Biblia na reference ya vitabu vya kipagani

Biblia na reference ya vitabu vya kipagani

Habari za jioni wana JF natumaini wote humu ni wazima.
View attachment 885770
Nlipokuwa naipitia uzi huu Mjue Yoabu - Jenerali Mkuu wa Mfalme Daudi, Katili na asiyeogopa chochote! - JamiiForums

Mkuu Elungata aliibua hoja kuhusu Daudi kuwa na mahusiano ya jinsia moja na nathan ila muanzisha uzi alipotaka ushahidi aliuwekea condition hii.




Baada ya kusoma hii comment nilisikitika sana na nilijiuliza sana kwamba inakuaje kila story ya watu waliotajwa kwenye bible watu wanataka reference kutoka ndani ya Biblia pekee as if Biblia imeandika kila kitu?? Kwanini tunapenda kujifunga akili kiasi hicho?


Baada ya kuona mentality hiyo imeanza kukua humu JF intelligence nikaona nilete mada jinsi Biblia yenyewe imetutuma tukasome vitabu vingine nje ya Biblia ili tuongeze ufahamu kuhusu baadhi ya watu na matukio ambayo Bibila yenyewe haikuandika yote kwa upana wake, hivyo nia ya uzi huu ni kwa wale waliojifunga kwenye kusoma maandiko pekee wabadilike na kuwa na fikra huru na kuruhusu maarifa kutoka kona zote kwa mithiri ya kujifunza zaidi na kupanua uelewa wa mambo.
View attachment 885772
Kwa kuanzia tu labda nitumie nafasi hii kumjibu mkuu wangu maishapopote kuwa hata biblia yenyewe inakiri kuwa maisha yote ya Daudi yameelezewa vizuri zaidi nje ya Biblia hivyo imetutuma tukasome vitabu hivyo mnavyoita vya kipagani ili tujifunze kwa ufanisi zaidi

1 NYAKATI 29:29
29 Basi habari za mfalme Daudi, mwanzo na mwisho, angalia, zimeandikwa katika tarehe ya Samweli, mwonaji, na katika tarehe ya Nathani, nabii, na katika tarehe ya Gadi, mwonaji.

Vitabu vilivyotajwa hapa ni Book of Gad the seer,Book of Nathan the prophet, Book of Samuel the seer (Sio samuel 1&2) ambavyo kwenye biblia havikuwekwa . Sasa kama Biblia inakiri kuwa sio kila story yake imeongelewa kwa upana wake katika biblia je kwanini siku hizi watu wakijengea hoja kuhusu personality za biblia mnalazimisha reference iwe ndani ya bible pekee??? Ina maana waandishi wa Biblia ni wajinga hadi watutume tukasome hivyo vitabu vingine ambavyo mnaviita vya kipagani??

MAANDIKO
Hapa chini nimeambatanisha vifungu vya Biblia hivyo ningeomba tuisome kwa makini kabla ya kuchangia hoja. Neno Tarehe kwenye maandiko haya kwa kiswahili rahisi inamaanisha Nyaraka/rekodi/kitabu au kwa kizungu book/journal/Annal.
View attachment 885773

1. Kitabu cha Yehu

2 Nyakati 20:34
34 Na mambo yote ya Yehoshafati yaliyosalia, ya kwanza na ya mwisho, angalia, yameandikwa katika tarehe ya Yehu mwana wa Hanani, iliyotiwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli.

2. Kitabu cha Nabii Gadi muonaji/ Kitabu cha shemaya

2 Nyakati 13:22
22 Na mambo ya Abiya yaliyosalia, na njia zake, na maneno yake, yameandikwa katika kitabu cha maelezo cha nabii Ido.

2 Nyakati 12:15
15 Basi mambo yake Rehoboamu, ya kwanza na ya mwisho, je! Hayakuandikwa katika tarehe za Shemaya nabii na Ido mwonaji, kwa jinsi ya kuandika nasaba? Kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu siku zote.

1 Nyakati 29:29
29 Basi habari za mfalme Daudi, mwanzo na mwisho, angalia, zimeandikwa katika tarehe ya Samweli, mwonaji, na katika tarehe ya Nathani, nabii, na katika tarehe ya Gadi, mwonaji.

