Benki zina kinga gani dhidi ya uchawi?

Izzi

JF-Expert Member
Nov 30, 2016
553
1,107
Hakuna asiependa pesa (Hapo sasa nimekuwa semaji la binadamu wote), na kama yupo basi ana raha sana. Tutakubaliana pia, hakuna asiependa njia za mkato (shortcuts) za kurahisisha mambo. Njia mojawapo ya mkato ni kutumia uchawi kupata kile unachokitaka.... nimekua katika jamii ambayo inaamini ili utoboe kimaisha ni lazima utumie uchawi. Na mtu yeyote akitajirika basi lazima atahusishwa na uchawi 'bai difoti' (by default). Lakini, ambacho sijawahi kusikia ni kwamba kuna mchawi mmoja amekomba pesa zote kutoka benki fulani. Au yupo sema mimi ndio sikusikia? Kama hayupo, kwanini hizi 'softiwea'(software) za kichawi hazitumiki kubeba pesa kutoka benki?

Kuna ambao wanasema mchawi hawezi kutumia uchawi wake kuvuta pesa kutoka benki, kwasababu benki zenyewe zinalindwa na Uchawi 'Pro Max'/ Majini 'first class'. Kundi jingine kubwa zaidi ni la sisi ambao hatuelewi kwanini wachawi hawawezi kuvuta pesa kutoka benki. Inasemekana pia, mchawi hata akija kwako usiku kukuroga/kukukaba/ kukunyonya damu/ kukuchezea, halafu ukawa umeweka pesa hata pembeni ya kitanda kwa mfano, atafanya vyote lakini hawezi kuchukua ile pesa.

Nilisoma mahali fulani wanasema uchawi sio halisi, ni viinimacho tu - manaake uchawi hauna madhara/matokeo kwa ambae haamini au haogopi uchawi. Kwa lugha rahisi uchawi ni mchezo wa kisaikolojia tu, hauna uhalisia kwa hiyo hauna madhara kwa vitu vinavyoonekana/ kushikika, isipokuwa panapo imani na hofu; Ukiamini basi kitatokea ulichokiamini, na ukiogopa lazima madhara yatokee kwasababu ya hofu yako (Kumbuka: Sio kwasababu ya uchawi!)

Bahati mbaya sijawahi kumpata mchawi anijibu maswali yangu, kukidhi udadidi wangu tu. Lakini tuna jukwaa lililosheheni watu wenye asili tofauti tofauti, watu wenye fikra tunduizi, watu makini kabisa wenye uzoefu na masuala anuai. Naombeni mnisaidie kufahamu, wachawi wanakwama wapi kubeba shekeli zile kutoka benki?

Naomba kuwasilisha.
 
naomba nimkaribishe ndugu mshana jr kwa ufafanuzi zaidi
Mchawi halisi hahitaji pesa! Pesa ni mzigo mzito wenye kuhitaji michakato mingi.. Akili ya kibinadamu ni kumiliki pesa ili anunue atachacho..
Mchawi hahitaji kwenda bank akaibe pesa kwakuwa kwanza wizi ni kosa kwa mchawi .. Anaweza kuwasaidia wengine sio afanye yeye
Mbili mchawi hahitaji pesa kwakuwa anapata kila atakacho bila pesa na hata akizihitaji ataziita zitamfuata hapo alipo na sio kujisumbua kwenda mpaka bank
Tatu kuna mazingaombwe na ushirikina wa kuchukua pesa bank lakini hujichukulii tu marundo kuna kiasi .. Ni kama chuma ulete hawezi kuchukua pesa ya kufanya maendeleo ni ya kumtosha kwa siku moja tuu tena mahitaji muhimu kama chakula

Nne hata kama atatokea mtu akapiga ndefu bank .. Unadhani Bank itatangaza? Au unadhani mwizi atajitangaza kwamba kapiga ndefu bank?

