Biblia na reference ya vitabu vya kipagani

Biblia na reference ya vitabu vya kipagani

1. Mkuu naposema standard bible namaanisha hii set kama ya Genesisi to Revelation but nachojua vilikuwepo vitabu mbalimbali mfano Torah na vitabu vya manabii wengine wa kiyahudi kwa mamia yake (sio 39 pekee) na wote tunajua kuna baadhi ya vitabu kama ufunuo wa yohana imeandikwa miaka mingi baada ya Yesu kufa hivyo unaposema standard bible ilikuwepo wakati wa Yesu hatuwezi kuwa realistic.

Kuhusu vitabu hivyo vilivyoachwa kuwa vitakatifu ni evident sababu tunaona Yuda na Petro wakifanya direct quotation ya maandiko ya Kitabu cha Henoko.... Hivyo kma sio matakatifu sidhani kama wangeweza kuyaquote na kujengea hoja kama ambavyo waliquote vitabu vya isaya,zaburi n.k

2. Kuhusu compilation
Kwa uelewa wangu kufikia AD 300 kulikuwa na vitabu na nyaraka mamia yanasambaa yakidai ni maneno ya mitume sasa ili kuzima hiyo sintofahamu ikabidi wafanya new testament canonization ili wapate standard bible ya kutumika ulimwengu kote.... Mfano Council of Rome kufikia AD 382 ndipo walipotoa complete list ya vitabu vya Biblia ambavyo ndio halali kabisa na kwa mara ya kwanza kanisa likatambua vitabu 27 ingawa kabla ya hapo vitabu vilikuwa vingi vinazagaa so baada ya mchakato wa kuvikagua ndio wakafikia conclusion kuwa Biblia halali ni hii kwa mara ya kwanzo ilikuwa 382 ikimaanisha kabla ya hapo hakukuwa na standard Biblia hivyo mnaposema kuwa vitabu vilivyoachwa vinakinzana na maneno ya mitume sidhani ni sahihi unless ungesema watu waliocompile Biblia waliamua kugawa vile vinavyokubaliana kutoka kwa vinavyopingana (Collect like terms) ila mnaposema vinakinzana na manabii it's as if Biblia (yaani vitabu 66/72 n.k) ilikuwepo ndipo vikaandikwa hivyo vingine kma cha Enock au Jasher ili viipinge Biblia hicho ndio nachoona sio sahihi.

3. Pia unasema vilivyopo ndio vinakidhi vigezo.... Sasa hivyo ambavyo unasema havikidhi vigezo ni kwanini Biblia inaviquote na kuvirefer tukasome??

Kama vinatosha sasa kivipi kanisa ulimwenguni liliruhusu kuwa na Biblia tofauti mfano catholic wawe na 72, protestant 66 hapo bado martin Luther naye alipunguza baadhi ya vitabu ambavyo protestants wengine wanavitumia (refer luther bible) hapo bado kuna orthodox la tokea enzi na enzi la huko Ethiopia lina vitabu 84!!! Sasa kwa staili hii who is right and who is wrong?? Na kama one is wrong kuongeza au kupunguza vitabu je ni kwanini Mungu ameliruhusu hilo kuwa kanisa lipotoshwe na watu wachache??

Embu tuwekane sawa mkuu maana kupitia maswali haya tunajifunza mengi, ubarikiwe

1: stanard bible ya wqkati wake mkuu sio agano la kale na jibya. Naamini kabisa katika maandishi yote ya wakati wa Yesu yalikuwa hayapewi hadhi sawa. Yalikuwepo maandishi na '' Maandiko matakatifu''. Hata Yesu alitenganisha kati ya "maandiko matakatifu'' na ''Desturi za wazee''.
Ikiwa yalikuwepo, na huko nyuma nimesema kulikuwa na utaratibu wa kuyahifadhi. Naomba ushahidi kuwa hadi kitabu cha enoch kilikuwa sehemu ya hebrew holy inspired writings maana hata Apokrifa havikuwa sehemu ya Bibilia. Hata Jerome alipocompile vulgate alivitenganisha na vingine kuonyesha kuwa havina hadhi sawa.
Na ninachokisisitiza msingi wa utambuzi wa maandiko matakatifu ni resonance ya waandishi hao wasiopingana na hakuna anayefundisha kitu kipya.
Katika reference zote za Yesu na manabii anarefer wa vitabu vinavyofahamika na havipingani na mafundisho ya bibilia.

2:Nadhani kuna sababu nyingi zilizopekelea hivyo vitabu visiwe sehemu ya maandiko nanvingine viwe sehemu ya maandiko.
ambazo zinamashiko na hata mimi nakubaliana nazo ukijumuisha na za martino luther. najifunza zaidi hapo. Ila unapoleta hoja za 300AD unapaswa kuchanganya na hoja za Karne ya pili BC ambapo wasomi wa kiyahudi zaidi ya 70 walipokutanika alexandria nadhani kuandika agano la kale kuyoka kiebrania kwenda kigiriki na hivyo vitabu unavyovitetea mfano Enoch na Jubilee. kumbe utagundua pamoja na mavitabu mengi kuwepo enzi hizo za kale lakini sio yote yalipewa hadi za kuwa maandiko matakatifu. Kitu kingine historia ya wakristo ktk karne ya awali pia kuliibuka watu wengi kama alivyoahidi Paulo pale troa kuwa wataibuka mbwa mwitu wasiwahurumie, waliibuka watu wengi walifundisha mambo mengi yasiyofaa. na pia sidhani kama kila balua ilikuwa intended kuwa sehemu ya maandiko, hata wewe leo ukipata mafunuo kutoka kwa Mungu tutayapokea kwa kuyapima kama yanaumana na wenzakomwa kale waliovuviwa na kuyakubali ila haiayawi bibilia au sehemu ya bibilia bali maagizo tu ya Mungu kwetu yanayotufanya tumuamini zaidi yeye na mitume wake.
Nitajifunza zaidi na Inshallah mwenyezi Mungu akinipa neema nitapita kutia neno la ziada kwenye hoja mbalimbali.

3:kanisa unamaanisha nini mkuu? kuhusu Luther alikataa baadhi lkn baadae alivielewa akavijumuisha. Kuhusu apokrifa kwa katolīki licha ya kukataa vitabu vingine vingi, ni tamko la kidini la mtaguso wa Trent ndio lililohalalisha hizo apokrifa. Tena kutoa kemeo la kitisho '' anaethma'' kwavatayevipinga, wanaweza kukaa mitaguso mingine hata mtaguso wa '' hong kong'' wakavitoa japo wanasema yale makubaliano ya trent ni ''ex cathedra'' hayapingiki. hata jerome alipoandika vulgate ile kwa mujibu ya wananzuoni(kama nakosea utanirekebisha) alivitenga pembeni maana hata scholars wa kiyahudi hawakuvihesabu kama ni miongoni mwa vitabu vilivyovuviwa ila vinaelezea matukio halisi kihistoria. Hata KJV ilipoandikwa viliwekwa vikatengwa pembeni pia (apokrifa) wenda kwa manufaa hayohayo.
Wengine hasa catholic wanavikubali maana ndiko waliopatia mafundisho yao (Dogma) mengine ni kama nguzo ya kanisa, mfano ibada za wafu na wamakabayo. Hakuna tendo la ibada ya wafu nje ya wamakabayo kwenye vitabu vingine. Waandishi karibu wote wamekubaliana kuwa mtu akifa analala, na ibada za wafu zinaonekana kwa wapagani zaidi. Na sio salama kujenga fundisho kwenye kafungunkaboja ambako jakaungwi mkono na vyanzo vingine.
Binafsi na nawapendekezea wote wasome bibilia 66Books, inakila utetezi na Lengo la Mungu kutupa maneno yake liko uchi kabisa kama sio wazi kabisa.
Huko kwingine kusomwe kama kujiburudisha na kujua mambo ya pembeni ili kutanua ubongo na uelewa wa mambo ya nje ya bibilia ili uiamini zaidi na sio ili uwe muasi, mtukana Mungu, mtu aliyechanganyikiwa na kuishi bila matumaini ya Uzima wa milele kupitia Yesu.