3. Kitabu cha mfalme Ahasuero

Nehemiah 12:23
23 Wana wa Lawi, wakuu wa mbari za mababa, wameandikwa katika kitabu cha tarehe, hata siku za Yohana mwana wa Eliashibu

Pia kinatajwa Esther 10:2, 2:23, 6:1

4. Matendo ya Mfalme suleiman

1 wafalme 11:41
41 Nayo yaliyosalia ya Sulemani, mambo yake na yote aliyoyafanya, na hekima yake, je! Hayo siyo yaliyoandikwa kitabuni mwa mambo yake Sulemani (Book of Acts of Solomon)

5. Nyakati za wafalme wa Israel & Yuda

1 wafalme 14:19
19 Na mambo yake Yeroboamu yaliyosalia, ya kupigana na ya kutawala, tazama, yameandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli.(chronichles of the kings of israel/Judah)

6. Kitabu cha Hozai

2 Nyakati 33:19
19 Sala yake pia, na jinsi Mungu alivyomtakabali, na dhambi yake yote, na kosa lake, na mahali alipopajenga mahali pa juu, na kupasimamishia maashera na sanamu za kuchonga, kabla ya kujinyenyekeza; tazama, hayo yameandikwa katika tarehe ya Hozai.

Hivi ni kwa uchache tu ila kuna vitabu vingine zaidi ya 20 vinatajwa kama reference point kwenye biblia ilihali havipo kwenye Biblia na wala havitambuliki na kanisa lakini leo hii akijengea mtu hoja anaonekana shetani!!
View attachment 885774

HITIMISHO
Baada ya uzi huu nisingetegemea tena kusikia wana JF wakitaka reference kutoka kwenye biblia pekee ilihali Biblia yenyewe inataka tukarefer kwenye vitabu vingine ambavyo vingi ni vya kipagani tu ili tupate uelewa zaidi ya watu muhimu kwenye bible.

However ningependa tujiulize maswali haya ili kupanua fikra zaidi

1. Kwanini vitabu hivi ambavyo Biblia inaturefer tukasome ili kuelewa baadhi ya matukio havikuwekwa kwenye biblia??

2. Na kama havikuwekwa kwa sababu yeyote ile je ina maana ni vya kipagani??

3. Na kama ni vya kipagani ni kwanini vimekuwa referred kwenye bible?

4. Kuna vitabu vingine ambavyo vimenakiliwa hapa ni halali kabisa katika kanisa la kale lakini kwa sasa viko categorized kama vitabu vilivyopotea.... Je nini hatma ya Biblia kama maneno ya Mungu ilihali yanaweza kupotea??

5. Na kama yamepotea je ina maana biblia haijakamilika sababu sehemu ya stori yake imepotea??

Naomba kuwasilisha

Cc: Wana JF intelligence wote bila kuwasahau kina Mchawi Mkuu Malcom Lumumba Elungata Da'Vinci Mshana Jr Eiyer Kudo900 Vi rendra N J subi Bujibuji Kipanga boy Kiranga Che mittoga Ip man 3 mitale na midimu Mzee wa Torano Blaki Womani Grahnman za chembe jimmykb197 911sep11 afsa Francis3 mtu chake NJOLO Msolo Shubiri Pori Pendael24 Mr Miller Elli Khalifavinnie Kennedy Son of Gamba Kanungila Karim Mgambilwa ni mntu Mr FCB Mr Q geesten66 Jerry Ekky Mnabuduhe Chrisvern Dabby Jr kibuyu180 IGWE SALA NA KAZI
Wick Dukeson lifecoded Daimler monde arabe mtu watu
Nipo late kuona Hio thread.
Lakini argument yako kuhusu thread ya jamaa ambayo Elungata alileta nadharia zake kuhusu Daud kujihusisha na homosexual habits. Hazikujengwa na kutoka kwenye kitabu chochote credible Bali aliyoa kwenye site ambayo inajaribu kutetea ushoga kwa kufanya false interpretation ya vi verse Fulani vya bible. Hata ukisoma maelezo yake. I hisia za yule mwandishi tu hamna evidence wala hoja yoyote ya msingi.






2.pili thread yako inahoji kuhusu biblia kutoa baadhi ya reference ambqzo hazipo kwenye modern canon
Answer.
Hivo unavotaja ni historical books na vipo vingi sana ulitaka vyote viwekwe kwenye bible kwa lengo gani?? Kwani biblia ni chuo cha history ?? Machache ya MUHIMU yameandikwa kwenye some historical books within the bible na wakaweka references kama utaitaji more information kuhusu maswala husika iende uko ukapate more knowledge.


