Biblia na reference ya vitabu vya kipagani

Basi tusaidie kwanini kitabu cha Nabii Gadi hakipo kwenye biblia??? Kwanini kitabu cha Jasher na Enoko havipo katika Biblia??
Ni vema utambue kuwa Biblia tuliyonayo ni mkusanyiko wa Vitabu mbalimbali vya kiimani.

Pili, ni Vitabu vile ambavyo vilivyopatikana wakati wakiiandaa Biblia ndivyo vilivyounda Biblia, Vitabu vingine havikupatika na hivyo havikujumuishwa kwenye Biblia.

Tatu, kuna Vitabu vinasadikika kuwa vya kiimani vilivyodaiwa kuwa viingizwe kwenye Biblia lkn havikukidhi canonical rules kuijumuishwa kwenye Biblia maana vinaonekana viko tafauti kabisa na vinapingana vitabu vinginevyo. Mfano ni kinachodaiwa kuwa ni Injili ya Barnaba.

Vv
 
Natumai unaongelea hicho kitabu, sio vyote!
 
Natumai unaongelea hicho kitabu, sio vyote!
Mkuu ww ulikataa vitabu nje ya Biblia sio vya kipagani ndio nmekuonyesha mifano ya hivyo viwili jinsi vilivyo kinzana so nataka kwanza ukubali je ni vya kipagani au lah?? Na kama umekubali unazungumziaje kitabu kitakatifu kuchukua reference ya vitabu vya kipagani?? Huu ndio mzizi wa hoja
 
1. Vitabu vingapi?? Alikusanya nani?? Mbona kila kanisa lina vitabu vyake?? Nani yuko sahihi?? Kma namba zinakinzana iweje uviite vya kiimani ilihali tunajua Mungu hajipingi mwenyewe

2. Una maanisha Biblia haijakamilika? maana unadai kuna vitabu vya kiimani vilivyopotea? Je una maana neno la Mungu linaweza kupotea kama gazeti la uwazi tu??

3. Canonical rules ni zipi?? Kama zilikuwepo hizo rules kwanini namba ya vitabu inatofautiana?? To be specific unaongelea Biblia gani maana kila Biblia ina canonical rules zake!! hivyo kitabu A kinaweza kiwe halali Catholic ila kikawa haramu Anglican!
 
Biblia ni mkusanyiko wa vitabu 66, viliunganishwa pamoja kwa kuangalia vitabu vyenye manufaa kwa watu wa Mungu, unataka vitabu vinavyoongelea "ushoga" wa Daudi(Kama unavyodai) ili ujifunze nini hapo? Vitabu vipo vingi sana zaidi ya hivyo 66 au 72, lakini havina mantiki ya kuwekwa kwenye Bible, hakuna cha kujifunza. Kuna wafalme, manabii na watu wengine wa kawaida, lakini ni kwamba hawakuandika kwa utashi wa kufundisha njia za wokovu; bali waliongelea historia(nyingne binafsi) na maanguko ya watu! Bila kufundisha matendo mema; kwanini kuhangaika navyo? Havina sense ya mafundisho kwa watu wa Mungu,
 
Wapi nimesema daudi alikuwa shoga unaweza ukaweka hapa hyo post??

Swali langu sio vitabu 66 au 72 nachouliza ni upi msimamo wako kwa Bible ambacho ni kitabu kitakatifu kuchukua reference kwenye vitabu ambavyo ni vya kipagani?? Hili ndio hoja yangu
 
Wakatoliki wana Biblia ya vitabu 72, Madhehebu ya Kiprotestanti wana Vitabu 66 (vingine kama Tobiti , Makabayo, Yoshua bin Sila na ambavyo Wakatoliki wanavitumia, Waprotestant hawavikubali kama havikidhi canonical rule yao). Hizo canonical rules naamini ni kanuni ya kukubaliana kwa maandiko ingawa kutoka Nabii mmoja hadi mwingine wamepishana kwa karne nyingi. Unaweza kutafuta zaidi mwenyewe.

Makanisa ambayo hayatumii au kukubali Biblia hiyo wanazo Biblia zao kama vile Mashahidi wa Yehova wanaotumia New Word Translation na madhebu mengine yanayohesabika kuwa cults eg Momorns, Unification church, Jehova Witnesses etc).

Biblia iliyopo imekamilika na inajitosheleza kwa mafundisho. Hata hivyo kuna baadhi ya Maandiko na Nyaraka zilipotea au hazijapatikana mfano Waraka wa Paulo kwa Walaodikia (Kolosai 4:16), Vitabu vya manabii kama Gadi nk.

