Biashara ya Uchawi Tanzania

Maji Moto!
Where the hell do you get all this information?
Do you dream, are you getting it from your sunday school?
Please come up with an answer. Am deadly scared.
my bed is full of dolls. my sitting also. Ina maana naishi na majini?

Ndugu yangu Mlachake,
Kuwepo au kutokuwepo kwa majini nyumbani kwako, inatengemea nguvu uliyonayo kwenye ulimwengu usioonekana
.
 
Watawala wa Taifa la Tanzania, kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, walifanya kila aina ya mbinu chafu za kuimarisha utawala wao, ili waweze tena kuongoza taifa la Tanzania.

Nimesema walifanya mbinu chafu zenye makufuru makubwa, na katika ulimwengu usiooneka walionekana waziwazi waliyokuwa wakiyafanya.

Moja ya kufuru walilofanya ni kuwekwa ndani ya majeneza na kushushwa makaburini, ambako walilala huko usiku mzima, huku wachawi wa nchi wakicheza uchi wa nyama juu ya makaburi hayo. Kisha waliapishwa na majini.

Lakini kibao kiligeuzwa ghafula katika ulimwengu usiooneka baada ya kuingiliwa na kundi kubwa la wanadamu waliokuwa wanamlilia Mwenyenzi Mungu juu ya hatima ya baadaye ya taifa la Tanzania.

Katika ulimwengu usioonekana, utawala uliokuwa ukioonekana kama mlima Kilimanjaro, uligeuzwa kichwa chini miguu juu, ulisagwasagwa, ukasambaratishwa kutoka jiwe la mlima hadi kuwa mavumbi matupu.

Kimsingi utawala wa taifa la Tanzania ulioliongoza taifa hili kutoka mwaka 1961 ulikoma rasmi mwezi Septemba 2010 katika ulimwengu usioonekana.

Kazi inayoendelea sasa ni kufanya yale yaliyotendeka katika ulimwengu usioonekana, yadhihirike katika ulimwengu unaooneka. Kawaida nguvu ya mtu au ya taifa ipo katika ulimwengu usioonekana, na matokeo yake hujitokeza taratibu kwenye ulimwengu unaoonekana.

Kwa sababu taifa la Tanzania kwa sasa hivi halipo kabisa katika ulimwengu usioonekana, yapo mambo kadhaa ambayo ni lazima yajitokeze katika ulimwengu unaoonekana.

a) Watawala walioondolewa katika ulimwengu usioonekana, kila jambo watakalojaribu kulifanya au kutenda katika ulimwengu unaoonekana wataishia kwenye aibu ya kukata na shoka.

b) Mambo hayo ya aibu yatakuwa yanafuta hati yao batili ya utawala polepole kwenye utawala unaoonekana.

c) Mwenyenzi Mungu hawezi kusimamisha utawala mpya kwenye utawala uliofanya makufuru makubwa kiasi hicho hadi, utawala huo ufutike kabisa katika ulimwengu unaooneka kama ulivyogeuzwa mavumbi katika ulimwengu usioonekana.

d) Njaa italiandama taifa, kwa sababu Mungu amegeuka, uso wake haupo tena juu ya taifa hili hadi makufuru yaliyofanyika yafutike.

e) Waliofanya makufuru hayo wajitayarishe kwa hasira kali ya Mwenyenzi Mungu.

Hili jambo ni hakika na kweli, na litatimia kwa asilimia 100%
 
Watawala wa Taifa la Tanzania, kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, walifanya kila aina ya mbinu chafu za kuimarisha utawala wao, ili waweze tena kuongoza taifa la Tanzania.

Nimesema walifanya mbinu chafu zenye makufuru makubwa, na katika ulimwengu usiooneka walionekana waziwazi waliyokuwa wakiyafanya.

Moja ya kufuru walilofanya ni kuwekwa ndani ya majeneza na kushushwa makaburini, ambako walilala huko usiku mzima, huku wachawi wa nchi wakicheza uchi wa nyama juu ya makaburi hayo. Kisha waliapishwa na majini.

