Nyankurungu2020
JF-Expert Member
- Oct 2, 2020
- 4,086
- 6,568
Wewe mwenyewe ulishuhudia na uliona namna alivyotekeleza
👇
===
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Innocent Bashungwa amesema Serikali imejenga vituo vya afya 234 kutokana na fedha za tozo ya miamala ya simu ndani ya mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwake.
Bashungwa ameyasema hayo leo Septemba Mosi wakati akizungumzia manufaa ya tozo hizo ambazo zimekuwa zikipingwa na wadau mbalimbali kwa sababu tofauti ikiwemo kutozwa mara mbili au zaidi.
Amesema hadi kufikia Desemba 2020, Serikali ilikuwa imejenga hospitali za wilaya 102, vituo vya afya 487 na zahanati 1,198.
Amesema serikali ilifanya tathmini ya hali ya hospitali hizo na kuja na mradi wa kujenga vituo vya afya kwenye kila tarafa.
Amesema katika tarafa 570, tayari serikali imejenga vituo vya afya 234 kwenye tarafa 207 ndani ya mwaka mmoja wa Rais Samia Suluhu Hassan ambaye aliingia madarakani Machi 19, 2021 baada ya kifo cha mtangulizi wake, Hayati John Magufuli.
“Kupitia tozo za miamala ya simu, tumeweza kujenga vituo vya afya 234 kwa Sh117 bilioni kwenye hizi tarafa 207 na kila kituo cha afya kimetugharimu Sh500 milioni.
“Ukiangalia toka nchi yetu imepata uhuru na awamu zote zilizotangulia, kuweza kujenga vituo vya afya 234 ndani ya mwaka mmoja, si jambo la kawaida,” amesema Bashungwa.
Amesema kinachopatikana kutoka kwenye kodi jumuishi, kinakwenda kutibu kiu ya wananchi ya kupata huduma za msingi kama vile afya, elimu na barabara na inasaidia kupunguza pengo kati ya wenye nanchi na wasio nacho.
“Tutaendelea kuhakikisha kwamba tunazitumia fedha hizi kutoa huduma bora za afya ya msingi katika maeneo mbalimbali nchini,” amesisitiza Bashungwa.
Kwa upande wa sekta ya elimu, amesema kutokana na idadi kubwa ya wanafunzi wanaojiunga na kidato cha kwamba, serikali inatakiwa kuendelea kujenga madarasa 15,000 kila mwaka ili kukidhi mahitaji hayo.
“Tathmini ambayo tumeifanya tunahutaji kuendelea kujenga madarasa yasiyopungua 15,000 kila mwaka hadi hawa waliopo kidato cha kwanza watakapoingia kidato cha sita, niwaombe Watanzania hii nchi ni ya kwetu tuendelee kuipa ushirikiano Serikali,” amesema Bashungwa.
Chanzo: Mwananchi
👇
===
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Innocent Bashungwa amesema Serikali imejenga vituo vya afya 234 kutokana na fedha za tozo ya miamala ya simu ndani ya mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwake.
Bashungwa ameyasema hayo leo Septemba Mosi wakati akizungumzia manufaa ya tozo hizo ambazo zimekuwa zikipingwa na wadau mbalimbali kwa sababu tofauti ikiwemo kutozwa mara mbili au zaidi.
Amesema hadi kufikia Desemba 2020, Serikali ilikuwa imejenga hospitali za wilaya 102, vituo vya afya 487 na zahanati 1,198.
Amesema serikali ilifanya tathmini ya hali ya hospitali hizo na kuja na mradi wa kujenga vituo vya afya kwenye kila tarafa.
Amesema katika tarafa 570, tayari serikali imejenga vituo vya afya 234 kwenye tarafa 207 ndani ya mwaka mmoja wa Rais Samia Suluhu Hassan ambaye aliingia madarakani Machi 19, 2021 baada ya kifo cha mtangulizi wake, Hayati John Magufuli.
“Kupitia tozo za miamala ya simu, tumeweza kujenga vituo vya afya 234 kwa Sh117 bilioni kwenye hizi tarafa 207 na kila kituo cha afya kimetugharimu Sh500 milioni.
“Ukiangalia toka nchi yetu imepata uhuru na awamu zote zilizotangulia, kuweza kujenga vituo vya afya 234 ndani ya mwaka mmoja, si jambo la kawaida,” amesema Bashungwa.
Amesema kinachopatikana kutoka kwenye kodi jumuishi, kinakwenda kutibu kiu ya wananchi ya kupata huduma za msingi kama vile afya, elimu na barabara na inasaidia kupunguza pengo kati ya wenye nanchi na wasio nacho.
“Tutaendelea kuhakikisha kwamba tunazitumia fedha hizi kutoa huduma bora za afya ya msingi katika maeneo mbalimbali nchini,” amesisitiza Bashungwa.
Kwa upande wa sekta ya elimu, amesema kutokana na idadi kubwa ya wanafunzi wanaojiunga na kidato cha kwamba, serikali inatakiwa kuendelea kujenga madarasa 15,000 kila mwaka ili kukidhi mahitaji hayo.
“Tathmini ambayo tumeifanya tunahutaji kuendelea kujenga madarasa yasiyopungua 15,000 kila mwaka hadi hawa waliopo kidato cha kwanza watakapoingia kidato cha sita, niwaombe Watanzania hii nchi ni ya kwetu tuendelee kuipa ushirikiano Serikali,” amesema Bashungwa.
Chanzo: Mwananchi