Hii haiwezi Kutumika kama hoja ya kuvalidate matumizi ya tungo dhahania zisizo hata na credible information kutumika kama reference yako kuelewa jambo Fulani katika bible.


Na kama unavyo hivo vitabu na una uhakika navyo asilimia 100% (vilivotajwa kama reference) vitumie tu maadam ulipewa reference so ndokazi ya reference hio mkuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa kama Lutu aliweza kulala na binti yake kwanini unaamini daudi hawezi fanya uhuni?? Mbona alimlala mke wa mwanajeshi wake na baadae akamuua kabisa?? Who is David mpaka asifanye huo uhuni??
Uzuri biblia matukio kama hayo inayaandika haiyafichi ndomana mmeyaona waandishi wangeweza pia kufuta usione !!!


Ishu ya lutu kasome vizuri mabinti zake walimlevya hakufanya kwa hiyari yake hivo hatuwezi kumuhukumu

Mfano wewe zitto Jr vidume vilivoshiba kama kumi vikakumata na kukufanyia ulawiti utataka tuje kukulaumu kwanini umefanya uchafu wa jinsia moja ilihali tunajua ulifanywa bila hiyari yako kwanguvu na ulichukia tendo hilo ??


Pili binti zake walidhani ulimwengu mzima wamebaki watu watatu tu baada ya sodoma kuangamizwa!! Waliona it is the only way Ku restart human generation lasivyo human species ingetoweka,na kwakutumia precedence ya awali ya uumbaji kipindi cha adamu ndugu walioana ili waongezeke so yeah they were right in their stupidity hawakuwa ma taarifa kuhusu other peoples existence.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Soma vizuri mada...... Huyo Nabii Gadi au Nabii Nathan vitabu vyao HAVIPO kwenye Biblia maana kanisa limeviterm vitabu vyao kama Pseudepigrapha/Apocrypha hivyo havitambuliki kwenye Bible na vinahesabika ni vya kipagani tu.

Sasa nikuhoji wwe... Je kwanini basi Biblia inatoa reference kutoka vitabu vya kipagani?? Ila sisi wana JF tukitoa reference kutoka vitabu vya nje ya bible mnakataa hoja zetu??

Tuanzie hapo kwanza
Nabii gadi kitabu chake kinakuwaje apocrypha ,correct me if I'm wrong lakini nijuavyo apocrypha age ilikuwa bado sana maana ipo mbele huku nyakati za makabayo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa kama mtu ana maandiko kwanini mnayakataa kisa hayapo kwenye Biblia ilihali Biblia yenyewe inatuambia habari za Daudi kwa upana wake tutavikuta kwenye vitabu vya Gadi,Nathan n.k ilihali vitabu hivyo vinahesabika ni vya kipagani kwa kanisa???

Yaani kwanini kuna double standards mkuu
Jamaa alitumia reference ya gay site unataka tuichukulie serious???

Yaani unafananisha reference ya gay site ( site ya kuteteta ushoga ) na kitabu kilichoandikwa na gadi na Samwel ??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
N
Nipo late kuona Hio thread.
Lakini argument yako kuhusu thread ya jamaa ambayo Elungata alileta nadharia zake kuhusu Daud kujihusisha na homosexual habits. Hazikujengwa na kutoka kwenye kitabu chochote credible Bali aliyoa kwenye site ambayo inajaribu kutetea ushoga kwa kufanya false interpretation ya vi verse Fulani vya bible. Hata ukisoma maelezo yake. I hisia za yule mwandishi tu hamna evidence wala hoja yoyote ya msingi.






2.pili thread yako inahoji kuhusu biblia kutoa baadhi ya reference ambqzo hazipo kwenye modern canon
Answer.
Hivo unavotaja ni historical books na vipo vingi sana ulitaka vyote viwekwe kwenye bible kwa lengo gani?? Kwani biblia ni chuo cha history ?? Machache ya MUHIMU yameandikwa kwenye some historical books within the bible na wakaweka references kama utaitaji more information kuhusu maswala husika iende uko ukapate more knowledge.


