Biashara ya Uchawi Tanzania

Biashara ya wanadamu ni kubwa sana inayofanyika katika ulimwengu usioonekana. Vijana na watoto ndio walegwa wakuu katika soko hili haramu.

Watu wengi wamekuwa wakijifariji kwa maneno kama "kazi ya Mungu haina makosa", " Bwana alitoa na Bwana ametwaa Jina la Bwana libarikiwe" , "RIP (Rest in Peace) n.k.

Kwanza ieleweke wazi kuwa MUNGU kamwe hajawahi na hatawahi kuumba au kutengeneza kitu kinachoitwa ugonjwa wa aina yoyote ile kwa ajili ya mwanadamu, narudia hajawahi kabisa kufanya hivyo.

Zipo aina nne, wachawi wa nchi wanazotumia kuhamisha watu kutoka ulimwengu unaoonekana kwenda ulimwengu usioonekana.

1. Utasikia maumivu makali sana ya kuumwa kichwa, sehemu ya mbele ya paja la uso na baada muda mfupi sana utasikia mtu amefariki.
Kinachofanyika ni kuwa, wachawi wanakutumia jini linaingia ndani ya mwili wako, kisha jini linailaza roho yako, na mtu huyo huonekana amekufa, baada ya mazishi, wachawi usiku hufukua kaburi na kukutoa, wanakupulizia dawa za kichawi na lile jini lililoikaba roho yako huachia na kuzinduka. Kisha unaambiwa ukimbie kuelekea pande nne za dunia, baadaye wanakupulizia dawa nyingine ya kukupumbaza na kuondoka na wewe.

2. Usiku utasikia unaitwa jina lako, ukiwa umelala, unapoitika unawafuata hao wachawi waliokuita ukiwa mzima mzima.Ndugu wanabaki kukutafuta polisi, mahospitalini, matangazo kwenye tv na kila mahali lakini kamwe hawatakupata tena.

3. Wachawi wanatengeneza dawa na kukuona ndani ya kioo au TV ya kichawi, kisha huanza kuzungumza na wewe kirafiki wakikumbembeleza sana uonane nao, ukikubali utawafuata mwenyewe popote pale walipo kwa kutembea kwa miguu. Ukifika unakaribishwa, wanakupulizia dawa za kichawi kuondoa ufahamu wako, kisha wanakuvua nguo zote. Kuna dawa wanayokupaka mwili wako mzima kuazia kichwani kwenye nywele hadi chini ya nyayo za miguu, ni lazima dawa hiyo ifunike mwili wako wote, unapotembea nje watu hawakuoni kabisa lakini wewe unawaona.

Kisha huita pepo na kulivika zile nguo zako walizokuvua, lile pepo huchukua sura na umbo lako kabisa, pepo linafanana na wewe kama mapacha. Kisha huliachia hilo pepo na kurudi kule nyumbani kwako ulikotoka, pepo likifika huanza kusingizia ugonjwa, ndugu wanaanza kazi ya kukuuguza, kawaida hilo pepo muda wake wa kuishi ni siku saba tu. Lakini wachawi wanaweza kuliongezea muda ili pesa yenu iendelee kupotea mkiuguza pepo.

4. Wachawi wanachukua roho ya mtu na mwili wake unabaki ukiwa hai.
Wachawi hupendelea sana aina hii ya kuchukua watu, nitajaribu kuelezea nini kinafanyika, na naamini kabisa maelezo nitakayotoa huenda katika familia au watu unaowajua yupo mtu mwenye dalili hizi.

a) Unaweza ukawa na mtoto na anasoma shule na maendeleo yake shuleni ni mazuri sana, siku moja akiwa anarudi nyumbani mtoto akaanguka chini ghafula, baadaye akazinduka na kuamka na akarudi nyumbani, lakini akarudi akijisikia vibaya au anaumwa. Mtoto akatibiwa na kupona kabisa. Lakini baadaye utaona tabia ya mtoto inaanza kubadilika sana, anakuwa mjeuri, maendeleo yake shuleni yanakuwa mabaya, anakuwa mtu wa kusahau na anakuwa ni mtu wa kukumbushwa kila kitu. Mbaya zaidi anapokuwa ni mtoto wa kike wazazi wanahisi mtoto wao kaanza tabia mbaya ya umalaya n.k.

b) Kumetokea kifo katika familia yenu, labda baba amefariki.
Wakati wa kuaga maiti kaka au dada mkubwa au ndugu yeyote anaaguka na kupoteza fahamu, anahudumiwa na anazinduka, lakini akiwa bado katika hali ya maumivu na kuchanganyikiwa na anakuwa amesahau mambo mengi.Siku zinapoendelea hali yake ya afya nayo inazidi kuzorota, anakuwa ni mtu wa kulala kitandani muda wote. Ndugu na marafiki wanaishia kusema kaka yetu kweli alimpenda baba, kiasi kwamba baba alipokufa tu ndiyo siku alianza kuchanganyikwa.

