Beating the Drum on One Side: Confusing the People on Both Sides

Beating the Drum on One Side: Confusing the People on Both Sides

I love JF! I real enjoyed reading this thread one contribution after the other. Nilichojifunza;
1. Kuna mada ipo mezani na inatibua vitu ambavyo vimeshawahi kuwasilishwa na mmoja wa wanajukwaa hapo mwanzo.
2. Kuna wachangiaji ambao wanajadili hoja iliyopo mezani na kwa kufanya hivi wanasaidia sana kutoa elimu kwa wengine.
3. Kuna wachangiaji wengine kazi yao ni kuvuruga mjadala ilimradi tu wanayempenda wao aonekane ana watetezi. Kejeli na matusi ndiyo style ya uandishi wao.

Kama wasomi na watanzania tunaoipenda nchi yetu, ni vizuri kuifikiria nchi hii kwanza na vizazi vijavyo badala ya kuwaza kupata umaarufu usio hata na maana yeyote. Kusema uongo ili mradi tu lengo la mhusika litimie haitakiunganisha kizazi kijacho bali ni mbegu ya chuki ambayo itakigawa.

Tupendane sote sababu tuliowakuta walitufundisha upendo. Mijadala ya dini 'hainaga' mshindi.

Tafakari.
 
Sina shida, nilikuwa nataka kuujuwa ukweli tu. Kama na wewe huujuwi basi nisameh sana, sitong'ang'ania tena.

Labda Mag3 atakuja nisaidia swali langu hilo kama alivyosema Ritz.

Pole sana.

Ukhti FF

Nipe wewe basi hilo jibu inaonekana unalijua
 
Last edited by a moderator:
Nimesoma mjadala huu kuanzia uzi wa kwanza mpaka wa mwisho (bandiko la 422). Nimepata elimu na burudani pia. Ahsanteni.
 
Tatizo lako bwana Mohamed Said 'ukiguswa' kidogo tuu, wewe unatiririka na evidences na references za kutosha.

Kufanya mjadala na wewe, mtu anatakiwa ajipange sana vinginevyo ataishia kutukana tuu.
 
Tatizo lako bwana Mohamed Said 'ukiguswa' kidogo tuu, wewe unatiririka na evidences na references za kutosha.

Kufanya mjadala na wewe, mtu anatakiwa ajipange sana vinginevyo ataishia kutukana tuu.

akili ya Mzee Mohamed Said haina tofauti na akili ya Gavana kule jukwaa la dini! Kila kitu ni mabandiko ya page 10 kwa swali la kawaida
 
Last edited by a moderator:
Hilo swali tunaliita Beating the Drum on One Side.

Ngoja tuendelee kuwasubiri wasomi wetu wa JF labda watakuja na jibu.

Labda Mag3 anaweza kujibu ili swali murua!

hata huelewi ulichoandika!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Sana mi nikifikiria mradi Wa kandambili halafu mwingine akadevelop huo mradi utasema wewe ndo muundaji?

Swali linaweza kuja Kama akina Sykes walikuwa na hilo wazo why hawakuliweka kwenye practice mpaka 1954?

Inakuaje tangu WW2 watu wakae na wazo tuu?

Lusungo,
Suali hilo ulilouliza nami nilipata kumuuliza marehemu Mzee Tewa
Said Tewa
na ikatokea kwa wakati ule pia kupata taarifa nyingine
kwa TANU kuja kuasisiwa mwaka 1954.

Hadi Abdul anakuja kuunda TANU yeye mwenyewe alipita hatua
kadhaa.

Hatua hizi ndizo zilizompa ujuzi katika uongozi wa kuhamasisha
umma.

Kuna historia muhimu sana ya Abdul katika Dockworkers Movement
mwaka 1947 na mgomo uliotokea mwaka ule yaani General Strike.

Mtafiti yoyote ambae atapuuza kipindi hiki hataweza kujua vipi Abdul
aliweza kuja kufanya mapinduzi na kufanikiwa kuuangusha uongozi
wa TAA chini ya baba yake mkubwa Mwalimu Thomas Sauti Plantan
akiwa rais na Clement Mohamed Mtamila akiwa katibu.