Hii haiwezi Kutumika kama hoja ya kuvalidate matumizi ya tungo dhahania zisizo hata na credible information kutumika kama reference yako kuelewa jambo Fulani katika bible.


Na kama unavyo hivo vitabu na una uhakika navyo asilimia 100% (vilivotajwa kama reference) vitumie tu maadam ulipewa reference so ndokazi ya reference hio mkuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
NaZani wewe ni MTU uliyejibu hoja wengine hawakutaka Hata kuvisikia hivyo vitabu vya reference

Nikuulize aliecombine bible alitumia vigezo gani kuweka vitabu na kutoa?
 
Vimeitwa vya kipagani toka kanisa la kwanza AD 300 kuanzia Jerusalem hadi Carthage.... Pia kanisa naongelea mfano Council of Trent iliokuwa kama conference kubwa ya kanisa katoliki ndio ilipitisha baadhi ya vitabu kuwa halali na vingine vikaachwa kama Apocrypha yaani vina kasoro kadhaa hivyo havikidhi viwango vya kuwa kwenye Bible na hata leo vinahesabika kama forgery/Feki na vinahesabika vya kipagani kabisa.

Ndio sasa nauliza kama Vitabu hivi vimatambulika vya kipagani je ni kwanini biblia imevitumia kama reference??

Na kama ww unaviona ni halali je ni kwanini basi havijaingiziwa kwenye biblia??

Na kama havifai na bado biblia imevitumia je ni kwanini tukijengea hoja mnazikataa??

Embu jikite kwenye mada tafadhali na kabla ya kuchangia kajifunze kidogo kuhusu Apocrypha na Pseudepigraphi ili ueleww nachosema
Nadhani hoja yako ni weak haina basis yoyote ya kusimamia

Hata kama kuna baadhi ya vitabu kadhaa vilikuwa referenced ( of which I told you earlier kama ur 100% sure you have that book una haki kabisa ya kusoma na kuongeza maarifa ) but tatizo hivi vitabu vingi vya kihistoria preservation zake haziaminiki maana vingi hata wayahudi hawakutumia kwenye canon yao kwahio ulinzi wa material content ni wa mashaka sana

Na vingi ukivisoma ( kwa vile vilivyopo available) vina information nyingi sana za ukweli hasa za kihistoria lakini bado haviwezi kutika kama spiritual books (in level with canonical) vinakosa authority kutokana na mashaka mengi mnoo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uzuri biblia matukio kama hayo inayaandika haiyafichi ndomana mmeyaona waandishi wangeweza pia kufuta usione !!!


Ishu ya lutu kasome vizuri mabinti zake walimlevya hakufanya kwa hiyari yake hivo hatuwezi kumuhukumu

Mfano wewe zitto Jr vidume vilivoshiba kama kumi vikakumata na kukufanyia ulawiti utataka tuje kukulaumu kwanini umefanya uchafu wa jinsia moja ilihali tunajua ulifanywa bila hiyari yako kwanguvu na ulichukia tendo hilo ??


Pili binti zake walidhani ulimwengu mzima wamebaki watu watatu tu baada ya sodoma kuangamizwa!! Waliona it is the only way Ku restart human generation lasivyo human species ingetoweka,na kwakutumia precedence ya awali ya uumbaji kipindi cha adamu ndugu walioana ili waongezeke so yeah they were right in their stupidity hawakuwa ma taarifa kuhusu other peoples existence.

Sent using Jamii Forums mobile app
Niko Hapo unapodai mabinti walidhani ulimwengu mzima umeteketea,lutu aliishi sodoma lakini nduguye Abraham aliishi SI mbali na hapo,
Sawa na tuchukue umbali toka kariakoo Hadi pugu ama ubungo,Hapa nakisia,lakini hata kwa Leo ukipima um
Jamaa alitumia reference ya gay site unataka tuichukulie serious???

Yaani unafananisha reference ya gay site ( site ya kuteteta ushoga ) na kitabu kilichoandikwa na gadi na Samwel ??

