Biashara nyingi zinazofanikiwa Tanzania ni ushirikiano wa familia na ndugu wa karibu, bila hii silaha unaweza kuichukia biashara, heri ujaribu ajira

gearbox

JF-Expert Member
Apr 20, 2024
240
684
Mifano ni matajiri wengi tunaowajua kina Mo, Bakhresa, GSM, ni biashara za familia na ndugu wa karibu, ni team work.

Pia kwa upande wetu watanzania wa asili ukienda kwenye masoko makubwa utawakuta wengi wanaofanikiwa ni biashara za familia na ndugu wa karibu wanapambana pamoja, ukienda ofisi zao ukichunguza vizuri kuna watu kadhaa ni wanafamilia na ndugu wa karibu.

Ni team work wanafamilia na ndugu wa karibu wana maduka Mbeya, Iringa, Moro, Dar, wakitaka kujumua mzigo wanakusanya pesa wanaagiza mzigo mkubwa kwa discount kubwa, wewe unaeagiza mwenyewe utaendelea kulalamika faida ni ndogo, bidhaa mnayouza wote elf 5 wewe unapata faida ya jero wao elf 2, wakipunguza bei unaanza kulalamika wanataka kukumaliza

Kwenye matatizo / changamoto wanafamilia na watu wa karibu inakuwa rahisi kuji organize kuyatatua ila wewe ukitaka kuvunja chawa kwa kidole kimoja utateseka mno,

Damu ni nzito kuliko maji, kufanya biashara kwa kuungana na marafiki muda wowote mambo hubadilika (kuzulumiana, kugeukana, kukosa msimamo wa malengo, n.k)
 
Andiko safi sana, tatizo watu weusi ni kama tuna laana hatupendani, wala hatupendi mafanikio ya watu wetu wa karibu
kuna biashara za watu weusi za kifamilia zinaenda fresh tu

Isipokuwa kwa biashara zetu waafrika zinadumu kwa muda mfupi kwasababu watoto wakianza kuoa na kuolewa kuna watu wa nje wanakuwa sehemu ya familia, hawa ndio wanaanza tamaa mwishowe biashara zinakufa
 
kuna biashara za watu weusi za kifamilia zinaenda fresh tu

Isipokuwa kwa biashara zetu waafrika zinadumu kwa muda mfupi kwasababu watoto wakianza kuoa na kuolewa kuna watu wa nje wanakuwa sehemu ya familia, hawa ndio wanaanza tamaa mwishowe biashara z

kuna biashara za watu weusi za kifamilia zinaenda fresh tu

Isipokuwa kwa biashara zetu waafrika zinadumu kwa muda mfupi kwasababu watoto wakianza kuoa na kuolewa kuna watu wa nje wanakuwa sehemu ya familia, hawa ndio wanaanza tamaa mwishowe biashara zinakufa
Mimi naongea kwa ujumla mkuu, usianze kutafuta biashara moja moja za watu weusi waliofanikiwa kwa ushirikiano wa kifamilia.

Mfano mzuri wa jamii inayofanya biashara kwa kushirikiana na ndugu ni wahindi, wapo vizuri sana

wengi wao hawajengi nyumba za kuishi wanakodisha appartment wanaishi wengi kwenye appartment moja na ushirikiano mkubwa kwenye biashara zao
 
Mimi naongea kwa ujumla mkuu, usianze kutafuta biashara moja moja za watu weusi waliofanikiwa kwa ushirikiano wa kifamilia.

Mfano mzuri wa jamii inayofanya biashara kwa kushirikiana na ndugu ni wahindi, wapo vizuri sana

wengi wao hawajengi nyumba za kuishi wanakodisha appartment wanaishi wengi kwenye appartment moja na ushirikiano mkubwa kwenye biashara zao
Overall ni kweli huo ndio uhalisia

Lakini main point ni kwamba hata sisi weusi tukifanya tunaweza japo wengi hawataki, Mifano halisi ukienda masoko makubwa unajionea zipo biashara kubwa za kifamilia zilizofanikiwa.

Ila tatizo la waarabu, wahindi, wasomali wanaishi sehemu moja kwa kuoana kindugu na kiukoo, mtu kuoa binamu yake ni kawaida.
 
Hayo mambo wanayaweza hao waarabu na wahindi, sisi black pipo kwenye familia buku ten tu tunafarakana.
Hata sisi wapo walioweza, utawaona ukienda masoko makubwa

Lakini idadi bado ni ndogo kiujumla.

point ni kwamba umoja ni nguvu,
 
Wachaga wanajitahidi
Ni mfano mzuri, wengine ni wakinga pale Kariakoo, unafika dukani unawakuta wanafamilia na ndugu wa karibu, wanahaso pamoja.

Ni baadhi ya jamii ambazo walau zimejitahidi japo hata ndani ya hizo sio wote, bado wengi waliobaki wanapenda style ya jeshi la mtu moja.

