Barua: Zitto akataa posho za vikao

Barua: Zitto akataa posho za vikao

mbunge wa kigoma kaskazini, zitto kabwe, ameiandikia barua ofisi ya bunge kuiomba isimamishe kumlipa posho zake zinazotokana na vikao vya bunge kuanzia juzi. Zitto ametoa ombi hilo kwa barua rasmi aliyoiwakilisha kwa katibu wa bunge, dk thomas kashililah juni 7 mwaka huu.

barua yenyewe hii hapo chini

huyu jamaa anafanya anachosema, safi sana kwani hizo zote kimsingi ni double payment zilizohalalishwa na kanuni mbovu za nchi yetu, zikibebwa na wataalam wetu ili kuwaziba midomo wawakilishi wetu kuhoji

View attachment 31767
 
uko kwenye right track mzee, kaza buti utaifikia tu target.

imekuwaje tena wachukue posho? Au ndo kauli ya sita ya kuwa mnafiki sifa yake ni kusema kwa kukataa huku akimezea mate posho, safi zito simama hapo hapo usiachie
 
nilisema tokea zamani, ifikapo kwenye pesa wote ubadilika! Kama wote wamezichukua na kuzitia mifukoni mwao wana tofauti gani na shibuda aliyetaka posho zipandishwe mpaka 500,000/=?!!!!!

Ningeelewa kidogo, endapo watasema ziliingizwa kwenye akaunti zao na zimekusanywa hivyo zitatumika kuwasaidia watanzania maskini badala ya kuzila na kusingizia "eti si unajua ukishasaini karatasi ya maudhuria basi posho zinapalekwa kwenye akaunti yako"!

kama wamezichukua na kuzitumia kama pesa zao nyingine basi ni wanafiki period
!
naunga mkono hoja mia kwa mia!! Kwani hii sio posho bali ni ujira wa mwiha bora walivyoungana na shibuda na hawana sababu ya kumfukuza; kwani wote ni dugu moja!
 
imekuwaje tena wachukue posho? Au ndo kauli ya sita ya kuwa mnafiki sifa yake ni kusema kwa kukataa huku akimezea mate posho, safi zito simama hapo hapo usiachie
Huwezi kwenda haja kubwa bila kwenda haja ndogo. Ila unaweza kwenda haja ndogo bila kwenda haja kubwa.
 
Ninakupongeza Mh. Zitto, na wengine wanaweza kuonyesha mfano kwa vitendo na sio lazima ikiwa hawajajiridhisha kuwa pesa inayookolewa inaingia katika mfuko sahihi, Cha msingi zaidi ni SERA inayohubiriwa na pongezi zinaenda kwa wote pia wanaoiunga mkono japo kwa maneno. Tatizo ni wale wasiokubaliana na sera hiyo alafu badala ya kutoa difence ya ulafi wao wanakimbilia kuhoji wale waliochukua posho hata kama hawakubaliani na suala hilo.
 
Mbowe aliachia shangingi lenye thamani ya shilingi milioni mia mbili na mafuta yake na dereva wake .<br />
<br />
Posho ya kikao kwa siku ni shilingi 70,000 na wabunghe wamekaa Dodoma kwa siku 50 na hivyo kuzifanya hizo posho kuwa ni shilingi milioni tatu na nusu tuu <b>(3,500,000</b>) ....... whats a big deal ?
<br />
<br /

Big deal kwa wapiga kura ni kusimamia yale unayoyahubiri, haswa Mbowe akiwa kama kiongozi wa kambi ya upinzani alipaswa kuonyesha mfano, hana excuse kwenye jambo hili hata kama ni kwa sh 70,000. Lazima tumpongeze makamu wake mhe. Zitto kwa kuonyesha msimamo dhabiti.
 