KwA UFUPI
1: Hao wakkristo waliokitana miaka ya 300 AD sio watu wa kwanza kucompile maaandiko. Bali watu wa kwanza tukianza na agano la kale ni Ezra na Nehemia chini ya Uonhozi wa Mungu. Lkn pia Kwa Mujibu wa Muratori flagments za 1740 zilikutwa na almost vitabu vyote vya agano la jipya ambayo aliyevicompile ni mtu anayeitwa Pius askofu wa kanisa la kikristo huko rumi mwaka 150AD miongo karibu 15 kabla ya hao wa 300AD. Peshito Syriac nauo ikataja vitabu vingi tu vya agano jipya tunavyotumia sasa ikiwemo hadi ufunuo wa Yohana miaka mingi kabla ya hao wa 300AD , vimetajwa pia hadi na wakina polycap askofu wa efeso na anasaidikiwa alikuwa mwanafunzi wa yohana pia. ninachpfahamu limitation ya technology nayo ilichangia upatikanaji wa wakati mmoja wa maandishi ya watu zaidi ya 30 walioandika katika range ya miaka 1500, hivyo hata makusanyo lazima iwe process kureflect uhalisia. Na hii ni moja ya sababu ya mimi Kuamini bibilia. Haikushushwa ni maneno ya Mungu yaliyoandikwa na binadamu halisi kwa mazingira na ugumu wao halisi kwa lugha yetu rahisi binadamu kuelewa.


2:Bibilia ni ukuaji, sio dude lililodondoka kutoka mbinguni. Hata Baada ya Kutoka babeli Bibilia au maandiko ya wakati huo yalyokusanywa na Nehemia na Ezra hayakuwa bibilia tulionayo sasa, Vitabu vingine havikuwepo. Hata mwanahistoria Josephus anayaita hayo maandiko matakatifu ya enzi zake '' Against Apion'' na Yesu kayathibitisha pote katika kauli zake. Hakuwahi kuzunhumiza au kuquote cha Apokrifa wala pseudo.... wa'la enoch maana havikuwa sehemu ya maandiko matakatifu ya wayahudi ambayo Yesu alijifunza utotoni na ujanani.

3:Kingine kuhusu enoch na vingine kuwa quoted, nimejifunza uhalali na usahihi wa nani kamkopi nani ni debate kubwa.
Hata mtetezi mkuu wa hivyo vitabu humu jukwaani anaitwa Eiyar ukimbana anakwambia vimefichwa, mara viko sijui etjiopia, mara siwezi kukwambia kama ninacho au la, yaani vimekaa kinjamanjama ambapo vinaonyesha sio vya kuaminika. Hata wewe huwa unaibuka unasema kuna maneno ya Mungu yamefichwa sijui vatican na kuna wengine hudai yamefungiwa Medicci Library huko Florence Binafsi mkuu huwa siamini sana hizo sarakasi na usiti wa maandiko matakatifu. Haya Yaliyopo Yamekamilika,



mkuu nimetoa maoni ya jumlajumla unaweza ukaokota vipande vya dhahamu humo sina shaka.
 
Habari za jioni wana JF natumaini wote humu ni wazima.
View attachment 885770
Nlipokuwa naipitia uzi huu Mjue Yoabu - Jenerali Mkuu wa Mfalme Daudi, Katili na asiyeogopa chochote! - JamiiForums

Mkuu Elungata aliibua hoja kuhusu Daudi kuwa na mahusiano ya jinsia moja na nathan ila muanzisha uzi alipotaka ushahidi aliuwekea condition hii.




Baada ya kusoma hii comment nilisikitika sana na nilijiuliza sana kwamba inakuaje kila story ya watu waliotajwa kwenye bible watu wanataka reference kutoka ndani ya Biblia pekee as if Biblia imeandika kila kitu?? Kwanini tunapenda kujifunga akili kiasi hicho?


Baada ya kuona mentality hiyo imeanza kukua humu JF intelligence nikaona nilete mada jinsi Biblia yenyewe imetutuma tukasome vitabu vingine nje ya Biblia ili tuongeze ufahamu kuhusu baadhi ya watu na matukio ambayo Bibila yenyewe haikuandika yote kwa upana wake, hivyo nia ya uzi huu ni kwa wale waliojifunga kwenye kusoma maandiko pekee wabadilike na kuwa na fikra huru na kuruhusu maarifa kutoka kona zote kwa mithiri ya kujifunza zaidi na kupanua uelewa wa mambo.
View attachment 885772
Kwa kuanzia tu labda nitumie nafasi hii kumjibu mkuu wangu maishapopote kuwa hata biblia yenyewe inakiri kuwa maisha yote ya Daudi yameelezewa vizuri zaidi nje ya Biblia hivyo imetutuma tukasome vitabu hivyo mnavyoita vya kipagani ili tujifunze kwa ufanisi zaidi

1 NYAKATI 29:29
29 Basi habari za mfalme Daudi, mwanzo na mwisho, angalia, zimeandikwa katika tarehe ya Samweli, mwonaji, na katika tarehe ya Nathani, nabii, na katika tarehe ya Gadi, mwonaji.

Vitabu vilivyotajwa hapa ni Book of Gad the seer,Book of Nathan the prophet, Book of Samuel the seer (Sio samuel 1&2) ambavyo kwenye biblia havikuwekwa . Sasa kama Biblia inakiri kuwa sio kila story yake imeongelewa kwa upana wake katika biblia je kwanini siku hizi watu wakijengea hoja kuhusu personality za biblia mnalazimisha reference iwe ndani ya bible pekee??? Ina maana waandishi wa Biblia ni wajinga hadi watutume tukasome hivyo vitabu vingine ambavyo mnaviita vya kipagani??

MAANDIKO
Hapa chini nimeambatanisha vifungu vya Biblia hivyo ningeomba tuisome kwa makini kabla ya kuchangia hoja. Neno Tarehe kwenye maandiko haya kwa kiswahili rahisi inamaanisha Nyaraka/rekodi/kitabu au kwa kizungu book/journal/Annal.
View attachment 885773

1. Kitabu cha Yehu

2 Nyakati 20:34
34 Na mambo yote ya Yehoshafati yaliyosalia, ya kwanza na ya mwisho, angalia, yameandikwa katika tarehe ya Yehu mwana wa Hanani, iliyotiwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli.

2. Kitabu cha Nabii Gadi muonaji/ Kitabu cha shemaya

2 Nyakati 13:22
22 Na mambo ya Abiya yaliyosalia, na njia zake, na maneno yake, yameandikwa katika kitabu cha maelezo cha nabii Ido.

2 Nyakati 12:15
15 Basi mambo yake Rehoboamu, ya kwanza na ya mwisho, je! Hayakuandikwa katika tarehe za Shemaya nabii na Ido mwonaji, kwa jinsi ya kuandika nasaba? Kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu siku zote.

1 Nyakati 29:29
29 Basi habari za mfalme Daudi, mwanzo na mwisho, angalia, zimeandikwa katika tarehe ya Samweli, mwonaji, na katika tarehe ya Nathani, nabii, na katika tarehe ya Gadi, mwonaji.

