Biblia na reference ya vitabu vya kipagani

zitto junior

JF-Expert Member
Oct 7, 2013
19,037
28,685
Habari za jioni wana JF natumaini wote humu ni wazima.
images (60).jpg

Nlipokuwa naipitia uzi huu Mjue Yoabu - Jenerali Mkuu wa Mfalme Daudi, Katili na asiyeogopa chochote! - JamiiForums

Mkuu Elungata aliibua hoja kuhusu Daudi kuwa na mahusiano ya jinsia moja na nathan ila muanzisha uzi alipotaka ushahidi aliuwekea condition hii.
ntaleta maandiko hapa tuyachambue

sawa ila hakikisha hayo maandiko yanaongea unachosema,tukubaliane hakuna reference nje ya biblia!

Baada ya kusoma hii comment nilisikitika sana na nilijiuliza sana kwamba inakuaje kila story ya watu waliotajwa kwenye bible watu wanataka reference kutoka ndani ya Biblia pekee as if Biblia imeandika kila kitu?? Kwanini tunapenda kujifunga akili kiasi hicho?


Baada ya kuona mentality hiyo imeanza kukua humu JF intelligence nikaona nilete mada jinsi Biblia yenyewe imetutuma tukasome vitabu vingine nje ya Biblia ili tuongeze ufahamu kuhusu baadhi ya watu na matukio ambayo Bibila yenyewe haikuandika yote kwa upana wake, hivyo nia ya uzi huu ni kwa wale waliojifunga kwenye kusoma maandiko pekee wabadilike na kuwa na fikra huru na kuruhusu maarifa kutoka kona zote kwa mithiri ya kujifunza zaidi na kupanua uelewa wa mambo.
images (61).jpg

Kwa kuanzia tu labda nitumie nafasi hii kumjibu mkuu wangu maishapopote kuwa hata biblia yenyewe inakiri kuwa maisha yote ya Daudi yameelezewa vizuri zaidi nje ya Biblia hivyo imetutuma tukasome vitabu hivyo mnavyoita vya kipagani ili tujifunze kwa ufanisi zaidi

1 NYAKATI 29:29
29 Basi habari za mfalme Daudi, mwanzo na mwisho, angalia, zimeandikwa katika tarehe ya Samweli, mwonaji, na katika tarehe ya Nathani, nabii, na katika tarehe ya Gadi, mwonaji.

Vitabu vilivyotajwa hapa ni Book of Gad the seer,Book of Nathan the prophet, Book of Samuel the seer (Sio samuel 1&2) ambavyo kwenye biblia havikuwekwa . Sasa kama Biblia inakiri kuwa sio kila story yake imeongelewa kwa upana wake katika biblia je kwanini siku hizi watu wakijengea hoja kuhusu personality za biblia mnalazimisha reference iwe ndani ya bible pekee??? Ina maana waandishi wa Biblia ni wajinga hadi watutume tukasome hivyo vitabu vingine ambavyo mnaviita vya kipagani??

MAANDIKO
Hapa chini nimeambatanisha vifungu vya Biblia hivyo ningeomba tuisome kwa makini kabla ya kuchangia hoja. Neno Tarehe kwenye maandiko haya kwa kiswahili rahisi inamaanisha Nyaraka/rekodi/kitabu au kwa kizungu book/journal/Annal.
original_story.jpg


1. Kitabu cha Yehu

2 Nyakati 20:34
34 Na mambo yote ya Yehoshafati yaliyosalia, ya kwanza na ya mwisho, angalia, yameandikwa katika tarehe ya Yehu mwana wa Hanani, iliyotiwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli.

2. Kitabu cha Nabii Gadi muonaji/ Kitabu cha shemaya

2 Nyakati 13:22
22 Na mambo ya Abiya yaliyosalia, na njia zake, na maneno yake, yameandikwa katika kitabu cha maelezo cha nabii Ido.

2 Nyakati 12:15
15 Basi mambo yake Rehoboamu, ya kwanza na ya mwisho, je! Hayakuandikwa katika tarehe za Shemaya nabii na Ido mwonaji, kwa jinsi ya kuandika nasaba? Kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu siku zote.

