Hayo ya umaarufu wa kisiasa mimi sijui chochote , ila kuwa shangingi limerejeshwa ndio na kwa wiki mbili za mwisho wa Bunge alikuwa analitumia John Joel ambaye alikuwa ni kaimu katibu wa Bunge na dereva alikuwa ni yule yule wa Mbowe ndio alikuwa anamwendesha huyo kaimu katibu wa Bunge.
Nafikiri kuliachia ulikuwa ni uamuzi wa Kambi kwani walikaa kama kambi na kukubaliana kuwa alikabidhi na ndio maana siku ya kulirejesha walikuwa wabunge wote hivyo ni kitu walichokuwa wanakijua na ilikuwa ni majira ya saa mbili usiku , mengine baadae .
wana siasa wote wanafiki tu
Nawatakia IDD NJEMA na Mungu awabariki.
Mangi, Zitto ha-sign mahudhurio na mwanzoni kulikuwa na malumbano kidogo kati ya ofisi ya spika na zitto maana kanuni zinasema kama mbunge hatohudhuria vikao vitatu mfululizo bila idhini ya Spika basi aweza kupewa adhabu ikiwa ni pamoja na kufukuzwa. Shida imekuwa kwenye tafsiri ya neno 'vikao', je vikao kwa maana ya jumatatu, jumanne n.k? au vikao kwa maana ya msimu e.g kikao jun, jan or nov? Hapa ndio issu huku watu wakivuta pumzi.
Na hapa ndio nasema inawekezekana kabisa kama wabunge wote kwa ujumla wao hawaku-sign mahudhurio kwa kanuni za sasa kukawa na madhara, hasa ukizangatia CHADEMA ndio wanaunda kami rasmi ya ubunge na Mbowe ndio kiongozi wa kambi ya upinzani buneni. Hata hivyo mara kadhaa wamekuwa wanasisitiza kuwepo kwa vitabu viwili vya mahudhurio kimoja kwa wale wanaokubaliana na posho na kingine kwa wale wanaokataa posho. Ofcourse hii imekataliwa. Kwa ujumla hii issue bado kuna vizingiti wanatakiwa wavuke.
John Mnyika ni msomaji mzuri hapa jamvini, ningependa niamini atatolea ufafanuzi zaidi na complications zilizopo kwa sasa.
Zitto pamoja na kuwa controvertial figure, lakini vilevile ni steadfast kwenye kile anachokisimamia.
Zitto kwenye hili la posho ameonesha ukomavu wa juu kabisa kisiasa kwa ku WALK THE TALK.
Haijalishi kama ni mkakati wake wa kufikia malengo ya uongozi wa juu au vipi, sababu kila mwanasiasa
ultimately angependa afike kwenye highest position possible. Sema wengine wana limitations za uwezo.
Kwa hili nasema tena BIG UP Zitto, wasiokukubali waache maana hawaijui siasa, wakikua watakukubali.
Kimsingi tunachohitaji kwenye taifa letu changa ni katiba mpya itakayojenga STRONG INSTITUTIONS.
Hii habari za vyama, sikuwahi kuamini kuna chama cha wanamageuzi wa kweli, wanaokua willing kushiriki
uchaguzi kwenye katiba hii hii miaka nenda miaka rudi. Maana yake ni kuwa wako tayari na wao kutawala
kwa katiba hii hii na kuleta usiri uleule kwenye mambo nyeti, na unyonyaji uliotukwamisha miaka yote.
Na habari hii imezidi kucement what i already knew about our politicians, wengi ni wachumia matumbo tu.
Tofauti ni kuwa wengine wameona CCM kumebana "kuna wenyewe", nawao wakaamua waanzishe chama mbadala
na huko nako utasikia "kuna wenyewe"...kama anavyoshambuliwa Shibuda na wakati wote wamelamba posho!!!
<br />Acheni kisingizio cha kutenganisha fomu kuwa kigezo cha kuendelea kupokea hizo posho.<br />
<br />
Kwani akiisha saini mahudhurio ni lazima achukue pesa yote? Si achukue ile anayoona ni halali yake na kuacha ile anayoiona ni haramu???<br />
<br />
CDM ni Unafiki mtupu!
<br />....Kwani akiisha saini mahudhurio ni lazima achukue pesa yote? Si achukue ile anayoona ni halali yake na kuacha ile anayoiona ni haramu???...
Naunga mkono! maana hoja ya msingi haikuwa kususia posho bali zifutwe ili kupata pesa za kisaidia nchi katka vipaumbele muhimu vya kijamii. maadam hilo lilikataliwa na magamba, hakuna sababu ya kuziacha kwa sababu mnamuachia nani wakati mlikotaka ziende magamba wamekataa zisiende?Nitauafiki msimamo wa ZITTO endapo tuu atajua wapi fedha yake itaenda tujue hii nchi ya kifisadi kususia fedha kutafanya mafisadi watanue nadhani kwasasa wachukue fedha ili ziwasaidie katika kukuza CDM kichujue dola and thereafter ndio wafute chini ya usimamizi wa CDM chama makini. HUKUNA MAANA KUSUSIA MIFUPA KWA FISI.
Katika mpango wa miaka 15 uliozinduliwa na Kikwete pale Dodoma, moija ya mpango ni kuzipitia upya posho zote na kuziondoa au kuzipunguza inapobidi. Nawashangaa magwanda kuidakia hiyo hoja na kuipiga zumari kama vile ni hoja yao. Hii ni plagiarism at its best. Mnawazuga majuha wenzenu, wengine saa sita kamili.
Butola, huwezi kusema eti Mbowe ameshindwa kuachia posho ya shilingi 70,000 kwa siku ambayo kwa siku 50 za ubunge ni sawa na shilingi milioni tatu na nusu 3,500,000 kwa kipindi chote cha bunge la bajeti halafu ujenge hoja hapa.
Pamoja na kumpa pongezi Zitto , ila Mbowe anapaswa kupewa pongezi pia kwani alipinga mashsngingi na kuamua kuliacha bila masharti na nafikiri kuna haja kuliangalia hili pande zote.