Barua: Zitto akataa posho za vikao

Barua: Zitto akataa posho za vikao

Jifunze kuandika kwanza, panga sentensi zako vizuri, zingatia alama za kuuliza na alama za mashangao, ni hayo tu. sina la kuchangia hapa thread haijapangiliwa vizuri kunishawishi kuchangia.

Mkuu, unapotuambia huwezi kuchangia kwa sababu ya mpangilio, tunakuwa na wasiwasi na uwezo wa akili yako. Kama vipi changia bana, ukigundua hakuna nukta wewe weka tuone tofauti.

Muulize Zitto fedha za kununulia hammer alifanya biashara gani halali kumfanya posho halali aone ndio mahali pa kuhoji uhalali, japo siziungi mkono hizo posho.

Maamuzi yake amekishirikisha chama au anataka kutenda ili aonekane kama anavyojipembua kwa hammer!!! ha ha ha haa! nitarudi baadae
 
This is Double Standards "mimi posho sitaki, lakini nataka zipelekwe kwetu. vile vile CHADEMA wamekosa leadership katika hilii, kama ni kweli limo katika bajeti kivuli iliyopitishwa na chama how on earth wabunge wake wataendelea kupokea hizo posho. Wasipokuwa makini suala hili litaback fire kwao kama amabavyo limeanza kwa kila mtu kuwa na lwake.

Mkuu ni kweli hapa kuna tatizo. Kuna tatizo la umaarufu wa mtu mmoja mmoja badala ya umaarufu wa Chama. Kama ni uamuzi wa Chama na unatekelezwa na Zitto tu basi kuna shida. Tatizo ni kwamba humu ndani tunataka kujifanya ni Mbuni hasa linapokuja suala la kujadili matatizo ya CHADEMA. Haiingii akilini kwamba Zitto peke yake ndio atekeleze maamuzi ya Chama tena kwa kujipigia pasi eti pesa ziende KDI.

Wako wapi wabunge wengine wa Chadema? Zitto sasa ndio shujaa wa Chadema kwa kukataa posho wakati akina Joseph Selasini, Joseph Mbilinyi na kadhalika wanazichukua. Tuangalie mambo kwa mioyo iliyopondeka ni kuangalia kwa ukengeufu wa mawazo.

Kwa hili la posho tuangalie muda si muda patawaka mioto kama si moto
 
mkuu, unapotuambia huwezi kuchangia kwa sababu ya mpangilio, tunakuwa na wasiwasi na uwezo wa akili yako. kama vipi changia bana, ukigundua hakuna nukta wewe weka tuone tofauti. muulize zitto fedha za kununulia hammer alifanya biashara gani halali kumfanya posho halali aone ndio mahali pa kuhoji uhalali, japo siziungi mkono hizo posho. maamuzi yake amekishirikisha chama au anataka kutenda ili aonekane kama anavyojipembua kwa hammer!!! ha ha ha haa! nitarudi baadae

karibu tena msee wangu
 
tena unafiki wa kutaka kuoneka mzuri machoni pa watanzania,,leo kuna familia ngapihuko jimboni mwako maskini wa kutupwakwa nini usingepeleka hizo posho moja kwa moja kwenye familia maskini kabisaili ziweze kuwasaidia kwa sababu ni pesa zaonarudia huo ni unafiki wa kutaka kuoneka mzuri machoni pa watanzania

Ni kweli posho amezikataa ila umesikia kasema zipelekezwe wapi? Au unabwatuka tu.
 