1 Nyakati 29:29
29 Basi habari za mfalme Daudi, mwanzo na mwisho, angalia, zimeandikwa katika tarehe ya Samweli, mwonaji, na katika tarehe ya Nathani, nabii, na katika tarehe ya Gadi, mwonaji.

3. Kitabu cha mfalme Ahasuero

Nehemiah 12:23
23 Wana wa Lawi, wakuu wa mbari za mababa, wameandikwa katika kitabu cha tarehe, hata siku za Yohana mwana wa Eliashibu

Pia kinatajwa Esther 10:2, 2:23, 6:1

4. Matendo ya Mfalme suleiman

1 wafalme 11:41
41 Nayo yaliyosalia ya Sulemani, mambo yake na yote aliyoyafanya, na hekima yake, je! Hayo siyo yaliyoandikwa kitabuni mwa mambo yake Sulemani (Book of Acts of Solomon)

5. Nyakati za wafalme wa Israel & Yuda

1 wafalme 14:19
19 Na mambo yake Yeroboamu yaliyosalia, ya kupigana na ya kutawala, tazama, yameandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli.(chronichles of the kings of israel/Judah)

6. Kitabu cha Hozai

2 Nyakati 33:19
19 Sala yake pia, na jinsi Mungu alivyomtakabali, na dhambi yake yote, na kosa lake, na mahali alipopajenga mahali pa juu, na kupasimamishia maashera na sanamu za kuchonga, kabla ya kujinyenyekeza; tazama, hayo yameandikwa katika tarehe ya Hozai.

Hivi ni kwa uchache tu ila kuna vitabu vingine zaidi ya 20 vinatajwa kama reference point kwenye biblia ilihali havipo kwenye Biblia na wala havitambuliki na kanisa lakini leo hii akijengea mtu hoja anaonekana shetani!!
51fWJURUiXL._SX361_BO1,204,203,200_.jpg


HITIMISHO
Baada ya uzi huu nisingetegemea tena kusikia wana JF wakitaka reference kutoka kwenye biblia pekee ilihali Biblia yenyewe inataka tukarefer kwenye vitabu vingine ambavyo vingi ni vya kipagani tu ili tupate uelewa zaidi ya watu muhimu kwenye bible.

However ningependa tujiulize maswali haya ili kupanua fikra zaidi

1. Kwanini vitabu hivi ambavyo Biblia inaturefer tukasome ili kuelewa baadhi ya matukio havikuwekwa kwenye biblia??

2. Na kama havikuwekwa kwa sababu yeyote ile je ina maana ni vya kipagani??

3. Na kama ni vya kipagani ni kwanini vimekuwa referred kwenye bible?

4. Kuna vitabu vingine ambavyo vimenakiliwa hapa ni halali kabisa katika kanisa la kale lakini kwa sasa viko categorized kama vitabu vilivyopotea.... Je nini hatma ya Biblia kama maneno ya Mungu ilihali yanaweza kupotea??

5. Na kama yamepotea je ina maana biblia haijakamilika sababu sehemu ya stori yake imepotea??

Naomba kuwasilisha

Cc: Wana JF intelligence wote bila kuwasahau kina Mchawi Mkuu Malcom Lumumba Elungata Da'Vinci Mshana Jr Eiyer Kudo900 Vi rendra N J subi Bujibuji Kipanga boy Kiranga Che mittoga Ip man 3 mitale na midimu Mzee wa Torano Blaki Womani Grahnman za chembe jimmykb197 911sep11 afsa Francis3 mtu chake NJOLO Msolo Shubiri Pori Pendael24 Mr Miller Elli Khalifavinnie Kennedy Son of Gamba Kanungila Karim Mgambilwa ni mntu Mr FCB Mr Q geesten66 Jerry Ekky Mnabuduhe Chrisvern Dabby Jr kibuyu180 IGWE SALA NA KAZI
Wick Dukeson lifecoded Daimler monde arabe mtu watu
 
Swali la kwanza kukuuliza Ndugu mwandishi,,wewe ni dini gani?? Labda kwa bahati mbaya wewe nawe ni mkristo,,uko dhehebu gani??
Dini inaingiaje hapa?? Tujikite kwenye hoja kwamba JF wafia dini mbadilike mfungue akili yenu na mkubali maarifa kutoka vyanzo tofauti sio kila hoja mpaka bible

Anyway nimeweka hapo maswali labda tusaidiane kujadili hayo tupate majibu
 
Sitegemei mtu mwenye akili timamu akasema Daudi Alikuwa basha!! Wazungu wanaita ridiculous au pia total crap au pia utter nonsense.
Sasa kama Lutu aliweza kulala na binti yake kwanini unaamini Daudi hawezi fanya uhuni?? Mbona alimlala mke wa mwanajeshi wake na baadae akamuua kabisa?? Who is David mpaka asifanye huo uhuni??
 
Yaani kitabu cha reference kiandikwe na mtu mwenye kupakwa mafuta ya kipekee kama Nabii Samuel,,au nabii Gadi au nabii Elisha watu wenye roho ya tofauti ndani yao na wewe uite vitabu vyao kuwa vya kipagani??? Mtu wa kawaida kama wewe mwandishi Unaweza kuhoji credibility ya kitabu kilichoandikwa na Nabii mwenye permanent connection na mbingu?? Uwezo wako ungehoji credibility ya vitabu vya Charles Darwin,,au da Vinci.
 
Yaani kitabu cha reference kiandikwe na mtu mwenye kupakwa mafuta ya kipekee kama Nabii Samuel,,au nabii Gadi au nabii Elisha watu wenye roho ya tofauti ndani yao na wewe uite vitabu vyao kuwa vya kipagani??? Mtu wa kawaida kama wewe mwandishi Unaweza kuhoji credibility ya kitabu kilichoandikwa na Nabii mwenye permanent connection na mbingu?? Uwezo wako ungehoji credibility ya vitabu vya Charles Darwin,,au da Vinci.
Soma vizuri mada...... Huyo Nabii Gadi au Nabii Nathan vitabu vyao HAVIPO kwenye Biblia maana kanisa limeviterm vitabu vyao kama Pseudepigrapha/Apocrypha hivyo havitambuliki kwenye Bible na vinahesabika ni vya kipagani tu.

Sasa nikuhoji wwe... Je kwanini basi Biblia inatoa reference kutoka vitabu vya kipagani?? Ila sisi wana JF tukitoa reference kutoka vitabu vya nje ya bible mnakataa hoja zetu??

Tuanzie hapo kwanza
 
Sasa kama Lutu aliweza kulala na binti yake kwanini unaamini daudi hawezi fanya uhuni?? Mbona alimlala mke wa mwanajeshi wake na baadae akamuua kabisa?? Who is David mpaka asifanye huo uhuni??
Ukiona kitabu chenye hayo maelezo basi ndio Unatakiwa uhoji uhalisia wake..Lutu kulala na wanawe sio kigezo cha Daudi kumpiga miti mwanaume mwenzie.Ni dharau iliopita heshima ya mtu
 
Ukiona kitabu chenye hayo maelezo basi ndio Unatakiwa uhoji uhalisia wake..Lutu kulala na wanawe sio kigezo cha Daudi kumpiga miti mwanaume mwenzie.Ni dharau iliopita heshima ya mtu
Sasa kama mtu ana maandiko kwanini mnayakataa kisa hayapo kwenye Biblia ilihali Biblia yenyewe inatuambia habari za Daudi kwa upana wake tutavikuta kwenye vitabu vya Gadi,Nathan n.k ilihali vitabu hivyo vinahesabika ni vya kipagani kwa kanisa???

Yaani kwanini kuna double standards mkuu
 
Soma vizuri mada...... Huyo Nabii Gadi au Nabii Nathan vitabu vyao HAVIPO kwenye Biblia maana kanisa limeviterm vitabu vyao kama Pseudepigrapha/Apocrypha hivyo havitambuliki kwenye Bible na vinahesabika ni vya kipagani tu.

Sasa nikuhoji wwe... Je kwanini basi Biblia inatoa reference kutoka vitabu vya kipagani?? Ila sisi wana JF tukitoa reference kutoka vitabu vya nje ya bible mnakataa hoja zetu??