Lakini kibao kiligeuzwa ghafula katika ulimwengu usiooneka baada ya kuingiliwa na kundi kubwa la wanadamu waliokuwa wanamlilia Mwenyenzi Mungu juu ya hatima ya baadaye ya taifa la Tanzania.

Katika ulimwengu usioonekana, utawala uliokuwa ukioonekana kama mlima Kilimanjaro, uligeuzwa kichwa chini miguu juu, ulisagwasagwa, ukasambaratishwa kutoka jiwe la mlima hadi kuwa mavumbi matupu.

Kimsingi utawala wa taifa la Tanzania ulioliongoza taifa hili kutoka mwaka 1961 ulikoma rasmi mwezi Septemba 2010 katika ulimwengu usioonekana.

Kazi inayoendelea sasa ni kufanya yale yaliyotendeka katika ulimwengu usioonekana, yadhihirike katika ulimwengu unaooneka. Kawaida nguvu ya mtu au ya taifa ipo katika ulimwengu usioonekana, na matokeo yake hujitokeza taratibu kwenye ulimwengu unaoonekana.

Kwa sababu taifa la Tanzania kwa sasa hivi halipo kabisa katika ulimwengu usioonekana, yapo mambo kadhaa ambayo ni lazima yajitokeze katika ulimwengu unaoonekana.

a) Watawala walioondolewa katika ulimwengu usioonekana, kila jambo watakalojaribu kulifanya au kutenda katika ulimwengu unaoonekana wataishia kwenye aibu ya kukata na shoka.

b) Mambo hayo ya aibu yatakuwa yanafuta hati yao batili ya utawala polepole kwenye utawala unaoonekana.

c) Mwenyenzi Mungu hawezi kusimamisha utawala mpya kwenye utawala uliofanya makufuru makubwa kiasi hicho hadi, utawala huo ufutike kabisa katika ulimwengu unaooneka kama ulivyogeuzwa mavumbi katika ulimwengu usioonekana.

d) Njaa italiandama taifa, kwa sababu Mungu amegeuka, uso wake haupo tena juu ya taifa hili hadi makufuru yaliyofanyika yafutike.

e) Waliofanya makufuru hayo wajitayarishe kwa hasira kali ya Mwenyenzi Mungu.

Hii ni jambo ni hakika na kweli, na limeshafanyika kwa asilimia 100 (%)

I have always been a big fan of this thread, Lakini sasa huku inakoelekea sijui ni wapi? majimoto unapatikana wapi?
 
sasa hivi zipo shule kabisa za kufundisha uchawi nchini tanzania, shule moja ipo temeke masomo yake huchukua miaka saba hadi unahitimu.

Ukimaliza temeke, unaweza kujiunga na elimu ya juu katika fani ya uchawi, chuo kipo tanga hapo wanatoa digrii ya kwanza ya uchawi kwa miaka mitano.

Wanatoa pia digrii ya pili ya elimu ya ulozi ambapo utakaa darasani kwa miaka mingine mitano.

Master digrii ya ulozi, bado hapa nchini hakuna chuo, inapidi uende mombasa nchini kenya ndipo kilipo chuo kikuu cha elimu ya ulozi.
mkuu umezungumzia elimu ya juu zaidi vip hiyo miaka 7 ni ya primary na secondary au imekaaje hapa? Na yote haya umeyajuaje? kama kuna mchawi hapa naomba anitambue kuwa mimi ni nani?? Make nasikia wananguvu hizo!
 
Watawala wa Taifa la Tanzania, kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, walifanya kila aina ya mbinu chafu za kuimarisha utawala wao, ili waweze tena kuongoza taifa la Tanzania.

Nimesema walifanya mbinu chafu zenye makufuru makubwa, na katika ulimwengu usiooneka walionekana waziwazi waliyokuwa wakiyafanya.

