Barua: Zitto akataa posho za vikao

Barua: Zitto akataa posho za vikao

Katika mpango wa miaka 15 uliozinduliwa na Kikwete pale Dodoma, moija ya mpango ni kuzipitia upya posho zote na kuziondoa au kuzipunguza inapobidi. Nawashangaa magwanda kuidakia hiyo hoja na kuipiga zumari kama vile ni hoja yao. Hii ni plagiarism at its best. Mnawazuga majuha wenzenu, wengine saa sita kamili.
Mpango wa miaka 15 ? nilijuwa huna akili lakini sikudhani u mwepesi kichwani kiasi hiki,kuna MPANGO WA MWAKA 1 pia wa kuwauza nje wote wenye fikra kama zako.
 
Acheni kisingizio cha kutenganisha fomu kuwa kigezo cha kuendelea kupokea hizo posho.<br />
<br />
Kwani akiisha saini mahudhurio ni lazima achukue pesa yote? Si achukue ile anayoona ni halali yake na kuacha ile anayoiona ni haramu???<br />
<br />
CDM ni Unafiki mtupu!
<br />
<br />
 
shida yako unatumia masaburi kufikiri! pesa inangia kwenye accout hawapewi kama sokon! cdm songa mbele haiwezi kuwa vita bila wapinzani kama hawa.
 
Kwani haiwezekani kurejesha pesa zikishaingia kwenye akaunti yako? <br />
Kama una utashi utaandika cheki kwa Katibu wa Bunge ili arejeshe hiyo pesa serikalini.
Hiyo cheki utaandika kwa kufanya malipo ya kitu gani na kwa sheria ipi? Na ikirudishwa serikalini itatambuliwa kama malipo kutoka wapi? Na huko serikalini ni wizara ipi au taasisi ipi au idara ipi itahusika kupokea hiyo pesa na itatambuliwa kuwa malipo halali ya kitu gani na kwa sheria ipi? Na Zitto akishalipa hiyo pesa atapewa risiti? Hiyo risiti atapewa na nani???
 
Acheni kisingizio cha kutenganisha fomu kuwa kigezo cha kuendelea kupokea hizo posho.

Kwani akiisha saini mahudhurio ni lazima achukue pesa yote? Si achukue ile anayoona ni halali yake na kuacha ile anayoiona ni haramu???

CDM ni Unafiki mtupu!

hawachukui mkononni,zinawekwa moja kwa moja kwenye account zao bank. sasa hata ukiziacha zingine ndani ya acc yako bado umezipokea tu.
au wewe unashauri wafanyaje mkuu?
 
Real By-now I trust in Dr. Slaa, Mbowe, Mnyika and Lissu...and in CCM I do only still remain with Dr. Magufuli and a bit kind of Mwandosya but with some exceptions.

Others use what we call patriotism of their bowels......
Naona itikadi inakusumbua. Pole, better you be realistic
 
Katika mpango wa miaka 15 uliozinduliwa na Kikwete pale Dodoma, moija ya mpango ni kuzipitia upya posho zote na kuziondoa au kuzipunguza inapobidi. Nawashangaa magwanda kuidakia hiyo hoja na kuipiga zumari kama vile ni hoja yao. Hii ni plagiarism at its best. Mnawazuga majuha wenzenu, wengine saa sita kamili.

Mara nyingine pia mtatuzuga namna hiyo! Unasema katika mpango wa miaka 15,kwanza sidhani kuna mpango km huo! pia km upo mbona wadau hatujauona?Kwa hiyo kwa kuwa hatujauona basi unatuzuga tu kwamba jambo hilo limo! Na km limo mbona linapingwa na wabunge wake? au Cccm kwa CCM wanapingana!

Hii hoja ni ya Chadema maana wanayo kwenye ilani ya uchaguzi 2010( nina copy -Ilani ya CHADEMA 2010-2015),japo namna ya kuitekeleza ndio inaleta uatata,Lakini kwa kuwa kuna nia,basi itatekelezeka tu!
 