Mchawi ana miliki pesa za aina tatu
1. Za kuvuta toka popote atakapo kulingana na uwezo wake
2. Za kutengeneza kimazingara/mazingaombwe
3. Za kuletewa na wateja
 
Hakuna asiependa pesa (Hapo sasa nimekuwa semaji la binadamu wote), na kama yupo basi ana raha sana. Tutakubaliana pia, hakuna asiependa njia za mkato (shortcuts) za kurahisisha mambo. Njia mojawapo ya mkato ni kutumia uchawi kupata kile unachokitaka.... nimekua katika jamii ambayo inaamini ili utoboe kimaisha ni lazima utumie uchawi. Na mtu yeyote akitajirika basi lazima atahusishwa na uchawi 'bai difoti' (by default). Lakini, ambacho sijawahi kusikia ni kwamba kuna mchawi mmoja amekomba pesa zote kutoka benki fulani. Au yupo sema mimi ndio sikusikia? Kama hayupo, kwanini hizi 'softiwea'(software) za kichawi hazitumiki kubeba pesa kutoka benki?

Kuna ambao wanasema mchawi hawezi kutumia uchawi wake kuvuta pesa kutoka benki, kwasababu benki zenyewe zinalindwa na Uchawi 'Pro Max'/ Majini 'first class'. Kundi jingine kubwa zaidi ni la sisi ambao hatuelewi kwanini wachawi hawawezi kuvuta pesa kutoka benki. Inasemekana pia, mchawi hata akija kwako usiku kukuroga/kukukaba/ kukunyonya damu/ kukuchezea, halafu ukawa umeweka pesa hata pembeni ya kitanda kwa mfano, atafanya vyote lakini hawezi kuchukua ile pesa.

Nilisoma mahali fulani wanasema uchawi sio halisi, ni viinimacho tu - manaake uchawi hauna madhara/matokeo kwa ambae haamini au haogopi uchawi. Kwa lugha rahisi uchawi ni mchezo wa kisaikolojia tu, hauna uhalisia kwa hiyo hauna madhara kwa vitu vinavyoonekana/ kushikika, isipokuwa panapo imani na hofu; Ukiamini basi kitatokea ulichokiamini, na ukiogopa lazima madhara yatokee kwasababu ya hofu yako (Kumbuka: Sio kwasababu ya uchawi!)

Bahati mbaya sijawahi kumpata mchawi anijibu maswali yangu, kukidhi udadidi wangu tu. Lakini tuna jukwaa lililosheheni watu wenye asili tofauti tofauti, watu wenye fikra tunduizi, watu makini kabisa wenye uzoefu na masuala anuai. Naombeni mnisaidie kufahamu, wachawi wanakwama wapi kubeba shekeli zile kutoka benki?

Naomba kuwasilisha.
Bank haziwezi kuwa na kinga dhidi ya wachawi kwakuwa zile pesa sio zake bali ni za wateja na kila pesa inayopokewa bank inaingia na nguvu yake kiroho
Nyingine ni za wizi
Nyingine ni za dili
Zingine ni za mauaji zinanuka damu
Nyingine ni za dili chafu kama madawa nk
Zingine ni za makafara nknk
 
Mchawi halisi hahitaji pesa! Pesa ni mzigo mzito wenye kuhitaji michakato mingi.. Akili ya kibinadamu ni kumiliki pesa ili anunue atachacho..
Mchawi hahitaji kwenda bank akaibe pesa kwakuwa kwanza wizi ni kosa kwa mchawi .. Anaweza kuwasaidia wengine sio afanye yeye
Mbili mchawi hahitaji pesa kwakuwa anapata kila atakacho bila pesa na hata akizihitaji ataziita zitamfuata hapo alipo na sio kujisumbua kwenda mpaka bank
Tatu kuna mazingaombwe na ushirikina wa kuchukua pesa bank lakini hujichukulii tu marundo kuna kiasi .. Ni kama chuma ulete hawezi kuchukua pesa ya kufanya maendeleo ni ya kumtosha kwa siku moja tuu tena mahitaji muhimu kama chakula

Nne hata kama atatokea mtu akapiga ndefu bank .. Unadhani Bank itatangaza? Au unadhani mwizi atajitangaza kwamba kapiga ndefu bank?

Mchawi ana miliki pesa za aina tatu
1. Za kuvuta toka popote atakapo kulingana na uwezo wake
2. Za kutengeneza kimazingara/mazingaombwe
3. Za kuletewa na wateja
Tumekuelewa mkuu

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom