Bashungwa hayati JPM alijenga vituo vya afya 1000 bila tozo. Acha kuzebeza wananchi

Nyankurungu2020

JF-Expert Member
Oct 2, 2020
4,086
6,568
Wewe mwenyewe ulishuhudia na uliona namna alivyotekeleza
👇

===
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Innocent Bashungwa amesema Serikali imejenga vituo vya afya 234 kutokana na fedha za tozo ya miamala ya simu ndani ya mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwake.

Bashungwa ameyasema hayo leo Septemba Mosi wakati akizungumzia manufaa ya tozo hizo ambazo zimekuwa zikipingwa na wadau mbalimbali kwa sababu tofauti ikiwemo kutozwa mara mbili au zaidi.

Amesema hadi kufikia Desemba 2020, Serikali ilikuwa imejenga hospitali za wilaya 102, vituo vya afya 487 na zahanati 1,198.

Amesema serikali ilifanya tathmini ya hali ya hospitali hizo na kuja na mradi wa kujenga vituo vya afya kwenye kila tarafa.

Amesema katika tarafa 570, tayari serikali imejenga vituo vya afya 234 kwenye tarafa 207 ndani ya mwaka mmoja wa Rais Samia Suluhu Hassan ambaye aliingia madarakani Machi 19, 2021 baada ya kifo cha mtangulizi wake, Hayati John Magufuli.

“Kupitia tozo za miamala ya simu, tumeweza kujenga vituo vya afya 234 kwa Sh117 bilioni kwenye hizi tarafa 207 na kila kituo cha afya kimetugharimu Sh500 milioni.

“Ukiangalia toka nchi yetu imepata uhuru na awamu zote zilizotangulia, kuweza kujenga vituo vya afya 234 ndani ya mwaka mmoja, si jambo la kawaida,” amesema Bashungwa.

Amesema kinachopatikana kutoka kwenye kodi jumuishi, kinakwenda kutibu kiu ya wananchi ya kupata huduma za msingi kama vile afya, elimu na barabara na inasaidia kupunguza pengo kati ya wenye nanchi na wasio nacho.

“Tutaendelea kuhakikisha kwamba tunazitumia fedha hizi kutoa huduma bora za afya ya msingi katika maeneo mbalimbali nchini,” amesisitiza Bashungwa.

Kwa upande wa sekta ya elimu, amesema kutokana na idadi kubwa ya wanafunzi wanaojiunga na kidato cha kwamba, serikali inatakiwa kuendelea kujenga madarasa 15,000 kila mwaka ili kukidhi mahitaji hayo.

“Tathmini ambayo tumeifanya tunahutaji kuendelea kujenga madarasa yasiyopungua 15,000 kila mwaka hadi hawa waliopo kidato cha kwanza watakapoingia kidato cha sita, niwaombe Watanzania hii nchi ni ya kwetu tuendelee kuipa ushirikiano Serikali,” amesema Bashungwa.

Chanzo: Mwananchi
 
Magufuli aliongoza kwa kukopa na huyu anawaibia wananchi kwa jina la tozo huku akiendelea kukopa.

Wote wawili ni incompetent and failures.
 
Ukiondoa maumivu ya tozo,ukweli hivyo vituo vya afya vinajengwa na vinasaidia sana vijijini hususani wakinamama. Na ajira pia vinatoa.

Ila serikali iangalie namna bora nyingine ya kutafuta hizo fedha.
 
Wewe mwenyewe ulishuhudia na uliona namna alivyotekeleza
👇

===
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Innocent Bashungwa amesema Serikali imejenga vituo vya afya 234 kutokana na fedha za tozo ya miamala ya simu ndani ya mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwake.

Bashungwa ameyasema hayo leo Septemba Mosi wakati akizungumzia manufaa ya tozo hizo ambazo zimekuwa zikipingwa na wadau mbalimbali kwa sababu tofauti ikiwemo kutozwa mara mbili au zaidi.

Amesema hadi kufikia Desemba 2020, Serikali ilikuwa imejenga hospitali za wilaya 102, vituo vya afya 487 na zahanati 1,198.

Amesema serikali ilifanya tathmini ya hali ya hospitali hizo na kuja na mradi wa kujenga vituo vya afya kwenye kila tarafa.

Amesema katika tarafa 570, tayari serikali imejenga vituo vya afya 234 kwenye tarafa 207 ndani ya mwaka mmoja wa Rais Samia Suluhu Hassan ambaye aliingia madarakani Machi 19, 2021 baada ya kifo cha mtangulizi wake, Hayati John Magufuli.

“Kupitia tozo za miamala ya simu, tumeweza kujenga vituo vya afya 234 kwa Sh117 bilioni kwenye hizi tarafa 207 na kila kituo cha afya kimetugharimu Sh500 milioni.

“Ukiangalia toka nchi yetu imepata uhuru na awamu zote zilizotangulia, kuweza kujenga vituo vya afya 234 ndani ya mwaka mmoja, si jambo la kawaida,” amesema Bashungwa.

Amesema kinachopatikana kutoka kwenye kodi jumuishi, kinakwenda kutibu kiu ya wananchi ya kupata huduma za msingi kama vile afya, elimu na barabara na inasaidia kupunguza pengo kati ya wenye nanchi na wasio nacho.

“Tutaendelea kuhakikisha kwamba tunazitumia fedha hizi kutoa huduma bora za afya ya msingi katika maeneo mbalimbali nchini,” amesisitiza Bashungwa.

Kwa upande wa sekta ya elimu, amesema kutokana na idadi kubwa ya wanafunzi wanaojiunga na kidato cha kwamba, serikali inatakiwa kuendelea kujenga madarasa 15,000 kila mwaka ili kukidhi mahitaji hayo.

“Tathmini ambayo tumeifanya tunahutaji kuendelea kujenga madarasa yasiyopungua 15,000 kila mwaka hadi hawa waliopo kidato cha kwanza watakapoingia kidato cha sita, niwaombe Watanzania hii nchi ni ya kwetu tuendelee kuipa ushirikiano Serikali,” amesema Bashungwa.

Chanzo: Mwananchi
Tupe Orodha maana seems wewe unaelewa kuliko serikali..

Ulivyo poyoyo unashindwa kuelewa kwamba toka uhuru Tanzania haina hata vituo vya afya 1,000..

Basi tufanye kwamba kulikuwa hakuna kituo Cha afya hata kimoja ila alijengwa Mwendazake 😆😆
 

Attachments

  • Screenshot_20220402-214712.png
    Screenshot_20220402-214712.png
    181.7 KB · Views: 6
  • Screenshot_20220402-215025.png
    Screenshot_20220402-215025.png
    51.5 KB · Views: 5
Kwa uwelewa wangu mdogo...
Kuwa hizi tozo zina bana maskini ila wao viongozi bado wana kula maisha na V8.
 
Back
Top Bottom