Kulikuwa kuna ulazima gan kwa Bunge kutoa taarifa kuhusu nani kachukua Posho na nani hajachukua Posho????
 
Katika mpango wa miaka 15 uliozinduliwa na Kikwete pale Dodoma, moija ya mpango ni kuzipitia upya posho zote na kuziondoa au kuzipunguza inapobidi. Nawashangaa magwanda kuidakia hiyo hoja na kuipiga zumari kama vile ni hoja yao. Hii ni plagiarism at its best. Mnawazuga majuha wenzenu, wengine saa sita kamili.

Inaonekana una mtindio fulani, ukifuatilia kila post inayowekwa jamvini, hata kama huna cha kuchangia lazima utapike. Nakushauri uende pale milembe wanatoa huduma nzuri tu kwa watu kama wewe
 
Mara nyingine pia mtatuzuga namna hiyo! Unasema katika mpango wa miaka 15,kwanza sidhani kuna mpango km huo! pia km upo mbona wadau hatujauona?Kwa hiyo kwa kuwa hatujauona basi unatuzuga tu kwamba jambo hilo limo! Na km limo mbona linapingwa na wabunge wake? au Cccm kwa CCM wanapingana!

Hii hoja ni ya Chadema maana wanayo kwenye ilani ya uchaguzi 2010( nina copy -Ilani ya CHADEMA 2010-2015),japo namna ya kuitekeleza ndio inaleta uatata,Lakini kwa kuwa kuna nia,basi itatekelezeka tu!

Ilani ya Chadema na huo mpango wa miaka 15 kipi kilitangulia? Kama ni ila ya CDM, basi tuna serikali sikivu imechukuwa ilani ya chama mpinzani na kupanga utekelezaji wake.
 
Hoja iliyopo ni ngumu kwani kwa mfano nikiuliza hivi itakuwaje Mbunge ambaye hakusaini mahudhurio na yupo Bungeni wakati wa kupiga kura je?Kura yake itakuwa halali ama laa na kama sio halali wakati wa kusema ndio na hapana sauti yake huwa inahesabiwa?

.....Wala msizunguke saaana hapa, hasara pekee ya kutosaini ni kwa Mbunge binafsi kukosa posho jambo ambalo ni gumu sana kwa Wabunge wanaojali Maslahi Binafsi...
 
[TABLE="align: center"]
[TR]
[TD="class: ntable, bgcolor: #b1c3d9, colspan: 2, align: left"]Democratic Party (DP) [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: ntable, width: 150"]Party Leaders
[/TD]
[TD="class: ntable"]Rev. Christopher Mtikila - Chairman
Mrs. Georgia Mtikila - Secretary General
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: ntable, width: 150"]Contact Address
[/TD]
[TD="class: ntable"]Mchikichini Ilala
P.O.Box 63102 Dar es Salaam
Mob: 0713-430516
0713-625349
Email: dp- watanganyika@yahoo.com
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: ntable, width: 150"]Date of Registration
[/TD]
[TD="class: ntable"]Jun 7, 2002

hapo kwenye majina ya viongozi wa chamaa, heri yetu sie CDM na posho hatuchukui ng'o[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 
<br />
<br />
Unalipwa posho iwapo tu umehudhuria kikao na kusaini mahudhurio. Kama hujasaini hata kama umehudhuria hulipwi posho ya kikao hicho.
Kwa hiyo kama hutaki kuingiziwa fedha hizi kwenye akaunti yako, unaacha tu kusaini mahudhurio. Mie sijaingiziwa malipo ya posho za vikao toka tarehe 8 Juni mwaka 2011. Nyaraka zangu za malipo yaonyesha 0 katika malipo ya posho za vikao.
Kwa nini habari hii imetoka sasa? Kwanza mimi sijaiona kwenye magazeti. Lakini pili ni lazima habari kama hii imekuwa leaked kimkakati ili kuonyesha kuwa chadema sio chama makini. Hivyo inawezekana kuna watu wanataka kuweka mjadala huu kama sehemu ya propaganda za kampeni huko Igunga nk.
Wabunge wa chadema ni wanafiki? Hapana. Wabunge wa chadema wamechukua hatua ya kuandika kwa Spika kwamba fomu za mahudhurio na fomu za posho ziwe mbili tofauti. Ofisi ya Spika haijafanya hivyo.
Suala langu lilikuwa personal kidogo. Wabunge wa ccm walianza kunishambulia mimi binafsi na hivyo nikachukua maamuzi ambayo yanawaziba mdomo moja kwa moja.
Mkakati wa chama ni kusaini daftari la mahudhurio tofauti na daftari la posho.
Mengine ni tafsiri za watu kulingana na mapenzi au chuki zao kwa Zitto au chama changu.

