Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,272
- 9,716
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, kwanza nikupe Hongera ya kuendelea kuaminiwa kuendelea kuwa RC wa DSM, Ni heshima kubwa kwako kwa kuwa Mkuu wa mkoa wa jiji la kwanza kiuchumi na kibiashara, kiuwekezaji na hata mchango wake katika Pato la Taifa,
Ni mkoa ambao ndio Tanzania yenyewe ambapo hata sisi wa mikoani ukitoka dar unahis umetoka Washington au New york marekani au Paris ufaransa au London uingereza, Ni mkoa ambao viongozi wote wa kitaifa wa serikali au hata wale wa vyombo vya ulinzi na usalama wapo hapo, Ni mkoa ambao Balozi zote au Taasisi zote za kimataifa zipo hapo, ni lango la kibiashara kwa nchi za Sadc, Ni mkoa wenye kila kitu, Lakini Ni mkoa ambao Rais wa nchi na Amiri Jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama anaishi hapo pamoja na wakuu wote wa vyombo vya ulinzi na usalama, Kiufupi ndio Tanzania yenyewe hapo
Mkuu wa Mkoa nimeyaeleza hayo ili ujuwe unaongoza mkoa wa namna gani na hadhi yako ipoje ukilinganisha na mikoa mingine, Dar ndio Taswira ya nchi yetu na hata ukitaka kuharibu uchumi wa nchi Basi wewe haribu DSM, ukitaka Tanzania ichafuke Basi wewe ichafue DSM,
Mh mkuu wa mkoa hivi karibuni kumejitokeza suala la vitoto vinavyojiita Panya Road vikitesa kuumiza kupiga kujeruhi na hata kuuwa watu wa maeneo tofauti tofauti ya DSM, japo ni vitoto lakini madhara yake yamekuwa makubwa na kuleta hofu kwa wananchi, Nataka nisema kwako kuwa Jambo Hilo limeleta hofu na wasiwasi kwa wakazi wako hapo DSM
Ushauri wangu kwako ni kuwa kuanzia ngazi ya mitaa kuundwe vikundi vya kisiri vya sungusungu vitakavyofahamika kwa Mwenyekiti na wajumbe wake pekee, uchaguzi wa vijana hao uwe pia wa Siri baada ya kuwatathimini tabia na mienendo yao ili isije tokea wahalifu wanakuwa sehemu ya vikundi hivyo na kupelekea kuvuja kwa Siri na mikakati ya vikundi vya sungusungu,
Pili mh mkuu wa mkoa hakikisha kuwa Doria za jeshi la polisi zinaongezeka na kuwepo muda wote na vitendea kazi vinakuwepo muda wote hasa magari ili kuweza kufika kwa haraka maeneo ya matukio yanapokuwa yameripotiwa na wananchi au viongozi wa serikali za mitaa, Polisi wafike kwa wakati na kwa mikakati na mbinu sitahiki ili ikiwezekana hao vibaka wasipate nafasi ya kutoka eneo la tukio pasipo kukamatwa
Tatu wananchi waelimishwe juu ya kushirikiana katika kujilinda na kupambana na hao vibaka pale wanapokuwa wamebaini nyumba fulani imevamiwa, Hilo sis wananchi wa mikoani mbona tumeliweza? Sisi huku hatuwakimbii vibaka Ila vibaka ndio wanawakimbia wananchi kuogopa kutiwa mikononi maana wanajuwa hakuna huruma kwa wahalifu
