Barua: Zitto akataa posho za vikao

Barua: Zitto akataa posho za vikao

Hebu tupe ufafanuzi kwa mambo yafuatayo.
Nadhani waliowengi wamekuelewa kutokana na ufafanuzi wako. Labda kwa kuongezea hapo nitoe pia maelezo kuwa hata Mh. Mbowe alishalitolea ufafanuzi jambo hili tena kwa umahiri mkubwa sana. Katika kumbukumbu zangu Mh. Mbowe alisema, Swala si kufuta POSHO zipo zilizohalali kama Per DieM lakini siyo SITTING Allowance. Pia likazuka suala la Spika MAKINDA kukemea wabunge wote wanaokataa posho hizo kwamba watachukuliwa hatua za kinidhamu kwa sababu ni kukiuka kanuni za Bunge. Swali linakuja Nani aliyewachanganya Wabunge ni Spika au Mh. Zitto! Jambo la msingi ilikuwa ni kufuta posho zote kuanzia kwa Wabunge hadi Serikalini rejea maneno ya WAZIRI Mkuu –Posho zisizo za lazima kufutwa, swali je hayo yametekelezwa? Kwa mantiki hiyo endapo Chadema wangezikataa ina maana hata baadhi ya stahiki zao zilizo halali wangezikosa kwa sababu form za kusaini posho hizo hazikutenganishwa. Ingekuwa ni halali kwa wananchi kuwalaumu Chadema ikiwa tu form hizo zingekuwa zimetenganishwa kisha wakaamua kuzichukua zote, lakini kwa hili hatuwezi kuwatupia lawama chadema. Swali langu kwa Mh. Zitto. Unatuambia nini wananchi kuhusu Posho yako kupelekwa Jimboni kwako, je zimekwishapelekwa? Ikiwa zitapelekwa je utasaini form hizo? Sasa kutakuwa na tofautigani na Wabunge waliozichukua kisha wakaenda majimboni mwao na kuwasaidia wapigakura wao? Bado ni kizungumkuti kwani inaonekana Serikali haijawa tayari kutekeleza adhima hiyo ya kufuta posho legelege. Ni mawazo tu yenye mlengo wa kati.
Mkuu wangu nadhani unashindwa kumsoma Zitto vizuri kwa sababu umeshindwa kufuatia utaratibu wa posho zenyewe. Zitto hakutaka posho hizo lakini ilikuwa lazima uchukue kama utaweka sahihi daftari la mahudhulio.. Fedha zinaingizwa direct ktk account yako, hivyo kwa ushauri wa mbali kwanza Zitto alitoa ombi la fedha hizo zipelekewe moja kwa moja ktk account ya NGo ya jimbo lake.

Ikakataliwa na hakika nadhani Bunge linaweza chukua mfano huu kuutumia zaidi ya kuwapa wabunge fedha hizo. Yaani kila mbunge atapewa posho hii kupitia NGo ya jimbo lake kwa kila anayoweka sahihi pia ingesaidia kuyawezesha majimbo na wananchi zaidi ya kumpa Mbunge fedha mkononi kwendsa kununua viwanja na kufungua miradi yao binafsi..Kwani mwisho wa siku kila NGO nchini hutakiwa kuwakilisha mapato na matumizi yake kama NGO tofauti na fedha ambayo mbunge kapewa yeye.

Hivyo Bunge lilipokataa ombi hilo ndipo Zitto alipokataa kuweka sahihi ktk daftari la mahudhulio na inamweka yeye ktk nafasi mbaya ya kuenguliwa bungeni. katika nafasi Chadema iliposimama haiwezekani wabunge wake wote waache kuweka sahihi ktk daftari hili kwa sababu ndicho CCM na CUF wanakitaka na kwa uhakika watawaengua wabunge wote wa Chadema bila hata mshipa kuwashtuka na nafasi zao zitachukuliwa na mshindi wa pili ktk kila jimbo..