3. Kitabu cha mfalme Ahasuero

Nehemiah 12:23
23 Wana wa Lawi, wakuu wa mbari za mababa, wameandikwa katika kitabu cha tarehe, hata siku za Yohana mwana wa Eliashibu

Pia kinatajwa Esther 10:2, 2:23, 6:1

4. Matendo ya Mfalme suleiman

1 wafalme 11:41
41 Nayo yaliyosalia ya Sulemani, mambo yake na yote aliyoyafanya, na hekima yake, je! Hayo siyo yaliyoandikwa kitabuni mwa mambo yake Sulemani (Book of Acts of Solomon)

5. Nyakati za wafalme wa Israel & Yuda

1 wafalme 14:19
19 Na mambo yake Yeroboamu yaliyosalia, ya kupigana na ya kutawala, tazama, yameandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli.(chronichles of the kings of israel/Judah)

6. Kitabu cha Hozai

2 Nyakati 33:19
19 Sala yake pia, na jinsi Mungu alivyomtakabali, na dhambi yake yote, na kosa lake, na mahali alipopajenga mahali pa juu, na kupasimamishia maashera na sanamu za kuchonga, kabla ya kujinyenyekeza; tazama, hayo yameandikwa katika tarehe ya Hozai.

Hivi ni kwa uchache tu ila kuna vitabu vingine zaidi ya 20 vinatajwa kama reference point kwenye biblia ilihali havipo kwenye Biblia na wala havitambuliki na kanisa lakini leo hii akijengea mtu hoja anaonekana shetani!!
View attachment 885774

HITIMISHO
Baada ya uzi huu nisingetegemea tena kusikia wana JF wakitaka reference kutoka kwenye biblia pekee ilihali Biblia yenyewe inataka tukarefer kwenye vitabu vingine ambavyo vingi ni vya kipagani tu ili tupate uelewa zaidi ya watu muhimu kwenye bible.

However ningependa tujiulize maswali haya ili kupanua fikra zaidi

1. Kwanini vitabu hivi ambavyo Biblia inaturefer tukasome ili kuelewa baadhi ya matukio havikuwekwa kwenye biblia??

2. Na kama havikuwekwa kwa sababu yeyote ile je ina maana ni vya kipagani??

3. Na kama ni vya kipagani ni kwanini vimekuwa referred kwenye bible?

4. Kuna vitabu vingine ambavyo vimenakiliwa hapa ni halali kabisa katika kanisa la kale lakini kwa sasa viko categorized kama vitabu vilivyopotea.... Je nini hatma ya Biblia kama maneno ya Mungu ilihali yanaweza kupotea??

5. Na kama yamepotea je ina maana biblia haijakamilika sababu sehemu ya stori yake imepotea??

Naomba kuwasilisha

Cc: Wana JF intelligence wote bila kuwasahau kina Mchawi Mkuu Malcom Lumumba Elungata Da'Vinci Mshana Jr Eiyer Kudo900 Vi rendra N J subi Bujibuji Kipanga boy Kiranga Che mittoga Ip man 3 mitale na midimu Mzee wa Torano Blaki Womani Grahnman za chembe jimmykb197 911sep11 afsa Francis3 mtu chake NJOLO Msolo Shubiri Pori Pendael24 Mr Miller Elli Khalifavinnie Kennedy Son of Gamba Kanungila Karim Mgambilwa ni mntu Mr FCB Mr Q geesten66 Jerry Ekky Mnabuduhe Chrisvern Dabby Jr kibuyu180 IGWE SALA NA KAZI
Wick Dukeson lifecoded Daimler monde arabe mtu watu

chief imani ni hali fulani yenye nguvu, nzuri na inasaidia sana ila pia ni mbaya sana kama mtu ataibeba bila kushirikisha ufahamu na utashi wake.
 
Mkuu zito anatoa reference zinazoeleweka kwanini nyie mshindwe kuweka reference ya kuhusu kupasuka kwa mwezi au na nyie hamjui au hamna uhakika wa mahadithi mnayosimuliwa??!
Reference zitolewe mara ngapi ?
 
Hujanielewa labda kama unasoma kwa wasiwasi. Nitakuwa mwehu kusema Yesu alisoma Injili wakati hakukuwa na injili wakati wake. Hadi alipoondoka maisha yake na mambo aliyoagiza yakaandikwa. Nazungumzia Vitabu vya Musa, wafalme na wanabii.

Kuhusu hao vijana kuandika huku walikuwa "Sio Wasomi/ Learned" inaonyesha pia kuna haja ya kufahama Jewish education system. Inabidi uelewe Mungu alimaanisha nini alipowaambia wazazi wa kiyahudi maneno ya Torati 6:6-9

Yesu alijifunza kusoma na Kuandika Nyumbani kwa mama na baba yake. Ila uelewa wake ulikuwa mkubwa sana kwa wasomi wa kiyahudi pale hekaluni alipokuwa na miaka 12 alipojichanganya kwenye darasa la marabi katika shule iliyokuwepo pale hekaluni na uwezo wake na maswali yake yaliwashangaza maana yalikuwa ya kiwangu cha juu kuliko uelewa wa waalimu hao.

Timotheo alijifunza miguuni kwa Bibi yake Loisi na mama yake Yunisi. Aliishi mji wa kipagani Listra ambao haukiwa hata na sinagogi. Ndio ujue wamama wa kiyahudi sio wamchezo.

Kwa ufupi kusoma na kuandika watoto wa kiyahudi walijifunzia nyumbani hasa wale masikini kama wakina Yesu. Huyu bado alikiwa anatambuliwa kama mtu mjinga tu maana walikuwepo kwenye shule za marrabi, na mafarisayo chini wa waalimu nguli kama gamalieli. Wazazi wake paulo walimpeleka jeruslaem kutoka huko tarso akabobee kwa huyu mwalimu.
Pia kutokujua kusoma na kuandika sio mipaka kwa Mungu, Yeremia nabii hakuwahi kuandika kitu, ila Yote aliandikiwa na msaidizi wake Baraki.

Kuhusu Quran rudi ujifunze, ujue na watu 700 waliokuwa wamekariri maneno ya mtume na walifia vitani, hofu hiyo ikapelekea kaandikwe kwenye kitabu maana wale waliokariri wakifa na chenyewe kitakufa. Kumbuka pia ali na uthman walikiwa sio kitu kimoja kama unavyofikiri. Na kuna scholars wanasema hata hiyo aliyoandika haikukubalika na kila mtu sema ilibidi ikubalike kwa sababu ya nguvu ya dola. Rudi usome fitna za wakati huo kutoka kwenye vyanzo vya kuaminika vya kiimani wenda ukajifunza upya. Ila kwa sababu sio mada naishia hapa, tujifunze zaidi. Maana mimi nilifuatilia history ya Islam series Karibu 22 na hiyo source ilikuwa ya hukohuko. Na sioni kama walichokuwa wanasimulia kinapingwa sana ukiacha moja juu ya imani kuw kitabu kile kiko perfect na ni direct maneno ya Allah japo hatufafanuliwi kwa kina hapo kwa uthman na uhakika wa nini kilichukuliwa na nini kiliachwa.
Kama hawakubaliana Lazima had leo ingekuwepo nakala ya maandiko amnayo ingesema hichi kiliachwa au hichi kimeonvezwa haikikuwepo aababu watu waliokuwa a wamehifadh Quran ni wengi kama ambavyo ipo kwenye bible na kibaya ndugu yangu unasima sana history za mashia lakin hata wao hawana Quran mbadala...nikuuukize wwwe unaamini kwenye bibe ya bitabu 72,66 au 82 na nani yupi sahihi kati ya hao na kwanini vingine viwepo kwa wengine visiwepo.!
 
