Benjamin William Mkapa nimjuaye...

Benjamin William Mkapa nimjuaye...

Yes I said it.

Najua hili sio popular hapa lakini facts lazima ziwekwe wazi na majungu yaachwe. So far yanayosemwa hapa kuhusu Mkapa ni majungu tu kama vile vinavyoandikwa kuhusu Mwinyi na Kikwete vinapoitwa majungu na hivyo kufutwa au kupelekwa kwenye udaku.

Kama hakuna wa kushuhudia ufisadi wa Mkapa beyond reasonable doubt, basi Mkapa ataendelea kuwa mtanzania safi (kama inavyomstahili).

Ok.. and pope is not catholic!
 
Madela,

Ni convention wisdom kwa wengi hapa kutafuta favor na mkuu wa sasa huku wakitumia kila wanachoweza kumponda na kumchafua mkuu aliyetoka. Lakini pamoja na hayo, ukweli na uwazi wa forum hii lazima pia ufuatane na facts na sio vinginevyo.

Au wewe unasemaje?


Kitendo cha mkuu kuacha vijana wake waibe mbele ya uso wake tu ni ufisadi mkubwa, achilia mbali kufanya biashara binafsi kwa kutumia umaarufu wa jengo la serikali na cheo chake.
 
Hapana Madela, hapo nilikuwa na haki ya kuuliza swali ili kujenga context ya swali la msingi.

Mazungumzo yeyote rasmi na hata yale ya Yanga na Simba kule Kichwele Street hufuata mkondo wa kujibu hoja kwanza kisha kuleta hoja, sivyo tafrani ya mazungumzo huzaliwa.
Jibu swali.
 
Kitendo cha mkuu kuacha vijana wake waibe mbele ya uso wake tu ni ufisadi mkubwa, achilia mbali kufanya biashara binafsi kwa kutumia umaarufu wa jengo la serikali na cheo chake.

Lakini Madela,

Imewekwa hapa JF mara nyingi kuwa Mkapa ndiye kinara wa ufisadi hata kufikia hatua ya kuwekwa kwenye list ya watu wanao - iscrew Tanzania (tensi ya kuendelea) hadi leo hii.

Sioni kama ulichoweka hapa kinajaza hiyo hukumu dhidi ya Mkapa.
 
Mazungumzo yeyote rasmi na hata yale ya Yanga na Simba kule Kichwele Street hufuata mkondo wa kujibu hoja kwanza kisha kuleta hoja, sivyo tafrani ya mazungumzo huzaliwa.
Jibu swali.

Nitarahisisha hili ili kuendeleza mjadala.

Ninajibu swali - Kwa kweli simjui mmiliki wa Kiwira (kwa hakika).

Je wewe unamjua?
 
Wakuu msimshambulie mwenzenu,yeye anavyoona(kwa mtizamo wake) ni kwamba Mkapa sio fisadi,so cha msingi ni kumsaidia tu kwa kuainisha ufisadi wa Mkapa(japo yalishaainishwa mengi) kwa kuweka mambo ambayo yatamfanya ndugu yetu Solomon aamini kuwa Mkapa ni Fisadi badala ya kuanza kumshambulia kwa kusema mara sijui katumwa mara nini..tumuache autumie uhuru wake jamani,tusimshambulie,tumsaidie,hajui kitu huyo........
 
Lazima na mimi niseme. Lowassa sio fisadi, RA sio fisadi. Toeni ushahidi kama mnabisha. Au niulize nani anahusuka na Kadoga, Epa, Richmond etc etc. Mgodi wa kiwira Mkapa hakujiuzia, na wala hakuna kitu kinachoitwa ANBEM ni uzushi tu mengi ni uzushi tu. Mkuu Solomon David anaweza kuthibitisha hilo. Hata ufisadi uliotokea kwenye utawala wake Mkapa alikuwa hajui kinachooendelea, hata ndege ya Rais, Radar vyote alipinga.
 
Wakuu msimshambulie mwenzenu,yeye anavyoona(kwa mtizamo wake) ni kwamba Mkapa sio fisadi,so cha msingi ni kumsaidia tu kwa kuainisha ufisadi wa Mkapa(japo yalishaainishwa mengi) kwa kuweka mambo ambayo yatamfanya ndugu yetu Solomon aamini kuwa Mkapa ni Fisadi badala ya kuanza kumshambulia kwa kusema mara sijui katumwa mara nini..tumuache autumie uhuru wake jamani,tusimshambulie,tumsaidie,hajui kitu huyo........

