Biblia na reference ya vitabu vya kipagani

Biblia na reference ya vitabu vya kipagani

Kitabu kilichoandikwa na Nabii wa Mungu wa Ibrahim Isaac na Jakob hakiwezi kuwa cha kipagani..labda hilo kanisa lenye hayo maelezo liwe haya madhehebu ya wachawi na wachumia tumbo wa miaka hii ya karibuni.
Basi tusaidie kwanini kitabu cha Nabii Gadi hakipo kwenye biblia??? Kwanini kitabu cha Jasher na Enoko havipo katika Biblia??
 
Dini inaingiaje hapa?? Tujikite kwenye hoja kwamba JF wafia dini mbadilike mfungue akili yenu na mkubali maarifa kutoka vyanzo tofauti sio kila hoja mpaka bible

Anyway nimeweka hapo maswali labda tusaidiane kujadili hayo tupate majibu
Nimehoji dini yako maana katika maandiko yako nimeona alama zenye harufu isio nzuri. Pia kukusaidia kila dini na ibada yake kuna uhusika wa roho au viumbe vyenye nguvu visivyoonekana.kila dini kuna roho yenye kuambatana nayo, ukristo una roho yenye kuambatana nao, hivyo kama kuna cha kuhoji au kisichoeleweka ataulizwa huyo roho na atatoa majibu yalio kamili. Sio watu kutafuta Maarifa kwenye vitabu vilivyoandikwa kwa akili nyepesi isiyo na mashiko.
 
Nadhani kwa maoni yangu tunajaribu kuigeuza Bibilia kitabu cha kubishania badala ya Kitabu cha mahusiano kati ya Mungu na wanadamu.
Picha kubwa ya biblia ambayo kila mtu anapaswa kuiona ni
1:Mungu aliumba Dunia na Wanadamu wakamilifu.
2:Adam na hawa wakachagua kumsikiliza shetani badala ya kauli ya Mungu na kutuingiza wanadamu wote katika shida japo Wapo kama wakina henoko na Abraham walitembea kwa Imani Mungu akawatukuza.
3:Mungu aliandaa mpango wa Wokovu, Kupitia Yesu Kila amwaminie na kumtii apate uzima wa milele na raha wenda zaidi ya ile ya adam na hawa bustanini baada ya hukumu ya Haki.

Picha kubwa kati ya Pambano la Wema na uovu na hitimisho lake Haipaswi kuhafifishwa na story nyingine yoyote.
Hii inaitoa Bibilia kwenye level ya Kitabu cha Kisomi na kukifanya Kitabu kinachomtambulisha Mungu muumbaji kwa kiumbe chake kilichopotea. Bibilia ni kitabu chenye lengo la kuleta mahusiano kati ya Mwanadamu na Mungu. Hii ndiyo inatakiwa kuwa output ya mtu kusoma bibilia. ie Daily connection with God until restoration.

Kuchimbua mambo ili kuhalalisha au kuharamisha mawazo flani ni kutoka nje ya BIG PICTURE YA KWA NINI BIBILIA.
Nimekuelewa mkuu sasa basi kwa maoni yako vitabu hivyo wote tunafahamu kuwa vinaitwa Pseudepigraphi yaani havitambuliki na kanisa je ni kwanini Biblia inavitolea reference??? Na kama Biblia inavitolea reference je ni kwanini bado havitambuliki na kanisa mpaka leo?? Na je tukijengea hoja kupitia hivyo vitabu tunakuwa sahihi??

Nina shauku sana ya kuelewa hii sintofahamu, ubarikiwe
 
Mtazamo wangu,

Kwa ujumla, dini(imani) ambazo hua zinatumia maandiko/vitabu yalioshushwa/vilivyoshushwa toka mbinguni (Mfano hizi mbili, Christianity - Bible, Islam -Quran) kwenye swala la reference kuhusiana na mambo/jambo ambalo halipo katika hayo maandiko/vitabu (1st Reference), hua wanaruhusiwa na baadhi ya articles kurefer katika vitabu vingine.

Kwa kifupi, hakuna kitabu/maandiko yoyote ambayo yapo STRICTLY FIXED WITHOUT OTHER REFERENCE, vitabu vyote vina exeption clause ya reference (for further reference).

Mfano mmoja mzuri ametoa zitto junior kuhusiana na thread yake ya bible, ambao namuunga mkono kwa alichoandika 100%.

Mfano wa pili, hata waislamu pindi wanapokutana na jambo ambalo halipo/halijawekwa wazi katika Quran, hua wana refer kwenye vitabu vingine (Kama vile vitabu vya Hadith - Vitabu vya Bukhari Na Muslim n.k).