Mkuu mitale na midimu nimeona ntapandisha uzi kuhusu Canonicity ya Biblia na ntaeleza shida ilipoanzia maana naona imekuwa topic kubwa kidogo..... Labda kwa ufupi tu nkijibu hoja zako
1. Greek Septuagint iliinclude apocrypha/Deuterocanonical books na ndio iliyotumika kipindi cha Yesu na HAVIKUTENGANISHWA kabisa.... sema baada ya masoretic texts kuja ndio wakavitenga.... Na hapo unaposema manabii hawakunakiri nimeshasema mara 100 humu kuwa new testament imequote baadhi ya Apocrypha mfano hicho kitabu cha Enock na kama sio naomba unisaidie mistari hii imequotiwa kutoka kitabu gani cha agano la kale na kama hajatoa huko kivipi ufanane na kitabu cha Enock

Yuda
14 Na Henoko, mtu wa saba baada ya Adamu, alitoa maneno ya unabii juu ya hao, akisema, Angalia, Bwana alikuja na watakatifu wake, maelfu maelfu,
15 ili afanye hukumu juu ya watu wote, na kuwaadhibisha wote wasiomcha Mungu....

Yuda
6 Na malaika wasioilinda enzi yao wenyewe, lakini wakayaacha makao yao yaliyowahusu, amewaweka katika vifungo vya milele chini ya giza kwa hukumu ya siku ile kuu.

Naomba kwa vyanzo vyako ukahoji kokote hizo reference za Yuda wanatheolojia wanakiri aliquote kwa Book of Enoch hasa sura ya 6.

2. Mkuu hapo nmeshaeleza Greek Septuagint ilikuwa na apocrypha zote bila kutenganishwa na ndio maana wakatoliki wameiadopt ikapelekea kuwa na vitabu 7 zaidi (nafkiri ntaliongelea zaidi kwenye huo uzi wa canonicity ya Biblia) ila nilichosema mimi kufikia AD 382 ndipo standard Bible hasa vitabu vya agano jipya ndipo vilikubalika labda wwe unaweza nipa source ya uwepo wa canon ya OT na NT katika mjumuisho wake kabla ya 380 AD.

3. Naposema kanisa namaanisha East orthodox church inayokubali baadhi ya apocrypha hivyo ina vitabu kama 68, Tawahedo Orthodox la Ethiopia lina vitabu 81, Protestants kama pentecost,lutherans,SDA wana vitabu 66, Roman Catholic vitabu 73!!! Ndio hapo nauliza huoni kuna shida?? Kwanini Mungu aruhusu kila kanisa kuwa na Biblia yake?? Je waliongozwa kweli na roho wakati wa kucompile (hili pia ntaliongelea zaidi kwenye ule uzi)

Kuhusu maswala ya nyongeza

1.Mkuu kuhusu NT Canon kabla ya council of Rome hyo AD 382 kulikuwa na wengi waliocompile lakini hawakufikia conclusion kuhusu canonicity ya baadhi vitabu mfano ufunuo,2 peter hivyo wengine waliviacha wengine waliviinclude lakini hao council of Rome ndio wakafanya cross reference na kufikia hitimisho RASMI kuwa NT iwe na Vitabu 27 ambavyo ni hivi tulivyonavyo.

2.Pia hakuna mahala niliposema Enoch ni kitabu kitakatifu ila nachosema manabii wa enzi hizo walivisoma pia na ndio maaana kuna makanisa kama ya Orthodox kama hilo la Ethiopia limekitumia mpaka leo tokea enzi za Yesu na walikuwa wanakisoma kanisani tokea AD 300... Na ndio maana nikaleta huu uzi kuhoji kwamba licha ya (Enoch,jasher,Acts of solomon) kutokuwa vya kitakatifu lakini mbona mitume wamevinakiri?? Na ndio maana hapo juu nimeuliza tu naomba unisaidie Yuda alitoa wapi reference kuhusu maneno ya Henoko kwenye mstari wa 4,6,13 n.k??

3. Hakuna debate yeyote mbona wanatheolojia wameshaconclude tu... Unajua shida ya sisi tunakuwa biased mfano Yohan akicopy maneno ya Isaya au stefano akicopy maneno ya Yakobo watu wanasema amecopy OT ila mtu akinakiri book of jasher au Enoch au acts of solomon utaulizwa "una uhakika gani kama hicho kitabu alichonakiri ndio kile original"!!! Sasa kwanini kwa mathayo hamkuhoji kama ni kitabu cha "mwanzo" halisi ila kwa Yuda na Joshua mtahoji hivyo?? Hii bias ndio inaleta debate lakimi tukiamua kuwa objective tutagundua kuwa ukweli ni mmoja TU

Kuhusu mkuu Eiyer naweza muunga mkono sababu mfano hicho kitabu cha Gad the seer kimekuwa termed as LOST BOOK!! hata kitabu kinachodaiwa kuandikwa na Mfalme Ogu nacho kimekuwa termed as LOST BOOK ingawa kuna script moja ya wanatheolojia wanadai sio kma vimepotea bali vimefichwa!! Otherwise labda nikuulize wwe vitabu vya watakatifu kama Nabii Gadi au Nabii Samuel inakuaje vipotee?? Ina maana maneno ya Mungu yanaweza potea tu kama toilet paper??

Ubarikiwe mkuu
 
Nulikuwa nimekaa pemben kwenye mjadala baada ya mtuoa uzi alipo onya juu kuwa mabishano juu ya Quran na biblie haikuwa lengo lake lakin sasa nao jamaa wamehamia kwenye kumshambulia muhammad kama ambavyo imekuwa kwa miaka yote haswa kwa waafrica sababu ndugu zetu waafrica kufanya utafiti ni jambo baba mke sisi ni wazee wa kuamin kichwa kichwa na dini za kurithi sasa sijiui kama mjadala huo unaruhusiwa humu tuanze kushusa nondo maana wao wanamsambulia muhamad na sio mafundisho yake wala dini yake sababu wanadhan sisimsingi wetu wa iman ni Muhammad kama ilivyo kwao kwa Yesu....sisi Muhhamad ni mtume tu ana daraja yake ila hutuamuabudu na yote akiyofundisha ni maagizo ya Mungu hana maagizo yake binafsi..so kumshanbulia yeye haijawahi kuwa msaada sana ku justfy iman yenu kaanza kushambuliwa since yupo wapo waliomuita mchawi,wakamuita msoma mshairi so nyue hamna jipya,

Muhhamad alioa aisha akiwa na miaka 9 kwa ridhaa ya baba ake abubalary ila amehamia kwenye nyumba ya muhammad akiwa na miaka 16 ...sheria ya kiialam ya kuoa ni kuwa mwanaume au amepevuka na mwanamke awe amepevuka haijalish umri gani ilimrad muwe baleghe...lakin wapotishaji wanasema alioa mtoto wa 6 kitu ambacho sio kweli..!
● "Narrated Hisham's father: Khadija died three years before the Prophet departed to Medina. He stayed there for two years or so, and then he married `Aisha when she was a girl of six years of age, and he consumed that marriage when she was nine years old." (Sahih Bukhari 3896)

● "Narrated `Aisha: That the Prophet (Muhammad) married her when she was six years old, and he consummated his marriage when she was nine years old, and then she remained with him for nine years (i.e., till his death). (Sahih Bukhari 5133)