Kwa hiyo maamuzi ya Zitto kama mmoja wa viongozi wa Chadema lazima uchukuliwe kama ni mpango mzima wa mkakati wa kupinga hizi posho na sio ushindani ndani ya Chadema. Kwanza tazameni lengo la Zitto na sio ushindani baina yake na viongozi wengine wa Chadema..
 
Hivyo Bunge lilipokataa ombi hilo ndipo Zitto alipokataa kuweka sahihi ktk daftari la mahudhulio na inamweka yeye ktk nafasi mbaya ya kuenguliwa bungeni. katika nafasi Chadema iliposimama haiwezekani wabunge wake wote waache kuweka sahihi ktk daftari hili kwa sababu ndicho CCM na CUF wanakitaka na kwa uhakika watawaengua wabunge wote wa Chadema bila hata mshipa kuwashtuka na nafasi zao zitachukuliwa na mshindi wa pili ktk kila jimbo....

Kwanza hakuna sheria inayohalalisha aliyeshika nafasi ya pili kwenye uchaguzi wa Ubunge kuchukua nafasi ya Mbunge atakayeenguliwa, lakini pia CCM dhaifu haiwezi kamwe kufanya kosa la kuwafukuza Wabunge wa Chadema eti kwa kosa la kukataa posho, CCM inajua tabu iliyoipata kwa kumfukuza Zitto Bungeni kwa hoja ya Buzwagi, haiwezi ikafanya kosa hilo sasa.

Lakini ata kama ingekuwa hivyo, Mbunge hawezi kufukuzwa unless awe hajaudhuria mikutano mitatu ya Bunge mfululizo,hivyo Wabunge Wa Chadema ambao wameendelea kusaini hawajafanya hivyo kwa kuogopa kuvunja kanuni hiyo atleast kwa mkutano uliopita, na ata kama wangeendelea kutosaini kwa mikutano mitatu mfululizo na CCM wakafanya kosa la kuwafukuza, huo ungekuwa mtaji mzuri sana kisiasa kwa Chadema.
.
 
Kwanza kabisa mapenda kunukuu maneno ya Mh. Zitto. Kisha ningependa kumuuliza maswali kwa ufahamu zaidi.