Kwa mwenye idea ya maswala/elimu ya Theology natumai atakua amenielewa.
 
Basi tusaidie kwanini kitabu cha Nabii Gadi hakipo kwenye biblia??? Kwanini kitabu cha Jasher na Enoko havipo katika Biblia??
Wakijibu hili swali na mimi nachangia kwa hoja na ufanisi mkubwa ili jamii itambue umuhimu wa kuficha vitabu kadhaaa katika biblia na kuifanya jamii kushindwa kuconnect dots ili kupata mtiririko mzuri wa jinsi ulimwengu wa mwanadamu ulivyopata kuwa..


Pia kuna vitabu kama the Gospel of Mary Magdalena havipo kwenye biblia ya leo..

The Gospal of Thomas pia inakosekana katika edition mpya kitu ambacho ukimtolea reference mtu aliyebase na edition ya sasa hivi mtabishana mpaka kunakucha..

The Gospal of the lost twins kinakosekana kwenye edition ya bible iliyopo...

Yan wakati hivyo vitabu ndo vinajaribu kuwa na source at least ya kuweza kupata walau moja mbili tatu juu ya ukweli wote..

The last Super inaelezewa vizuri tena kwa mfumo mkubwa sana wa itifaki lakini kinakosa nafasi ya kuingizwa kwenye biblia iliyopo..

Mpaka hapo nachoka kwa uchovu mkubwa sana juu ya bibl kuwa kama source pekee ya kila kitu kinachohujiwa ndani...


The bible can not be the source of informations and at the same time stands as a reference point to explain the inside mentioned issues.
 
Nimehoji dini yako maana katika maandiko yako nimeona alama zenye harufu isio nzuri.Pia kukusaidia kila dini na ibada yake kuna uhusika wa roho au viumbe vyenye nguvu visivyoonekana.kila dini kuna roho yenye kuambatana nayo,,,ukristo una roho yenye kuambatana nao,,,,hivyo kama kuna cha kuhoji au kisichoeleweka ataulizwa huyo roho na atatoa majibu yalio kamili.sio watu kutafuta Maarifa kwenye vitabu vilivyoandikwa kwa akili nyepesi isiyo na mashiko.
Twende taratibu..... Biblia yenyewe ndio inatoa reference alafu unataka tusijengee hoja kupitia hivyo vitabu mpaka tukaombe kwanza?? Anyway ningependa unipe jibu straight bila kuzunguka zunguka

Je kwanini vitabu hivyo viliachwa ilihali biblia imevirefer??

Na kama Biblia imevirefer ni kwanini tukijengea hoja mnazipinga kisa tu zipo nje ya Biblia??

Embu naomba ujibu hayo usikimbilie kumuingiza Roho mtakatifu ilihali ulipoanza ulitumia akili zako binafsi alafu sasa ndio unamrushia kesi.....

Nasubiri
 
Basi tusaidie kwanini kitabu cha Nabii Gadi hakipo kwenye biblia??? Kwanini kitabu cha Jasher na Enoko havipo katika Biblia??
Kitabu cha Gadi kinahusu matukio yaliohusiana na utawala wa daudi maana gadi alikuwa nabii wa daudi kumwelewesha yale Mungu aliyotaka ayafanye,,kitabu cha yashari kimeandikwa Wakati wa utawala wa Suleiman na baadhi waliomrithi ufalme,,,wamekiita kitabu cha tarehe,,,yaani rekodi ya matukio,,,kwa leo tungekuwa tunaita diary....

Inawezekana kulikuwa na mambo ya kuandikwa na yaliandikwa kwa sehemu na ndio maana umevijua ila biblia zote sahihi ni maandiko yaliochaguliwa kwa mwongozo wa roho alie nyuma ya ukristo ili kuwaelewesha Mambo ya adili wakristo na sio wasome diary zenye history ya wafalme pasi na kuwa hizo Habari zina elimu kwa maisha ya kiroho ya wakristo.
 
lifecoded,
Dah mkuu umenigusa sana..... Umeshasoma gospel of judas iskariot?? Imenifungua kichwa sana itabidi nianzishie uzi wake kabisa maana inaelezea chanzo halisi cha Yuda kumsaliti Yesu na "injili" ya kweli ambayo Yuda pekee ndio alipewa na mengine mengi yenye uhalisia ila ndio hivyo kimetolewa nacho..... Anyway nasubiri mkuu utueleze kidogo hapo kuhusiana na sababu kwanini baadhi ya vitabu imebidi vifichwe

Ubarikiwe
 
Twende taratibu..... Biblia yenyewe ndio inatoa reference alafu unataka tusijengee hoja kupitia hivyo vitabu mpaka tukaombe kwanza?? Anyway ningependa unipe jibu straight bila kuzunguka zunguka

Je kwanini vitabu hivyo viliachwa ilihali biblia imevirefer??