Mh Zitto. kwanza nashukuru kwa kujitokeza na kutoa ufafanuzi. Lakini mimi pengine sikuielewa hoja ya CDM vizuri, kwa sababu nadhani mwanzisha thread ameamua kupotosha hoja ya CDM ionekane ilihusu posho za wabunge tu. Hoja ilikuwa ni posho zote zisizo na tija serikalini including sitting allowances za wabunge na wafanyakazi wa serikali zifutwe. Tafsiri ni kuwa pesa hizo zikiokolewa zipangiwe matumizi mengine yenye tija kwa wananchi wote kama Umeme, maji, barabara nk.
Na ieleweke kwamba wabunge wa CDM hawakupinga kwa sababu wana pesa nyingi sana na kwamba wakipewa hizo pesa watakosa pa kuzitumia.
hoja ni kuwa kwa uhalisia wa maisha ya waTz, pesa hizo ziokolewe na kupangiwa matumizi yenye tija na vipaumbele kwa wote. Hivyo wabunge wa CDM kuziacha hizo pesa hakutasaidia kutimiza walichokikusudia maana wabunge wa CCM kwa wingi wao hawajali vipaumbele vya waTz ambavyo pesa hiyo ingeweza kutumika kuvitatua
Wabunge wa CDM hata wakiziacha hizo posho, swali ni kuwa zitaenda wapi kama si kukwapuliwa na magamba? maana serikali ya magamba imegoma. Hoja si wabunge wa CDM au Zitto kuacha kuchukua posho (maana kaziacha lakini zinatusaidiaje?) kwanza zitafujwa tu maana hazijapangiwa matumizi yeyote. Ndio maana Zitto alikuwa analazimishwa azichukue.
Nadhani kuchukua au kutochukua hizo pesa si hoja ya msingi. hoja hapa ni kuwa CDM imepinga posho si kwa kuwa wana pesa nyingi au hawazihitaji, bali kwa kuwa wameona shida zetu nyingi katika jamii ambazo zingeweza kupunguzwa kwa hizo pesa. WANANCHI TUMEWAONA; TUMEWASIKIA MLIVYOTUTETEA NA KUBEZWA KWA AJILI YETU. Mungu pia amewasikia na kuwaona lakini zaidi amewaona hao majambazi na VIBUDA wanaotaka ujira wa MWIHA eti za kutoa kwenye misiba tukifa, maana kwao hoja si kutenga pesa kuzuia vifo, bali wapewe posho za kuhani misiba yetu maana wameisoma bajeti na wanajua misiba itakuwa mingi hivyo waongezewe ujira wa MWIHA kuwasidia watakapokuwa wanazunguka misibani.
Wabunge CDM chukueni hizo posho wala msiogope maana hata mkiziacha lengo la hoja yenu halitatimia. 2015 tutawaongeza muwe wengi ili muwe na nguvu zaidi kuwashinda watesi wetu.
 
Hongera Zitto. Katika mapambano si lazima wote muanza kwa wakati mmoja wengne watajiunga baadae. Naamini huo ni mwanzo mzur kwa Zito, muda si mrefu wengne wataunga mkono kwa vitendo isipokuwa Shibuda. Kila la kher kamanda Zito.