Mwanangu wa miaka sita anajua Mkapa ni FISADI. Huyu mleta hoja ni mtu mzima na bila shaka ameenda shule. Anachotaka kufanya hapa ni kutupotezea muda kujadili mambo muhimu. Ni nani katika Tanzania hajui madudu yaliyofanywa na Mkapa akiwa madarakani?. Inatia hasira kuyakumbuka madudu hayo, na hiyo inasababisha mleta hoja kujibiwa kijeuri na kimkato hapa JF.

Mkapa akiwa Ikulu alivunja katiba ambayo aliipa kuilinda kwa kufungua na kufanya biashara. Alijimirikisha mgodi wa kiwira yeye na rafiki zake kwa gharama za watanzania ambazo tutazilipa miaka nenda rudi. Wizi wa mapesa ndani ya BOT (EPA) ulitokea wakati wa Mkapa na kwa ruhusa yake. Mkapa anaijua fika Kagoda na Meremeta na kwa baraka zake hizi kampuni zilitenda madudu ambayo mpaka sasa ni mzigo kwa watanzania.

TICTS pale bandarini mpaka sasa wanatupa matatizo na hasara, hiyo yote ni matunda ya Mkapa. Sasa sioni haja ya kuendelea kuandika mengine ili kumfahamisha mleta hoja, nina amini anajua na anatambua hilo. Labda kama ametumwa kwa lengo analolijua yeye. Linga gwagile angukukoma
 
Yes I said it.
Najua hili sio popular hapa lakini facts lazima ziwekwe wazi na majungu yaachwe. So far yanayosemwa hapa kuhusu Mkapa ni majungu tu kama vile vinavyoandikwa kuhusu Mwinyi na Kikwete vinapoitwa majungu na hivyo kufutwa au kupelekwa kwenye udaku.
Kama hakuna wa kushuhudia ufisadi wa Mkapa beyond reasonable doubt, basi Mkapa ataendelea kuwa mtanzania safi (kama inavyomstahili).
oh,mkuu naomba umsalimie GEMBE(only if u know him) because u share with him/her the same ideology.
 
Nitarahisisha hili ili kuendeleza mjadala.

Ninajibu swali - Kwa kweli simjui mmiliki wa Kiwira (kwa hakika).

Je wewe unamjua?

Mkapa,Yona na watu wengine kadhaa wana hisa kwenye mgodi huu.
Ushahidi wa kesi za Kimafia unadhihirisha wazi kwamba mkuu Mkapa ni fisadi.

Kumbuka hii si kesi ya mwizi wa kuku ambayo ni lazima tumshike na mnofu kinywani ili kuthibitisha wizi wake, kwani kumshika na kuku wako kwapani kwake bado haitoshi kumpa mvua, pengine alikuwa akijaribu kumrejesha kuku wako alopotea???.!!!!

Sisi tumemtuhumu Mzee Mkapa kuwa ni Fisadi, je wewe unaweza kuleta utetezi wa maana kwamba Nkapa si Al-Fisad?
Kushindwa kwetu kwa namna yeyote kuleta ushahidi wa wazi juu ya Ufisadi wa mkapa hakumuondelei Mzee huyu Wadhifa na heshima hiyo chafu. Rais wa nchi hawezi kudai kwamba hajui wala hahusiki na wizi wa Billion za kulipa madeni nje ya nchi. Suala la kulipa madeni nje ya nchi lilikuwa namba moja kwa Mkapa, ni vipi hakujua account ya EPA inachotwa kwa Machepeo???
Watu wote kabisa wakiwemo mzee Kingunge na Rostam Azizi mpaka wafagizi ikulu wajue kuna wizi wa Mabillioni lakini ina kuwa habari mpya kwa Rasi wa nchi???

Alikuwa akilipa Madeni ya nje au alikuwa akituongezea??
Ndiyo maana Kesi zote za Wizi wa Kimafia zina Mahakama zake na upelelezi wa aina yake.
Huwezi kuwatuma Polisi wakaao kwenye Mabanda ya mabati, shule hakuna, upeo duni, wauaji hawana hamu na nia ya kazi huku wana vibyongo vya njaa kupeleleza wizi wa Kifisadi!!!

Tumemtuhumu mzee huyu kwa Ufisadi, tupe utetezi wako kuthibitisha kauri yako halali " Mkapa sio Fisadi".
 
Jamani mnataka hadi akalale Keko ndio mtaamini....pia mtasema kuwa tuiachie mahakama.........jamaa ametumia office vibaya.....amekopa pesa zetu za nssf amepeleka anakojua yeye..kiwara imezima kabisa....hakuna hata mia aliopeleka kule.....hili ni moja tukianza kuhesabau hapa ...............
 