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, ameiandikia barua Ofisi ya Bunge kuiomba isimamishe kumlipa posho zake zinazotokana na vikao vya Bunge kuanzia juzi. Zitto ametoa ombi hilo kwa barua rasmi aliyoiwakilisha kwa Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah Juni 7 mwaka huu.
Mbona NDESAMBURO hAPOKEI HATA SH 10?????????????! nA AMEANZA TOKA KITAMBO chadema TUpo Juuuuuuu
 
tena unafiki wa kutaka kuoneka mzuri machoni pa watanzania,,leo kuna familia ngapi
huko jimboni mwako maskini wa kutupwa
kwa nini usingepeleka hizo posho moja kwa moja kwenye familia maskini kabisa
ili ziweze kuwasaidia kwa sababu ni pesa zao
narudia huo ni unafiki wa kutaka kuoneka mzuri machoni pa watanzania

Zitto kwa kuzikataa hizo posho anawasaidia wapiga kura wake wa Kigoma kwani sasa serikali itakuwa na fedha zaidi [ kuliko kama angekomba hiyo posho] za kuwanunulia madawa kwenye vituo vyao vya afya!! Hapo unafiki wa Zitto uko wapi?
 
mkuu, unapotuambia huwezi kuchangia kwa sababu ya mpangilio, tunakuwa na wasiwasi na uwezo wa akili yako. kama vipi changia bana, ukigundua hakuna nukta wewe weka tuone tofauti. muulize zitto fedha za kununulia hammer alifanya biashara gani halali kumfanya posho halali aone ndio mahali pa kuhoji uhalali, japo siziungi mkono hizo posho. maamuzi yake amekishirikisha chama au anataka kutenda ili aonekane kama anavyojipembua kwa hammer!!! ha ha ha haa! nitarudi baadae

Ndugu hili la kununua hammer ndio linakutoa roho!!, sawa anaweza akawa ufisadi ila sijui, lakini Mh Zitto kawa mbunge siku nyingi kwani hammer inauzwa Sh ngapi! kwani Mh Zotto hakopesheki Bank, acha mawazo finyu, kukopa Bank Tsh 100 to 500 million ni kawaida kwa watu wa kada ya kati kwa TZ siku hizi, inategemea unalipwa kiasi gani na unavitega uchumi vipi na vinazalisha kiasi gani!
 
Nadhani yale maradhi yanayomsubuwa Zitto (Mungu amuondoshee) yanamfanya apoteze uwezo wa kuwa makini na fufikiri vizuri licha ya kumzdishia uzembe.a

Lakini kwa upande mwingine anaonesha mfano na anataka aigwe, Sasa tutazame, Jee ni wangapi watamfuata.

Ushauri wa kuanza kutowa posho yake nilimpa jana kwenye ile nyuzi yenye Taarifa ya upinzani ya bajeti, kama sikosei kwenye post #49, na wakati huo alikuwepo JF, nashkuru kuwa ameufanyia kazi ushauri wangu.
 
hiki ni kipimo cha dhati kwa wabunge wote wapambanaji, na wala wasirudi nyuma kwa hilo tuko pamoja.hiyo hele hata magamba itawasuta mbona wataiacha wote? lazima mwanzo watu wajitoe muhanga ili kufikia malengo
 
Oooooh CDM... mkombozi wetu kwa vitendo zaidi

hongera mh zitto najua una baraka zote za chama, wengine watakufuata
 
Kudos Zitto.

Kiongozi ni yule anayeongoza kwa mfano. Aja ya mja kunena, muungwana ni kitendo.
 
naomba nieleweke,kususia posho inamsaidia nini???maaana yangu hizo posho ange bypass ziwaendee familia zilizo maskini kabisa kwenye jimbo lake,nafikiri ni usahuri wa maana
tatizo lenu mnapenda kukurupuka na kuunga mkono kila jambo hata kama ni upumbavu!
Zito hajasusia posho ila amezielekeza jimboni kwake, jambo ambalo ni zuri tu. Wewe hujaelewa unakurupuka na kuleta ushauri wako usio na maana hapa. Unatakiwa uisome taarifa vizuri ndio utoe ushauri mwafaka. Posho ya kikao haiwezi kusaidia familia mojamoja maskini, wala umaskini hauwezi kuondolewa kwa kugawia fedha kila familia kwani kwa kufanya hivyo utazifanya familia hizo kuwa tegemezi milele. Jawabu hapo ni kuwawezesha familia mojamoja kuzalisha chakula chao na mahitaji yao mengine. Hilo ndilo alilo lenga Kabwe. Labda utuambie unachuki binafsi na Zito na ndio maana unamshambulia hapa na kututukana sisiwachgiaji wa thread yako ya ovyo.
 