Mgomo huu ndiyo uliokuja kumtambulisha Abdul kwa wananchi
kama kiongozi wa Waafrika.

Lakini kilichofanya hasa Abdul aje kung'aa ni kifo cha baba yake
Mzee Kleist.

Alipokufa baba yake ikawa sasa Abdul katoka kwenye kivuli chake
na watu wanamuona yeye kama kiongozi wao na si baba yake.

Abdul hakuwa mwanasiasa wa kupanda jukwaani na hapa nadhani
ndipo muhimu sana katika kuielewa TANU ilivyokuja asisiwa.

Abdul angekuwa mwanasiasa wa majukwaa bila shaka TANU
isingechelewa kuja.

Abdul hakutaka yeye kuwa kiongozi wa juu na moja ya sababu ni
kuwa yeye hakuchukua siasa kama ajira.

Katika miaka ile ya 1950 Abdul alikuwa kijana wa kujiweza sana
kifedha.

Fikra yake ilikuwa kwa Chief David Kidaha Makwaia atoke kule
alikokuwa katika Legico aachane na Waingereza aje huku kwa
wananchi awe rais wa TAA na kisha waunde TANU na yeye Chief
Kidaha
akiwa rais.

Mpango ule ule ambao Abdul aliutekeleza kwa ufanisi kwa Nyerere
mwaka 1953 ambako Nyerere walimchagua akawa rais wa TAA
Abdul akiwa makamu wake na 1954 wakaunda TANU Nyerere
akawa rais na Mzee Rupia makamu wa rais.

Sasa tuje kwenye "practice" ulosema.

Kuna TAA Political Subcommittee iliyoundwa mwaka 1950 ikiwa
na wajumbe hawa: Mufti Sheikh Hassan bin Amir, Abdul Sykes,
Dr. Vedasto Kyaruzi, Hamza Mwapachu, Said Chaurembo na
Steven Mhando.


Hapa ndipo palipotoka msukumo wa kuunda TANU.

Kamati hii ndiyo iliyoandika memorandum kwa Gavana Twining
kutaka Legco ipigiwe kura na Waingereza wakabidhi nchi baada
ya miaka 13.

Kamati hii ndiyo iliyoandika ile hotuba ya Nyerere aliyosoma
UNO mwaka wa 1955 na waraka huu ulijadiliwa katika mkutano
wa kuasisi TANU mwaka 1954.

Sasa haya si mambo mepesi kwa mtu wa nje kuyajua.
Mimi nimeyafahamu kwa kuwa ni mtoto wa nyumbani.

Si kitu rahisi Nyerere aje Dar es Salaam ya 1950 hana amjuae,
hana fedha, hana watu, hana ofisi aunde TANU chama mara moja
kikubalike na kupata nguvu na wanachama.

Ndiyo siku zote mimi husema na hata Abdul Sykes mwenyewe
alipata kumuambia Ahmed Rashad Ali kuwa ikiwa Nyerere anataka
''credit,'' ya kuunda TANU mwacheni aichukue.

Hiki ni kisa kingine.
Ndugu yangu Lusungo si kama mimi ni mjanja sana kuyajua haya.

Haya ndiyo yalikuwa maisha katika maisha yangu nyumbani kwetu
ilikuwa lazima niyajue sembuse ikawa nawauliza wazee wangu
historia yao.

Mambo ni mengi sana hatuwezi kuyasema yote hapa.

Nadhani umeshatambua kuwa mfano wako wa "biashara ya kandambili"
hapakuwa pake hapa.

Ukipenda kusoma zaidi kuhusu haya ingia hapa:
http://www.mohammedsaid.com/2014/01/ahmed-rashad-ali-bingwa-wa-propaganda_5272.html

http://www.mohammedsaid.com/2014/03/abdulwahid-sykes-and-dar-es-salaam_7.html
 
Tatizo lako bwana Mohamed Said 'ukiguswa' kidogo tuu, wewe unatiririka na evidences na references za kutosha.