Nne mh mkuu wa mkoa pia naunga mkono kauli yako, Nasema hivi hao vibaka ni lazima waonyeshwe kwa matendo kuwa gharama ya matendo yao Ni kubwa Sana, lazima wajuwe Ni hatari na nijambo lisilowezekana kumwaga damu ya mtu asiye na hatia kwa tamaa ya kupora Mali, lazima wajuwe nafasi yao ya kuwa salama Ni ndogo Sana au haipo wakibainika na kukamatwa kwa ushahidi wakifanya vitendo hivyo vya kinyama, lazima waonyeshwe njia ya kupita kwa watu wa aina yao, lazima waonyeshwe na kufundishwa kuwa hawawezi wakabaki na mapanga mikononi wakati serikali IPO ni lazima wapokonywe silaha zao na vitu vyao walivyoshika mikononi mwao kujeruhia na kuulia watu wasio na Hatia
Wakazi wa DSM wamechoka kuteswa,kuishi kwa hofu, kudhalilishwa, kujeruhiwa, kuuwawa, kuporwa vitu vyao,kuvunjiwa mirango na kufanya waishi Kama wapo uhamishoni, wanataka Hatua zichukuliwe, wanataka amani itawale, wanataka kuona vitendo hivyo havijirudii kila mara, wanataka kuona adabu inatawala, wanataka kuona matendo na siyo maneno, wanataka kuona jiji linapitika muda wote na maeneo yote yanafikika kwa amani, wanataka utulivu wa jiji ili watulie kwa amani warejeapo toka makazini kwao, wanataka wasisikie milango ikigongwa kwa mawe na mateke, wanataka Amani kwa kuwa no Haki yao kulindwa na serikali yao
Mk mkuu wa mkoa matumaini ya wanadaresalaamu yapo kwako, wote wanakutazama wewe, wote wanakusikiliza wewe, wote wanafuatilia kauli zako, wote wanataka uchukue hatua, Ni wakati wako kuingia kazini kwa nguvu kuwakabili hao vibaka kimya kimya maana umeshazungumza tayari, ingia kazini maana vyombo vyote unavyo, Rasilimali watu unao, Amri ipo mikononi na kinywani pako, Tuliza jiji litulie Kama bahari,
Kwa Sasa iwe mwanzo na mwisho kwa hao vibaka kujitawala hapo DSM maana umepewa kila kitu, unataka Nini kingine ambacho hao vibaka wamekuzidi wewe na vyombo vyako vya ulinzi na usalama? Ni Mimi Lucas Mwashambwa, kijana toka mkoani mzalendo na mpenda nchi yangu
Ni mkoa ambao ndio Tanzania yenyewe ambapo hata sisi wa mikoani ukitoka dar unahis umetoka Washington au New york marekani au Paris ufaransa au London uingereza, Ni mkoa ambao viongozi wote wa kitaifa wa serikali au hata wale wa vyombo vya ulinzi na usalama wapo hapo, Ni mkoa ambao Balozi zote au Taasisi zote za kimataifa zipo hapo, ni lango la kibiashara kwa nchi za Sadc, Ni mkoa wenye kila kitu, Lakini Ni mkoa ambao Rais wa nchi na Amiri Jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama anaishi hapo pamoja na wakuu wote wa vyombo vya ulinzi na usalama, Kiufupi ndio Tanzania yenyewe hapo
Mkuu wa Mkoa nimeyaeleza hayo ili ujuwe unaongoza mkoa wa namna gani na hadhi yako ipoje ukilinganisha na mikoa mingine, Dar ndio Taswira ya nchi yetu na hata ukitaka kuharibu uchumi wa nchi Basi wewe haribu DSM, ukitaka Tanzania ichafuke Basi wewe ichafue DSM,
Mh mkuu wa mkoa hivi karibuni kumejitokeza suala la vitoto vinavyojiita Panya Road vikitesa kuumiza kupiga kujeruhi na hata kuuwa watu wa maeneo tofauti tofauti ya DSM, japo ni vitoto lakini madhara yake yamekuwa makubwa na kuleta hofu kwa wananchi, Nataka nisema kwako kuwa Jambo Hilo limeleta hofu na wasiwasi kwa wakazi wako hapo DSM