● "Narrated 'Urwa: The Prophet (Muhammad) wrote the (marriage contract) with `Aisha while she was six years old, and consummated his marriage with her while she was nine years old, and she remained with him for nine years (i.e. till his death)." (Sahih Bukhari 5158)

● "Narrated `Aisha: The Prophet (Muhammad) used to lean on my lap and recite Qur'an while I was in menses." (Sahih Bukhari 297)

● "Narrated Um Salama: While I (Aisha) was laying with the Prophet (Muhammad) under a single woolen sheet, I got the menses. I slipped away and put on the clothes for menses. He said: "Have you got "Nifas" (menses)?" I replied: "Yes." He then called me and made me lie with him under the same sheet." (Sahih Bukhari 298)

● "Narrated `Aisha: The Prophet (Muhammad) and I used to take a bath from a single pot while we were Junub. During the menses, he used to order me to put on an Izar (dress worn below the waist) and used to fondle me. While in I`tikaf, he used to bring his head near me and I would wash it while I used to be in my periods (menses)." (Sahih Bukhari 299, 300, 301)

● "Narrated `Abdur-Rahman bin Al-Aswad: (on the authority of his father) `Aisha said: "Whenever Allah's Messenger (Muhammad) wanted to fondle anyone of us during her periods (menses), he used to order her to put on an Izar and start fondling her." `Aisha added, "None of you could control his sexual desires as the Prophet (Muhammad) could." (Sahih Bukhari 302)

● "I (Aisha) said (to the Prophet): "I feel that your Lord hastens in fulfilling your wishes and desires." (Sahih Bukhari Volume 6, Book 60, Number 311)

● "Narrated 'Aisha: I used to wash the traces of Janaba (semen) from the clothes of the Prophet (Muhammad) and he used to go for prayers while traces of water were still on it (water spots were still visible)." (Sahih Bukhari Volume 1, Book 4, Number 229)

● "Narrated 'Aisha: I used to wash the semen off the clothes of the Prophet (Muhammad) and even then I used to notice one or more spots on them." (Sahih Bukhari Volume 1, Book 4, Number 233)
 
Ngoja nikuoe historia yangu ndogo mi nimezaliwa kwenye familia ya kikiristo lutheran na baadae nikawa Athiest baada ya maswali yangu mengi kushindwa kujibiwa had na viongozi wangu wa kiiman au kupata amjibu yadiridhisha na kwa nikakaa kwa kipindi kirefu bila kuamin kwenye dini yoyote wakati huo nikawa naendele kufanya utafiti wangu, na jad kufikia kurudi kwemye mrengo kidini imenichukua miaka 6 na ndivyo Mungu anavyotaka Umtefute wengi wenu humu ni waislam sababu umezaliwa kwemye iman ya kiislam au mkikristo sababh umezaliwa kwemye iman ya kiksristo namshukuru Baba angu alisema sitalazimisha mtoto juu masula ya imani akipata akili atachahua mwenyewe hiyo ilinipa nafasi tofauti na wezangu nyie mkuja kupata akili tayari ni brain washed hamkupata firsa ya kuchagua iman sahihi na mafunzo juu ya iamn zingine mnachofundishwa ni kwanini iman ile.sio nzuri mi nina weza kukuchambulia mazuri ya iman zote na mapingufu yake ninachokieleza kuhusu Quran na uislam nakijua nakijua lengo la watu wengi wanafanya biashara kubwa dunian ukiandika vitabu kuhusu uislam na ukijienga hoja against it unapata biashara kubwa sababu unapata sababu unapata support kubwa kutoka ulaya na america na wanakuwa famous.!,,

Zaburi,injili,na torah ni vitabu vya na mamneno yawenyeziMungu kama ilivyo Quran vitabu hivyo kusema vipo kwenye Quran unakuwa hauko sawa inaweza kuwepo maaagizo waliuopowa watu wa kipindi revalation hizo na Quran imeyarudia sababu vitabu vyote vimekuja na ujumbe mmoja wa Kuabudiwa Mungu mmoja na wanadamu kujisalimisha na kumtegemea mwenziMungu pekee hiyo ndio dini alikija kufundisha kuanzia Noah ambaye ndio mtu wa kwanza kutumwa kwa watu had muhammad wote walikuja na message moja kitendo hicho kwa lugha ya kiaarabu kinaitwa ISLAM..!
Kule nyuma umesema uislam unaenea kwa kasi sana ulaya na marekan.Na makundi kwa makundi ya wazungu wanaingia katika uislam.hiyo inamaanisha kuwa uislam umeanza kukubalika kwa kasi sana huko ulaya na marekani.
Sasa hapa unasema;UKIANDIKA KTABU CHOCHOTE KILCHO AGAINST NA UISLAM, UTAPATA SAPOT KUBWA KTOKA ULAYA NA MALEKAN.
SWALI: huko uraya na marekani wanaishi jamii gani?.
Iweje wazungu waupokee uislam kwa kasi..
Alafu hao hao wanao upokea uislam kwa kasi..akitoke mtu kama gwajima akaandika kitabu kinachoupinga uislam wanamsapot.

Maelezo yako yanakanganya sana na hii n kwasababu mnaamin na kuabudu vitu visivyo kuwepo.
 
Tukutane uwanja wa hukumu...kila mtu ujumbe umemfikia ni akili yako...

Allaha amesema " tutawaonesha ishara zetu had watakaposema hii ni kweli na hatutamuhumu yoyote ila tu yule tuliyemfikishia ujumbe..!"

Am out on this
 
Nimekuelewa mkuu sasa basi kwa maoni yako vitabu hivyo wote tunafahamu kuwa vinaitwa Pseudepigraphi yaani havitambuliki na kanisa je ni kwanini Biblia inavitolea reference??? Na kama Biblia inavitolea reference je ni kwanini bado havitambuliki na kanisa mpaka leo?? Na je tukijengea hoja kupitia hivyo vitabu tunakuwa sahihi??

Nina shauku sana ya kuelewa hii sintofahamu, ubarikiwe
Nilipokuwa nikisoma canonicity nilifundishwa vigezo vilivyotumika kuweka vitabu kwenye Biblia na moja ya vigezo ni kunukuliwa na Bwana Yesu. Kwa mfano Yesu katika huduma yake alinukuu vitabu vingi vya agano la kale lakini hakuna ushahidi wa kutosha kuwa Bwana Yesu alinukuu yale mavitabu ya apokrifa.
Sisi wakristo kiongozi wetu ni Bwana Yesu na zaidi katupa roho mtakatifu anayeshuhudia ndani yetu. Only common people with common mind cannot comprehend
 
Nilipokuwa nikisoma canonicity nilifundishwa vigezo vilivyotumika kuweka vitabu kwenye Biblia na moja ya vigezo ni kunukuliwa na Bwana Yesu. Kwa mfano Yesu katika huduma yake alinukuu vitabu vingi vya agano la kale lakini hakuna ushahidi wa kutosha kuwa Bwana Yesu alinukuu yale mavitabu ya apokrifa.
Sisi wakristo kiongozi wetu ni Bwana Yesu na zaidi katupa roho mtakatifu anayeshuhudia ndani yetu. Only common people with common mind cannot comprehend
Sasa mbona Joshua na Yuda wamenukuu Apokrifa ila bado vitabu vyao vipo kwenye Biblia?? Unaweza kutusaidia kwanini?? Pia utueleze kivp Mwandishi wa samuel na wafalme alinukuu vitabu vya apokrifa pia lakini mbona vipo kwenye Biblia bado??