Wachawi wa nchi wanapokusudia kumchukua mtu kwa staili hii, hujitokeza katika hali ya kutokuonekana na watu wengine lakini mhusika huwaona na humpulizia dawa inayoondoa ufahamu wake na ananguka chini, anapoanguka wachawi huchomoa roho yake ndani ya mwili wake, na kwa sababu mwili bila roho hauwezi kuishi, huchukua pepo na kuliingiza ndani ya mwili kisha humpulizia dawa nyingine ya kumzindua.

Pepo aliyeingizwa ndani ya mwili anakuwa hajui chochote alichokuwa akifanya huyo mtu kabla, pepo huanza kujifunza kuishi maisha ya kibinadamu, ndiyo maana kama ni mwanafunzi husahau kila kitu, husahau hata chumba gani alikuwa analala, na magonjwa kwa huyo mtu huwa hayaishi.
 
Mkuu wewe umejuaje mambo ya uchawi kama simteja wao mbona hujajitaja lazima utakuwa mteja wamekulia sana mshiko jama ndo umekuja nayo hii mana hapa watu wengi waliwa baadae ndo wanasuka lakini tayari kisu kimepita

Mikoa saba nchini Tanzania ndiyo tishio kwa kuwa na nguvu kubwa za uchawi
1. Tanga ndio kinara
2. Lindi unafuatilia
3. Dar es Salaam
4. Mtwara
5. Tabora
6. Kigoma
7. Mwanza

Mikoa yenye wachawi wengi, kwa maana kwamba karibu kila kaya kuna mchawi
1. Sumbawanga (Rukwa) ndio kinara
2. Ruvuma inafuatialia
3. Mbeya
4. Singida

Mikoa ambayo wananchi wake ndio wateja wakuu wa wachawi
1. Kilimanjaro inaongoza
2. Morogoro inafuatilia
3. Kagera

Wateja wengine wa wachawi
1. Wafanyabiashara
2. Wasanii
3. Kina mama wa nyumbani
4. Wanafunzi wa shule za sekondari hasa wa kidato cha pili.
 
Wacheza mpira huu wa kibongo inakuwaje?

Hao ndiyo usiseme, ni dunia nzima!

Kulikuwa hata na program niliiona kwenye BBC iliyokuwa inazungumzia uchawi kwenye soccer, yule jamaa mtangazaji aliwarekodi kwa siri basi hivo vituko vilikuwa kichekesho cha aina yake.
 
dah umenikumbusha kituko kiomja hivi kuna jamaa alikuwa anafanya kazi kampuni ya abood bus service yule jamaa alipikiwa majungu na wenzake na mkuu wao akamfukuza jamaa kazi basi huyu jamaa aliyechukua nafasi ya mwenzake alipokaa kwenye siti tu inasemekana alikua anatokwa na majipu mwilini akishuka yanapotea,

Acheni masihara, gusa madereva gov, wakienda likizo gari agusi mtu, mhh na Musoma vijijini kewtu huku mhh ni noumer
 
dah umenikumbusha kituko kiomja hivi kuna jamaa alikuwa anafanya kazi kampuni ya abood bus service yule jamaa alipikiwa majungu na wenzake na mkuu wao akamfukuza jamaa kazi basi huyu jamaa aliyechukua nafasi ya mwenzake alipokaa kwenye siti tu inasemekana alikua anatokwa na majipu mwilini akishuka yanapotea,
Du hii kali na hatari!
 
Umeikosea Kigoma hyo haikosi top 3. Ni hatar kwa uchawi radi zinauzwa kuanzia 50tsh, kuna kijiji chaitwa Nyamnyusi ni balaa. Unafikiri y waganga wanatoka Sumbawanga, Kigoma na Tanga then wengne wanafuatia? Huko Ujiji kuna international staff aliibiwa laptop akaenda kwa mganga maarufu akamwambia yeye anaua tu sio kurudisha kitu. Iringa nao hawajambo hasa wakinga, wapangwa wana kitu kinaitwa tego ukiiba wanateketeza hadi vijukuu na vitukuu, mifugo na kila unachomiliki.
 
kigoma ilikua zamani kuna kijiji nliambiwa kinaitwa Makere-ushingo-wilaya ya Kibondo. .... unanunua radi na majaribio wayafanya hapo hapo....