Nashangaa kuwa unashangaa kuna vitabu vilipotea, ni kuwa hata hivyo vilivyokusanywa kwenye Biblia kuna kazi kubwa ilifanyika, manuscripts zilipatikana sehemu tofauti tofauti, kwa hiyo sio ajabu nyingine hazijapatikana na zilizopatikana zinathibitisha kuwa vipo vitabu vingine kama maandishi ya Nabii Gadi na Waraka kwa Walaodikia. Ikiwa vitapatikana na kufikia viwango vilivyopo kwenye canonical rules huenda vikaongezwa kwenye Biblia ingawa vilivyopatikana kama hivyo vinavyodaiwa kuwepo kama Injili ya Thomaso na Barnabas.

Vv
 
Ila mkuu dhambi ile ya daudi ambayo hata kwenye biblia iliandikwa tumeona pia adhabu aliyopewa Daudi na alikemewa juu ya hiyo dhambi ila hiyo dhambi nyingine sijaona Nabii gani alienda kumkemea na adhabu yake ilikua ipi?
Taja hizo dhambi ili tukufahamishe mahali pa kusoma.

Vv
 
. Ikiwa vitapatikana na kufikia viwango vilivyopo kwenye canonical rules

Vv
Ndio rules zipi hizo mkuu maana canonical rules zinafika mamia je ni za Tawahedo church... Za Eastern orthodox... Za Council of Nicaea,Trent au alexandria.... ?? Be specific unieleweshe mkuu.

Biblia iliyopo imekamilika na inajitosheleza kwa mafundisho.

Vv
Biblia ipi mkuu?? Ya vitabu 66 au 73 au 84 au 68?? Be specific na iliyojitosheleza ni ipi kiasi wengine waongeze vitabu na wengine wavipunguze.... Kama unashauri mtu kama mimi je nitumie ipi kati ya hizo??

Ubarikiwe
 
Wakatoliki wana Biblia ya vitabu 72, Madhehebu ya Kiprotestanti wana Vitabu 66 (vingine kama Tobiti , Makabayo, Yoshua bin Sila na ambavyo Wakatoliki wanavitumia, Waprotestant hawavikubali kama havikidhi canonical rule yao).
Vv
Canonical rule ya protestants ndio ipi hiyo?? Unaweza kutusaidia hapa?? Wakati Biblia inapitishwa kwa mara ya kwanza tokea AD 300+ kulikuwa na protestants?? Ila mbona kulikuwa na Biblia ya vitabu 66??

Embu tuwekane sawa hapo mkuu
 
Canonical rule ya protestants ndio ipi hiyo?? Unaweza kutusaidia hapa?? Wakati Biblia inapitishwa kwa mara ya kwanza tokea AD 300+ kulikuwa na protestants?? Ila mbona kulikuwa na Biblia ya vitabu 66??

Embu tuwekane sawa hapo mkuu
Kwa mtazamo wa kimadhehebu ukiondoa cults, Wakatoliki wameongeza vitabu zaidi kutoka 66 hadi 72 wakati Waprotestant wamegoma kuvitambua vitabu vilivyoongezeka kwenye Biblia kutoka 66 hadi 72. Kwa historia uliyeweka kama ni sahihi, basi kuna vitabu vingine vilipatikana baadaye na Wakatoliki wakaona viingie kwenye Biblia wakati Waprotestanti wakavikataa.

Bila kujali authority ya vitabu vilivyopo, ukweli kuwa kuna vitabu havijulikani kuwa viko au haviko/kupotea, ikiwa vitapatikana utakuwa ni uamuzi wa kanisa vijumuishwe kwenye Biblia au Biblia ibaki kama ilivyo sasa.

Vv
 

Kweli kabisa mkuu , hivyo vitabu wanavyodai vya kipagani ndvyo vimejaa maisha halisi kwa kirefu na upana zaidi kuhusu wahusika wote wa kwenye biblia.

Sikujua kama King Solomon alikua anatumia majini na Ndio waliokua wanampa utajiri , akili na nguvu za ajabu, kuna kitabu nilikisoma ( sipendi kukitaja jina ) kuhusu mfalme Suleiman , kimejaa mambo ya kishetani na ya kutisha , kinafundisha hadi mbinu ya kuyaita majini aliyokua akiyatumia suleman

Vile vile sikujua temple aliyoijenga Solomon Ndio msingi halisi wa Freemason .

