Twilumba
JF-Expert Member
- Dec 5, 2010
- 11,540
- 12,398
LANGO KUU LA KUZIMU LA DAR ES SALAAM
Kuzimu ni shimo la giza lililopo duniani katika ulimwengu usiooneka, hapo ndipo yalipo makao makuu ya shetani katika dunia tunayoishi. Shetani ameshikilia tawala za mataifa mengi, anamiliki utajiri na fahari zake zote na humpa ampendaye kwa sharti ni lazima umsujudie.
Lango kuu la kuingilia kuzimu la Upanga Dar es Salaam linajulikana kwa jina la MUSTALLAH. Ndani ya shimo la Mustallah kuna aina kumi na mbili za majini makatili sana yanayoangamiza jamii ya watu wa jiji la Dar es Salaam. Wachawi wa nchi huenda mara kwa mara shimoni kuongeza nguvu za uchawi wao, kabla ya kuingia shimoni ni lazima ufunge kwa siku tatu. Hapa tunajifunza kuwa shetani naye huwa anafunga.
Tuangalie sasa aina za haya majini ya Mustallah na kazi zao.
1. Ratafari ni jini linalosimamia laana zote za ukoo.
Wapo watu wanasema ukoo wetu unasumbuliwa sana na ugonjwa wa pumu, kisukari, presha, kutokuolewa na mambo mengi ambayo utakuta ukoo unakuwa na tatizo moja linalofanana kwa kila mwanaukoo, hili jini ndilo linasimamia laana hizo zimalize ukoo hadi kifo.
2. Muzaphari ni jini linalozuia mafanikio.
Ukitupiwa hili jini, hutaweza kufanya jambo lolote ukafanikiwa. Ukikopa shs 500,000 bank kwa ajili ya kuanza bishara, utafilisika na kuingia kwenye deni, na dhamana yako uliyoweka bank kuuzwa. Ukitaka kujiendeleza kimasomo yatatokea matatizo mengi yatakayosababisha kusimamisha masomo yako.
3. Latifu hili jini linasimamia mambo matatu, ufukara, mateso, na pesa zako kupotea katika mazingara ya ajabu ajabu.
4. Jujan ni jini linalosababisha watu kula udongo.
5. Jahad ni jini la kutorosha mali
Makarani wa bank ndio hasa wanaoadhirika na hili jini, utakuta karani anafanya kazi kwa uangalifu mkubwa, lakini kila siku ana shoti ya pesa. Pia kwenye maduka ya kawaida na hasa supermarket.
6.Hazinan hili jini linalosimamia pombe, uvutaji wa sigara, madawa ya kulevya na mirungi.
7. Jube ni jini linalosimamia utasa, vipimo vya hospitali vitaonyesha kuwa huna tatizo lakini mtoto kamwe hapatikani.
8. Sifafiru hili ni jini linalosimamia ukahaba. Likimwingia mtu yeyote, kwa siku atatembea na watu zaidi ya watano bila hamu ya mapenzi kumalizika.
9. Subian hili ni jini linalosimamia ajali. Chakula cha hili jini ni damu.
Linasababisha wanawake wasipate siku zao, wengine wanapata maumivu makali sana wakiwa katika hedhi, utasikia tumbo linakata kuanzia kushoto kwenda kulia na hali hiyo huendelea kwa muda hadi unanza kusikia maumivu makali ya mgongo.
10. Sumri jini hili linanyonga watoto wakiwa tumboni kabla ya kujifungua, pia linajihusisha na kuchukua watoto hospitali kichawi.
11. Munsar hili ni jini linalosimamia ndoa ya jinsia moja.
mwanamke kwa mwanamke au mwanamume kwa mwanamume.
12. Waidadat hili jini linasababisha vijana wa kiume kuvaa hereni, kusuka nywele na rasta.
Haya majini yamesumbua familia nyingi kwa kiwango cha kutisha, kuyaondoa ni rahisi sana na kwa muda mfupi.
Mkuu simulizi zinatisha... unafanyeje kupona na haya majitu?