Sent using Jamii Forums mobile app
Sijui ulitaka bible iandike waziwazi,kitendo Cha bible kudai mwana wa Saul alimpenda Daud Ni redflag,
Kitendo Cha sauli kumgombeza mwanae kuwa ameitia aibu family kwa urafiki wake na Daud pia Ni gunsmoke
 
Screenshot_20200410-012721.png
 
Nadhani hoja yako ni weak haina basis yoyote ya kusimamia

Hata kama kuna baadhi ya vitabu kadhaa vilikuwa referenced ( of which I told you earlier kama ur 100% sure you have that book una haki kabisa ya kusoma na kuongeza maarifa ) but tatizo hivi vitabu vingi vya kihistoria preservation zake haziaminiki maana vingi hata wayahudi hawakutumia kwenye canon yao kwahio ulinzi wa material content ni wa mashaka sana

Na vingi ukivisoma ( kwa vile vilivyopo available) vina information nyingi sana za ukweli hasa za kihistoria lakini bado haviwezi kutika kama spiritual books (in level with canonical) vinakosa authority kutokana na mashaka mengi mnoo

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu hoja yako ni contradictory kabisa.

Nachosema ni kwanini mfano Joshua achukue simulizi za Book of Jasher kuwaeleza issue ya jua kusimama alafu mimi nikichukua simulizi za kitabu hiko hiko nionekane sipo credible?

Kama ina mashaka kwanini Joshua alitumia

Unaweza ukatuweka sawa hapo
 
Jamaa alitumia reference ya gay site unataka tuichukulie serious???

Yaani unafananisha reference ya gay site ( site ya kuteteta ushoga ) na kitabu kilichoandikwa na gadi na Samwel ??

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu toka mwanzo nilisema hoja hapa sio daudi kuwa shoga au lah ila concern yangu ni kwanini source outside the bible imekatazwa na huyo mchangiaji?.

Sasa ndio nauliza kama Bible yenyewe imeturefer kwa outside sources ili kuweza kuongeza maarifa ya historia husika kwanini basi tukijengea hoja kutumia hizo historia iwe nongwa??

Kama hizo source sio credible kwanini basi hao manabii wa Biblia wazitumie kujengea hoja?? Mfano Yudah kujengea hoja zake kutumia Kitabu cha Enock
 
Nabii gadi kitabu chake kinakuwaje apocrypha ,correct me if I'm wrong lakini nijuavyo apocrypha age ilikuwa bado sana maana ipo mbele huku nyakati za makabayo

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu Padre jerome wakati ana tafsiri Bible aliigawa hivyo yaani NT,OT na vile alivyohisi havina uvuvio vikawekwa kipengele cha Apocrypha whether kiliandikwa kabla au wakati wa silent period!!

Otherwise vinaitwa pseudepigraphi kwamba ni vitabu halali kabisa ila vina utata mahali fulani ndio maana vikaachwa

Lakini cha kujiuliza Song of songs na Hebrews ni pseudepigrapha ila havijatolewa kwa bible? Unaweza kutupa maoni yako
 
Uzuri biblia matukio kama hayo inayaandika haiyafichi ndomana mmeyaona waandishi wangeweza pia kufuta usione !!!


Ishu ya lutu kasome vizuri mabinti zake walimlevya hakufanya kwa hiyari yake hivo hatuwezi kumuhukumu

Mfano wewe zitto Jr vidume vilivoshiba kama kumi vikakumata na kukufanyia ulawiti utataka tuje kukulaumu kwanini umefanya uchafu wa jinsia moja ilihali tunajua ulifanywa bila hiyari yako kwanguvu na ulichukia tendo hilo ??


Pili binti zake walidhani ulimwengu mzima wamebaki watu watatu tu baada ya sodoma kuangamizwa!! Waliona it is the only way Ku restart human generation lasivyo human species ingetoweka,na kwakutumia precedence ya awali ya uumbaji kipindi cha adamu ndugu walioana ili waongezeke so yeah they were right in their stupidity hawakuwa ma taarifa kuhusu other peoples existence.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu najaribu kujenga picha kwa muktadha wa Nabii wa Mungu kazaa na mabinti zake!! Yaani hata uleweshwe kweli ubakwe tu na mabinti zako kirahisi hivyo?? Kwanini isingetokea radi iwamalize hao watoto??

Nachosema ni hiki..... Kila binadamu yuko prone kwa dhambi bila kujali status yake kwenye Biblia

Mfalme suleiman tunaambiwa ndio mwenye hekima zaidi ila ndio mfalme aliyepelekea anguko la Israel, Samson cjui daudi wote walipotea kabisa kisa ngono ndio sembuse nani??