Napenda nifafanue masuala kadhaa hapa. <br />
Moja, sisi kama Kambi ya Upinzani inayoundwa na CHADEMA tulikwishaamua kwamba posho za vikao sio stahili sahihi kwa Mbunge. Mnadhimu Mkuu wa Kambi alikwishaandika kwa Spika wa Bunge kutaka kutenganisha fomu za mahudhurio na fomu za posho. Mbunge wenje pia katika moja ya michango yake alisema Bunge litengenishe fomu hizi mbili.<br />
Kuhusiana na mimi kama an indivual MP, nilipewa kazi na chama kama Waziri kivuli Fedha na tangazo la posho alilitoa Naibu wangu ndugu christina Lissu. Mie nikalitolea ufafanuzi kwa vyombo vya habari. Wabunge wa CCM wakaanza kunishambulia na kusema ni unafiki kwamba ninatangaza posho zifutwe ilhali nazichukua. Nikamwandikia Spika barua kuwa posho zangu ziende kwenye charity org jimboni kwangu. Hili nalo likaonekana kama ni unafiki pia. Nikaamua kuzikataa kabisa. Hivyo toka tarehe 8 Juni mimi sipokei posho ya vikao. Njia ninayotumia ni kutosaini mahudhurio Bungeni ili wasipate sababu ya kunilipa.<br />
Sasa kuna mchangiaji hapa kasema usiposaini ndani ya siku tatu unaadhibiwa. Kanuni inasema Mbunge asipohudhuria MIKUTANO mitatu ya Bunge anakuwa amejifukuza ubunge. Tutofautishe mikutano na VIKAO. Kikao ni kila siku na mkutano ni session nzima, mfano session iliyopita ilikuwa ni mkutano wa 4 wa Bunge nk.<br />
Sasa, ikitokea sitasaini pia katika mkutano wa 5 na wa 6 wanaweza kuanza mchakato wa kunifukuza Ubunge. Lakini je mchakato huo utategemea karatasi za mahudhurio tu? Kwa mfano, nikiwa Bungeni ninauliza swali au kuchangia hoja, hansard inarekodi kuwa nilikuwepo Bungeni. Karatasi ya mahudhurio inaonyesha sikuwepo Bungeni. Audio na video records zinaonyesha nilikuwepo Bungeni, watanifukuza kwa vigezo vipi? <br />
Katika harakati lazima ni lazima kuchallenge rules ili zibadilike. Nadhani katika hili tutafanikiwa.<br />
Hivyo, wabunge wa chadema sio wanafiki kwani tayari wameandika rasmi kutaka fomu tofauti za kujaza mahudhurio. Pili, Zitto hasaini kama njia ya kutoa changamoto kwa rules. Lakini pia ninaamini kwa dhati kabisa kwamba posho ya kikao (sitting allowance) sio stahili halali (legitimate?)Kwa mbunge anayelipwa mshahara kwa kazi ile ya kukaa na kutunga sheria, kuisimamia serikali na kuwakilisha wananchi.
<br />
<br />

Asante sana Zitto kwa ufafanuzi ulioutoa. Na hasa kwa style uliyoamua kuitumia ili kuona kama watakuchukulia hatua na hapo kuweza kui challenge hiyo rule ya kusaini mahudhurio kama njia pekee ya kuthibitisha kuwa mbunge alihudhuria mkutano au la. As I once said, you'll always be my hero!
 
Butola, huwezi kusema eti Mbowe ameshindwa kuachia posho ya shilingi 70,000 kwa siku ambayo kwa siku 50 za ubunge ni sawa na shilingi milioni tatu na nusu 3,500,000 kwa kipindi chote cha bunge la bajeti halafu ujenge hoja hapa.

Hii ni kutokana na ukweli kuwa Mbowe alionyesha kwa vitendo kwa kuachia Shangingi V8 Jipya , mafuta ya shangingi hilo,dereva na ukiangalia kimahesabu unaweza kuona kuwa hata mafuta aliyoweka KWENYE gari lake kwa safari zake wakati akiwa Dodoma kama zile za kwenda Arusha , Igunga, DSM kwenye vikao mbalimbali vya chama ni zaidi ya hizo milioni tatu na nusu , penye ukweli tuuseme na penye sppining tuseme wazi kwanio hata habari ilivyotolewa kwenye gazeti linaloheshimika ni kuwa kwa mara ya kwanza linasema bila kuonyesha kuwa nani kasema ila wanasema tuu ni Bunge ... huu ni mkakati wa ...........

Pamoja na kumpa pongezi Zitto , ila Mbowe anapaswa kupewa pongezi pia kwani alipinga mashsngingi na kuamua kuliacha bila masharti na nafikiri kuna haja kuliangalia hili pande zote.
mheshimiwa, hebu kwanza jitambulishe vizuri maana sikuelewi, wewe ni Mbowe au una personal interest gani? kuna mambo unaelekea kuwa na ufahamu wa kina sana... mafuta aliyotumia kwenye hizo safari zake yanacost zaidi ya posho alizochukua!au kuna kitu hapa nashindwa kuelewa? watu wanamsifu Zitto na wewe unawakataza unataka wamsifu Mbowe kwa kurudisha shangingi, kwanini usiache wamsifu Zitto kwa yale wanayokubaliana nayo na wewe utoe point za Mbowe zinazoeleweka na tukiona inafaa tumsifu kiongozi wetu? kwani gazeti hilo limeandika uongo Mbowe hapokei posho? nashukuru unatambua gazeti hilo linaheshimika na pia halina tabia za upendeleo ndio sababu linasomwa na watu wengi, ingekua uongo sote tungeshaona kwenye yale magazeti yenu ya tanzania daima na mwanahalisi ambayo tumezoea kuona mkiandika vibaya kumchafua Zitto. hakuna mkakati wowote hapa ila wewe unaonekana ndie unaetaka kuleta mkakati wako na tumekushtukia
 