Kufanya mjadala na wewe, mtu anatakiwa ajipange sana vinginevyo ataishia kutukana tuu.

Ndibalema,
Nataka nikuambie kitu kimoja cha faida sana kwa mtu alopita katika madrasa.
Kwanza tunafundishwa "hifdh," yaani ile "power of retention."

Maalim anakusomesha na wewe unatakiwa uhifadhi ile ilm kichwani uweze
kuisoma "ghibu," yaani kutoka kichwani.

Si tu uisome kutoka kichwani ujue na "isnad," yaani rejea yake.

Mwanazuoni yupi kasema nini na yupi mwingine katika somo hilo hilo nini
msimamo wake.

Sasa FF dada yangu husema sisi huenda chuoni wadogo wengine wanakwenda
chuoni watu wazima.

Ndiyo maana unaona kila anaejaribu kumvaa Faiza hafiki mbali anakuwa
keshamshinda.

Kuna msemo wa Kiarabu unasema kuwa anachojifunza mtu utotoni ni kama
maandishi yaliyochongwa kwenye jiwe.

Hayafutiki.

Nadhani elimu hii ya madrasa ndiyo imenifanya niwe hivyo kuwa nisemapo
jambo lazima hadhira niifahaishe hicho kitu nimekitoa wapi.
 
Ukhti FF

Nipe wewe basi hilo jibu inaonekana unalijua

Nimekwambia juu huko na nnarudia tena, mimi nataka uhakika pengine nijuavyo mimi si sawa ndiyo maana nimeuliza, maana kuna ma professor wamenichanganya hapa.
 
Mkuu Mohamed Said

Nakubaliana nawe ktk logic juu ya nani hasa walikerwa na ukoloni na walitoa msukumo Wa kuwaondoa....

Naturally makoloni mengi ya wazungu walitekeleza makubaliano ya Berlin kulinda ukristo ktk colonies zao...

In a logical manner isingekua rahisi anayelindwa ama kubebwa akapambana na anayempa ulinzi au anayembeba....

Lusungo,
Nimekusoma kaka.
 
Nikupe historia yanini wakati mi nahitaji logic toka kwa hoja zenu?

Utaniulizaje maswali ambayo Mimi nimechota kwenye hoja zenu zilizojaa contradictions?

Nyerere kukaa kwa akina Sykes ndo kunakupa shuhuda gani wewe?

Jibu swali inakuwaje huyo mnaesema alikua na wazo hakulitekeleza kaja kutekeleza Nyerere?

Hapa kuna facts na si logic. Kwa kukushauri tu, ikiwa unatafuta logic kwa jambo usilokuwa na ilmu nalo itakuwia vigumu sana.

Ohh kumbe "umechota" kutoka kwetu? ahsante kwa kukiri hilo.

Hilo la "Nyerere kukaa kwa akina Sykes" ni swali nililokuuliza hujalijibu bado. Kama ambavyo hujajibu kuhusu Mau Mau na Wajerumani.

Hilo la mwisho naona Al Alama Mohamed Said kishakujibu kutokea ndani.
 
Last edited by a moderator:
Sasa inakuwaje aliyeasisi asipate kadi nr.1?

Utasemaje TANU kaanzisha Sykes wakati front line anaonekana Nyerere?

Mkuu hapa inahitajika logic tu sio rejea za kitabu chako.

Lusungo,
Unafikiri sawasawa na mimi siwezi kukulaumu kwa hilo.
Mantiki inaweza ikaangushwa na kitu kingine.

Ungejua kadi za TANU zilivyogawiwa ungelijua na kwanini Abdul mkubwa
kapata kadi na. 3 na Ally mdogo kadi yake ni na. 2.

Kadi ya Nyerere ilikuwa lazima iwe na. 1 kwa heshima yake kama rais
wa TANU.

Kadi zile zilinadiwa.
Mwenye dau kubwa anatangulia kuchukua kadi.

Hukuyajua haya.
Ndipo nikasema nakuwia radhi na mantiki si inakuwa sawa muda wote.
 
Nyakageni njoo msome lusungo.