  1. Napenda nifafanue masuala kadhaa hapa.
    Moja, sisi kama Kambi ya Upinzani inayoundwa na CHADEMA tulikwishaamua kwamba posho za vikao sio stahili sahihi kwa Mbunge. Mnadhimu Mkuu wa Kambi alikwishaandika kwa Spika wa Bunge kutaka kutenganisha fomu za mahudhurio na fomu za posho. Mbunge wenje pia katika moja ya michango yake alisema Bunge litengenishe fomu hizi mbili.
    Kuhusiana na mimi kama an indivual MP, nilipewa kazi na chama kama Waziri kivuli Fedha na tangazo la posho alilitoa Naibu wangu ndugu christina Lissu. Mie nikalitolea ufafanuzi kwa vyombo vya habari. Wabunge wa CCM wakaanza kunishambulia na kusema ni unafiki kwamba ninatangaza posho zifutwe ilhali nazichukua. Nikamwandikia Spika barua kuwa posho zangu ziende kwenye charity org jimboni kwangu. Hili nalo likaonekana kama ni unafiki pia. Nikaamua kuzikataa kabisa. Hivyo toka tarehe 8 Juni mimi sipokei posho ya vikao.
    Njia ninayotumia ni kutosaini mahudhurio Bungeni ili wasipate sababu ya kunilipa.
    Sasa kuna mchangiaji hapa kasema usiposaini ndani ya siku tatu unaadhibiwa. Kanuni inasema Mbunge asipohudhuria MIKUTANO mitatu ya Bunge anakuwa amejifukuza ubunge. Tutofautishe mikutano na VIKAO. Kikao ni kila siku na mkutano ni session nzima, mfano session iliyopita ilikuwa ni mkutano wa 4 wa Bunge nk.
    Sasa, ikitokea sitasaini pia katika mkutano wa 5 na wa 6 wanaweza kuanza mchakato wa kunifukuza Ubunge. Lakini je mchakato huo utategemea karatasi za mahudhurio tu?
    Kwa mfano, nikiwa Bungeni ninauliza swali au kuchangia hoja, hansard inarekodi kuwa nilikuwepo Bungeni. Karatasi ya mahudhurio inaonyesha sikuwepo Bungeni. Audio na video records zinaonyesha nilikuwepo Bungeni, watanifukuza kwa vigezo vipi?
    Katika harakati lazima ni lazima kuchallenge rules ili zibadilike. Nadhani katika hili tutafanikiwa.
    Hivyo, wabunge wa chadema sio wanafiki kwani tayari wameandika rasmi kutaka fomu tofauti za kujaza mahudhurio. Pili, Zitto hasaini kama njia ya kutoa changamoto kwa rules. Lakini pia ninaamini kwa dhati kabisa kwamba posho ya kikao (sitting allowance) sio stahili halali (legitimate?)Kwa mbunge anayelipwa mshahara kwa kazi ile ya kukaa na kutunga sheria, kuisimamia serikali na kuwakilisha wananchi.
Mkuu umetoa ufafanuzi mzuri sana. Mimi bado naamini wabunge wengine ni wanafiki tu. Kama wasingekuwa wanafiki wangetumia njia ambayo unatumia wewe ili kuzikataa hizo posho na kulazimisha hizo rules kurekebishwa lakini kwa kuwa wanazikataa posho kinafiki ndio maana wanaendelea kusign mahudhurio na kujinyakulia posho za vikao. Hakika nakuambia kama wabunge wote wa CHADEMA wangekataa kusign kama afanyavyo Zitto na hivyo kutolipwa posho basi posho za vikao zingekuwa zimeishafutwa tena na kikao hicho kilichoisha wiki iliyopita. Lakini kwa kuwa CHADEMA (ex -Zitto) bado wanazipenda basi wanaipa nafasi serikali kuendelea kuzilipa. Naomba waache unafiki kijacho waache kusaign ili wasilipwe posho kushinikiza pia kubadilika kwa rules kama alivyosema Zitto. Vinginevyo nitaendelea kuwaita WANAFIKI TU.
 
Yani makeke yote yale ya mbowe kuhusu posho kumbe ni Usanii tu! Kweli nimeamini posho ni tamu! Hongera Zitto kwa Ukweli wako!
 
Ni rahisi sana kuwalaghai watanzania......tunachotaka na wanavyovifanya ni tofauti kabisa!!,ila sijui kwanini tunawapongeza.
 
Katika mpango wa miaka 15 uliozinduliwa na Kikwete pale Dodoma, moija ya mpango ni kuzipitia upya posho zote na kuziondoa au kuzipunguza inapobidi. Nawashangaa magwanda kuidakia hiyo hoja na kuipiga zumari kama vile ni hoja yao. Hii ni plagiarism at its best. Mnawazuga majuha wenzenu, wengine saa sita kamili.

Mrembo FF ulipotea! Ilikuwa ni swaumu nini? Naona umebip kwa kuona 30 ni leo.
Vipi mambo ya helkopta halikuwa desa hilo? Vipi kuhusu kuchangia chama kwa sms? nk.
Ninavyojua mimi chama kilichofulia sera ni CCM, kazi kudandia tu. Kwanza wanakatakataa km mwanamke halafu, wanaichukua nzimanzima.
 
Yani makeke yote yale ya mbowe kuhusu posho kumbe ni Usanii tu! Kweli nimeamini posho ni tamu! Hongera Zitto kwa Ukweli wako!

Mbowe aliachia shangingi lenye thamani ya shilingi milioni mia mbili na mafuta yake na dereva wake .

Posho ya kikao kwa siku ni shilingi 70,000 na wabunghe wamekaa Dodoma kwa siku 50 na hivyo kuzifanya hizo posho kuwa ni shilingi milioni tatu na nusu tuu (3,500,000) ....... whats a big deal ?
 
