Lusungo,
Suali hilo ulilouliza nami nilipata kumuuliza marehemu
Mzee Tewa
Said Tewa na ikatokea kwa wakati ule pia kupata taarifa nyingine
kwa TANU kuja kuasisiwa mwaka 1954.
Hadi
Abdul anakuja kuunda TANU yeye mwenyewe alipita hatua
kadhaa.
Hatua hizi ndizo zilizompa ujuzi katika uongozi wa kuhamasisha
umma.
Kuna historia muhimu sana ya
Abdul katika Dockworkers Movement
mwaka 1947 na mgomo uliotokea mwaka ule yaani General Strike.
Mtafiti yoyote ambae atapuuza kipindi hiki hataweza kujua vipi
Abdul
aliweza kuja kufanya mapinduzi na kufanikiwa kuuangusha uongozi
wa TAA chini ya baba yake mkubwa
Mwalimu Thomas Sauti Plantan
akiwa rais na
Clement Mohamed Mtamila akiwa katibu.
Mgomo huu ndiyo uliokuja kumtambulisha
Abdul kwa wananchi
kama kiongozi wa Waafrika.
Lakini kilichofanya hasa
Abdul aje kung'aa ni kifo cha baba yake
Mzee Kleist.
Alipokufa baba yake ikawa sasa
Abdul katoka kwenye kivuli chake
na watu wanamuona yeye kama kiongozi wao na si baba yake.
Abdul hakuwa mwanasiasa wa kupanda jukwaani na hapa nadhani
ndipo muhimu sana katika kuielewa TANU ilivyokuja asisiwa.
Abdul angekuwa mwanasiasa wa majukwaa bila shaka TANU
isingechelewa kuja.
Abdul hakutaka yeye kuwa kiongozi wa juu na moja ya sababu ni
kuwa yeye hakuchukua siasa kama ajira.
Katika miaka ile ya 1950
Abdul alikuwa kijana wa kujiweza sana
kifedha.
Fikra yake ilikuwa kwa
Chief David Kidaha Makwaia atoke kule
alikokuwa katika Legico aachane na Waingereza aje huku kwa
wananchi awe rais wa TAA na kisha waunde TANU na yeye
Chief
Kidaha akiwa rais.
Mpango ule ule ambao
Abdul aliutekeleza kwa ufanisi kwa
Nyerere
mwaka 1953 ambako
Nyerere walimchagua akawa rais wa TAA
Abdul akiwa makamu wake na 1954 wakaunda TANU
Nyerere
akawa rais na
Mzee Rupia makamu wa rais.
Sasa tuje kwenye "practice" ulosema.
Kuna TAA Political Subcommittee iliyoundwa mwaka 1950 ikiwa
na wajumbe hawa:
Mufti Sheikh Hassan bin Amir, Abdul Sykes,
Dr. Vedasto Kyaruzi, Hamza Mwapachu, Said Chaurembo na
Steven Mhando.
Hapa ndipo palipotoka msukumo wa kuunda TANU.
Kamati hii ndiyo iliyoandika memorandum kwa Gavana Twining
kutaka Legco ipigiwe kura na Waingereza wakabidhi nchi baada
ya miaka 13.
Kamati hii ndiyo iliyoandika ile hotuba ya
Nyerere aliyosoma
UNO mwaka wa 1955 na waraka huu ulijadiliwa katika mkutano
wa kuasisi TANU mwaka 1954.
Sasa haya si mambo mepesi kwa mtu wa nje kuyajua.
Mimi nimeyafahamu kwa kuwa ni mtoto wa nyumbani.
Si kitu rahisi
Nyerere aje Dar es Salaam ya 1950 hana amjuae,
hana fedha, hana watu, hana ofisi aunde TANU chama mara moja
kikubalike na kupata nguvu na wanachama.
Ndiyo siku zote mimi husema na hata
Abdul Sykes mwenyewe
alipata kumuambia
Ahmed Rashad Ali kuwa ikiwa
Nyerere anataka
''credit,'' ya kuunda TANU mwacheni aichukue.
Hiki ni kisa kingine.
Ndugu yangu
Lusungo si kama mimi ni mjanja sana kuyajua haya.
Haya ndiyo yalikuwa maisha katika maisha yangu nyumbani kwetu
ilikuwa lazima niyajue sembuse ikawa nawauliza wazee wangu
historia yao.
Mambo ni mengi sana hatuwezi kuyasema yote hapa.
Nadhani umeshatambua kuwa mfano wako wa "biashara ya kandambili"
hapakuwa pake hapa.
Ukipenda kusoma zaidi kuhusu haya ingia hapa:
AHMED RASHAD ALI BINGWA WA PROPAGANDA ZA UKOMBOZI WA AFRIKA SEHEMU YA PILI - Mohamed Said
Abdulwahid Sykes and Dar es Salaam Dockworkers' Union, 1948 Part Three - Mohamed Said