Benjamin William Mkapa nimjuaye...

Benjamin William Mkapa nimjuaye...

"Sasa Mkapa anatetewa na watu au vipi?? Mbona yeye yupo kimnya sana."
________________________

JM: Na hicho kitu ndiyo mie huzimia kabisa, watanzania jinsi tulivyo! Hivi Mkapa anashindwa nini kuita press conference na kujitetea tuhuma baada ya tuhuma na kuruhusu aulizwe maswali?

Anaogopa nini? Akina RA, Manji na mapapa wengine wa ufisadi (walioiba wakati wa utawala wake) angalau wamekwenda mahakamani kumshitaki mzee mengi kwa kuwakashifu. Yeye Mkapa kwa nini hafanyi hivyo hasa dhidi ya magazeti yanayomuandika kila siku?

Au anatumia mapesa kuwalipa watu kumtetea humu JF, na Bungeni -- kama vile yule Mbunge Serukamba juzi alipobwatuka hovyo Bungeni kumkingia kifua? na Mzindakaya ambaye alifaidika kwa mkopo wa mabilioni ya utata kutoka BoT?

hawa hawana uchungu wowote wa nchi yao.

Kua wewe! so akiita press conference na kusema hajaiba na akatoa vithibitisho vya uongo! utakubli? hivi kwa nini watanzania wengi wanamawazo ya kidakudaku?? kama ameba tunamamlaka apelekwe jela.Wale vibaka wote segera waliitisha press conference?

Mkapa kawe hatumii pesa wewe! kama wewe unajua mwizi wenzako hawajui hivyo, ndio maana tunasema serikal ipo kuwashtaki watu kama hao! pi ujue kuwa yuko juu bado aliku kionozi nchi usiji-kujicompare naye wewe!

Sentensi zako za mfa maji, ndio maaa kuna haja ya CCM wote wondoke madarakani!

mara yuko kimya, anahonga,mara sijui nini huku anakula analala, unabaki kusema sema tu humu kama chiriku, tukisema jiandikisheni vyama kama chadema tuiondoe CCM HUNA MUDA HUO!

suppose JK na serikali yake hawataki kumpeleka mahakamani utafanya nini??
 
siamini iwapo wataondoka na hawa vibaraka wanaowatetea humu JF! Sidhani.

Hii sentensi inabidi ujiangalie sana, inaonekana kila atakayekuwa kinyume na wewe kuhusiana na tuhumaza kiongozi yeyote au mtu yeyote ni kibaraka! kwako wewe tuhuma hizi ni kweli, sijajua mpaka sasa umeshachoma moto vibak wangapi uliposikia kelele za mwizi, maana kwako wewe tuhuma hizi unachukulia fanatic hat kama wewe ni gullible.

Tuhum za kifisadi ziko hivi

1. Za kweli
2. Za kusingiziwa

jinsi ya kuzishughulikia ni

1. Mahakama, then waende jela au

Kama ulichagua CCM basi wanapaswa wafanye hivyo, au mtu kama mimi nmchukulia kila mtu ni innocent, la kama CCM wanawalinda adui yangu RA wala BMW ni CCM, ili kikiingia chama kingine kiwakamate n kuwafunga!

kelele zako JK nazipenda sana maana

1. Huoni kuwa hafanyi kitu-statue
2. mafisadi wengine wengi wanaiba sana hawajulikani kwani mawazo yenu yako kwa individuals na siyo society, jamii yetu wengi ni mafisadi na solution ni viongozi bora, siyo kuwa akifa leo BWM,RA then ufisadi hamna

kwa hiyo uangalie comment na idea za watu, si kila anayemtetea BWM ni kibaraka au fisadi,wengine wanaangalia mzizi wakati wewe unataka ku-prune jani liliokauka!

nadhani umeelewa!
 