Mbowe aliachia shangingi lenye thamani ya shilingi milioni mia mbili na mafuta yake na dereva wake .<br />
<br />
Posho ya kikao kwa siku ni shilingi 70,000 na wabunghe wamekaa Dodoma kwa siku 50 na hivyo kuzifanya hizo posho kuwa ni shilingi milioni tatu na nusu tuu <b>(3,500,000</b>) ....... whats a big deal ?
<br />
<br />
Kama jambo huliwezi usilishabikie! Hii ni aibu kwa Mbowe! A big shame!
 
Nakumbuka hapa hapa JF watu walitoa lawama kwa Mh Zitto kuwa anaichukulia hoja ya Kukataa Posho kwa Maslahi binafsi! Sasa mnajifunza nini hapa nani mnafiki kati ya Zitto na Mbowe na Wabunge wengine wa CDM? Zitto you are a shining star always and forever!
 
Kama Mwenyekiti wa Chama na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Mbowe, ameshindwa kuonyesha uongozi na kuendekeza maslahi yake binafsi, hawa Wabunge wengine wataweza vipi??akina Sugu, Wenje, na Lema kwa uchache wataziacha vip hizo pesa? sio rahisi kama unavyodhani, inahitaji sana kujitoa na kujikana kwa dhati...

Zitto anastahili sana pongezi kwa hili, kaonyesha kwa vitendo kuwa yupo juu ya maslahi yake binafsi, ata kama Wabunge wengine wa Chadema pamoja na wa CCM hawatamuunga mkono kwa muda mrefu ujao, Watanzania wanajua...

Butola, huwezi kusema eti Mbowe ameshindwa kuachia posho ya shilingi 70,000 kwa siku ambayo kwa siku 50 za ubunge ni sawa na shilingi milioni tatu na nusu 3,500,000 kwa kipindi chote cha bunge la bajeti halafu ujenge hoja hapa.

Hii ni kutokana na ukweli kuwa Mbowe alionyesha kwa vitendo kwa kuachia Shangingi V8 Jipya , mafuta ya shangingi hilo,dereva na ukiangalia kimahesabu unaweza kuona kuwa hata mafuta aliyoweka KWENYE gari lake kwa safari zake wakati akiwa Dodoma kama zile za kwenda Arusha , Igunga, DSM kwenye vikao mbalimbali vya chama ni zaidi ya hizo milioni tatu na nusu , penye ukweli tuuseme na penye sppining tuseme wazi kwanio hata habari ilivyotolewa kwenye gazeti linaloheshimika ni kuwa kwa mara ya kwanza linasema bila kuonyesha kuwa nani kasema ila wanasema tuu ni Bunge ... huu ni mkakati wa ...........

Pamoja na kumpa pongezi Zitto , ila Mbowe anapaswa kupewa pongezi pia kwani alipinga mashsngingi na kuamua kuliacha bila masharti na nafikiri kuna haja kuliangalia hili pande zote.
 