Mkuu Makere ipo wilaya ya kasulu, hadi leo radi zipo kuanzia 50tsh na hazikopeshi, magraduate huwa wanapiga radi .kuonyeshana maskilz.
 
jamaa yangu mmoja aliwahi simulia habari ya kgm inatisha, anasema aliingia chini ya maji ziwani na kumkuta mwenyejiwao lakini sehemu hiyo ya chini ilikuwa kavu tu -

alipelekwa na kigagula kilichokuwa kimemuhusudu tu kwa kuona aina ya mabangili aliyokuwa anavaa mkono wa kushoto(kama wamaasai), jamaa yangu huyo ana asili ya south africa, aliondoka kwao kipindi cha machafuko ya 76 akawa mkimbizi. kwa sasa yupokwao serikali imemsaidia kuseto.

simulizi hiyo ni ndefu na ya kusisimua sana.


Amani yetu inatumiwa vibaya.
 
lisemwalo lipo,similar tukio nililisikia 1987 kwa mchungaji mmoja ambaye alitokea huko kigoma na kuokoka :)
jamaa yangu mmoja aliwahi simulia habari ya kgm inatisha, anasema aliingia chini ya maji ziwani na kumkuta mwenyejiwao lakini sehemu hiyo ya chini ilikuwa kavu tu -

alipelekwa na kigagula kilichokuwa kimemuhusudu tu kwa kuona aina ya mabangili aliyokuwa anavaa mkono wa kushoto(kama wamaasai), jamaa yangu huyo ana asili ya south africa, aliondoka kwao kipindi cha machafuko ya 76 akawa mkimbizi. kwa sasa yupokwao serikali imemsaidia kuseto.

simulizi hiyo ni ndefu na ya kusisimua sana.


Amani yetu inatumiwa vibaya.
 
Majimoto, hii simulizi yako niliiangalia kwenye kipindi cha This is my story cha ATN itakuwa ndiyo DVD uimeitaja? Jamaa alisimulia maisha yake mpaka unaogopa.Kweli tunamuhitaji YESU atulinde maana Yeye peke yake ndiye kiboko cha wachawi na majini.
 
jamaa yangu mmoja aliwahi simulia habari ya kgm inatisha, anasema aliingia chini ya maji ziwani na kumkuta mwenyejiwao lakini sehemu hiyo ya chini ilikuwa kavu tu -

alipelekwa na kigagula kilichokuwa kimemuhusudu tu kwa kuona aina ya mabangili aliyokuwa anavaa mkono wa kushoto(kama wamaasai), jamaa yangu huyo ana asili ya south africa, aliondoka kwao kipindi cha machafuko ya 76 akawa mkimbizi. kwa sasa yupokwao serikali imemsaidia kuseto.

simulizi hiyo ni ndefu na ya kusisimua sana.


Amani yetu inatumiwa vibaya.
Inapatikana wapi hiyo simulizi?
 
Malaika Watakatifu, shetani, na majini ni baadhi ya viumbe wanaoishi kwenye ulimwengu usioonekana. Watu wengi wamekuwa wakifikiri kuwa ulimwengu usioonekana uko mbali sana na ulimwengu huu tunaoishi, ukweli ni kwamba wote tunaishi ulimwengu mmoja na barabarani huwa tunapishana, ingawa sisi hatuwaoni, lakini wao wanatuona kwa kila jambo tunalolifanya.

Shetani anayo majeshi yake makubwa ajabu, kwa mfano hapo ulipo sasa kuna jeshi la shetani lenye askari wapatao 500 hadi 1000, wakigojea amri ya kushambulia, kuumiza na kuuwa.

