianzie kwenye kuzaliwa hadi sasa. kakangu eiyer alisema asubuhi labda vile wamama wanaenda kwenye siasa na kazini so watoto wanakosa malezi ya mama hadi wanashindwa jinsi ya kuishi na wenza wao? (i am looking for causal-effect relationships,lol!)
Hongera sana FF kwa kufikisha miaka 30 ya ndoa lakini nitakuwa simtendei haki Mumewe FF kwa ustahimilivu mkubwa.Kuishi na Mamaa wa mipasho miaka 30 si mchezo hata kidogo.Mwanzoni nilidhani FF ana miaka kati ya 18 - 20s baada ya kusoma hii bandiko nimebaini nilikuwa simtendei haki FF kuanzia leo FF nitamwita Dada FF.Tunapishana na Dada FF kwenye baadhi ya mada lakini kuna baadhi ya mambo Dada FF ananikosha sana [1] Hakimbiii mada aliyoianzisha Nape anastahili kujifunza hili.[2] Ni mjuzi wa kutetea hoja hatukani ingawa mipasho si haba.[3] Anaipenda dini yake Islam ikiguswa anakuwa mkali kama pilipili kichaa.
aisee hii kali..shida nini mkuu.
Kwa kweli ana stahili hongera FF, du ina maana FF anagonga kama 50 years hivi kama aliolewa na 20 years! sasa nikifikiria na ukada wake wa CCM, na misimamo yake kweli inaingia akilini, nilikuwa nashindwa kuelewa , kumbe umri umekwenda!
mkuu inawezekana JF ndiyo mahali pake pa kupigia story na kumwaga utumbo na hasira zote, akiwa mtaani, rafiki yake ni mumewe tu. inawezekana pia ni mke mzuri sana huyo FF-anaweza hata akakuogesha huyo.
Mwenye siri ni mumewe!
Nampongeza FF kwa miaka 30 ya ndoa. Mimi nimesherehekea ya kwangu ya miaka 33 Jan 1, 2011
Kama ametulia kiasi hicho asijidhalilishe kutetea SIASA UCHWARA (by Rostam). Nina imani hakuna chuo kikubwa kuliko ndoa. Ushirikiano na familia yake ni msingi tosha na ushahidi wa kuvumilia hoja mbadala hata za kisiasa.
Faiza, Zawadi zangu naona uzitakiNimecheeeeka, yaani wewe mke mzuri ni wakukuogesha tu? Hayo mbona ni kawaida, muhim ni nini unachogeshewa si kuogeshwa!<br />
<br />
Ahsante sana.
Hongera sana mamito.
Mungu akupe afya njema.
Hongera sana! big up Faiza