Kwanza kabisa mapenda kunukuu maneno ya Mh. Zitto. Kisha ningependa kumuuliza maswali kwa ufahamu zaidi.
  1. Napenda nifafanue masuala kadhaa hapa. Moja, sisi kama Kambi ya Upinzani inayoundwa na CHADEMA tulikwishaamua kwamba posho za vikao sio stahili sahihi kwa Mbunge. Mnadhimu Mkuu wa Kambi alikwishaandika kwa Spika wa Bunge kutaka kutenganisha fomu za mahudhurio na fomu za posho. Mbunge wenje pia katika moja ya michango yake alisema Bunge litengenishe fomu hizi mbili. Kuhusiana na mimi kama an indivual MP, nilipewa kazi na chama kama Waziri kivuli Fedha na tangazo la posho alilitoa Naibu wangu ndugu christina Lissu. Mie nikalitolea ufafanuzi kwa vyombo vya habari. Wabunge wa CCM wakaanza kunishambulia na kusema ni unafiki kwamba ninatangaza posho zifutwe ilhali nazichukua. Nikamwandikia Spika barua kuwa posho zangu ziende kwenye charity org jimboni kwangu. Hili nalo likaonekana kama ni unafiki pia. Nikaamua kuzikataa kabisa. Hivyo toka tarehe 8 Juni mimi sipokei posho ya vikao. Njia ninayotumia ni kutosaini mahudhurio Bungeni ili wasipate sababu ya kunilipa. Sasa kuna mchangiaji hapa kasema usiposaini ndani ya siku tatu unaadhibiwa. Kanuni inasema Mbunge asipohudhuria MIKUTANO mitatu ya Bunge anakuwa amejifukuza ubunge. Tutofautishe mikutano na VIKAO. Kikao ni kila siku na mkutano ni session nzima, mfano session iliyopita ilikuwa ni mkutano wa 4 wa Bunge nk. Sasa, ikitokea sitasaini pia katika mkutano wa 5 na wa 6 wanaweza kuanza mchakato wa kunifukuza Ubunge. Lakini je mchakato huo utategemea karatasi za mahudhurio tu? Kwa mfano, nikiwa Bungeni ninauliza swali au kuchangia hoja, hansard inarekodi kuwa nilikuwepo Bungeni. Karatasi ya mahudhurio inaonyesha sikuwepo Bungeni. Audio na video records zinaonyesha nilikuwepo Bungeni, watanifukuza kwa vigezo vipi? Katika harakati lazima ni lazima kuchallenge rules ili zibadilike. Nadhani katika hili tutafanikiwa. Hivyo, wabunge wa chadema sio wanafiki kwani tayari wameandika rasmi kutaka fomu tofauti za kujaza mahudhurio. Pili, Zitto hasaini kama njia ya kutoa changamoto kwa rules. Lakini pia ninaamini kwa dhati kabisa kwamba posho ya kikao (sitting allowance) sio stahili halali (legitimate?)Kwa mbunge anayelipwa mshahara kwa kazi ile ya kukaa na kutunga sheria, kuisimamia serikali na kuwakilisha wananchi.
Hebu tupe ufafanuzi kwa mambo yafuatayo. Nadhani waliowengi wamekuelewa kutokana na ufafanuzi wako. Labda kwa kuongezea hapo nitoe pia maelezo kuwa hata Mh. Mbowe alishalitolea ufafanuzi jambo hili tena kwa umahiri mkubwa sana. Katika kumbukumbu zangu Mh. Mbowe alisema, Swala si kufuta POSHO zipo zilizohalali kama Per DieM lakini siyo SITTING Allowance. Pia likazuka suala la Spika MAKINDA kukemea wabunge wote wanaokataa posho hizo kwamba watachukuliwa hatua za kinidhamu kwa sababu ni kukiuka kanuni za Bunge. Swali linakuja Nani aliyewachanganya Wabunge ni Spika au Mh. Zitto! Jambo la msingi ilikuwa ni kufuta posho zote kuanzia kwa Wabunge hadi Serikalini rejea maneno ya WAZIRI Mkuu –Posho zisizo za lazima kufutwa, swali je hayo yametekelezwa? Kwa mantiki hiyo endapo Chadema wangezikataa ina maana hata baadhi ya stahiki zao zilizo halali wangezikosa kwa sababu form za kusaini posho hizo hazikutenganishwa. Ingekuwa ni halali kwa wananchi kuwalaumu Chadema ikiwa tu form hizo zingekuwa zimetenganishwa kisha wakaamua kuzichukua zote, lakini kwa hili hatuwezi kuwatupia lawama chadema. Swali langu kwa Mh. Zitto. Unatuambia nini wananchi kuhusu Posho yako kupelekwa Jimboni kwako, je zimekwishapelekwa? Ikiwa zitapelekwa je utasaini form hizo? Sasa kutakuwa na tofautigani na Wabunge waliozichukua kisha wakaenda majimboni mwao na kuwasaidia wapigakura wao? Bado ni kizungumkuti kwani inaonekana Serikali haijawa tayari kutekeleza adhima hiyo ya kufuta posho legelege. Ni mawazo tu yenye mlengo wa kati.
Hakika Mh.Zitto ktk hili ni mfano wa kuigwa kifuatacho ni kufuatilia hela hizo kwa sasa zinamnufaisha nanai?
 
