Siyo kweli. Nyie katoliki tunawaangamiza. Mpaka muanze kuikimbia dini yenu.
Author:
Paul Bonaventure
@Phbhimself
"Kwenye anga la operesheni za kisaikolojia, kitu cha kwanza kinachofanyiwa forensic scan ni chanzo cha tamko, target yake, na intention yake.
Ukiangalia tamko la TEC kwa macho ya kawaida linaweza kuonekana kama statement ya imani, lakini tukitumia lenzi za intel, picha halisi inaonekana tofauti kabisa.
Tamko lile halikuwa la kidini, halikuwataka waumini wachukue upande wa dhehebu, na halikutaja taasisi yoyote ya dini kama adui.
Lilikuwa briefing ya taasisi ya kiroho iliyotimiza wajibu wa kulinda watu wake, si kwa misingi ya dini, bali kwa misingi ya utu na ukweli.
Katika lugha ya ndani tunasema kwamba, Source haikuingia kwenye operation kama sect, iliingia kama conscience of the nation.
Na hilo ndilo lililoshtua baadhi ya wahusika.
Kwa sababu tamko la TEC halikufanya operesheni ya identity mobilization. Halikusema Wakatoliki. Halikusema Kanisa. Halikuweka alama za utambulisho za kidini.
Lilichofanya ni kuwasilisha intel ya uhalisia wa ardhi, ripoti ya kinachoendelea Tanzania kwa sasa, jinsi watu wanavyouawa, kutoweka, kujeruhiwa.
Na jinsi taifa linavyoingia kwenye kile ambacho katika uwanja wetu huitwa national trauma loop.
Kwa lugha ya kitengo cha uchambuzi wa migogoro, tamko lile lilikuwa, Faith based early warning on human security breach.
Na hapa ndipo sintofahamu imezaliwa.
Wale wanaotaka kugeuza kila kitu kuwa vita ya utambulisho wanataka tamko ligeuzwe na kuonekana kama shambulio la kidini.
Ilhali waliojua kusoma alama za intel wanaona kilichoandikwa ni protection alert, kwa raia wanaonyamaza kwa sababu ya woga, si kwa sababu ya imani.
TEC hawakuzungumza kama kanisa walizungumza kama walinzi wa dhamiri za watu wao.
Na katika operesheni ya maadili ya taifa, hilo ni jukumu ambalo halihitaji kibali cha mtu yeyote.
Hivyo kauli zinazojaribu kulichora tamko lile kama propaganda ya dini ni sehemu ya kile katika kitengo cha psychological operations tunaita.
"narrative misdirection" mbinu ya kuhamisha mjadala kutoka maovu yaliyotendeka hadi kwenye utambulisho wa mtoa taarifa.
Lakini hoja inabaki palepale. Tamko la TEC halikutaja dini nyingine, halikutaja kiongozi wa dhehebu lolote, halikutangaza mgawanyiko.
Lilieleza tu kile ambacho raia wanaona, lakini wanaishi kama vile hawakioni kwa sababu ya hofu, vitisho na propaganda.
Na kwenye ardhi ya intel tunajua kanuni moja isiyopingika. Kwamba, unapopaza sauti juu ya majeraha ya taifa, wale walioumiza au wanaonufaika na ukimya ndio wanaopiga kelele zaidi.
Kwa hiyo jitihada za kugeuza tamko lile kuwa mbegu ya mgawanyiko wa kidini hazina msingi ni jaribio la kupoteza umma msituni ili wasiulize maswali ya msingi kuhusu uhalifu uliotokea na unaoendelea.
Katika nchi yenye msongo kama Tanzania ilivyo sasa, sauti yoyote inayosema ukweli bila kificho inaonekana kama mshambuliaji.
TEC hawakuendesha operesheni ya dini.
Waliendesha operesheni ya dhamiri.
Na dhamiri inapoongea, wahusika wa giza ndio wa kwanza kupiga makelele.
"
View: https://x.com/Phbhimself/status/1991182669057790433