Mkuu Kidatu,

heshima kwako mkuu, lugha hiyo mkuu. lugha hiyo!

Kwa leo naizuia hasira yangu,lkn ukirudia kuleta madudu yako hapa kwenye jamii ya greatest thinkers nitakupa unachostahili kupewa!

Kama ni issue ya without beyond reasonable doubt basi HAMNA FISADI tz maana hamna hata mmoja aliyetiwa hatiani na mahakama zetu!

Ndiyo ina maana mtu kama Mkapa aliyechukua Kiwira yetu au uporaji wa mke wake majumba ya msajili,lkn pasipo wote kutofikishwa mahakamani nakuhukumiwa kwa hiyo sio fisadi!?

Upo Hovyoooooo!na kama huna hoja please SHUT-UP!
 
Ajabu ni kwamba mtu anayetetewa yeye mwenyewe hana ubavu hata wa kujitokeza hadharani na kujibu mapigo. Anajua alichofanya. Sasa sijui kwa nini mtu anasumbuka kumtetea fisadi aliye hai na ambaye anao uwezo wa kuongea na kujitetea yeye mwenyewe.

kama kweli MKapa sio fisadi, na awe wa kwanza kutoa kauli ya kujisafisha, hapo ndio tuanzie kujenga hoja based on kauli yake. Otherwise katika historia ya TZ haijawahi kutokea na ninaamini haitakaa itokee kamwe kiongozi wa nchi kuwa fisadi kama Mkapa. Shame on him; "Mr. Clean"
 
Kwa leo naizuia hasira yangu,lkn ukirudia kuleta madudu yako hapa kwenye jamii ya greatest thinkers nitakupa unachostahili kupewa!

Kama ni issue ya without beyond reasonable doubt basi HAMNA FISADI tz maana hamna hata mmoja aliyetiwa hatiani na mahakama zetu!

Ndiyo ina maana mtu kama Mkapa aliyechukua Kiwira yetu au uporaji wa mke wake majumba ya msajili,lkn pasipo wote kutofikishwa mahakamani nakuhukumiwa kwa hiyo sio fisadi!?

Upo Hovyoooooo!na kama huna hoja please SHUT-UP!

Haya mkuu mwenye hoja, mimi nina-shut up
 
Yes I said it.

Najua hili sio popular hapa lakini facts lazima ziwekwe wazi na majungu yaachwe. So far yanayosemwa hapa kuhusu Mkapa ni majungu tu kama vile vinavyoandikwa kuhusu Mwinyi na Kikwete vinapoitwa majungu na hivyo kufutwa au kupelekwa kwenye udaku.

Kama hakuna wa kushuhudia ufisadi wa Mkapa beyond reasonable doubt, basi Mkapa ataendelea kuwa mtanzania safi (kama inavyomstahili).
tunashukuru kwa matusi yako, maana kwa akili yako nzuri tu, unataka kujixxxx fanya kwamba hujui au hufahamu matatizo aliyo leta shwetani mkapa, mpaka leo hii umerudia swali ambalo linaeleleweka wazi kwa watanzania 90% ingawa wengine walifaidika kwa wizi wa mkapa , lakini wana akili ya kutmbua hilo, sasa sijui wewe aidha unatujaribu au unaelewa lakini unajaribu kutafuta njia za kumtetea au za kujitetea (* mkapa) kwa mambo aliyo ifanyia nchi hii. kama mdau moja alivyo sema hakuna na haitotokea raisi mbovu kama yeye, mimi nilikuwepo wakati wa Alhaji, lakini alicho fanya Che Nkapa, waulize waarusha na mererani ya tanzanite yao, watu wamusoma/mza/tbr na zahabu yao na samaki wa nyanza, wa tanzania na NBC, tanesco, nyumba za serikali etc etc, lakini kwa sababu tuwavumulivi/wastaarabu tunashukuru kwa matusi yako, lakini dhambi aliyo fanya hasa hasa kutukana mababu zake haitokwenda hivi hivi , nenda kamwambie hivyo, na adhabu yake kama sio kwake itaikumba jamii yake hivyo afanye upesi kabla siku zake hazijafika kwenda kumuomba kilaini/pengo/kikwete/simba kwamba angependa kutubu zambi zake. Wakati ni huu, ni shauri yake na yako kama msingependa kuchukua nafsi hii.
 
my understanding ,i think Mkapa was taken over by greed family &friends who took advantage of Ikulu to acquire natioal properties greedly.However from this reason mkapa should be responsible because of his failure to manage and control his family.
 
Back
Top Bottom