Barua: Zitto akataa posho za vikao

Barua: Zitto akataa posho za vikao

Tena unafiki wa kutaka kuoneka mzuri machoni pa watanzania,,leo kuna familia ngapi, huko jimboni mwako maskini wa kutupwa
kwa nini usingepeleka hizo posho moja kwa moja kwenye familia maskini kabisa, ili ziweze kuwasaidia kwa sababu ni pesa zao?

Narudia huo ni unafiki wa kutaka kuoneka mzuri machoni pa Watanzania.

Jamani, sio nyinyi mliokuwa wa kwanza kumtaka aziache hizo posho? Kaziacha imekuwa maneno!
Hata nyinyi acheni unafiki
 
Tena unafiki wa kutaka kuoneka mzuri machoni pa watanzania,,leo kuna familia ngapi, huko jimboni mwako maskini wa kutupwa
kwa nini usingepeleka hizo posho moja kwa moja kwenye familia maskini kabisa, ili ziweze kuwasaidia kwa sababu ni pesa zao?

Narudia huo ni unafiki wa kutaka kuoneka mzuri machoni pa Watanzania.

Kweli Zitto ni mnafiki kwa kitendo chake cha kugawa Posho yake kwa taasisi badala ya kusaidia familia zenye shida.

Twende hatua ya pili na kutafakari nani ni mnafiki zaidi kati ya Zitto na wafuatao?

1. Anayesafiri nje kila mwezi wakati wagonjwa wanalala chini mahospitalini.

2. Anayetembea na msafara wa magari 20 wakati watoto wa shule wanasoma kwenye vumbi bila madawati

3. Mawaziri wanaoruhusu bilioni 90 zitumke kwa vitafunio maofisini wakati wanafunzi wa vyuo vikuu wananyimwa mikopo ili wasome.

4. Chama kinachotumia mabilioni kwa ajili ya sherehe za uhuru wakati wafanyakazi wanalipwa mshahara kiduchu

5. Chama kinachoruhusu wizara kuagiza timu ya brazili kuja kucheza nchini kwa gharama ya mamilioni za nchi wakati mamia ya wananchi hawajui kesho watakula nini.

6. Mawaziri wanaoshindwa kukumea wizi wa wazi unaofanywa kwenye taasisi za umma, wakati nchi inazidi kudididmia kiuchumi

7.Chama kinachoruhusu nchi isiwe na umeme miaka 50 baada ya uhuru na kutokuwa na ufumbuzi wa kudumu wa tatizo hilo.
 
Binafsi nalitazama kwa mtazamo tofauti hili la zitto, nafikili na suala la ujasili na uzalendo zaidi, kwani issue hapa ni kupereka message na kusimamia anachokiamini na kutekerenza kwa vitendo ni jukumu la viongozi wetu kwa maana ya wabunge na pengine na mawaziri wetu kuchukua hatuta madhubuti kama dhamira ya kunyenyua maisha ya watanzania,

Binafsi napenda niliongelee hivyo ukiwa msimamo wangu binafsi pasina kuangalia ushabiki au tofauti za kifalsafa kama mtu atafika atacha ubinafsi wa kukataa pesa iliapate sifa macho kwa watanzania nahisi ni dhana nzuri, naitafika sehemu mtu atakataa rushwa au ufisadi ili aonekane mwema machoni mwa watanzania atakuwaanfaa, hiyo binafsi nahisi itakuwa ni hatua ya kwanza muhimu, Hatua ya pili itafika mtu atasutwa na kusukumwa na dhamira yake na kumuogopa mungu wake, lakini hatuwezifika hatua ya pili kabla ya hatua ya kwanza.

Nawasilisha.
 
Kwani kupeleka kwenye jumuiya ya maindeleo ya kigoma sio kusaidia masikini, akili yako imekaa kigambagamba tu. Uko mtupu mno kifikra. Tumia muda kidogo kufikiri, kutafakari na kuchukau hatua.

Nadhani yeye anamhitaji Mh. Zitto achukue hizo hela mkononi halafu aende anapita nyumba kwa nyumba anazigawia wananchi maskini. Mbona akifanya hivyo hata Kigoma hazitafika? Zitaishia hapa tu kwa watani zangu akina agwe, hata jimboni kwake hatazifikisha, unless apande ndege wakati wa kuzipeleka. Maana kama ni hivyo wanachi maskini hata hapa Dar es salaam tumejaa! Utachukua hela kwa ajili ya watanzania maskini, halafu usafiri nayo uko ndani ya gari, kutoka dodoma au dar es Salaam halafu kweli ufike nayo Kigoma? Thubutu, lazima tu uzalendo utakushinda, sababu kubwa ikiwa ni kwamba, kwanza, ile hela ni ya watanzania wote!
 