Choveki,.....Kwa nini usi-type kwenye GOOGLE na utapata habari zote hizi. Acheni uvivu jamani wa utafutiwe hata habari kama hizi......KILIMANJARO AIRPORT UP FOR GRAB FOR JUST 1000 US

Hapana ndugu Sikonge si uvivu bali ni kwamba muda mwingi inabidi nirudie kusoma marudio ya kijana mtanashati na jinsi alivyo na akili finyu ukilinganisha na uncle Ben, wakati miye nataka nisome ya uncle Ben W, ila kutokana na watu kurudia rudia mambo ya kijana mtanashati, inanibidi nitumie muda mrefu zaidi kutafuta ya rais mstaafu ili nielewe mabaya yake pia, kwani mabaya ya kijana wetu yapo nje nje na sihitaji kukumbushwa!

Kinachosikitisha ni kuwa uwanja wa KIA umekodishwa kwa dola 1000 kwa mwaka na bado huyo aliyekuwa mkuu wa nchi anapewa sifa ya kimungu mungu!, Hapo hujaangalia NBC, Kiwira, Tanesco, akina TANGOLD, Meremeta, Radar, EPA-malipo hewa benki kuu-, ndege ya Raisi nk.

Pia nashangaa kuwa badala ya kujadili ishu tunaleta ushabiki ushabiki tu, je unadhani Tz tutaendelea?, Kitakachotokea ni kuwa tutaendelea kubadilisha na kuchagua maraisi vilaza mmoja baada ya mwingine kila baada ya miaka kumi mpaka tushike adabu zetu!! Unadhani ule msemo wa Wajinga ndiyo waliwao maana yake nini? Maraisi tuwachaguao huwa wanatupaka mafuta kwa migongo ya chupa nasi tunahisi ati wanatupenda kama watanzania wenzao.

Anayeongelewa ni huyu:
Benjamin William Mkapa nimjuaye...
(kama kielezavyo kichwa cha habari) kuna mijadala lukuki ya JK, kwanini na huu tuupeleke kwa JK?
mnapenda kulazimisha mambo! haya maoni ya watu, akili zao, muda wao, malengo yao, huwezi kuwapangia watu waseme nini na lini, wala usijione una akili, nionyeshe thread moja tu ya JF ambayo watu waliajadili same thing bila kwenda nje kidogo ya maada! utapata pressure za bure kuhangaika kuwa kiranja humu! sema ulilonalo moyoni usaidiwe! acha kutapatapa!

Hapana Mkuu Waberoya, nilichokumbusha ni kuwa sioni sababu ya kumjadili JK kwenye mjadala wa BWM, kwani huu mjadala siyo wa kuwalinganisha hawa jamaa wawili, bali kujadili BWM na alivyotuingiza mjini. Pia si kwamba nalazimisha mambo, nadhani aliyelazimisha huu mjadala ni Kaniki, kwani ameeleza kinagaubaga kuwa anamsifu BWM kwa mazuri yake ndipo na wengine wakaamua kuandika mabaya yake! Kilichonitatiza ni kuwa badala ya kushusha nondo za huyu muungwana BWM, nondo zinazoshushwa ni za muungwana JK. Mimi nilichokumbusha ni kuwa mijadala ya JK ni mingi mno, na ukisoma mengi yaandikwayo unatamani kulia machozi kuisikitikia Tanzania yetu, na nikawa nakumbusha kuwa huu ni wa BWM siyo JK.
La mwisho ni kuwa pressure itanipata kwa sababu naipenda Tanzania kupita kiasi na kila baada ya miaka kumi tunachagua nunda mpya wa kutuingiza mjini!
 
Last edited:
Sio PM wala Jk wala Bunge wanaoweza kumsafisha Mkapa but ni Wananchi ndio watu pekee wanaweza kufanya hivyo. Kuna haja ya kura za maoni ziitishwe ili tujue kama kweli wananchi wanamchukia Mkapa au vipi??


Hakuna swala la kumpenda au kumchukia B W Mkapa!! Swala ni TUHUMA za WIZI na UBADHIRIFU wa MALI ya Taifa chini ya UONGOZI wake niza kweli???? au si za kweli??? Ikiwa kuna ushahidi kuwa si za kweli,basi kama wanavyodai baadhi AACHWE APUMZIKE KWA AMANI. Na kama kuna ushahidi kuwa niza kweli,basi kama wanavyodai baadhi VYOMBO VYA SHERIA VIFANYE KAZI YAKE. Hakuna haja ya kupakana mafuta nakulaumiana kwa jambo ambalo liko wazi.
 