Mkuu Mohamed Said

Nakubaliana nawe ktk logic juu ya nani hasa walikerwa na ukoloni na walitoa msukumo Wa kuwaondoa....

Naturally makoloni mengi ya wazungu walitekeleza makubaliano ya Berlin kulinda ukristo ktk colonies zao...

In a logical manner isingekua rahisi anayelindwa ama kubebwa akapambana na anayempa ulinzi au anayembeba....

Halafu na wewe Nyakageni utupe maoni yako kuhusu haya ya lusungo.

Ukimaliza naomba unijibu, jee, Mau Mau walipigana na Wajerumani?
 
Last edited by a moderator:
Naomba nisaidie hili swali langu dogo; Mau Mau walipigana na Wajerumani?

FaizaFoxy.

Hebu soma hii chini hapa.

Serikali ya Uingereza imekubali kulipa fidia kwa waathiriwa wa vita vya Mau Mau vilivyofanyika nchini Kenya ambapo taifa hilo lilikuwa linapigana kuhakikisha linapata uhuru kutoka kwa wakoloni. Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza William Hague ameliambia Bunge nchini huko kwamba serikali inasikitishwa na kile ambacho kilifanywa wakati wa vita vya Mau Mau na hivyo itatoa fidia yenye thamani ya pauni milioni 19.9.

Hague amekiri tukio lililofanywa na wanajeshi wa Uingereza kwa kuwanyanyasa na kuwatesa wapiganaji na hata wananchi wa kawaida ambao walikuwa wanadaia uhuru wao katika kipindi cha miaka ya 1950.Serikali ya Uingereza imetangaza kuwalipa waathirika 5,228 waliopitia madhira mengi kipindi cha vita vya Mau Mau ambapo wanajeshi wa taifa hilo walivamia hadi kambi za raia wa Kenya kipindi cha vita hivyo.Londona kupitia Waziri Hague imeomba radhi kama ambavyo iliahidi na kisha kutangaza fidia hiyo kutokana na kuguswa na vitendo vya mateso vilivyowakumba wananchi wa Kenya walioshiriki vita vya Mau mau.Hatua ya Serikali ya London kuomba radhi na hatimaye kulipa fidia inakuja baada ya waathiriwa hao wa vita vya Mau Mau kufungua kesi wakilalamikia utesajwi waliokumbana nao wakati wa vita hivyo.Waathiriwa hao wa vita vya Mau Mau kwa miaka kadhaa sasa wamekuwa wakipambana kuhakikisha wanapata fidia hiyo baada ya kutokea vita vya kudai uhuru vilivyofanyika katika miaka ya 1950.



Sasa turudi kwenye hoja yetu Mau Mau waliopigana na Ujerumani?
 
Last edited by a moderator:
Lusungo,
Suali hilo ulilouliza nami nilipata kumuuliza marehemu Mzee Tewa
Said Tewa
na ikatokea kwa wakati ule pia kupata taarifa nyingine
kwa TANU kuja kuasisiwa mwaka 1954.

Hadi Abdul anakuja kuunda TANU yeye mwenyewe alipita hatua
kadhaa.

Hatua hizi ndizo zilizompa ujuzi katika uongozi wa kuhamasisha
umma.

Kuna historia muhimu sana ya Abdul katika Dockworkers Movement
mwaka 1947 na mgomo uliotokea mwaka ule yaani General Strike.

Mtafiti yoyote ambae atapuuza kipindi hiki hataweza kujua vipi Abdul
aliweza kuja kufanya mapinduzi na kufanikiwa kuuangusha uongozi
wa TAA chini ya baba yake mkubwa Mwalimu Thomas Sauti Plantan
akiwa rais na Clement Mohamed Mtamila akiwa katibu.

Mgomo huu ndiyo uliokuja kumtambulisha Abdul kwa wananchi
kama kiongozi wa Waafrika.

Lakini kilichofanya hasa Abdul aje kung'aa ni kifo cha baba yake
Mzee Kleist.

Alipokufa baba yake ikawa sasa Abdul katoka kwenye kivuli chake
na watu wanamuona yeye kama kiongozi wao na si baba yake.