Shida ya hizi biashara kwetu Africa baba ndie anaunganisha kila kitu, akifariki kila mtu anataka chake asepe kivyake, pia watu wapya wanaoingia kwenye familia kwa njia ya ndoa wengine wametokea kwenye familia za wavivu, wenye tamaa, n.k. hawa wanaharibu sana biashara
 
Unachosema ni kweli... ila bado unaweza kufanikiwaa kwa plan zozote unazoamini..
Suala kuu ni kuhusu uwezekano wa jambo kutokea(probability),

uwezekano wa kutoboa biashara ya kifamilia / ndugu wa karibu ni mkubwa zaidi kuzidi jeshi la mtu moja
 
Ni kweli ila unaweza kutengeneza team work sio lazima muwe ndugu.. profit sharing strategy inawezekanaa mkafanikiwaa
 
Shida ni uoga wa maisha na kukosa kuthubutu. Nina rafiki yangu yeye tokea zamani shule alikuwa kama anafosi sababu wazazi wanamsakama kusoma.

Ilikuwa ni vita hadi yeye kufika chuo. Ila kwasasa ni mfanyabiashara wa biashara tatu moja mkewe anashika usukani mbili ameshika yeye. Na mambo yanaenda na ndie anasaidia home kwa wazazi kuliko ndugu zake ambao wanaishi kwa ajira na wanamadeni sana.

Kuna kipindi mwamba alijaribu kuwaomba ndugu zake wamkopee pesa ili anunue mzigo, lakini ndugu zake walikuwa ni watu wa mashaka mashaka sana. Hawajiamini wanaona kama pesa hazitarudi na watakwenda kuingia madeni kama wakimkopea sehemu.

Kilichokuja kutokea, mkewe na jamaa alikuwa na shamba sehemu huko nje, akaweka hati ya shamba na hati ya nyumba rehani ili aweze kopa pesa kumdhamini kijana.

Zilikopwa kama milioni 30 hivi na kijana akamtoa yule mkewe pesa kidogo ya kutuliza wenge nyingine akaingia nayo mtaani. Ndani ya miaka mitano hapa jamaa akawa ameshairejesha na imezaa matunda ya hizo biashara.

Ndugu zake walishangaa tu kusikia jamaa anakuja Dar na gari yake Subaru Forester huku mkewe na watoto wawili wakaja na bombardier wiki baadae.


Sasa wanajaribu kutengeneza mazingira ya kutaka kuingia ubia kwenye biashara yake ila kijana amekaza. Sasa wameanza maneno ya kusema jamaa anajali sana ukweli Mwanamke kamshika masikio hawajui siri ya mafanikio ya jamaa kuwa ni mkono wa mkwe.
 
Shida ni uoga wa maisha na kukosa kuthubutu. Nina rafiki yangu yeye tokea zamani shule alikuwa kama anafosi sababu wazazi wanamsakama kusoma.

Ilikuwa ni vita hadi yeye kufika chuo. Ila kwasasa ni mfanyabiashara wa biashara tatu moja mkewe anashika usukani mbili ameshika yeye. Na mambo yanaenda na ndie anasaidia home kwa wazazi kuliko ndugu zake ambao wanaishi kwa ajira na wanamadeni sana.

Kuna kipindi mwamba alijaribu kuwaomba ndugu zake wamkopee pesa ili anunue mzigo, lakini ndugu zake walikuwa ni watu wa mashaka mashaka sana. Hawajiamini wanaona kama pesa hazitarudi na watakwenda kuingia madeni kama wakimkopea sehemu.

Kilichokuja kutokea, mkewe na jamaa alikuwa na shamba sehemu huko nje, akaweka hati ya shamba na hati ya nyumba rehani ili aweze kopa pesa kumdhamini kijana.

Zilikopwa kama milioni 30 hivi na kijana akamtoa yule mkewe pesa kidogo ya kutuliza wenge nyingine akaingia nayo mtaani. Ndani ya miaka mitano hapa jamaa akawa ameshairejesha na imezaa matunda ya hizo biashara.

Ndugu zake walishangaa tu kusikia jamaa anakuja Dar na gari yake Subaru Forester huku mkewe na watoto wawili wakaja na bombardier wiki baadae.


Sasa wanajaribu kutengeneza mazingira ya kutaka kuingia ubia kwenye biashara yake ila kijana amekaza. Sasa wameanza maneno ya kusema jamaa anajali sana ukweli Mwanamke kamshika masikio hawajui siri ya mafanikio ya jamaa kuwa ni mkono wa mkwe.
kuna uzi niliusoma jana humu unadai ukitaka kuanzisha ukoo wenye mafanikio inabidi uanze na damu mpya yani watoto wako, pia uoe mtu ambaye sio maskini wa fikra

jamaa anendelee na msimamo wake, ndugu hao wanaweza kutia doa hio biashara ndio kwanza ana forester, awekeze zaidi kwa watoto wake waje kuendeleza na kupanua biashara
 
Weusi hatupendani, roho za kwanini kwa sana. Nduguyo ndio anapamana usiendelee.
 
Back
Top Bottom