Kaniki
Big up sana pamoja na watanzania wote mtakaounga mkono hoja hii ya Kaniki. Mimi kwa mtazamo wangu Mkapa is much much much better and I hope one day tutakuja kutamani arudi madarakani lakini itakuwa too late. He was a strong leader na mtu yeyote mwenye akili lazima alitambue hilo. Watanzania acheni umbumbumbu, chambueni mambo kwa kina!!! Amkeni tena acheni kufuata mkumbo na kudanganyika kwa maneno matamu ya viongozi wasanii. Mkapa wa serious leader!!! Ciao
 
Kaniki
Big up sana pamoja na watanzania wote mtakaounga mkono hoja hii ya Kaniki. Mimi kwa mtazamo wangu Mkapa is much much much better and I hope one day tutakuja kutamani arudi madarakani lakini itakuwa too late. He was a strong leader na mtu yeyote mwenye akili lazima alitambue hilo. Watanzania acheni umbumbumbu, chambueni mambo kwa kina!!! Amkeni tena acheni kufuata mkumbo na kudanganyika kwa maneno matamu ya viongozi wasanii. Mkapa was serious leader!!! Ciao
 
Kaniki
Big up sana pamoja na watanzania wote mtakaounga mkono hoja hii ya Kaniki. Mimi kwa mtazamo wangu Mkapa is much much much better and I hope one day tutakuja kutamani arudi madarakani lakini itakuwa too late. He was a strong leader na mtu yeyote mwenye akili lazima alitambue hilo. Watanzania acheni umbumbumbu, chambueni mambo kwa kina!!! Amkeni tena acheni kufuata mkumbo na kudanganyika kwa maneno matamu ya viongozi wasanii. Mkapa was serious leader!!! Ciao
ingekuwa vizuri ukaweka point zako kwa counteract allegation against him, kama issue ya kiwira, net group, radar, ndege ya raisi, madini , nyumba za serikali, na mengineyo mengi tu yanayo semwa kama ubanafsi shaji wa NBC, ATCL, na madudu mengine aliofanyika PSRC nyumba na mali zingine za TTCL, na mengine ambayo yamesisha semwa huko nyuma badala ya kuweka a sweeping statement maana unachukua uchafu pamoja na usafi pamoja hivyo unashindwa kuuona huo uchafu.
 
Mnasahau wema wake, mnakumbuka ubaya wa siku moja lol !ben tenda wema nenda zako ! Ngoja tuangalie nani atasalimika tanzania itapogeuka rwanda. Hali ya vurugu haiepuki has ukizingatia hii govt ya sasa imekumbatia non-progressive agendas.
 
Give me a break. Magufuli waziri mkuu!!! Hivi hatuna vipimo vya kujua ni nani anaweza kuwa kiongozi bora!? Wana-JF mnaanza kumshabikia mvunjaji sheria mkubwa Bw Magufuli, au kwa vile hamkujua aliyoyafanya kwenye mabarabara kuwavunjia watu nyumba bila ya kujali haki zao za msingi, tena kwa kukataa kuheshimu sheria ambayo ilikuwa wazi! Alishauriwa kuhusu haki za wananchi kule Kigoma na Shinyanga ambao barabara iliwafuata na sio wao waliingilia kingo za barabara, akakataa kata kata, matokeo wananchi wakavunjiwa bila fidia na Mungu anajua kilichowapata wale walala hoi. ALipojaribu kufanya hivyo hivyo kule Rombo, fisadi Mramba akazuia kwa nguvu zote, na wananchi wa Rombo walilipwa na wanaendelea kulipwa fidia. WAROMBO walikuwa na msemaji, hao wengine hawakuwa na msemaji. Tena hata pale Rombo Magufuli alilkuwa akifanya vikao vya kuwakemea wananchi licha ya Mbunge wao kutafasiri sheria na kuwahakikishia haki itatendeka. Huyu ukimpa madaraka makubwa si atajeuza sheria zote ziwe kwake.