Yaani nini cha ajabu hadi Daudi ashindwe kutenda dhambi?
 
Mkuu najaribu kujenga picha kwa muktadha wa Nabii wa Mungu kazaa na mabinti zake!! Yaani hata uleweshwe kweli ubakwe tu na mabinti zako kirahisi hivyo?? Kwanini isingetokea radi iwamalize hao watoto??

Nachosema ni hiki..... Kila binadamu yuko prone kwa dhambi bila kujali status yake kwenye Biblia

Mfalme suleiman tunaambiwa ndio mwenye hekima zaidi ila ndio mfalme aliyepelekea anguko la Israel, Samson cjui daudi wote walipotea kabisa kisa ngono ndio sembuse nani??

Yaani nini cha ajabu hadi Daudi ashindwe kutenda dhambi?
Jamaa anashangaa Daud kuwa gay,Samson mwenyewe kwa mujibu wa Bible alikua muuaji mkubwa,anaua watu 1000 ili awakate magovi ya kulipa betting,Moses alikuwa muuaji,abrahamu alikuwa tapeli akimtumia mke wake kutega ugoni alipwe mifugo,Solomon alikua womaniser,etc
 
Jamaa anashangaa Daud kuwa gay,Samson mwenyewe kwa mujibu wa Bible alikua muuaji mkubwa,anaua watu 1000 ili awakate magovi ya kulipa betting,Moses alikuwa muuaji,abrahamu alikuwa tapeli akimtumia mke wake kutega ugoni alipwe mifugo,Solomon alikua womaniser,etc
Yote hii kwasababu wao pia walikuwa ni binadamu kama sisi tu hivyo kwa kuwa nao pia walizaliwa, wakaishi katika jamii yao kuna mazuri watafanya na yapo mabalaa kama hivyo. Sasa jamaa huwa wanawatazama kama watu waliokuwa clean sana wakati inaelezewa kabisa Hata Petro alikuwa Mvuvi mwenye silika ya ukorofi sana ukitazama uhalisia wa maisha ukiwa kiongozi hutapendwa na jamii nzima unadhani hao wanaokupinga nini kitawapata mbona ipo wazi. Hao nao walikuwa binadamu sasa watu wanawachukulia kama malaika.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mleta mada vitabu vilivyokataliwa kwanza vingine vilijaa uongo Wa wazi kabisa ambao mfano hauendani na mafundisho ya Yesu

Mfano kitabu cha Henoko kinatamka wazi kuwa gharika ilikuja sababu malaika walioa na kuzaa na wanadamu .Wakati Yesu alitamka wazi kuwa malaika Hawaoi wala kuolewa na hawazai

Kuhusu agano la kale kanisa halikupata shida kubwa kusema vitabu vipi likubali na vipi likatae sababu waisrael wana Biblia yao tayari.Na ndio agano la kale linawahusu na walitunza kumbukumbu zake vizuri sana .Kuanzia vitabu vya Musa kiongozi wao.
.Wana Biblia yao inaitwa Biblia ya waebrania au Hebrews Bible .Kwa hiyo kanisa lilichukua yote kama ilivyo na kuiweka kama agano la kale.Bila kuongeza wala kupunguza maneno

kwa Agano jipya vilichukuliwa vitabu vile tu vilivyoandikwa na mitume Wa Yesu sio wengineo.Hivyo vingine vikatupwa nje

Kwa hiyo Agano la kale wanalo wayahudi na wanavitumia hadi Leo ndio walikabidhi kanisa.Vitabu ambavyo wayahudi hawavitumii na hawavitambui kanisa pia halivitambui

Kwa hiyo habari zako za vitabu vyote vya agano la kale vilivyokataliwa na wayahudi kanisa halivitambui.Kiwe kitabu cha Henoko sikui japher sijui Jehu na matapeli wengine

agano jipya pia nje ya walichoandika mitume Wa Yesu hakikubaliki.
 
Nabii gadi kitabu chake kinakuwaje apocrypha ,correct me if I'm wrong lakini nijuavyo apocrypha age ilikuwa bado sana maana ipo mbele huku nyakati za makabayo

Sent using Jamii Forums mobile app
Wayahudi wenye nabii wao walikikataa hicho kitabu .Hawakikubali.Na kanisa likakikataa
 
1. Mkuu unaweza kutuambia hiyo Hebrew Bible
(a) Ina vitabu vingapi?
(b) vitaje.
2. Umesema kanisa lilipokea biblia ya kale kutoka kwa Hebrews na wakaitunza Kama walivyopewa bila kubadilisha chochote. Iweje leo zinatofautiana idadi ya vitabu?