Moja ya kufuru walilofanya ni kuwekwa ndani ya majeneza na kushushwa makaburini, ambako walilala huko usiku mzima, huku wachawi wa nchi wakicheza uchi wa nyama juu ya makaburi hayo. Kisha waliapishwa na majini.

Lakini kibao kiligeuzwa ghafula katika ulimwengu usiooneka baada ya kuingiliwa na kundi kubwa la wanadamu waliokuwa wanamlilia Mwenyenzi Mungu juu ya hatima ya baadaye ya taifa la Tanzania.

Katika ulimwengu usioonekana, utawala uliokuwa ukioonekana kama mlima Kilimanjaro, uligeuzwa kichwa chini miguu juu, ulisagwasagwa, ukasambaratishwa kutoka jiwe la mlima hadi kuwa mavumbi matupu.

Kimsingi utawala wa taifa la Tanzania ulioliongoza taifa hili kutoka mwaka 1961 ulikoma rasmi mwezi Septemba 2010 katika ulimwengu usioonekana.

Kazi inayoendelea sasa ni kufanya yale yaliyotendeka katika ulimwengu usioonekana, yadhihirike katika ulimwengu unaooneka. Kawaida nguvu ya mtu au ya taifa ipo katika ulimwengu usioonekana, na matokeo yake hujitokeza taratibu kwenye ulimwengu unaoonekana.

Kwa sababu taifa la Tanzania kwa sasa hivi halipo kabisa katika ulimwengu usioonekana, yapo mambo kadhaa ambayo ni lazima yajitokeze katika ulimwengu unaoonekana.

a) Watawala walioondolewa katika ulimwengu usioonekana, kila jambo watakalojaribu kulifanya au kutenda katika ulimwengu unaoonekana wataishia kwenye aibu ya kukata na shoka.

b) Mambo hayo ya aibu yatakuwa yanafuta hati yao batili ya utawala polepole kwenye utawala unaoonekana.

c) Mwenyenzi Mungu hawezi kusimamisha utawala mpya kwenye utawala uliofanya makufuru makubwa kiasi hicho hadi, utawala huo ufutike kabisa katika ulimwengu unaooneka kama ulivyogeuzwa mavumbi katika ulimwengu usioonekana.

d) Njaa italiandama taifa, kwa sababu Mungu amegeuka, uso wake haupo tena juu ya taifa hili hadi makufuru yaliyofanyika yafutike.

e) Waliofanya makufuru hayo wajitayarishe kwa hasira kali ya Mwenyenzi Mungu.

Hili jambo ni hakika na kweli, na litatimia kwa asilimia 100%
I'm speechless!!
 
I'm speechless!!

Duh jamaa deep na logical, sasa maisha ya watu wa kawaida ambao hawana uwezo wa maono ya ulimwengu usioonekana wataponaje na haya mambo?

Kama vile kuondokana na hizi nuksi?
 
uchawi upo dunia kama huamini nenda kibaha maili moja kafungue biashara yoyote pale kama utafanikiwa kwani kuna kabila linaitwa wagweno balaa,kibaha nzima wanafanya biashara wao ukienda mtu mwingine hufanyi biashara
 
Mikoa yenye wachawi wengi, kwa maana kwamba karibu kila kaya kuna mchawi
1. Sumbawanga (Rukwa) ndio kinara
2. Ruvuma inafuatialia
3. Mbeya
4. Singida

Nimesikitika sana hapo kwenye red na nimekuwa disapointed sana, sikutegemea.
 
