ZING SOKONI
JF-Expert Member
- Aug 1, 2014
- 19,512
- 57,105
Hakuna benki nzuri kukopa,kopa kwasababu maalum
Meru bankipo hivi mimi ni mwalimu, mfanyabishara na mkulima , mimi ni mkopaji mzuri sana , nilikuwa na mkopo kupitia salary nilikopa 2019 NMB, nimekuwa na mkopo wa biashara nimekopa CRDB, kwa sasa nimemaliza deni nadaiwa na bodi tu ya mikopo, nina uhitaji tena wa pesa kama milioni mia moja tu.
Nipeni ipi bank nzuri nikope. Ushauri wako uandane na uhalisia na vigezo.
Mshahara Kuanzia sh.ngapi!?Sasa mwalimi si uende kwenye hizo benki husika ili ukapate ABC!!
Na kama ni mkopo wa biashara, ni lazima uwe umekopa na kurejesha kwa muda mrefu + mzunguko mkubwa wa biashara, ndiyo utakuwa na uhakika wa kupata mkopo mkubwa.
Mkopo wa wafanyakazi, ni lazima uwe na mshahara mkubwa kazini. Hivyo vigezo unavyo?