Hujathibitisha hilo. Huu ndio ubaya wa kucopy mambo bila kuelewa mambo na kuyasoma kwa undani.
Tukio lilitokea zama za mtume Muhammad baada ya kuombwa na watu wa Makka afanye muujiza. Mwezi ulishuka kisha ukapasuka vipande kiasi ambacho kwa uwazi ule walikuwa wanauona mlima wa Hira,kwa mapokezi mengine yamepokelewa yakisema kipande kimoja kilikuwa kwake mbali na kipande kingine,kisha ukarudi katika hali yake ya kawaida.
Pili,muujiza hufanywa na Allah na mitume wake na manabii aliowateua ila kwa wachaji Allah ambao tunawaita Mawalii hawa huwa wanakuwa na karama kutenda mambo yasiyo ya kawaida. Hii nimekupa faida na kuna mawalii wa Allah na mawalii wa Shetani.
Lakini hitimisho lako la kuwa kisa ulipasuka na mbona uko mmoja kufikiri huku ni kufikiri kitoto na kukosa maarifa ya ndani,ule ulikuwa ni muujiza na mwezi uko mmoja,kawaida jambo lilitakiwa lifanyike kisha lirudi katika hali yake ya awali na hivi ndivyo walitaka iwe watu wa Makka ili wapate kumuamini mtume wa Allah amani iwe juu yake,kwahiyo jambo likafanyika kama walivyotaka kisha mwezi ukarudi katika hali yake ya kawaida.
Mkiamua kusoma msome kweli. Msitupotezee muda kwa hoja za kitoto na hila za kifadhuli.
Narudi......