Tuanzie hapo kwanza
 
Sasa mbona Joshua na Yuda wamenukuu Apokrifa ila bado vitabu vyao vipo kwenye Biblia?? Unaweza kutusaidia kwanini?? Pia utueleze kivp Mwandishi wa samuel na wafalme alinukuu vitabu vya apokrifa pia lakini mbona vipo kwenye Biblia bado??

Tuanzie hapo kwanza
Kama Yesu akivinukuu sio case. Jambo lingine je, unaamini ujazo wa Roho mtakatifu? Je, umezajwa Roho mtakatifu?
 
Kama Yesu akivinukuu sio case. Jambo lingine je, unaamini ujazo wa Roho mtakatifu? Je, umezajwa Roho mtakatifu?
Nimeandika nimefuta nimeandika nimefuta.... Hata sijui nijibuje!!

hivi tumefikia huku kwamba mtu akihoji basi hana Roho mtakatifu!! Kwahiyo wakristo wote wasihoji kitu!!
 
Nimeandika nimefuta nimeandika nimefuta.... Hata sijui nijibuje!!

hivi tumefikia huku kwamba mtu akihoji basi hana Roho mtakatifu!! Kwahiyo wakristo wote wasihoji kitu!!
Pasipo Roho mtakatifu Ukristo hauna maana. Ukiwa na Roho mtakatifu atakufunulia siri zote zilizositirika. Atakufundisha na kukusaidia kuomba, atakufundisha nini ufanye na nini usifanye. Atakupa uwezo wa kuishida dunia. Wakristo hatukuachwa yatima na wale wakristo wa kweli huwa hatubishani mambo ambayo ni controversial kwa common mind kwa sababu tuna Roho mtakatifu anayeishuhudia kweli ya Kristo ndani yetu katika hili hatuteteleki kwa sababu katika dunia hii mafundisho na dini za uongo zipo tangu zamani na wote wanatumia Biblia lakini hutawasikia wakimzungumzia Roho mtakatifu kwa vitendo.
Ukiwa mkiristo bila Roho mtakatifu, ukristo wako ni bure
 
Sasa mbona Joshua na Yuda wamenukuu Apokrifa ila bado vitabu vyao vipo kwenye Biblia?? Unaweza kutusaidia kwanini?? Pia utueleze kivp Mwandishi wa samuel na wafalme alinukuu vitabu vya apokrifa pia lakini mbona vipo kwenye Biblia bado??

Tuanzie hapo kwanza
Daah!!

Mkuu nimesoma baadhi tu ya page za uzi huu na mwishoni,nikipata wasaa kunako majaaliwa nitaupitia...

Hakuna namna yoyote mtu anaweza kubisha na kuondoa umuhimu wa vitabu vingine kuelezea mambo yaliyoko kwenye biblia kwa kina na hii inavifanya kuwa vitabu vya muhimu kwa muktadha huo...

LAKINI,vitabu vilivyoko kwenye biblia ni vitabu vilivyoandikwa kwa namna yake na inahitaji utulivu kweli kweli kuelewa mambo mengi kama si yote....

Ndio maana watu wanaishia tu kutoelewa na kuita hadithi....
 
Pasipo Roho mtakatifu Ukristo hauna maana. Ukiwa na Roho mtakatifu atakufunulia siri zote zilizositirika. Atakufundisha na kukusaidia kuomba, atakufundisha nini ufanye na nini usifanye. Atakupa uwezo wa kuishida dunia. Wakristo hatukuachwa yatima na wale wakristo wa kweli huwa hatubishani mambo ambayo ni controversial kwa common mind kwa sababu tuna Roho mtakatifu anayeishuhudia kweli ya Kristo ndani yetu katika hili hatuteteleki kwa sababu katika dunia hii mafundisho na dini za uongo zipo tangu zamani na wote wanatumia Biblia lakini hutawasikia wakimzungumzia Roho mtakatifu kwa vitendo.
Ukiwa mkiristo bila Roho mtakatifu, ukristo wako ni bure
Na huu ndio unafiki wa wana JF ulikuja na hoja ya kimwili kwamba apokrifa haikuwa quoted na BIBLE mie nikaleta ushahidi wa kimwili pia kuwa zilikuwa quoted.... Ndio sahivi unamuingiza roho mtakatifu kwenye hii mada kwanini na wwe usingeenda kwanza kuomba mungu kabla hujaja kujibu mada kwa kutumia "akili zako".

Kama hamtaki tuhoji mada za kiimani basi kusingekuwa na haja ya vyuo vya biblia, kusingekuwa ha haja ya bible study au kwenda kanisani bali tungejifunza tu maandiko wenyewe chumbani bila haja ya kusubiri ichambuliwe na mchungaji wako.

Kama ni hivi basi shule tusiende,kazi tusifanye tukae nyumbani tusubiri roho atufanyie kila kitu!!

Hizi defence mechanism za wafia dini, zinaua hili jukwaa.
 
Na huu ndio unafiki wa wana JF ulikuja na hoja ya kimwili kwamba apokrifa haikuwa quoted na BIBLE mie nikaleta ushahidi wa kimwili pia kuwa zilikuwa quoted.... Ndio sahivi unamuingiza roho mtakatifu kwenye hii mada kwanini na wwe usingeenda kwanza kuomba mungu kabla hujaja kujibu mada kwa kutumia "akili zako".

Kama hamtaki tuhoji mada za kiimani basi kusingekuwa na haja ya vyuo vya biblia, kusingekuwa ha haja ya bible study au kwenda kanisani bali tungejifunza tu maandiko wenyewe chumbani bila haja ya kusubiri ichambuliwe na mchungaji wako.

Kama ni hivi basi shule tusiende,kazi tusifanye tukae nyumbani tusubiri roho atufanyie kila kitu!!

Hizi defence mechanism za wafia dini, zinaua hili jukwaa.
Na hiyo Biblia kuisoma bila divine illumination na revelation inayotokana na Roho mtakatifu ni kazi bure.
 
Allah anasema hichi ni kitabu kisicho na shaka ndani yake
Na pia akasema "wanasema hii Quran umeindika wewe muhammad basi walete mfano wa kitabu hichi watafute na wasaidizi
Pia akasema walete mfano wa sura moja kama wanasema kweli

Pia akaseama hata tungelishusha Kitabu hichi kwa mfumo karatasi bado wasingesadiki

Na akasisitiza "hich ni kitabu chetu na tutakilinda kwa na aina upotofu"

Mtume Muhhamad aliteua waandish 12 akiwemo Uthuman na Zeyd ambae ndio anatajwa kuwa hafidh mkubwa wa Quran...wakati mtume yupo Quran ilikiwa imeandikwa kwenye magome ya miti na majani na na nyingine imehifadhiwa kwenye maktaba ya kiislam, wakati Umary ndio khalifa alimua kuiweka Quran katika mpangilio wake sababu wakati wa Umar tecnolijia ya kuandika kwenye ngozi ngumu ilikuwa imenza so akaamua kuipangilia kwa mfumo wa kitabu baada ya umary kuondoka akachukua madaraka Uthuman ambae alikiwa msomo na mmoja wa waandish wa Quran wakati wa mtume, alipoluwa safarin oman alikuta Watu wanasoma Quran amabayo imekosewa baashi ya matamshi kwa sababu wakati Muhhamad amewateua wale 12 hakuzuia wengine wanaoweza kuandika waandike wengine walikuwa wapita njia na walikuta muhhamad anateremsha aya nao waliziandika ila mtu ali double check tu kwa wale aliowateua so sababu kubwa ya hao watu kuwa na Quran yenye mapungufu ya kimtamsh ambayo yangebadili maana....