watu wanamsifu Zitto na wewe unawakataza unataka wamsifu Mbowe kwa kurudisha shangingi, kwanini usiache wamsifu Zitto kwa yale wanayokubaliana nayo na wewe utoe point za Mbowe zinazoeleweka na tukiona inafaa tumsifu kiongozi wetu? hakuna mkakati wowote hapa ila wewe unaonekana ndie unaetaka kuleta mkakati wako na tumekushtukia

Huyo ndio Mpaka Kieleweke!!

Sijui kwanini ana hofu sana kuona watu wakimsifu Zitto kwa hili...
 
Huyo ndio Mpaka Kieleweke!! <br />
<br />
Sijui kwanini ana hofu sana kuona watu wakimsifu Zitto kwa hili...
<br />
<br />
Huyu mpaka kieleweke ananipa mashaka, kama vile kuna jambo analiogopa! Seems ana ajenda yake ya siri, namsubiri aje atupatie majibu labda tutamuelewa!
 
Siungi mkono Suala la Posho za Wabunge, lakini nafikili hata Zito alipaswa kuchukua hiyo posho, kwa sababu hizo alizoacha zitaenda wapi? nafikili ni vema hizo pesa angechukua na kuzipeleka katika mfuko wa maendeleo kule Mwandiga, kitu ambacho nazani hata waheshimiwa wabunge wa CDM wengine watakifanya. Cha msingi ni kukazania kuhakikisha posho zinaondolewa kisheria.

Mie binafsi sikubaliani na mawazo na ushauri wako kwani kitendo cha kuchukua tu ni kosa tayari kwani technically unakuwa umepokea posho yako tayari. Ukiamua kugomea ni kwamba unakuwa umewapatia fumbo la kuwa wataamua wenyewe wazifanyie kazi gani hizo pesa. Kama wakiamua kuzila ndio watakutana na hasira za sisi wananchi ambao tunakatwa kodi mpaka katika kwapa zetu halafu watu wanazitumia kujitajirisha wenyewe. Kubadilisha sheria ni jambo la muda mrefu linaweza kuchukua miaka kama sio forever kwasababu mikataba ya kazi na malipo ni vitu vigumu sana kushughulikia. Hii inatokana na sababu zilizopewa kulipa hizo posho kama ujuzi wa mlipwaji, sheria za kazi, nafasi aliyokuwa nayo mwanzo, mahitaji ya mtu husika na kuendelea na kuendelea. Hadi vyote vikamilike ni miaka 10-40 imepita. Kinachotakiwa ni affirmative action (hatua za haraka) kunusuru kodi zetu zinaliwa na wakubwa wachache. Waliochukua posho wazirudishe tu Hazina kama wanataka kujenga uaminifu kwa wananchi venginevyo ni wanafiki!!!!!
 
attachment.php
 

Attachments

  • ImageUploadedByJamiiForums1427776904.221077.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1427776904.221077.jpg
    28.8 KB · Views: 1,841
inasaidia nini alivyokataa kuchukua posho za ubunge kwa upande mmoja, na upande wa pili anachukua mabilioni ya rushwa za tss ili kuuza chama chake? kunyamazia buzwagi?

Ni mnafiki tu!
 
Kwa mujibu wa waraka yote haya yalitarajiwa.kila uchao sredi za musicians mkidhani mnajenga hilo tawi LA ccm. poleni wasaliti, endeleeni kujenga kundi lenu jf huku makamanda tukifanya uponyaji site
 
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, ameiandikia barua Ofisi ya Bunge kuiomba isimamishe kumlipa posho zake zinazotokana na vikao vya Bunge kuanzia juzi. Zitto ametoa ombi hilo kwa barua rasmi aliyoiwakilisha kwa Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah Juni 7 mwaka huu.

Barua yenyewe hii hapo chini

View attachment 31767

Hivi hadi anatoka Bungeni alikuwa hachukui posho?
 
Back
Top Bottom