Na kama Biblia imevirefer ni kwanini tukijengea hoja mnazipinga kisa tu zipo nje ya Biblia??

Embu naomba ujibu hayo usikimbilie kumuingiza Roho mtakatifu ilihali ulipoanza ulitumia akili zako binafsi alafu sasa ndio unamrushia kesi.....

Nasubiri

Wewe unacho hicho kidayari/ki diary?? Ni hoja ipi uliijenga kupitia hivyo vitabu ikakataliwa,,,je unajua unakosea kuviita vya kipagani??au unataka hata ukijenga hoja kwa vitabu visivyo na muunganiko na ukristo ukubaliwe tu usipingwe??? Hayo ni mambo yanayowezekana kwenye physics math na bios,,sio dini ya ukristo
 
Mtoa mada, Naomba kukuuliza...
Je unaamini katika Biblia? na kwamba Mungu anaongea na sisi kupitia hiyo?
Kama hauamini basi ni halali yako kuhoji kwa namna hiyo.

NB; nimeuliza hayo kutokana na mada zako nyingi zinazohusu dini, Nadhani vitu vingine tutamuuliza Mungu tukifanikiwa kufika huko.
 
Habari za jioni wana JF natumaini wote humu ni wazima.
View attachment 885770
Nlipokuwa naipitia uzi huu Mjue Yoabu - Jenerali Mkuu wa Mfalme Daudi, Katili na asiyeogopa chochote! - JamiiForums

Mkuu Elungata aliibua hoja kuhusu Daudi kuwa na mahusiano ya jinsia moja na nathan ila muanzisha uzi alipotaka ushahidi aliuwekea condition hii.




Baada ya kusoma hii comment nilisikitika sana na nilijiuliza sana kwamba inakuaje kila story ya watu waliotajwa kwenye bible watu wanataka reference kutoka ndani ya Biblia pekee as if Biblia imeandika kila kitu?? Kwanini tunapenda kujifunga akili kiasi hicho?


Baada ya kuona mentality hiyo imeanza kukua humu JF intelligence nikaona nilete mada jinsi Biblia yenyewe imetutuma tukasome vitabu vingine nje ya Biblia ili tuongeze ufahamu kuhusu baadhi ya watu na matukio ambayo Bibila yenyewe haikuandika yote kwa upana wake, hivyo nia ya uzi huu ni kwa wale waliojifunga kwenye kusoma maandiko pekee wabadilike na kuwa na fikra huru na kuruhusu maarifa kutoka kona zote kwa mithiri ya kujifunza zaidi na kupanua uelewa wa mambo.
View attachment 885772
Kwa kuanzia tu labda nitumie nafasi hii kumjibu mkuu wangu maishapopote kuwa hata biblia yenyewe inakiri kuwa maisha yote ya Daudi yameelezewa vizuri zaidi nje ya Biblia hivyo imetutuma tukasome vitabu hivyo mnavyoita vya kipagani ili tujifunze kwa ufanisi zaidi

1 NYAKATI 29:29
29 Basi habari za mfalme Daudi, mwanzo na mwisho, angalia, zimeandikwa katika tarehe ya Samweli, mwonaji, na katika tarehe ya Nathani, nabii, na katika tarehe ya Gadi, mwonaji.

Vitabu vilivyotajwa hapa ni Book of Gad the seer,Book of Nathan the prophet, Book of Samuel the seer (Sio samuel 1&2) ambavyo kwenye biblia havikuwekwa . Sasa kama Biblia inakiri kuwa sio kila story yake imeongelewa kwa upana wake katika biblia je kwanini siku hizi watu wakijengea hoja kuhusu personality za biblia mnalazimisha reference iwe ndani ya bible pekee??? Ina maana waandishi wa Biblia ni wajinga hadi watutume tukasome hivyo vitabu vingine ambavyo mnaviita vya kipagani??

MAANDIKO
Hapa chini nimeambatanisha vifungu vya Biblia hivyo ningeomba tuisome kwa makini kabla ya kuchangia hoja. Neno Tarehe kwenye maandiko haya kwa kiswahili rahisi inamaanisha Nyaraka/rekodi/kitabu au kwa kizungu book/journal/Annal.
View attachment 885773

1. Kitabu cha Yehu

2 Nyakati 20:34
34 Na mambo yote ya Yehoshafati yaliyosalia, ya kwanza na ya mwisho, angalia, yameandikwa katika tarehe ya Yehu mwana wa Hanani, iliyotiwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli.