Ndipo Uthaman akarud Makka na akawaita wale waandishi by that time walikuwa wamebaki sita wakaandika Quran Upya kwenye ngozi kwa kipindi hicho teknolojia ilikuwa ime advance na kaagiza watu wote kwa kipindi hicho waende waka copy Quran ile walioyoiandika wao na kila mtu achome moto copy yoyote ambayo yupo nayo iwe ina mapungufu au haina mapungufu...na Quran ile aliyoiandika Uthaman ipo had leo maktaba ya Uturuki na ipo sawa sawa had leo ukilinganisha na Quran tuliyonayo leo..

Uthaman amendika Quran hiyo miaka 10 tu baada ya kufariki muhammad so watu wengi walihifadh Quran walikuwa bado wapo ndio maana hakujatokea utata qa copy za Quran na ukiitazama Quran kwa structure utagundua hakuna mwanadamu anaweza kuindika hata Uthaman angejaribu kuhujumu bado angeshindwa...kasome kitu kinairwa Quran in Numbers utaona miujiza ya kimoangilio na ndio maana Mungu kajitapa anaeweza alete japo mfano wa kitabu hiki,baadae akasema alete mfano sura moja baadae akasema alete mfano wa aya kumi baadae akasema alete japo mfano wa aya moja...hii yote ni kwa sababu ya structure yake na mahesabu ukiacha ujumbe uliyoibeba humu ndani...ndio maana inaitwa LIVING MIRACLE..!

Ujinga ujinga mwingi unaandikwa juu ya Quran na watu wengi tu ila ukiamua kufata vyanzo sahihi utaupata ukweli Quran ni moja tu duniani
Ahsante sana naomba majina ya hao watu 12(maswahaba As) waliokuwa wakiiandika Quran wakati wa mtume(saw)
1.Uthman
2.zeyd
3.
4.
12.
Na majina ya maswahaba(as)6 waliobakia na kuiandika tena upya baada ya Uthman kurudi Makkah
Nitashukuru
Nalog off
 
Kama hawakubaliana Lazima had leo ingekuwepo nakala ya maandiko amnayo ingesema hichi kiliachwa au hichi kimeonvezwa haikikuwepo aababu watu waliokuwa a wamehifadh Quran ni wengi kama ambavyo ipo kwenye bible na kibaya ndugu yangu unasima sana history za mashia lakin hata wao hawana Quran mbadala...nikuuukize wwwe unaamini kwenye bibe ya bitabu 72,66 au 82 na nani yupi sahihi kati ya hao na kwanini vingine viwepo kwa wengine visiwepo.!
66
 
Mkuu mitale na midimu nimeona ntapandisha uzi kuhusu Canonicity ya Biblia na ntaeleza shida ilipoanzia maana naona imekuwa topic kubwa kidogo..... Labda kwa ufupi tu nkijibu hoja zako
1. Greek Septuagint iliinclude apocrypha/Deuterocanonical books na ndio iliyotumika kipindi cha Yesu na HAVIKUTENGANISHWA kabisa.... sema baada ya masoretic texts kuja ndio wakavitenga.... Na hapo unaposema manabii hawakunakiri nimeshasema mara 100 humu kuwa new testament imequote baadhi ya Apocrypha mfano hicho kitabu cha Enock na kama sio naomba unisaidie mistari hii imequotiwa kutoka kitabu gani cha agano la kale na kama hajatoa huko kivipi ufanane na kitabu cha Enock

Yuda
14 Na Henoko, mtu wa saba baada ya Adamu, alitoa maneno ya unabii juu ya hao, akisema, Angalia, Bwana alikuja na watakatifu wake, maelfu maelfu,
15 ili afanye hukumu juu ya watu wote, na kuwaadhibisha wote wasiomcha Mungu....

Yuda
6 Na malaika wasioilinda enzi yao wenyewe, lakini wakayaacha makao yao yaliyowahusu, amewaweka katika vifungo vya milele chini ya giza kwa hukumu ya siku ile kuu.

Naomba kwa vyanzo vyako ukahoji kokote hizo reference za Yuda wanatheolojia wanakiri aliquote kwa Book of Enoch hasa sura ya 6.

2. Mkuu hapo nmeshaeleza Greek Septuagint ilikuwa na apocrypha zote bila kutenganishwa na ndio maana wakatoliki wameiadopt ikapelekea kuwa na vitabu 7 zaidi (nafkiri ntaliongelea zaidi kwenye huo uzi wa canonicity ya Biblia) ila nilichosema mimi kufikia AD 382 ndipo standard Bible hasa vitabu vya agano jipya ndipo vilikubalika labda wwe unaweza nipa source ya uwepo wa canon ya OT na NT katika mjumuisho wake kabla ya 380 AD.

3. Naposema kanisa namaanisha East orthodox church inayokubali baadhi ya apocrypha hivyo ina vitabu kama 68, Tawahedo Orthodox la Ethiopia lina vitabu 81, Protestants kama pentecost,lutherans,SDA wana vitabu 66, Roman Catholic vitabu 73!!! Ndio hapo nauliza huoni kuna shida?? Kwanini Mungu aruhusu kila kanisa kuwa na Biblia yake?? Je waliongozwa kweli na roho wakati wa kucompile (hili pia ntaliongelea zaidi kwenye ule uzi)

Kuhusu maswala ya nyongeza

1.Mkuu kuhusu NT Canon kabla ya council of Rome hyo AD 382 kulikuwa na wengi waliocompile lakini hawakufikia conclusion kuhusu canonicity ya baadhi vitabu mfano ufunuo,2 peter hivyo wengine waliviacha wengine waliviinclude lakini hao council of Rome ndio wakafanya cross reference na kufikia hitimisho RASMI kuwa NT iwe na Vitabu 27 ambavyo ni hivi tulivyonavyo.

2.Pia hakuna mahala niliposema Enoch ni kitabu kitakatifu ila nachosema manabii wa enzi hizo walivisoma pia na ndio maaana kuna makanisa kama ya Orthodox kama hilo la Ethiopia limekitumia mpaka leo tokea enzi za Yesu na walikuwa wanakisoma kanisani tokea AD 300... Na ndio maana nikaleta huu uzi kuhoji kwamba licha ya (Enoch,jasher,Acts of solomon) kutokuwa vya kitakatifu lakini mbona mitume wamevinakiri?? Na ndio maana hapo juu nimeuliza tu naomba unisaidie Yuda alitoa wapi reference kuhusu maneno ya Henoko kwenye mstari wa 4,6,13 n.k??

3. Hakuna debate yeyote mbona wanatheolojia wameshaconclude tu... Unajua shida ya sisi tunakuwa biased mfano Yohan akicopy maneno ya Isaya au stefano akicopy maneno ya Yakobo watu wanasema amecopy OT ila mtu akinakiri book of jasher au Enoch au acts of solomon utaulizwa "una uhakika gani kama hicho kitabu alichonakiri ndio kile original"!!! Sasa kwanini kwa mathayo hamkuhoji kama ni kitabu cha "mwanzo" halisi ila kwa Yuda na Joshua mtahoji hivyo?? Hii bias ndio inaleta debate lakimi tukiamua kuwa objective tutagundua kuwa ukweli ni mmoja TU

Kuhusu mkuu Eiyer naweza muunga mkono sababu mfano hicho kitabu cha Gad the seer kimekuwa termed as LOST BOOK!! hata kitabu kinachodaiwa kuandikwa na Mfalme Ogu nacho kimekuwa termed as LOST BOOK ingawa kuna script moja ya wanatheolojia wanadai sio kma vimepotea bali vimefichwa!! Otherwise labda nikuulize wwe vitabu vya watakatifu kama Nabii Gadi au Nabii Samuel inakuaje vipotee?? Ina maana maneno ya Mungu yanaweza potea tu kama toilet paper??

