- Mkuu hapo juu samahani sana kama nimekukwaza na hizo info nilizozitoa ambazo bado hazijakamilika, ukweli ni kwamba tunaoshirikiana katika matayarisho toka majuzi tumekua tukiwaarifu wananchi karibu wote walioko US, na hata nje kuhusu matayarisho haya, nia na madhumuni ni kuwapa nafasi wananchi wanaopenda kuja kushiriki nafasi ya kujipanga mapema kama vile ilivyokuwa kwenye sherehe ya kumuaga Balozi Chagula, Blalozi Mwakawago, kumuaga rais Mkapa, Kumpongeza Mzee Malecela kwa kuoa, kumkaribisha Mama Migiro njia iliyotumika ni hii hii ya kufahamishana mapema na baadye kupeana all the details, lakini cha muhimu ni kwamba itafanyika,
- Ingawa pia kuna tofauti moja ya hii sherehe kwamba itaanzia kwenye cookout, yaani nje maana zile zingine zote zilifanyika ndani mwanzo mpaka mwisho, tunahitaji wiki mbili kabla kupata uhakika wa 85%, kwamba hali ya hewa itakuwa muswanu hiyo siku au tutabadili tarehe, otherwise matayarisho yanaendelea kwa nguvu moja na ushirikiano wa hali ya juu sana baina yetu wananchi, punguza jazba maana hii ni socialization tu baina yetu wananchi badala ya kuisubiri serikali kutufanyia tunaweza kuji-organize na kufanya wenyewe,
- Hayo ya kupeleka nyama mbichi sijawahi kuyasikia hata siku moja, kwamba mtu akikualika kwenye cookout basi anategemea uende na nyama mbichi hayo ni mageni sana kwangu, nijuavyo watu huenda na vinywaji, vyakula vya aina mbali mbali, wengine huamua kuepeleka keki, lakini eti unategemewa kupeleka nyama mbichi au kule kwenye sherehe kuna anayesubiri upeleke nyama mbichi hayo mbona makubwa sana na ni ukuzaji wa mambo wa hali ya juu sana you must be an expert wa kutunga majungu mkuu, maana this is over the board and unheard off duh! Yaani ile shughuli ya cookout ya Columbus watu waliambiwa kwenda na nyama mbichi, I am lost na this!
Otherwise, kama upo hayo maeneo unakaribishwa sana, na wala usihangaike na kubeba nyama mbichi, labda huenda una experience flani ya kualikwa na kutegemwa kupeleka nyama mbichi, ninarudia tena kwamba not this one feel free kama una mpango wa kuja, na ukifika pale Wilson Woods nitafute kama unahitaji msaada nitakuwepo siku hiyo kuanzia asubuhi mpaka asubuhi tena shughuli zitakapokwisha kama zitafanyika siku hiyo kama zilivyopangwa, na wananchi wengi na viongozi wengi tayari wamethibitisha kuhudhuria hizi shughuli kama tulivyowatangazia.
- Na mwishoni mwa wiki hii nitakuwa na matokeo ya wataalam wa hali ya hewa na nitathibitisha kuwepo hiyo siku yaani tarehe 27, June 2009 kuanzia mchana saa saba mpaka asubuhi ya tarehe 28, June 2009.
Again samahani sana kama nimekukwaza, pole sana mkuu maana sio rahisi mtu kuandiak wka hasira kama ulivyoanza bila ya kukwazika, tusameheane ndugu yangu.
Ahsante.
William.