Wachawi wa nchi huwatumia sana hawa majini katika kutimiza dhamira zao mbaya za kudhuru maisha ya binadamu wenzao. Kimsingi hakuna tofauti kati ya wanaoitwa waganga wa kienyeji na wachawi (ni sawasawa na unaposema kuna askari na kuna polisi, wote ni walewale), watu wanapowaendea hawa wachawi kuaguliwa, huanza kwa kupiga manyanga na kuimba nyimbo za kichawi, wimbo huo ni wa kuita jini la utambuzi na tafasiri. Mtu anapowaza jambo fulani katika ulimwengu unaoonekana, katika ulimwengu usioonekana unaoongea kwa sauti kubwa kweli kweli, hili jini la utambuzi likifika linakaa karibu na wewe na kusikiliza kile unachowaza na kumweleza mchawi kwa lugha zao za kijini. Machawi akishaelezwa tatizo lako na jini, huanza kukueleza matatizo yako bila ya kukuuliza maswali yeyote, na watu wengi wamekuwa wakiishia kuwasifia sana hawa wachawi kuwa kabla hujasema anakuambia matatizo yako, asijue kuwa yeye mwenyewe ndiye aliyekuwa akiongea kwa kuwaza.

Kama umetupiwa jini, hawa wachawi hawana uwezo wa kuyaondoa majini yaliyowekwa mwilini mwako. Wanachofanya wanachukua jini mwingine mkubwa zaidi ya yule aliye ndani ya mwili wako, na anaelekezwa amtulize huyu jini asiendelee kufanya madhara ndani ya mwili wako. Jini mgeni naye inafika wakati anabadili tabia na kuanza kushambulia mwili wako, unapowaendea hawa wachawi wa nchi unavishwa jini mwenye nguvu zaidi kuwatuliza majini walio ndani ya mwili wako.

Kadri unavyowaendea wachawi ndivo unaondoka na mtaji wa majini mengi mwilini mwako.
 
unatisha mkuu,endelea kutoa nondoz,sijui unazitoa wapi?can we share u r source of this infor
Malaika Watakatifu, shetani, na majini ni baadhi ya viumbe wanaoishi kwenye ulimwengu usioonekana. Watu wengi wamekuwa wakifikiri kuwa ulimwengu usioonekana uko mbali sana na ulimwengu huu tunaoishi, ukweli ni kwamba wote tunaishi ulimwengu mmoja na barabarani huwa tunapishana, ingawa sisi hatuwaoni, lakini wao wanatuona kwa kila jambo tunalolifanya.

Shetani anayo majeshi yake makubwa ajabu, kwa mfano hapo ulipo sasa kuna jeshi la shetani lenye askari wapatao 500 hadi 1000, wakigojea amri ya kushambulia, kuumiza na kuuwa.

Wachawi wa nchi huwatumia sana hawa majini katika kutimiza dhamira zao mbaya za kudhuru maisha ya binadamu wenzao. Kimsingi hakuna tofauti kati ya wanaoitwa waganga wa kienyeji na wachawi (ni sawasawa na unaposema kuna askari na kuna polisi, wote ni walewale), watu wanapowaendea hawa wachawi kuaguliwa, huanza kwa kupiga manyanga na kuimba nyimbo za kichawi, wimbo huo ni wa kuita jini la utambuzi na tafasiri. Mtu anapowaza jambo fulani katika ulimwengu unaoonekana, katika ulimwengu usioonekana unaoongea kwa sauti kubwa kweli kweli, hili jini la utambuzi likifika linakaa karibu na wewe na kusikiliza kile unachowaza na kumweleza mchawi kwa lugha zao za kijini. Machawi akishaelezwa tatizo lako na jini, huanza kukueleza matatizo yako bila ya kukuuliza maswali yeyote, na watu wengi wamekuwa wakiishia kuwasifia sana hawa wachawi kuwa kabla hujasema anakuambia matatizo yako, asijue kuwa yeye mwenyewe ndiye aliyekuwa akiongea kwa kuwaza.

Kama umetupiwa jini, hawa wachawi hawana uwezo wa kuyaondoa majini yaliyowekwa mwilini mwako. Wanachofanya wanachukua jini mwingine mkubwa zaidi ya yule aliye ndani ya mwili wako, na anaelekezwa amtulize huyu jini asiendelee kufanya madhara ndani ya mwili wako. Jini mgeni naye inafika wakati anabadili tabia na kuanza kushambulia mwili wako, unapowaendea hawa wachawi wa nchi unavishwa jini mwenye nguvu zaidi kuwatuliza majini walio ndani ya mwili wako.

Kadri unavyowaendea wachawi ndivo unaondoka na mtaji wa majini mengi mwilini mwako.
 
Inapatikana wapi hiyo simulizi?