<br />
<br />
Kama jambo huliwezi usilishabikie! Hii ni aibu kwa Mbowe! A big shame!
Suala la posho ni msimamo wa chama na tayari Mnadhimu wa kambi alishaandika barua kwa spika akitaka uwepo wa fomu za mahudhurio na zile za posho ili wabunge wa chama waachane na zile za posho , sasa hapa wa kulaumiwa sio Mbowe na haswa ikizingatiwa kuwa posho hizi zinaingizwa kwenye akaunti ya mtu binafsi na inawezekana ikawa ngumu kujua nani kachukua nani hakuchukua .
 
Butola, huwezi kusema eti Mbowe ameshindwa kuachia posho ya shilingi 70,000 kwa siku ambayo kwa siku 50 za ubunge ni sawa na shilingi milioni tatu na nusu 3,500,000 kwa kipindi chote cha bunge la bajeti halafu ujenge hoja hapa.

Hii ni kutokana na ukweli kuwa Mbowe alionyesha kwa vitendo kwa kuachia Shangingi V8 Jipya , mafuta ya shangingi hilo,dereva na ukiangalia kimahesabu unaweza kuona kuwa hata mafuta aliyoweka KWENYE gari lake kwa safari zake wakati akiwa Dodoma kama zile za kwenda Arusha , Igunga, DSM kwenye vikao mbalimbali vya chama ni zaidi ya hizo milioni tatu na nusu , penye ukweli tuuseme na penye sppining tuseme wazi kwanio hata habari ilivyotolewa kwenye gazeti linaloheshimika ni kuwa kwa mara ya kwanza linasema bila kuonyesha kuwa nani kasema ila wanasema tuu ni Bunge ... huu ni mkakati wa ...........

Pamoja na kumpa pongezi Zitto , ila Mbowe anapaswa kupewa pongezi pia kwani alipinga mashsngingi na kuamua kuliacha bila masharti na nafikiri kuna haja kuliangalia hili pande zote.

Mkuu mbona ilishasemwa hapa kwamba huu ulikuwa ni mchezo wa kisiasa tu na kugombea umaarufu? Mbowe alipoona ZZK amekataa posho na kusimamia anachokiamini basi Mkuu wa Chama akaona amepigwa bao naye akakurupuka na kusema kuwa kaliacha shangingi ili naye apate umaarufu. Sijui kama alishalirudisha rasmi kwenye uongozi wa Bunge. Zitto anasema kukataa posho za vikao ni uamuzi wa Chama sijui kama kukataa gari ya KUB pia ni uamuzi wa Chama ama ulikuwa uamuzi wa Mkuu wa Chama!!
 
Mkuu mbona ilishasemwa hapa kwamba huu ulikuwa ni mchezo wa kisiasa tu na kugombea umaarufu? Mbowe alipoona ZZK amekataa posho na kusimamia anachokiamini basi Mkuu wa Chama akaona amepigwa bao naye akakurupuka na kusema kuwa kaliacha shangingi ili naye apate umaarufu. Sijui kama alishalirudisha rasmi kwenye uongozi wa Bunge. Zitto anasema kukataa posho za vikao ni uamuzi wa Chama sijui kama kukataa gari ya KUB pia ni uamuzi wa Chama ama ulikuwa uamuzi wa Mkuu wa Chama!!

Hayo ya umaarufu wa kisiasa mimi sijui chochote , ila kuwa shangingi limerejeshwa ndio na kwa wiki mbili za mwisho wa Bunge alikuwa analitumia John Joel ambaye alikuwa ni kaimu katibu wa Bunge na dereva alikuwa ni yule yule wa Mbowe ndio alikuwa anamwendesha huyo kaimu katibu wa Bunge.

Nafikiri kuliachia ulikuwa ni uamuzi wa Kambi kwani walikaa kama kambi na kukubaliana kuwa alikabidhi na ndio maana siku ya kulirejesha walikuwa wabunge wote hivyo ni kitu walichokuwa wanakijua na ilikuwa ni majira ya saa mbili usiku , mengine baadae .
 