2. Kitabu cha Nabii Gadi muonaji/ Kitabu cha shemaya

2 Nyakati 13:22
22 Na mambo ya Abiya yaliyosalia, na njia zake, na maneno yake, yameandikwa katika kitabu cha maelezo cha nabii Ido.

2 Nyakati 12:15
15 Basi mambo yake Rehoboamu, ya kwanza na ya mwisho, je! Hayakuandikwa katika tarehe za Shemaya nabii na Ido mwonaji, kwa jinsi ya kuandika nasaba? Kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu siku zote.

1 Nyakati 29:29
29 Basi habari za mfalme Daudi, mwanzo na mwisho, angalia, zimeandikwa katika tarehe ya Samweli, mwonaji, na katika tarehe ya Nathani, nabii, na katika tarehe ya Gadi, mwonaji.

3. Kitabu cha mfalme Ahasuero

Nehemiah 12:23
23 Wana wa Lawi, wakuu wa mbari za mababa, wameandikwa katika kitabu cha tarehe, hata siku za Yohana mwana wa Eliashibu

Pia kinatajwa Esther 10:2, 2:23, 6:1

4. Matendo ya Mfalme suleiman

1 wafalme 11:41
41 Nayo yaliyosalia ya Sulemani, mambo yake na yote aliyoyafanya, na hekima yake, je! Hayo siyo yaliyoandikwa kitabuni mwa mambo yake Sulemani (Book of Acts of Solomon)

5. Nyakati za wafalme wa Israel & Yuda

1 wafalme 14:19
19 Na mambo yake Yeroboamu yaliyosalia, ya kupigana na ya kutawala, tazama, yameandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli.(chronichles of the kings of israel/Judah)

6. Kitabu cha Hozai

2 Nyakati 33:19
19 Sala yake pia, na jinsi Mungu alivyomtakabali, na dhambi yake yote, na kosa lake, na mahali alipopajenga mahali pa juu, na kupasimamishia maashera na sanamu za kuchonga, kabla ya kujinyenyekeza; tazama, hayo yameandikwa katika tarehe ya Hozai.

Hivi ni kwa uchache tu ila kuna vitabu vingine zaidi ya 20 vinatajwa kama reference point kwenye biblia ilihali havipo kwenye Biblia na wala havitambuliki na kanisa lakini leo hii akijengea mtu hoja anaonekana shetani!!
View attachment 885774

HITIMISHO
Baada ya uzi huu nisingetegemea tena kusikia wana JF wakitaka reference kutoka kwenye biblia pekee ilihali Biblia yenyewe inataka tukarefer kwenye vitabu vingine ambavyo vingi ni vya kipagani tu ili tupate uelewa zaidi ya watu muhimu kwenye bible.

However ningependa tujiulize maswali haya ili kupanua fikra zaidi

1. Kwanini vitabu hivi ambavyo Biblia inaturefer tukasome ili kuelewa baadhi ya matukio havikuwekwa kwenye biblia??

2. Na kama havikuwekwa kwa sababu yeyote ile je ina maana ni vya kipagani??

3. Na kama ni vya kipagani ni kwanini vimekuwa referred kwenye bible?

4. Kuna vitabu vingine ambavyo vimenakiliwa hapa ni halali kabisa katika kanisa la kale lakini kwa sasa viko categorized kama vitabu vilivyopotea.... Je nini hatma ya Biblia kama maneno ya Mungu ilihali yanaweza kupotea??

5. Na kama yamepotea je ina maana biblia haijakamilika sababu sehemu ya stori yake imepotea??

Naomba kuwasilisha

Cc: Wana JF intelligence wote bila kuwasahau kina Mchawi Mkuu Malcom Lumumba Elungata Da'Vinci Mshana Jr Eiyer Kudo900 Vi rendra N J subi Bujibuji Kipanga boy Kiranga Che mittoga Ip man 3 mitale na midimu Mzee wa Torano Blaki Womani Grahnman za chembe jimmykb197 911sep11 afsa Francis3 mtu chake NJOLO Msolo Shubiri Pori Pendael24 Mr Miller Elli Khalifavinnie Kennedy Son of Gamba Kanungila Karim Mgambilwa ni mntu Mr FCB Mr Q geesten66 Jerry Ekky Mnabuduhe Chrisvern Dabby Jr kibuyu180 IGWE SALA NA KAZI
Wick Dukeson lifecoded Daimler
Kwa usahihi tamko tarehe limetoholewa kutoka katika lugha ya kiarabu likitamkwa "Tarekh". Kwa maana ya tamko hilo kilugha ni Historia.