Mikoa saba nchini Tanzania ndiyo tishio kwa kuwa na nguvu kubwa za uchawi
1. Tanga ndio kinara
2. Lindi unafuatilia
3. Dar es Salaam
4. Mtwara
5. Tabora
6. Kigoma
7. Mwanza

Mikoa yenye wachawi wengi, kwa maana kwamba karibu kila kaya kuna mchawi
1. Sumbawanga (Rukwa) ndio kinara
2. Ruvuma inafuatialia
3. Mbeya
4. Singida

Mikoa ambayo wananchi wake ndio wateja wakuu wa wachawi
1. Kilimanjaro inaongoza
2. Morogoro inafuatilia
3. Kagera

Wateja wengine wa wachawi
1. Wafanyabiashara
2. Wasanii
3. Kina mama wa nyumbani
4. Wanafunzi wa shule za sekondari hasa wa kidato cha pili.

Wapi Iringa???, wApi Mafia, wapi Waalimu wa shule za sec na Msingi, MH.
 
uchawi upo dunia kama huamini nenda kibaha maili moja kafungue biashara yoyote pale kama utafanikiwa kwani kuna kabila linaitwa wagweno balaa,kibaha nzima wanafanya biashara wao ukienda mtu mwingine hufanyi biashara
Wagweno!!! Ndio wa wapi hao!
 
Hili lisredi linakufa halafu linafufuka. Huyu maxence nae tulishamwomba jukwaa la uchawi na wanga ila sijui hajasikia.
 
Lango la Kuzimu la IGOSI, NJOMBE

Igosi ni mojawapo ya tarafa zinazounda wilaya ya Njombe (sasa hivi Njombe ni mkoa) ikiwa na idadi ya wakazi wanaokaribia kufikia alfu thelathini. Tarafa hii ya Igosi ndipo lilipo lango la kuzimu linalojulikana kama TWAFIFIRI.

Kwenye langu hili la Twafifiri kuna majini yanahudumia wachawi wa nchi yafuatayo:-

1. Zubedari ni jini linalosimamia uongo na uzushi, kama unaye rafiki au ndugu yako aliye muongo kupindukia basi tatizo lake ni hili jini.

2. Abadi ni jini linalosimamia umasikini, umalaya na wizi.

3. Muzafiri hili ni jini la matambiko ya Kiarabu. Inatokea familia ikajaliwa kupata mtoto, ikifika usiku huyu mtoto atalia usiku kucha, hadi apewe jina na babu au bibi wa ukoo aliyekufa miaka mingi.

4. Muhuduri ni jini linalosimamia umasikini, umalaya na wizi.

5. Luhadhiri ni jini linalosimamia umasikini, umalaya na wizi.

6. Uswabi ni jini linalosimamia umasikini, umalaya na wizi.

7. Jaitaba ni jini linalosimamia umasikini, umalaya na wizi.

8. Dubuwao ni jini linalo simamia umasikini, umalaya na wizi.

9. Rizat ni jini linalosimamia umasikini, umalaya na wizi.

10 Ashuran ni jini linalosimamia utasa na maradhi ya akina mama

Hili lango ta Twafifiri majini yake karibu yote yanasimamia matatizo yanayofanana, kufanya watu wawe masikini, kuwafanya wawe malaya wa kutupwa na wezi.
 
Lango la Kuzimu la IGOSI, NJOMBE

Igosi ni mojawapo ya tarafa zinazounda wilaya ya Njombe (sasa hivi Njombe ni mkoa) ikiwa na idadi ya wakazi wanaokaribia kufikia alfu thelathini. Tarafa hii ya Igosi ndipo lilipo lango la kuzimu linalojulikana kama TWAFIFIRI.

Kwenye langu hili la Twafifiri kuna majini yanahudumia wachawi wa nchi yafuatayo:-

1. Zubedari ni jini linalosimamia uongo na uzushi, kama unaye rafiki au ndugu yako aliye muongo kupindukia basi tatizo lake ni hili jini.

2. Abadi ni jini linalosimamia umasikini, umalaya na wizi.

3. Muzafiri hili ni jini la matambiko ya Kiarabu. Inatokea familia ikajaliwa kupata mtoto, ikifika usiku huyu mtoto atalia usiku kucha, hadi apewe jina na babu au bibi wa ukoo aliyekufa miaka mingi.

4. Muhuduri ni jini linalosimamia umasikini, umalaya na wizi.

5. Luhadhiri ni jini linalosimamia umasikini, umalaya na wizi.

6. Uswabi ni jini linalosimamia umasikini, umalaya na wizi.

7. Jaitaba ni jini linalosimamia umasikini, umalaya na wizi.

8. Dubuwao ni jini linalo simamia umasikini, umalaya na wizi.

9. Rizat ni jini linalosimamia umasikini, umalaya na wizi.

10 Ashuran ni jini linalosimamia utasa na maradhi ya akina mama

Hili lango ta Twafifiri majini yake karibu yote yanasimamia matatizo yanayofanana, kufanya watu wawe masikini, kuwafanya wawe malaya wa kutupwa na wezi.


Haya mkuu maji moto, je kuhusu malango ya tabra na kigoma? effect yake ni nini kwa watu wa karibu na hayo malango na je kuna mambo yoyote au dalili za kujua kuwa kuna nguvu za giza kwenye maeneo hayo? yaani najaribu kuvuta picha kama soko kuu la tbr, wanaofanya biashara mle hawatadhurika?

Amani yetu inatumiwa vibaya.
 
Hapa ndio naona umuhimu wa kumrudia Bwana.

Pombe nimeacha, Halafu sijaona jini la ulevi kwenye List. Hivi m2 unapata kiu ya bia mpaka unakosa usingizi sio majini yamekutawala kweli. maji moto hebu saidia hapa.

Kama haya majini ya ulevi yapo, Nimetokea kuacha Pombe ghafla kwa maamuzi yangu binafsi, ina maana hilo jini la Pombe lilijiondokea.

Msaada wako majimoto
 
Uchawi ni kazi inayofanyika kwa usiri mkubwa sana, endapo mchawi atatoa siri za wachawi wenzake adhabu yake huwa ni kifo. Ni vigumu sana kumtambua mchawi, licha ya baadhi ya makabila kuwashuku akina mama wazee wenye macho mekundu kuwa ndio wachawi, lakini ukweli siyo wachawi. Madhalani mkeo/mumeo anaweza akawa mchawi wa kutupwa lakini usiweze kumtambua kabisa.

Kawaida matayarisho ya kwenda kuwanga huanza jioni ya saa kumi na mbili hadi saa mbili usiku, kwa kuchoma ubani na kuomba dua, wachawi wanayo roho ya uchawi ndani yao, ambayo ikifika saa sita usiku, hiyo roho ya uchawi iliyo ndani yake humwamsha. Wachawi wanakuwa na madhabahu zao za kukutanikia usiku, kwa mfano wachawi wa Kariakoo wanayo madhabahu yao, wachawi wa Masaki wanayo madhabahu yao, Wachawi wa Mwananyamala madhabahu yao iko ndani ya hospitali ya Mwananyamala, ndiyo maana vitimbi ndani ya hospitali hiyo haviwezi kwisha bila ya kuivunja na kuisambaratisha hiyo madhabahu.

Mchawi anapoamka usiku wa manane huenda kwenye madhabahu yao, na kila madhabahu ina mwenyekiti na katibu wa kuandika taarifa za kikao. Kazi ya kikao ni kupokea mashitaka kutoka kwa wajumbe, kuyajadili na kuyafanyia maamuzi. Kwa mfano, mchawi anaweza kuleta shitaka kuwa jirani yake XYZ kila siku wanakaanga nyama na samaki, watoto wake wanasoma shule nzuri, na wanaringa sana. Hilo ni shitaka tosha la kujadiliwa kwenye madhabahu za wachawi.

Wachawi wakimaliza kumjadili ndungu XYZ, wanapanga adhabu ya kumwadabisha, adhabu inaweza kuwa, wamtupie mume jini afukuzwe kazi, au wampindishe mama miguu asiweze kutembea. Wakishachagua adhabu, huteua kamati ya utekelezaji ambayo, itahakikisha familia hiyo inaadhibiwa haraka iwezekanavyo. Idadi ya wajumbe inategemea ukubwa wa kazi, lakini mara nyingi huwa ni wachawi kati ya watatu hadi sita.