Kama Mwenyekiti wa Chama na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Mbowe, ameshindwa kuonyesha uongozi na kuendekeza maslahi yake binafsi, hawa Wabunge wengine wataweza vipi??akina Sugu, Wenje, na Lema kwa uchache wataziacha vip hizo pesa? sio rahisi kama unavyodhani, inahitaji sana kujitoa na kujikana kwa dhati...

Zitto anastahili sana pongezi kwa hili, kaonyesha kwa vitendo kuwa yupo juu ya maslahi yake binafsi, ata kama Wabunge wengine wa Chadema pamoja na wa CCM hawatamuunga mkono kwa muda mrefu ujao, Watanzania wanajua...
 
Katika mpango wa miaka 15 uliozinduliwa na Kikwete pale Dodoma, moija ya mpango ni kuzipitia upya posho zote na kuziondoa au kuzipunguza inapobidi. Nawashangaa magwanda kuidakia hiyo hoja na kuipiga zumari kama vile ni hoja yao. Hii ni plagiarism at its best. Mnawazuga majuha wenzenu, wengine saa sita kamili.

Ningeshangaa kama ingepita michango 10 bila kukuona!!
 
Kwanza kabisa mapenda kunukuu maneno ya Mh. Zitto. Kisha ningependa kumuuliza maswali kwa ufahamu zaidi.
  1. Napenda nifafanue masuala kadhaa hapa.
    Moja, sisi kama Kambi ya Upinzani inayoundwa na CHADEMA tulikwishaamua kwamba posho za vikao sio stahili sahihi kwa Mbunge. Mnadhimu Mkuu wa Kambi alikwishaandika kwa Spika wa Bunge kutaka kutenganisha fomu za mahudhurio na fomu za posho. Mbunge wenje pia katika moja ya michango yake alisema Bunge litengenishe fomu hizi mbili.
    Kuhusiana na mimi kama an indivual MP, nilipewa kazi na chama kama Waziri kivuli Fedha na tangazo la posho alilitoa Naibu wangu ndugu christina Lissu. Mie nikalitolea ufafanuzi kwa vyombo vya habari. Wabunge wa CCM wakaanza kunishambulia na kusema ni unafiki kwamba ninatangaza posho zifutwe ilhali nazichukua. Nikamwandikia Spika barua kuwa posho zangu ziende kwenye charity org jimboni kwangu. Hili nalo likaonekana kama ni unafiki pia. Nikaamua kuzikataa kabisa. Hivyo toka tarehe 8 Juni mimi sipokei posho ya vikao. Njia ninayotumia ni kutosaini mahudhurio Bungeni ili wasipate sababu ya kunilipa.
    Sasa kuna mchangiaji hapa kasema usiposaini ndani ya siku tatu unaadhibiwa. Kanuni inasema Mbunge asipohudhuria MIKUTANO mitatu ya Bunge anakuwa amejifukuza ubunge. Tutofautishe mikutano na VIKAO. Kikao ni kila siku na mkutano ni session nzima, mfano session iliyopita ilikuwa ni mkutano wa 4 wa Bunge nk.
    Sasa, ikitokea sitasaini pia katika mkutano wa 5 na wa 6 wanaweza kuanza mchakato wa kunifukuza Ubunge. Lakini je mchakato huo utategemea karatasi za mahudhurio tu? Kwa mfano, nikiwa Bungeni ninauliza swali au kuchangia hoja, hansard inarekodi kuwa nilikuwepo Bungeni. Karatasi ya mahudhurio inaonyesha sikuwepo Bungeni. Audio na video records zinaonyesha nilikuwepo Bungeni, watanifukuza kwa vigezo vipi?
    Katika harakati lazima ni lazima kuchallenge rules ili zibadilike. Nadhani katika hili tutafanikiwa.
    Hivyo, wabunge wa chadema sio wanafiki kwani tayari wameandika rasmi kutaka fomu tofauti za kujaza mahudhurio. Pili, Zitto hasaini kama njia ya kutoa changamoto kwa rules. Lakini pia ninaamini kwa dhati kabisa kwamba posho ya kikao (sitting allowance) sio stahili halali (legitimate?)Kwa mbunge anayelipwa mshahara kwa kazi ile ya kukaa na kutunga sheria, kuisimamia serikali na kuwakilisha wananchi.
Hebu tupe ufafanuzi kwa mambo yafuatayo.