Ushauri wangu kwako ni kuwa kuanzia ngazi ya mitaa kuundwe vikundi vya kisiri vya sungusungu vitakavyofahamika kwa Mwenyekiti na wajumbe wake pekee, uchaguzi wa vijana hao uwe pia wa Siri baada ya kuwatathimini tabia na mienendo yao ili isije tokea wahalifu wanakuwa sehemu ya vikundi hivyo na kupelekea kuvuja kwa Siri na mikakati ya vikundi vya sungusungu,
Pili mh mkuu wa mkoa hakikisha kuwa Doria za jeshi la polisi zinaongezeka na kuwepo muda wote na vitendea kazi vinakuwepo muda wote hasa magari ili kuweza kufika kwa haraka maeneo ya matukio yanapokuwa yameripotiwa na wananchi au viongozi wa serikali za mitaa, Polisi wafike kwa wakati na kwa mikakati na mbinu sitahiki ili ikiwezekana hao vibaka wasipate nafasi ya kutoka eneo la tukio pasipo kukamatwa
Tatu wananchi waelimishwe juu ya kushirikiana katika kujilinda na kupambana na hao vibaka pale wanapokuwa wamebaini nyumba fulani imevamiwa, Hilo sis wananchi wa mikoani mbona tumeliweza? Sisi huku hatuwakimbii vibaka Ila vibaka ndio wanawakimbia wananchi kuogopa kutiwa mikononi maana wanajuwa hakuna huruma kwa wahalifu
Nne mh mkuu wa mkoa pia naunga mkono kauli yako, Nasema hivi hao vibaka ni lazima waonyeshwe kwa matendo kuwa gharama ya matendo yao Ni kubwa Sana, lazima wajuwe Ni hatari na nijambo lisilowezekana kumwaga damu ya mtu asiye na hatia kwa tamaa ya kupora Mali, lazima wajuwe nafasi yao ya kuwa salama Ni ndogo Sana au haipo wakibainika na kukamatwa kwa ushahidi wakifanya vitendo hivyo vya kinyama, lazima waonyeshwe njia ya kupita kwa watu wa aina yao, lazima waonyeshwe na kufundishwa kuwa hawawezi wakabaki na mapanga mikononi wakati serikali IPO ni lazima wapokonywe silaha zao na vitu vyao walivyoshika mikononi mwao kujeruhia na kuulia watu wasio na Hatia
Wakazi wa DSM wamechoka kuteswa,kuishi kwa hofu, kudhalilishwa, kujeruhiwa, kuuwawa, kuporwa vitu vyao,kuvunjiwa mirango na kufanya waishi Kama wapo uhamishoni, wanataka Hatua zichukuliwe, wanataka amani itawale, wanataka kuona vitendo hivyo havijirudii kila mara, wanataka kuona adabu inatawala, wanataka kuona matendo na siyo maneno, wanataka kuona jiji linapitika muda wote na maeneo yote yanafikika kwa amani, wanataka utulivu wa jiji ili watulie kwa amani warejeapo toka makazini kwao, wanataka wasisikie milango ikigongwa kwa mawe na mateke, wanataka Amani kwa kuwa no Haki yao kulindwa na serikali yao
Mk mkuu wa mkoa matumaini ya wanadaresalaamu yapo kwako, wote wanakutazama wewe, wote wanakusikiliza wewe, wote wanafuatilia kauli zako, wote wanataka uchukue hatua, Ni wakati wako kuingia kazini kwa nguvu kuwakabili hao vibaka kimya kimya maana umeshazungumza tayari, ingia kazini maana vyombo vyote unavyo, Rasilimali watu unao, Amri ipo mikononi na kinywani pako, Tuliza jiji litulie Kama bahari,
Kwa Sasa iwe mwanzo na mwisho kwa hao vibaka kujitawala hapo DSM maana umepewa kila kitu, unataka Nini kingine ambacho hao vibaka wamekuzidi wewe na vyombo vyako vya ulinzi na usalama? Ni Mimi Lucas Mwashambwa, kijana toka mkoani mzalendo na mpenda nchi yangu