Mkuu katavi, kwanza samahani kwa kuchelewesha majibu. ukweli ni kwamba simulizi hiyo haikuwahi kuandikwa na msilimuliaji, hivyo inapatikana kwake mwenyewe na aliopata kuwasimulia. mimi niliamini kwa kuwa huyo ndugu aliwahi kukaa kwangu wakati akifanya mipango ya kurejea kwao, niligundua alikuwa msema kweli na mwaminifu sana.


Amani yetu inatumiwa vibaya.
 
LANGO KUU LA KUZIMU LA DAR ES SALAAM

Kuzimu ni shimo la giza lililopo duniani katika ulimwengu usiooneka, hapo ndipo yalipo makao makuu ya shetani katika dunia tunayoishi. Shetani ameshikilia tawala za mataifa mengi, anamiliki utajiri na fahari zake zote na humpa ampendaye kwa sharti ni lazima umsujudie.

Lango kuu la kuingilia kuzimu la Upanga Dar es Salaam linajulikana kwa jina la MUSTALLAH. Ndani ya shimo la Mustallah kuna aina kumi na mbili za majini makatili sana yanayoangamiza jamii ya watu wa jiji la Dar es Salaam. Wachawi wa nchi huenda mara kwa mara shimoni kuongeza nguvu za uchawi wao, kabla ya kuingia shimoni ni lazima ufunge kwa siku tatu. Hapa tunajifunza kuwa shetani naye huwa anafunga.

Tuangalie sasa aina za haya majini ya Mustallah na kazi zao.

1. Ratafari ni jini linalosimamia laana zote za ukoo.
Wapo watu wanasema ukoo wetu unasumbuliwa sana na ugonjwa wa pumu, kisukari, presha, kutokuolewa na mambo mengi ambayo utakuta ukoo unakuwa na tatizo moja linalofanana kwa kila mwanaukoo, hili jini ndilo linasimamia laana hizo zimalize ukoo hadi kifo.

2. Muzaphari ni jini linalozuia mafanikio.
Ukitupiwa hili jini, hutaweza kufanya jambo lolote ukafanikiwa. Ukikopa shs 500,000 bank kwa ajili ya kuanza bishara, utafilisika na kuingia kwenye deni, na dhamana yako uliyoweka bank kuuzwa. Ukitaka kujiendeleza kimasomo yatatokea matatizo mengi yatakayosababisha kusimamisha masomo yako.

3. Latifu hili jini linasimamia mambo matatu, ufukara, mateso, na pesa zako kupotea katika mazingara ya ajabu ajabu.

4. Jujan ni jini linalosababisha watu kula udongo.

5. Jahad ni jini la kutorosha mali
Makarani wa bank ndio hasa wanaoadhirika na hili jini, utakuta karani anafanya kazi kwa uangalifu mkubwa, lakini kila siku ana shoti ya pesa. Pia kwenye maduka ya kawaida na hasa supermarket.

6.Hazinan hili jini linalosimamia pombe, uvutaji wa sigara, madawa ya kulevya na mirungi.

7. Jube ni jini linalosimamia utasa, vipimo vya hospitali vitaonyesha kuwa huna tatizo lakini mtoto kamwe hapatikani.

8. Sifafiru hili ni jini linalosimamia ukahaba. Likimwingia mtu yeyote, kwa siku atatembea na watu zaidi ya watano bila hamu ya mapenzi kumalizika.

9. Subian hili ni jini linalosimamia ajali. Chakula cha hili jini ni damu.
Linasababisha wanawake wasipate siku zao, wengine wanapata maumivu makali sana wakiwa katika hedhi, utasikia tumbo linakata kuanzia kushoto kwenda kulia na hali hiyo huendelea kwa muda hadi unanza kusikia maumivu makali ya mgongo.

10. Sumri jini hili linanyonga watoto wakiwa tumboni kabla ya kujifungua, pia linajihusisha na kuchukua watoto hospitali kichawi.

11. Munsar hili ni jini linalosimamia ndoa ya jinsia moja.
mwanamke kwa mwanamke au mwanamume kwa mwanamume.

12. Waidadat hili jini linasababisha vijana wa kiume kuvaa hereni, kusuka nywele na rasta.

Haya majini yamesumbua familia nyingi kwa kiwango cha kutisha, kuyaondoa ni rahisi sana na kwa muda mfupi.
 
Duh! kwa hiyo ile story ya Manyoya pale salender ni ukweli.inamaana ni karibu na kituo cha police salenda bridge
Lango la Mustallah liko baharini kati ya daraja la Salenda na bomba kubwa la maji machafu lililoingia ndani ya bahari.
 
Back
Top Bottom