Abdul hakuwa mwanasiasa wa kupanda jukwaani na hapa nadhani
ndipo muhimu sana katika kuielewa TANU ilivyokuja asisiwa.

Abdul angekuwa mwanasiasa wa majukwaa bila shaka TANU
isingechelewa kuja.

Abdul hakutaka yeye kuwa kiongozi wa juu na moja ya sababu ni
kuwa yeye hakuchukua siasa kama ajira.

Katika miaka ile ya 1950 Abdul alikuwa kijana wa kujiweza sana
kifedha.

Fikra yake ilikuwa kwa Chief David Kidaha Makwaia atoke kule
alikokuwa katika Legico aachane na Waingereza aje huku kwa
wananchi awe rais wa TAA na kisha waunde TANU na yeye Chief
Kidaha
akiwa rais.

Mpango ule ule ambao Abdul aliutekeleza kwa ufanisi kwa Nyerere
mwaka 1953 ambako Nyerere walimchagua akawa rais wa TAA
Abdul akiwa makamu wake na 1954 wakaunda TANU Nyerere
akawa rais na Mzee Rupia makamu wa rais.

Sasa tuje kwenye "practice" ulosema.

Kuna TAA Political Subcommittee iliyoundwa mwaka 1950 ikiwa
na wajumbe hawa: Mufti Sheikh Hassan bin Amir, Abdul Sykes,
Dr. Vedasto Kyaruzi, Hamza Mwapachu, Said Chaurembo na
Steven Mhando.


Hapa ndipo palipotoka msukumo wa kuunda TANU.

Kamati hii ndiyo iliyoandika memorandum kwa Gavana Twining
kutaka Legco ipigiwe kura na Waingereza wakabidhi nchi baada
ya miaka 13.

Kamati hii ndiyo iliyoandika ile hotuba ya Nyerere aliyosoma
UNO mwaka wa 1955 na waraka huu ulijadiliwa katika mkutano
wa kuasisi TANU mwaka 1954.

Sasa haya si mambo mepesi kwa mtu wa nje kuyajua.
Mimi nimeyafahamu kwa kuwa ni mtoto wa nyumbani.

Si kitu rahisi Nyerere aje Dar es Salaam ya 1950 hana amjuae,
hana fedha, hana watu, hana ofisi aunde TANU chama mara moja
kikubalike na kupata nguvu na wanachama.

Ndiyo siku zote mimi husema na hata Abdul Sykes mwenyewe
alipata kumuambia Ahmed Rashad Ali kuwa ikiwa Nyerere anataka
''credit,'' ya kuunda TANU mwacheni aichukue.

Hiki ni kisa kingine.
Ndugu yangu Lusungo si kama mimi ni mjanja sana kuyajua haya.

Haya ndiyo yalikuwa maisha katika maisha yangu nyumbani kwetu
ilikuwa lazima niyajue sembuse ikawa nawauliza wazee wangu
historia yao.

Mambo ni mengi sana hatuwezi kuyasema yote hapa.

Nadhani umeshatambua kuwa mfano wako wa "biashara ya kandambili"
hapakuwa pake hapa.

Ukipenda kusoma zaidi kuhusu haya ingia hapa:
AHMED RASHAD ALI BINGWA WA PROPAGANDA ZA UKOMBOZI WA AFRIKA SEHEMU YA PILI - Mohamed Said

Abdulwahid Sykes and Dar es Salaam Dockworkers' Union, 1948 Part Three - Mohamed Said
Mzee Mohamed Said, shukran nafyonza ilm.
 
Last edited by a moderator:
Mwanakijiji,
Tusichanganye mambo huu uzi ni kuhusu Prof. Hirji.

Mnakasha unamchambua Sivalon na Bergen kwa sasa...

Fungua uzi mwingine In Sha Allah tujadili hayo mnayotaka huko.

Hata tukifungua nyuzi kumi Mzee Said hutatujibu; utatuzungusha maneno tu kwa mtindo ule ule...
 
Back
Top Bottom