3. Umesema hivi vitabu nje ya Bible Ni vya kitapeli mfano jasher, gadi,etc. Mbona biblia imevifanya reference?
Mleta mada vitabu vilivyokataliwa kwanza vingine vilijaa uongo Wa wazi kabisa ambao mfano hauendani na mafundisho ya Yesu

Mfano kitabu cha Henoko kinatamka wazi kuwa gharika ilikuja sababu malaika walioa na kuzaa na wanadamu .Wakati Yesu alitamka wazi kuwa malaika Hawaoi wala kuolewa na hawazai

Kuhusu agano la kale kanisa halikupata shida kubwa kusema vitabu vipi likubali na vipi likatae sababu waisrael wana Biblia yao tayari.Na ndio agano la kale linawahusu na walitunza kumbukumbu zake vizuri sana .Kuanzia vitabu vya Musa kiongozi wao.
.Wana Biblia yao inaitwa Biblia ya waebrania au Hebrews Bible .Kwa hiyo kanisa lilichukua yote kama ilivyo na kuiweka kama agano la kale.Bila kuongeza wala kupunguza maneno

kwa Agano vilichukuliwa vitabu vile tu vilivyoandikwa na mitume Wa Yesu sio wengineo.Hivyo vingine vikatupwa nje

Kwa hiyo Agano la kale wanalo wayahudi na wanavitumia hadi Leo ndio walikabidhi kanisa.Vitabu ambavyo wayahudi hawavitumii na hawavitambui kanisa pia halivitambui

Kwa hiyo habari zako za vitabu vyote vya agano la kale vilivyokataliwa na wayahudi kanisa halivitambui.Kiwe kitabu cha Henoko sikui japher sijui Jehu na matapeli wengine

agano jipya pia nje ya walichoandika mitume Wa Yesu hakikubaliki.

Sent using LEAGOO M12
 
1. Mkuu unaweza kutuambia hiyo Hebrew Bible
(a) Ina vitabu vingapi?
(b) vitaje.
2. Umesema kanisa lilipokea biblia ya kale kutoka kwa Hebrews na wakaitunza Kama walivyopewa bila kubadilisha chochote. Iweje leo zinatofautiana idadi ya vitabu?

3. Umesema hivi vitabu nje ya Bible Ni vya kitapeli mfano jasher, gadi,etc. Mbona biblia imevifanya reference?

Sent using LEAGOO M12
Hebrew Bible ina vitabu 39 viko kama vya agano la kale la Biblia yenye vitabu 66 .sio kama ile ya Catholic yenye vitabu 72

Catholic walichakachua agano la kale waligoma kupokea vitabu vya Biblia ya wayahudi .Wakaongeza vyao ambavyo havimo kwenye Biblia agano la kale la wayahudi

Agano la kale hasa wenye rekodi zao halisi ni wayahudi na rekodi wamezitunza vizuriHivyo vingine hawaviitambui
 
1. Mkuu unaweza kutuambia hiyo Hebrew Bible
(a) Ina vitabu vingapi?
(b) vitaje.
2. Umesema kanisa lilipokea biblia ya kale kutoka kwa Hebrews na wakaitunza Kama walivyopewa bila kubadilisha chochote. Iweje leo zinatofautiana idadi ya vitabu?

3. Umesema hivi vitabu nje ya Bible Ni vya kitapeli mfano jasher, gadi,etc. Mbona biblia imevifanya reference?

Sent using LEAGOO M12
Hizo reference hata wayahudi hawana sababu kubwa ya kukosekana mojawapo ni kuwa hivyo vilikuwa havitumiki hekaluni.Na haviko maktaba yoyote ya wayahudi .Kuna wahuni ndio walikuja kuandika kama Novel za enzi hizo wasio wayahudi wakaamua kuvitambua sio kama Novel Bali kama vitabu halali vya kidini

Reliance kubwa ya agano la kale ni biblia ya wayahudi .Hebrew Bible.
 
Back
Top Bottom