Jamani mnasahau hata ile barabara aliyoilazimisha kule jimboni kwake, yaani kuifikia barabara ya lami ya Magufuli unapita kwenye mashimo makubwa mno....kiongozi anayevuta kamba kwake, jamani jamani halafu mje mlaani tena kama mnavyomlaani kijana mtanashati mwenye sura na akili za kuvutia JK......SIONI cha kumuenzi Mkapa kwani kama raisi alitimiza wajibu wake na tukamlipa na tunazidi kumlipa, lakini hilo la kuiba na mashemeji, wakwe na wattoto wake ni lazima alilipie

Hivi humu hamna kitufe cha "kinyume cha Thanks" kitu kama "niemichukia sana" au "mbaya". Jamani wengine hatuna maneno mengi tunataka ku-express ubaya tu kwa post ambayo inakera.
 
Mnasahau wema wake, mnakumbuka ubaya wa siku moja lol !ben tenda wema nenda zako ! Ngoja tuangalie nani atasalimika tanzania itapogeuka rwanda. Hali ya vurugu haiepuki has ukizingatia hii govt ya sasa imekumbatia non-progressive agendas.
makosa yanayo tokea sasa yametokana na wizi wake, ambao ulimkosesha kauli dhabiti ya kutuongoza kupa mrithi wake aliye makini, kwani vijana walikuwa na madhambi yake mkononi, na zaidi ya hapo, hapa hatuzungumzi matatizo ya utawala wa sasa tunazungumzia matatizo yake, hivyo kama unataka kumuongelea Raisi wa sasa fungua thread on that fact utapata dondo au michango yake.
na zaidi ya hapo alikuwa anaambia bwana eh hiyo mikataba sio mizuri, lakini kwa makusudi mazima akatumia madaraka yake kutuingiza mkenge. Amekuwa kama Padri/Mwlimu wa Madrasa anaye baka wafuasi wake ambao wameenda kuomba ulinzi kwake, tena vitoto vidogo, ndivyo alivyo wafanyia watanzania waliompa kura wakiwa na imani naye.
 
....wa wale watakao pelekea huyu BWM kufikishwa mahakamani au kuondolewa kinga, ikibidi amani yetu itapumzishwa kwa kitambo ili kuingia msituni kupambana na watu wasiokumbuka fadhila za mh rais mstaafu,
MUNGU MUBARIKI NA KUMEPUSHA KUJIBU SHUTUMA PAMBIKIZI MH BWM .

Ama kweli kazi ipo ipo tu sana.
 
Mhe Ben alichapa kazi ila walimfisadi kuanzia late 1998 ndipo akapoteza dira akajiunga na wale wenzetu .
 
Baada ya mjadala wote huu nadhani sasa ni wakati wa Che-Mkapa kujotkeza hadharani na kujibu mapigo rasmi.
 
Hawezi kusema kabisa usitegemee kutokea na kusema hadharani kabisa. Sahau mzee wangu
 
Yuko tayari kuwatumia wengine kumsemea Bungeni kwa mfano, sijui anawalipa? Kuna akina Mzindakaya na RA (huyu akimtumia mpambe wake mkuu Peter Serukamba).
 
Katika hayo yote uliyoyataja baadhi ni kweli aliyatekeleza mwanzoni mwa utawala wake. Lakini baadaye jamaa alivurunda haijawahi tokea. Ubinafsi, upendeleo, kulindanana ndiyo zikawa sera badala ya ukweli na uwazi.

NINA AMINI WEWE ULIYETUMA HII POST HUKUMAANISHA ULIYOANDIKA BALI ULITAKA KUJUA MAONI YA MEMBER WA JF. NAFIKIRI UMEYAPATA. Jamaa kuna mazuri kafanya lakini mabaya ni mengi zaidi hivyo ni kama hajafanya kitu.
 
Uchunguzi wa kina ni lazima ufanywe kubaini KADCO iliyokodishiwa Kilimanjaro International Airport kwa $ 1000 kwa mwaka, inamilikiwa na nani? Huenda wanahisa ni hao hao washirika wa BWM ktk Kiwira Coalfields purchase.
 
Back
Top Bottom