Kuna siri nzito sana zimejaa kwenye maandishi, tujitahidi sana kusoma na vitabu vingine sio biblia pekee, ukitaka kuilewa biblia basi kasome vzur vitabu mnavyoviita vya kipagan

Warumi


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Vile vile sikujua temple aliyoijenga Solomon Ndio msingi halisi wa Freemason .


Sent from my iPhone using JamiiForums
Huu ni ukweli ambao wengi hawapendi kuusikia..... Ukisoma hata Muongozo wa ibada za Scottish rite freemasonry degree ya 6 inahusisha kutafuta missing pieces kwenye hekalu la suleiman. Kwahiyo kuna patterns unatakiwa uzitafute kwenye ramani ya lile hekalu ambapo inahusisha kusafiri kiroho/kiakili hadi wakati ule hekalu linajengwa.

Ni ibada nzito sana na kwenye katiba yao inaongelewa vizuri sana ila ukileta huo mjadala humu unaweza onekana ni ibilisi fulani hivi maana watu wamemsoma kwa upande mmoja tu.
 

Mwenye Sikio na asikie, na mwenye kuelewa aelewe....


Mambo mengine tunayoyasoma yanatisha sana , mpaka kuna mambo mengine ukiyasoma wanakwambia ule kiapo kabisa kabla hujaendelea kusoma kuwa chochote utakachokisoma kitabaki kuwa siri yako mwenyewe usimwambie mtu.

Ila ipo siku wataelewa tu unachokisema, hata mimi nilikua kama wao , nikisoma mambo kama haya najisemea maajent wa shetan at work [emoji16], ila kumbe nilikua nimejifunga kitanzi


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Nilipata bahati ya kuingia pale Masonic lodge ,enzi za Mzee sir Andy Chande, ndani mule kuna vitabu /biblia, kimoja ni kitabu cha Seleman

MTC | 101| [emoji769]
 
Pambania maisha na uzima wako ,kulia na pumzi za marehemu wa kale ni somehow Cracked Interest
 
Mkuu Zitto junior kwa kuwa nimeona unayo Imani juu ya maandiko au biblia basi naomba nikukumbushe kuwa Kusoma kwingi kuna geuza akili . Tunahitaji Maarifa yanayoweza kutupa Uzima wa milele hilo tu mengine yanabaki kuwa mbwembwe

Hivi kwa mfano ukijua King David alikuwa na mahusiano hayo uliyoyasema na Yonathan je utataka kuhalalisha Ushoga ?

"Zamani zile za ujinga Mungu alijifanya Kama hazioni ,bali Sasa anawaagiza watu wote kill mahali watubu " Mdo 17:30
Asante

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nashukuru kwa maoni yako, kiini cha mjadala haikuwa ushoga wa Daudi bali nahalalisha kwamba reference za kihistoria kwa characters wa Biblia hazipatikani tu ndani ya Biblia ila pia nje ya Biblia,

Hivyo inapaswa wasoma Biblia wote wasome na vitabu mbalimbali ili kuongeza maarifa ya masuala ya Biblia, mfano hatma ya Cain, utata wa Melchizedek, Mnara wa babeli n.k wameongelewa kwa undani katika kitabu cha Yashari lakini ukikifanya reference humu unaonekana mpagani ilihali Biblia hiyo imekinalili humo.

Yote kwa yote kuongeza maarifa na imani yetu sababu naweza kukuuliza swali mfano Biblia inaeleza kuanzia mwanzo 6 kuwa dunia ilichafuka kwa wanefili na hivyo gharika likaja. Lakini mara baada ya gharika ukifika mwanzo 14 utaona tena Wanefili/Warefai wamerudi. Sasa kama Nuhu pekee alipona hawa wanefili walirudije duniani ilihali kizazi chote duniani kilikufa???

Hili swali ukiweza kujibu kwa reference ya Biblia pekee basi nitaomba wana JF wote wapuuze huu uzi wangu.
 
Pambania maisha na uzima wako ,kulia na pumzi za marehemu wa kale ni somehow Cracked Interest
Hatuwezi kwenda mbele bila kujua tulipotoka..... Yaani huwezi amini tu kila kitu bila kuhoji. Naamini ukristo ni dini ya reasoning sio kufuata upepo tu. Kama wanaJF hatuoni faida ku-revisit history ili kuweka precedence kwenye imani yetu basi naweza kuelewa kwanni mitume na manabii wana wafuasi wengi vile wakiwauzia mafuta na sabuni za upako!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…