Nadhani waliowengi wamekuelewa kutokana na ufafanuzi wako. Labda kwa kuongezea hapo nitoe pia maelezo kuwa hata Mh. Mbowe alishalitolea ufafanuzi jambo hili tena kwa umahiri mkubwa sana. Katika kumbukumbu zangu Mh. Mbowe alisema, Swala si kufuta POSHO zipo zilizohalali kama Per DieM lakini siyo SITTING Allowance. Pia likazuka suala la Spika MAKINDA kukemea wabunge wote wanaokataa posho hizo kwamba watachukuliwa hatua za kinidhamu kwa sababu ni kukiuka kanuni za Bunge. Swali linakuja Nani aliyewachanganya Wabunge ni Spika au Mh. Zitto! Jambo la msingi ilikuwa ni kufuta posho zote kuanzia kwa Wabunge hadi Serikalini rejea maneno ya WAZIRI Mkuu –Posho zisizo za lazima kufutwa, swali je hayo yametekelezwa? Kwa mantiki hiyo endapo Chadema wangezikataa ina maana hata baadhi ya stahiki zao zilizo halali wangezikosa kwa sababu form za kusaini posho hizo hazikutenganishwa. Ingekuwa ni halali kwa wananchi kuwalaumu Chadema ikiwa tu form hizo zingekuwa zimetenganishwa kisha wakaamua kuzichukua zote, lakini kwa hili hatuwezi kuwatupia lawama chadema. Swali langu kwa Mh. Zitto. Unatuambia nini wananchi kuhusu Posho yako kupelekwa Jimboni kwako, je zimekwishapelekwa? Ikiwa zitapelekwa je utasaini form hizo? Sasa kutakuwa na tofautigani na Wabunge waliozichukua kisha wakaenda majimboni mwao na kuwasaidia wapigakura wao? Bado ni kizungumkuti kwani inaonekana Serikali haijawa tayari kutekeleza adhima hiyo ya kufuta posho legelege. Ni mawazo tu yenye mlengo wa kati.

Mh Zitto na SEAL Team 6 . kwanza nashukuru kwa kujitokeza na kutoa ufafanuzi. Nadhani hoja ya CDM inapotoshwa kwa makusudi ili ionekane ilihusu posho za wabunge tu. Hoja ilikuwa ni posho zote zisizo na tija serikalini including sitting allowances za wabunge na wafanyakazi wa serikali zifutwe. Tafsiri ni kuwa pesa hizo zikiokolewa zipangiwe matumizi mengine yenye tija kwa wananchi wote kama Umeme, maji, barabara nk.
Na ieleweke kwamba wabunge wa CDM hawakupinga kwa sababu wana pesa nyingi sana na kwamba wakipewa hizo pesa watakosa pa kuzitumia.
hoja ni kuwa kwa uhalisia wa maisha ya waTz, pesa hizo ziokolewe na kupangiwa matumizi yenye tija na vipaumbele kwa wote. Hivyo wabunge wa CDM kuziacha hizo pesa hakutasaidia kutimiza walichokikusudia maana wabunge wa CCM kwa wingi wao hawajali vipaumbele vya waTz ambavyo pesa hiyo ingeweza kutumika kuvitatua
Wabunge wa CDM hata wakiziacha hizo posho, swali ni kuwa zitaenda wapi kama si kukwapuliwa na magamba? maana serikali ya magamba imegoma. Hoja si wabunge wa CDM au Zitto kuacha kuchukua posho (maana kaziacha lakini zinatusaidiaje?) kwanza zitafujwa tu maana hazijapangiwa matumizi yeyote. Ndio maana Zitto alikuwa analazimishwa azichukue.
Nadhani kuchukua au kutochukua hizo pesa si hoja ya msingi. hoja hapa ni kuwa CDM imepinga posho si kwa kuwa wana pesa nyingi au hawazihitaji, bali kwa kuwa wameona shida zetu nyingi katika jamii ambazo zingeweza kupunguzwa kwa hizo pesa. WANANCHI TUMEWAONA; TUMEWASIKIA MLIVYOTUTETEA NA KUBEZWA KWA AJILI YETU. Mungu pia amewasikia na kuwaona lakini zaidi amewaona hao majambazi na VIBUDA wanaotaka ujira wa MWIHA eti za kutoa kwenye misiba tukifa, maana kwao hoja si kutenga pesa kuzuia vifo, bali wapewe posho za kuhani misiba yetu maana wameisoma bajeti na wanajua misiba itakuwa mingi hivyo waongezewe ujira wa MWIHA kuwasidia watakapokuwa wanazunguka misibani.
Wabunge CDM chukueni hizo posho wala msiogope maana hata mkiziacha lengo la hoja yenu halitatimia. 2015 tutawaongeza muwe wengi ili muwe na nguvu zaidi kuwashinda watesi wetu.
 