Ubarikiwe mkuu
asante mkuu kwa mrejesho mzuri.
Kuna mambo kadhaa kama hutaona tabu uyajumuishe kwenye Uzi wako utakaouleta.

1: Kuna ushahidi wowote kuwa vitabu vivyo hasa apokrifa vilikuwa ni sehemu ya cannon ya wayahudi?
2:Wakati Septugiant (LXX) inaandikwa Nusu ya kwanza ya karne ya tatu, Vitabu ambavyo vilikuwa na uhakika kuwa vimeandikwa au kuwa sehemu ya canon ya wayahudi ni Pentateuch au Torah. weka uthibitisho wa wanatholojia kuwa 100% wanauhakika kuwa kwenye pentateuch kulikuwa na Apokrifa kama jewish canon.
3: Je, Kuna ushahidi kuwa Apokrifa vilikuwa sehemu ya Jewish canon japo najua vilikuwepo kama vitabu vingine vingi ambayo list yake haifahamiki lakin nahoji canonicity yake?
4: Unamzungumziaje Jerome aliyetafsiri Septugiant na list ya vitabu vilivyokuwemo kwa wakati wake, Mwaka 345- 420, Na kwa akili yake timamu akaweka wazi kabisa hivyo sio sehemu ya Canon na Visitumike kuundia doctrine '' kama wenzetu wanavyovitumia kutengeneza doctrine ya kutolea sadaka za wafu na mambo mengine''. Na kwa sababu hilo zoezi alilifanyia hukohuko uyahudi katikati ya wayahudi huoni kama alijua nini kiliaminiwa na nini hakikuaminiwa kama cannon kwa wayahudi?
Japo aliviona vyafaa kusomwa, maana hata mimi naona hoja kwa sababu vinacover intertestimental period karibu miaka minne kati ya malaki na mathayo na angalau vinatujulisha nini kilitokea katika wakati huo wa ukimya.

5:Augustine ndiye aliyetoa pendekezo la kuandika iandikwe bibilia ya kilatini ili kuunganisha wale wa magharibi na wale wa mashariki walio kuwa wanatumia kigiriki. Na inaonekana yeye ndiye aliyependekeza hizo apocrifa kuwa na hadi ya inspired japo kwa wenzetu Catholic church zilipigiliwa msumari kwenye mtaguso wa Trent baada ya kuibuka upinzani wa waprotestant.
Hii unaizungumziaje, unaweza kukosoa au kuipinga uhalali wake kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya kitaalimungu katika uzi huo ili tupate vina vya mada.

6:Unawazaungumziaje Luther na Jerome wote kwa pamoja kutambua uwepo wa vitabu hivyo lkn sio katika level za canon au inspired na kuonya visitumike kudefine christian doctrine.


Kwa sababu Pseudepigraphical books sio apocrifa ie book of enoch na wezake, na quote za Yuda hapo ninahojankadhaa.

1: Kama unasema inakubalika kwa wanatheolojia wote katika utofauti wao, maana na wenyewe wanapingana (liberal, historical criticals, conservatieves etc) naomba hapo nisibishe ila niseme kuwa kiwepo au kisiwepo miongoni mwa sababu ya kukiacha ni kuwa mujibu wa wanatheolojia pia hata wayahudi hawakukipa hadhi ya kuwa cannon. Hivyo kuwa quoted ikiwa ndivyo ilivyo haikihalalishi uvuviwaji wake. Ndio maana huko nyuma nilikuambia Paulo alipoquote mtunga mashahiri wa athene haikuhalalisha kila kilichomo humo. Hivyo sioni hoja kwenye kuquote, au kuzungumziwa wa vitabu vilivyo hivyo.

2:Naunga mkono sio maandiko matakatifu kwa sababu pia kinapingana na maandiko mengine ambayo yanakubaliana kwenye some issues.

mfano
Yesu anasema wazi kuwa Mbinguni hakuna Ngono. Hivyo malaika sio Sexual beings. Sasa huyo wa Enoch anazungumzia habari za ngono na malaika. Japo najua hapo kuna mgogoro wa mwana wa Mungu vs wana wa wanadamu. Ila mimi namuamini Yesu ambaye aliyoka huko mbinguni kuwa No sex in heaven, hivyo angels are not sexual beings. Mathew 22:30
Kuna story nyingi za kufurahisha ambazo zinaleta migogoro mikubwa na waandishi wake.
Pia kinakadiliwa na baadhi ya wananzuoni kuandikwa karne ya kwanza BC hivyo kwa uzingativu wa nono-canonoicity wake hata story zake sio za kutumainiwa. Nawaunga mkono wote wanaovipinga hivi pamoja na apokrifa.




kuhusu Quote, au kuandikwa kwa vitu vingine kwenyw vitabu vilivyovuviwa nimesema na naendelea kusema sio tatizo na haivifanyi vitabu hivyo kiwa Vimevuviwa.
Pia Kristo Yesu kwa sisi wakristo hakuanzia Pale Bethrehemu alipozaliwa, alikuwepo Hata kabla ya waandishi wa Vitqbu Vyote, na vilivyovuviwa alishiriki hivyo kauli zake kwangu ni Zaidi ya Authority. Hakuwahi popote kuindorse mavitu yanayopingana na 66Books katika kauli yake.

Pia mimi kama SDA, kama kanisa na wanatheolojia wa kitengo cha utafiti wa Bibilia kwa kitafiti kwa kina na kwa msaada wa Roho mtakatifu hayo yanayoitwa maandishi ya siri, vilivyopotea, Apocrifa, pseudo... tumehitihisha 66 inspired books are our authority.
Na Vingine vyote nje ya hapo ni vitabu vizuri vunavyofaa ambavyo havijavuviwa na havifai kufanywa kama rejea kitabu kilichovuviwa. Ila naweza kurejea kitabu chochoote hata sio tu cha wayahudi, bali hata cha wahindu, freemasonry, wapagani afrika kumagnify kile bibilia ya 66 inachosisitiza, kama alivyofanya paulo au Yuda ikiwa kweli hicho kitabu cha enoch.

Mfano umenifundisha Kuhusu Cathage empire na Yule mbabe aliyekaribia kuangusha dola ya Rumi. Nikisimama popote kuzungumzia Unabii wa Daniel 2, 7, Ufuno 13 kuthibitisha kauli ya Mungu kuwa Roman empire haitaanguka, bali itqgawanyika na ushawishi wake utakuwepo hadinmwisho wq dunia nitawaonyesha watu jinsi ilivyoshindikana kuangushwa na watunisia/cathage.
Hii yote haiyafanyi maandishi ya kikathage au hizo historia nilipoquote hilo tukio nimevipa hadhi sawa na bibilia.

Mwisho
Point yangu kuu kwenye uzi huu ni ile niliyoiandika front page ya kwanza kabisa. Bibilia ni Kitabu cha Mahusiano kati ya Mwanadamu mdhambi na Mungu wake, Tukikosa big picture hii katika kujadili haya tutakuwa umeamua Kunywa maji ya kunawa kisha tukaondoka tukiwa tumeacha misosi mitamu na maji ya kunywa na kufa kwa njaa kwa upofu huo.


ubarikiwe mkuu zittoJr
 
Back
Top Bottom