Rijero sikushangai kwani wakati wa harakati za akina MALCOM X na MALTIN LUTHUR, Walikuwepo manigers walijipendekeza kwa mafolks, walihitwa 'UNCLE TOM' Endelea lakini ZITO has a dream.
 
bravo kamanda zitto.
umeonyesha kivitendo zaidi.Those are kind of leaders we need.
 
Nampongeza sana Zitto kwakuongoza kwa mfano.Ushauri wangu hii iwe ni hatua ya Awali yakutafuta kuungwa mkono na wabunge wenzako wa Cdm iwapo wataridhia pia basi hiyo posho yote ijumuishwe kwenye kapu moja kisha muitumie kwa lengo moja kwenye kila Jimbo la Wabunge wenu Kama nikujenga Maktaba ya Jimbo au vyovyote mtakavyo kubaliana kwa zamu kwa kwakufanya ivyo kiasi cha Ela kitakuwa nikikubwa na Impact zake zitaonekana wazi kwa Wananchi tofauti nakuzijumuisha kwenye mfuko mwingine ambao ulikuwa unafanya kazi tayari.
 
Mimi nadhani tufikie mahali tuheshimu mawazo na maamuzi, tena mazito anayotuonyesha Zito. Kwanza ni educated, self confident, patriot, na committed. Zito endelea, the new socialism is coming tomorrow.
 
1-97d46865e3.jpg
 
Hongera sana Zitto huo ni mfano wa kuigwa. Kwa wale mnaotaka azikatae kabisa unataka zirudishwe hazina zikaliwe na mafisi huko hazina?? Ni bora azichukue kuzipeleka katika shughuli za maendeleo ya wananchi. Huo ni uamuzi wa kishujaa na pia kuonyesha ishara kuwa anapinga posho zisizoingia akilini wanazolipwa wabunge bungeni huku wakipokea bado mshahara wa kuwa mbunge.
 
Hii kwa Zitto ina maana gani.Frankly sioni mantiki yake,kwa kuwa hata akiziacha mafisadi watazilamba.Ni heri akazichukua akachongeshea madawati au akazipeleka kwenye shuhuli nyingine yeyote ya maendeleo!
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, ameiandikia barua Ofisi ya Bunge kuiomba isimamishe kumlipa posho zake zinazotokana na vikao vya Bunge kuanzia juzi.

Zitto ametoa ombi hilo kwa barua rasmi aliyoiwakilisha kwa Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah Juni 7 mwaka huu.
 
safi,bila shaka Wabunge wote wa Chadema watafuata mkondo!
 
Hiki ndicho kilikuwa kinakosekana kwa wanasiasa wetu. Maneno bila vitendo. Zitto ametupeleka hatua 100 mbele katika mustkabali wa siasa zetu-tunampongeza. Asirudi nyuma. Mwanasiasa hapaswi kufanya jambo ambalo haliamini. Hata kama wengine wataendelea kupokea waendelee, lakini usikubali kusaliti utashi wako.
 
Tunawasubiri wabunge wengine wa chadema wafuate mkondo ili CCM wasambaratike vipande vipande. Chadema hii ni tiketi turufu kushinda mioyo ya watanzania. Kuna hospitali kama Muhimbili unakuta wagonjwa wanalala chini halafu unasikia mbunge anasema posho ya 200,000 kwa siku haimtoshi!!!!
 
well done Zitto!.. nadhani ni mfano mzurisana kwa wabunge wengine, si wa upinzani tuu, bali hata wa chama tawala!
 
Hii kwa Zitto ina maana gani.Frankly sioni mantiki yake,kwa kuwa hata akiziacha mafisadi watazilamba.Ni heri akazichukua akachongeshea madawati!

Ina maana sana. Kikubwa kuliko vyote ni kwamba mwanasiasa hapaswi kufanya mambo ambayo hayaamini. Siasa ni imani kuhusu jambo fulani. Hii kitu ni kubwa kuliko tunavyoweza kukiona kwa macho ya kisiasa za kiafrika!!
 
Hiki ndicho kilikuwa kinakosekana kwa wanasiasa wetu. Maneno bila vitendo. Zitto ametupeleka hatua 100 mbele katika mustkabali wa siasa zetu-tunampongeza. Asirudi nyuma. Mwanasiasa hapaswi kufanya jambo ambalo haliamini. Hata kama wengine wataendelea kupokea waendelee, lakini usikubali kusaliti utashi wako.

Vile vile Dr hii ni nafasi ya kuvuta nyoyo za wananchi kwani imejengeka picha kwa wananchi bunge ni sehemu ya ulaji na ufisadi. Chadema wakilifanya hilo litawajengea heshima kubwa mbele ya wananchi na sidhani CCM itaweza kupata kiti hata kimoja labda sehemu za kusini na pwani.
This is an opportunity in disguise Dr wananchi wamechoka!!!
 
Back
Top Bottom