Kama Mwenyekiti wa Chama na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Mbowe, ameshindwa kuonyesha uongozi na kuendekeza maslahi yake binafsi, hawa Wabunge wengine wataweza vipi??akina Sugu, Wenje, na Lema kwa uchache wataziacha vip? sio rahisi kama unavyodhani, inahitaji sana kujitoa na kujikana kwa dhati...

Zitto anastahili sana pongezi kwa hili, kaonyesha kwa vitendo kuwa yupo juu ya maslahi yake binafsi, ata kama Wabunge wengine wa Chadema pamoja na wala CCM hawatakuunga mkono kwa muda mrefu ujao, Watanzania wanajua...

Zitto, pamoja na kuwa huwa nakuaminia kwenye maamuzi yako kwa ajili ya umma wa watanzania , ila kwenye hili naona unakosea sana kulifanya liwe la kwako binafsi kwani litakufanya ukosee na ukijua kuwa unawindwa na hao wagalatia wenzako sasa lazima ujue kuwa unaweza kujijengea sifa binafsi kwa jambo dogo ila likakuharibia pia .

Kuwa mwangalifu katika kujitafutia hatua mbele ila jua na wenzako kwenye hili wanaweza kukuhujumu kwani inawezekana kabisa kuwa wakaja na salary sleep zako na kuzibandika hapa jamvini na haswa ikizingatiwa kuwa wanaweza kuzipata na haswa kutokea bungeni na kama utakumbuka hivi majuzi Waziri Mkullo alijaribu kuonyesha kuwa wewe na baadhi ya wajumbe wa kamati yako mlihongwa na CHC na nafikiri hii ni sehemu ya mkakati take care.

Igunga , ni CUF na nakushauri usikubali Zitto kuwa sehemu ya kwenda kuyaibika na kuingizwa kwenye kundi linalopingana na wenye imani kama ya kwako.
 
jamani wa2 wengine 2we na uelewa wa mambo yanayousu sahihi ze2 na umuhimu wake katika utendaji wa kazi na uwajibikaji we2 wa kila cku. nawalakini na uelewa wa kisheria wa baadhi ya wanajf katika hili japo mm cjasomea sheria ila sahihi ya m2 ni ki2 cha muhimu sana.nilikuwa napenda kutoa kama ufafanuzi kwanza nije kwenye hoja yangu ya mcngi kama ifuatavyo:
>nilivyo muellewa mh zito ni kwamba unapo saini ktk kitabu cha mauzurio ndicho kinacho2 mika kulipia posho. swalaliko hv unapokua na mcmamo nilazima uoneshe kwa vitendo ili lengo lako litimie ndio maana ya kutokusaini kwa mh. zito.
>utakapo saini na hata kama hutachukua hakuna atakae kuelewa kwani utaonekana mnafiki kwani sahihi yako ndio hukumu yako.jamani hata mahakamani tapeli anapokurubuni ukasaini umeliwa.
<""waungwana naomba kuwaclisha"">
 
Back
Top Bottom