Ukiambiwa rejea tarehe ya fulani,aidha ni kitabu cha muandishi fulani kinaelezea historia fulani au historia ya mtu fulani. Huo ndio usahihi wa maana ya tamko "Tarehe".

Naendelea kusoma kupata faida......
 
Kitabu cha Gadi kinahusu matukio yaliohusiana na utawala wa daudi maana gadi alikuwa nabii wa daudi kumwelewesha yale Mungu aliyotaka ayafanye,,kitabu cha yashari kimeandikwa Wakati wa utawala wa Suleiman na baadhi waliomrithi ufalme,,,wamekiita kitabu cha tarehe,,,yaani rekodi ya matukio,,,kwa leo tungekuwa tunaita diary....
Inawezekana kulikuwa na mambo ya kuandikwa na yaliandikwa kwa sehemu na ndio maana umevijua ila biblia zote sahihi ni maandiko yaliochaguliwa kwa mwongozo wa roho alie nyuma ya ukristo ili kuwaelewesha Mambo ya adili wakristo na sio wasome diary zenye history ya wafalme pasi na kuwa hizo Habari zina elimu kwa maisha ya kiroho ya wakristo.
1.Sasa kama hivyo vitabu ndio Biblia inasema vina historia kamili ya Daudi kwanini tukijengea hoja mnakataa?? Gadi kaongelea mengi ya Daudi ambayo Biblia haiyasemi je kwanini mnapinga hoja zake??

2.Na kama hivyo vitabu ni halali kwanini kwenye biblia haviwekwi??

3.Unaposema Vitabu vilivyowekwa kwa sasa vinasaidia wakristo hivyo vya Gadi havina maana je nkikuuliza kitabu cha wimbo ulio Bora unasaidiaje ukristo wako?? Au kitabu cha Samuel kina tofauti gani na kitabu cha Gadi kiasi mkiache ilihali vinafanana content??

Naomba ujibu kwa mtiririko huu huu
 
Kwa usahihi tamko tarehe limetoholewa kutoka katika lugha ya kiarabu likitamkwa "Tarekh". Kwa maana ya tamko hilo kilugha ni Historia.

Ukiambiwa rejea tarehe ya fulani,aidha ni kitabu cha muandishi fulani kinaelezea historia fulani au historia ya mtu fulani. Huo ndio usahihi wa maana ya tamko "Tarehe".

Naendelea kusoma kupata faida......
Nashukuru mkuu kwa clarification yako
 
Kwa kukusaidia vilivyoandikwa kwenye Bible ni vile tu vilivyokuwa tested na kuthibitika kweli, yale yasiyo na uhakika japo yaweza kuwa kweli yakatupwa nje.
Mkuu labda sijaeleweka
1. Biblia inatoa reference kuwa story nzima ya Daudi au rehoboam etc zinapatikana kwenye vitabu A, B na C??

Sasa swali linakuja kwanini tukifanyia reference vitabu hivyo hasa humu JF mada inapingwa kisa tu haipo kwenye Biblia??

Yaani why Biblia imefanyia reference ila sisi tukifanyia reference haikubaliki kwa mada za kiimani??
 
Tuko pamoja bro,kuna mifano kadhaa ya vitabu fulani nilitaka kuiweka hapa ila nikaona haina haja sana.

Tuendelee......
Karibu mkuu umwage nondo kwa faida ya wanajukwaa wote
 
Mtoa mada, Naomba kukuuliza...
Je unaamini katika Biblia? na kwamba Mungu anaongea na sisi kupitia hiyo?
Kama hauamini basi ni halali yako kuhoji kwa namna hiyo.

NB; nimeuliza hayo kutokana na mada zako nyingi zinazohusu dini, Nadhani vitu vingine tutamuuliza Mungu tukifanikiwa kufika huko.
Yes mkuu namuamini Mungu sana tu na ninaamini katika Biblia sana tu ila huwa napenda kuhoji mambo ambayo nayaona yanasintofahamu kwa lengo la kujifunza zaidi so hakuna kosa lolote hapo.

Na nafikiri kuhoji ni vizuri ili upanuke uelewa ndio maana Hata shuleni mwalimu akifundisha tunamhoji maswali naye anatupa majibu. Na nikiri tu kuna watu huwa kupitia mijadala ndio wanasoma Biblia ila bila kuwepo maswali hawawezi soma Biblia kwa undani zaidi.

Na nitoe changamoto tu kwa wakristo na waislam kuwa tujenge mazoea ya kupenda mijadala sababu mtakutana na asiyeamini utakosa hoja za kumhubiria

Ni hayo tu
 
Back
Top Bottom