Mimi nampongeza zitto kwa kutaa posho kaonyesha mfano kama yeye ni mpigaji anayeyetetea majority ya watanzania wanaoishi chini dola moja wakati wengine wanapigania posho ambazo zingepelekwa kujenga mabala kwenye shule za kata, kuongeza mishara ya walimu,kujenga zahanati nk. Huo sio unafiki ni mfano mzuri kwa wapigaji wengine.
 
Hongera Mh - Umeonesha njia sijui hizi ni pamoja na za vikao vya kawaida vya bunge au ni zile za kazi maalum. Which ever way - Hongera.
Ila sasa una kazi ya kufanya - kuwashawishi wengine waone mantiki ya kufanya hivyo ukianza na ndani ya CDM. Tunakuunga mkono kweny effort hizo. Nasema una kazi kwani ukibaki peke yako itakuwa kama ya Pinada kukataa shangingi la 280m/= akasema labda apewe mwingine(maana yake hakuwa tayari kushawishi na hata kwa kutumia nafasi yake kupendekeza yauzwe- the Rwanda way)

BIG UP CDM- TAKE LESSON!
 
naomba nieleweke,kususia posho inamsaidia nini???maaana yangu hizo posho ange bypass ziwaendee familia zilizo maskini kabisa kwenye jimbo lake,nafikiri ni usahuri wa maana
tatizo lenu mnapenda kukurupuka na kuunga mkono kila jambo hata kama ni upumbavu!

Join Date : 17th May 2011
Posts : 278
Thanks 3
Thanked 19 Times in 16 Posts Rep Power : 21

Umetumwa? Au ndio wale wale wa jamaa yetu, huyu kama sio Chiligati basi ni Nduga
i.
 
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, ameiandikia barua Ofisi ya Bunge kuiomba isimamishe kumlipa posho zake zinazotokana na vikao vya Bunge kuanzia juzi.

Zitto ametoa ombi hilo kwa barua rasmi aliyoiwakilisha kwa Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah Juni 7 mwaka huu.

CCM ought to know that the best way to win an argument is to keep quite. Bwana mmoja alipoulizwa alisema waanze wao kusamehe posho sasa huyo kaanza wabunge wengine wakifuata hatua ijayo ni kuanza CCM kuishi kwa kutumia breathing mashine.
 
Hongera Mh - Umeonesha njia sijui hizi ni pamoja na za vikao vya kawaida vya bunge au ni zile za kazi maalum. Which ever way - Hongera. Ila sasa una kazi ya kufanya - kuwashawishi wengine waone mantiki ya kufanya hivyo ukianza na ndani ya CDM. Tunakuunga mkono kweny effort hizo. Nasema una kazi kwani ukibaki peke yako itakuwa kama ya Pinada kukataa shangingi la 280m/= akasema labda apewe mwingine(maana yake hakuwa tayari kushawishi na hata kwa kutumia nafasi yake kupendekeza yauzwe- the Rwanda way)

BIG UP CDM- TAKE LESSON!
 
Zitto aache janja yake! Anatupiga tu wananchi changa la macho. Hii Kigoma Development Initiative(KDI) ni NGO yake mwenyewe! So hizo allowance zinamrudia yeye mwenyew


halafu wewe ni regia au mwanachadema mwenzake kabisaaa, yani unatia kinyaa kabisa unafiki utakuua na uroho na wewe fungua yako shetani kabisa
 
Kimbunga Zito Aseme kwa niaba ya chama kwani hizo posho huwa zinasainiwa na kuchukuliwa na chama? posho ni kwa ajili ya mbunge binafsi na hata kwenye kuzikataa kila mbunge yapaswa aandike barua yake mwenyewe(binafsi sio chama). wapo waliotangulia kuzikataa kabla ya zito, Ndesamburo posho upeleka kwenye mfuko wa maendeleo ya jimbo lake lkn hajajitangaza. kwa hiyo zito naye ameonyesha mfano na wengine wataiga na watafuata.
 
Back
Top Bottom