Zitto pamoja na kuwa controvertial figure, lakini vilevile ni steadfast kwenye kile anachokisimamia.

Zitto kwenye hili la posho ameonesha ukomavu wa juu kabisa kisiasa kwa ku WALK THE TALK.

Haijalishi kama ni mkakati wake wa kufikia malengo ya uongozi wa juu au vipi, sababu kila mwanasiasa
ultimately angependa afike kwenye highest position possible. Sema wengine wana limitations za uwezo.

Kwa hili nasema tena BIG UP Zitto, wasiokukubali waache maana hawaijui siasa, wakikua watakukubali.

Kimsingi tunachohitaji kwenye taifa letu changa ni katiba mpya itakayojenga STRONG INSTITUTIONS.

Hii habari za vyama, sikuwahi kuamini kuna chama cha wanamageuzi wa kweli, wanaokua willing kushiriki
uchaguzi kwenye katiba hii hii miaka nenda miaka rudi. Maana yake ni kuwa wako tayari na wao kutawala
kwa katiba hii hii na kuleta usiri uleule kwenye mambo nyeti, na unyonyaji uliotukwamisha miaka yote.

Na habari hii imezidi kucement what i already knew about our politicians, wengi ni wachumia matumbo tu.

Tofauti ni kuwa wengine wameona CCM kumebana "kuna wenyewe", nawao wakaamua waanzishe chama mbadala
na huko nako utasikia "kuna wenyewe"...kama anavyoshambuliwa Shibuda na wakati wote wamelamba posho!!!
 
Mbowe,Ndesamburo na Komu wa Utawala na Fedha makao makuu CDM wapo Chadema kimaslahi zaidi na ni wambea wakubwa ambao wamekua wakimsakama Zitto na kuona wivu kwa Uwezo na Msimamo wa Zitto! Mafisadi hao wa CDM Mbowe,Komu na Ndesamburo wamekua ndio wenye maamuzi kama vile kuuzia magari mabovu ya mbowe CDM kupanga wanawake Viti Maalum wengi wakiwa ni dada zao,watoto wao na wakwe wa Ndesamburo! Uchaga unaongelewa CDM unaendeshwa na Watatu hao! CDM itakuja kua na Nguvu na yenye Mwelekeo wakiondoka mafisadi hao! Wamekua watu hatari na hasa kuhusu suala la fedha CDM,wamemfanyia Majungu Zitto kupitia Gazeti la Mwanahalisi kisa kuambiwa mara nyingi ukweli na Zitto na Zitto kuwa na Msimamo kwenye mambo ya Msingi! Wametumia Vijana wao hapa JF nasitakusema kwa Ukabila kumshambulia Zitto!
My take: Hoja ya Posho Mbowe aliirukia gafla bila kujua kuwa inataka moyo wa dhati na sio kuigiza na wanasiasa wafanyabiashara! Hongera sana Zitto una future kubwa kwa siasa za Tanzania! Mungu akulinde!
 
Taarifa za nyongeza ni kuwa posho zote kuanzia sitting allowance , per diem na nyinginezo huwa zinalipwa kila ijumaa kwenye Account za wabunge , na huwa zinachanganywa pamoja na kuingizwa kwenye account husika ya Mbunge .

kuweka hili sawa ni kwamba kutosaini karatasi ya mahudhurio kunakosesha mbunge haki ya kuingiziwa kwenye akaunti posho zote(haramu na stahili)

Zitto anapinga posho haramu(sitting allowance) pekee kama ndivyo, kutosaini karatasi ya mahudhurio si suluhisho

mhe. Zitto kajichanganya na ni opportunist wa popularity kila nafasi inapopatikana
 
Wabunge makini waanzie huko majimboni kwao kwa kukataa posho za vikao vy madiwani, wakifanikiwa huko basi hata Bungeni wataweza vinginevyo huu ni usanii wa kujitafutia umaarufu wa muda.
 
Back
Top Bottom