Tuanzie hapo kwanza
Hivyo vitabu vya nabii Gadi ni vipi? Na ni kanisa gani lililoandika biblia likajua hiki ni kitabu cha nabii gadi au samweli na kuviweka pembeni kwa kuwa vimesemekana vya kipagani??

Wewe unajua history ya uandishi wa biblia?

Unaelewa maana ya kanisa?
 
Sasa kama mtu ana maandiko kwanini mnayakataa kisa hayapo kwenye Biblia ilihali Biblia yenyewe inatuambia habari za Daudi kwa upana wake tutavikuta kwenye vitabu vya Gadi,Nathan n.k ilihali vitabu hivyo vinahesabika ni vya kipagani kwa kanisa???

Yaani kwanini kuna double standards mkuu
Kitabu kilichoandikwa na Nabii wa Mungu wa Ibrahim Isaac na Jakob hakiwezi kuwa cha kipagani..labda hilo kanisa lenye hayo maelezo liwe haya madhehebu ya wachawi na wachumia tumbo wa miaka hii ya karibuni.
 
Nadhani kwa maoni yangu tunajaribu kuigeuza Bibilia kitabu cha kubishania badala ya Kitabu cha mahusiano kati ya Mungu na wanadamu.
Picha kubwa ya biblia ambayo kila mtu anapaswa kuiona ni
1:Mungu aliumba Dunia na Wanadamu wakamilifu.
2:Adam na hawa wakachagua kumsikiliza shetani badala ya kauli ya Mungu na kutuingiza wanadamu wote katika shida japo Wapo kama wakina henoko na Abraham walitembea kwa Imani Mungu akawatukuza.
3:Mungu aliandaa mpango wa Wokovu, Kupitia Yesu Kila amwaminie na kumtii apate uzima wa milele na raha wenda zaidi ya ile ya adam na hawa bustanini baada ya hukumu ya Haki.

Picha kubwa kati ya Pambano la Wema na uovu na hitimisho lake Haipaswi kuhafifishwa na story nyingine yoyote.
Hii inaitoa Bibilia kwenye level ya Kitabu cha Kisomi na kukifanya Kitabu kinachomtambulisha Mungu muumbaji kwa kiumbe chake kilichopotea. Bibilia ni kitabu chenye lengo la kuleta mahusiano kati ya Mwanadamu na Mungu. Hii ndiyo inatakiwa kuwa output ya mtu kusoma bibilia. ie Daily connection with God until restoration.

Kuchimbua mambo ili kuhalalisha au kuharamisha mawazo flani ni kutoka nje ya BIG PICTURE YA KWA NINI BIBILIA.
 
Hivyo vitabu vya nabii Gadi ni vipi? Na ni kanisa gani lililoandika biblia likajua hiki ni kitabu cha nabii gadi au samweli na kuviweka pembeni kwa kuwa vimesemekana vya kipagani??

Wewe unajua history ya uandishi wa biblia?

Unaelewa maana ya kanisa?
Vimeitwa vya kipagani toka kanisa la kwanza AD 300 kuanzia Jerusalem hadi Carthage.... Pia kanisa naongelea mfano Council of Trent iliokuwa kama conference kubwa ya kanisa katoliki ndio ilipitisha baadhi ya vitabu kuwa halali na vingine vikaachwa kama Apocrypha yaani vina kasoro kadhaa hivyo havikidhi viwango vya kuwa kwenye Bible na hata leo vinahesabika kama forgery/Feki na vinahesabika vya kipagani kabisa.

Ndio sasa nauliza kama Vitabu hivi vimatambulika vya kipagani je ni kwanini biblia imevitumia kama reference??

Na kama ww unaviona ni halali je ni kwanini basi havijaingiziwa kwenye biblia??

Na kama havifai na bado biblia imevitumia je ni kwanini tukijengea hoja mnazikataa??

Embu jikite kwenye mada tafadhali na kabla ya kuchangia kajifunze kidogo kuhusu Apocrypha na Pseudepigraphi ili ueleww nachosema
 
Back
Top Bottom