Wachawi huanza kazi ya ulozi nyumbani kwako, kwa kawaida muda wa kufanya ulozi ni kuanzia saa sita usiku hadi saa tisa usiku, kama siku hiyo hawakufanikiwa kuingia hadi saa tisa usiku, shughuli huairishwa hadi siku inayofuata, roho ya uchawi waliyo nayo huwafanya wachawi kupenya kwenye ukuta, kwa kupitia kwenye kona ya chumba. Wachawi wakikuta mtuhumiwa ni mcha Mungu mzuri huwa wanashindwa kumkaribia kwani mwili wake huwa unawaka moto, wakikuta familia yote haishikiki, basi kikao hungeuza adhabu kwenda kwa mfanyakazi wa ndani, biashara yako, au kwa ndungu zako wa karibu.

Wachawi wakikuta familia iko tupu, kazi ya ulozi huwa ni nyepesi sana, na matokeo yake huonekana mapema.
 
ZAZUNI Lango la kuzimu la Bagamoyo

Mji wa Bagamoyo ni mji wa kizamani uliokaliwa na Waarabu, na maendeleo yake yalikuwa duni sana hadi siku za hivi karibuni, wageni walipoanza kuingia na kuwekeza katika mji huo.

Lango la kuzimu la Zazuni liko ufukweni mwa bahari ya Hindi, likihudumiwa na majini kumi na mawili.



1. Ruyat ni jini linalosimamia ndoto mbaya

2. Al-Rahab ni jini linalosimamia shoti ya umeme na majanga ya moto, mfano wa majanga ya moto yaliyotokea katika mabweni ya kulala wanafunzi katika shule nyingi, jini hili lilihusika na kuwachukua watoto kuwapeleka msukuleni. Watoto hawa wote wapo hai, tangu vita hivi vya shetani vilipoanza mkoani Kilimanjaro katika shule ya wasichana ya Shauri Tanga, watoto hawa wanaishi katika mateso makubwa makubwa ajabu.

3. Hadarash ni jini katili sana linaloua kwa kukata shingo na kunyonya damu ya mtu

4. Anazihad ni jini linalokamata roho ya mtu, kisha mtu anaonekana amekufa, baada ya mazishi, wachawi huja na kusoma dua kaburi funguka na jini huiachia roho ya marehemu, ufahamu unapomrudia, wachawi huondoka naye.

5. Zuzuk ni jini la maafa. Jini hili likiingia mtaani au kijijini, hutokea vifo vingi sana, kila siku watu wanazika.

6. Munkar ni jini la makaburini. Jini hili linakutokea kwenye ndoto kama babu, bibi au mzazi wako waliokufa zamani, likiwataka mfanye jambo fulani au familia itaangamia. Kimsingi unapotekeleza maelekezo ya jini, mtakuwa mumejifunga wenyewe kwa kamba ya kifo toka kuzimu, na matatizo makubwa ya magonjwa na vifo huanza kwa familia.

7. Tatazu ni jini la uasherati, unafanya tendo la ndoa bila kujali magonjwa au uko kwenye kipindi cha hedhi.

8. Rabdi ni jini linalotumwa kwa Waislamu peke yake, kwa ajili ya kufanya fujo.

9. Balshebe ni jini linalosimamia magonjwa na madhaifu ya mwili

10. Sajidur ni jini linalosimamia pesa. Likitumwa kwako mshahara wako unapotea katika matumizi ya ajabu ajabu.

11. Subrah ni jini linalosimamia mafarakano, na kutokuelewana kwa viongozi wa Makanisa.

12. Lair Labi ni jini linalosimamia hofu na kukata tamaa.


Duh! speechless wakuu
 
Back
Top Bottom