Barabara ya Strabarg: Kielelezo cha ujinga wetu!

Barabara ya Strabarg: Kielelezo cha ujinga wetu!

Tatizo lako mleta thread una stress nyingi kichwani mwako,nipe jiji duniani ambalo halina foleni,nipe jiji duniani ambalo miundombinu yake haipanuliwi,mradi wa mabasi yaendayo kasi,ni wa historia ya tangu rais wa kwanza,michoro yake na kila kitu vilikuwepo,serikali ya awamu ya nne imekuja katika utekelezaji tu wa kile ambacho awamu tatu hazikufanya,ni sawa na daraja la kigamboni,michoro yake ipo toka jk.nyerere akiwa rais,kikwete kaja kutekeleza,punguza stress,soma vitu uvijue,na sii thread za kuandika ukiwa kwenye foleni.

Acha kutetea upumbavu.... Umeshasikia majiji kama London, New York, Paris na Munich watu wanatumia masaa zaidi ya mawili kufika makazini,,,,, yaan watanzania wengine n makondoo ambayo yanaswagwa hata hayajui yanapelekwa wapi? Hiyo barabara ni kichekesho na hakuna sehem yoyote duniani mabasi hayo eti yaendayo kasi yakatengenezewa barabara yake,,, Hilo bus lililoonyeshwa ni sawa na yanayotumka ulaya na yanatumia barabara moja kama magari mengine.... Ni upuuzi mtupu
 
Pro-Chadema kupinga kila kitu Strabarg wanafanya kazi mazingira yanawasumbua.

Nachelea kusema kuna baadhi ya watu kwao neno CHADEMA limekuwa kama booster kwa baadhi ya viungo vyao vya mwili. Ni ujinga usio na ulinganisho pale watu wanapojadili hoja ya msingi kiumbe Fulani anaibuka kusikojulikana na kuanza kuimba wimbo wa CHADEMA.
 
Usitukane wengine kwa kuwa Mungu amekujaalia kupata hicho kijigari chako cha Tshs Milioni 3 si wote wenye uwezo huo! pia Watanzania ndio wanaongoza kuwa na madereva wasio na ujuzi pamoja na Leseni haza wewe Leseni hauna na ndiyo maana ajali nyingi huwa zinatokea Dar kwa kutozingatia sheria za Barabarani kila mtu mwenye kijigali anataka kuwahi tu matokeo ndo hayo. Watanzania wenzangu pia tujifunze kutumia usafiri wa umma wenzetu wazungu wanafanya hivyo baada ya kubaini kuwa ni hasara kubwa kila mtu anaeenda Mjini kutumia usafiri binafsi ila sisu tunasikia fahari kwenda na IST yako Ofisini ili kila mtu akuone kuwa unausafiri wakati unaishi nyumba ya kupanga na kila siku unanyanyasika kwa jambo hili. Pia wakazi wa Dar hawana utaratibu wa maisha kwa utafiti uliofanyika Wakazi wa Dar wanaongoza kwa kuchafua mazingira na mifuko yao ya Rambo kwa kuitupa kila sehemu bila kujali na hasa kwenye mito jambo ambalo si sahihi, pia Wakazo wa Dar wanaongoza kwa kulalamika na kujiona wao ndo Tanzania ila wengine si Tanzania acheni tabia zenu za ajabu ajabu!

mada imehama kwenye Foleni,umeihamishia kwa wakaz wa dar,kaazi kwelikweli
 
Mbunge wa Temeke Mh. Mtemvu nakumbuka akicomment juu ya huu mradi alisema kuwa haoni lolote la maana zaidi ya michoro michoro mingi tu. Mwanzoni nilidhani ni sababu ya 'umbumbumbu' wake lakini taratibu naanza kukubaliana naye maana ukiangalia ukuaji wa majiji yetu na hasa hilo la DSM kisha kulink ni jinsi gani huu mradi utamaliza tatizo la usafiri wa abiria hapo haiingii akilini!
Kwa maana hata baadae labda 2020 wakiijenga barabara za Bagamoyo (ambayo tayari imejengwa 'kikawaida'!!!), Pugu, Kilwa bado wakaazi watahitaji kutoka kwenye maeneo yao duni (yasiyopimwa na kuwa na miundombinu) ili kufika kwenye hizo DART. Sielewi kwa kweli!
 
Ni kielelezo cha ujinga wa Magufulu... sio ujinga wetu.

Sio Magufuli tu sisi sote ni Wajinga huwezi niaminisha hata kwa mtutu wa Bunduki kuwa Watanzania tuna akili timamu sisi ni Majuha na Mambumbumbu.Samahani lakini ashkumu si matusi
 
Nipo barabarani kutokea kimara kuelekea mjini. Njiani ni balaa tupu kwa sababu kuna michepuko ya barabara isiyo na alama yoyote. Nimeingia barabara moja nikaenda kama kilometa 3 nikakuta kizuizi. Ikabidi nirudi tena nilikotoka. Kilometa 3! . Hakuna mataa na hakuna askari wa kuyaongoza magari yanayopita ovyo na mwishowe kuyabana magari mengine. Sote tumesimama. we know for sure it is useless? Nawaonea huruma watu wangu!

Hii wizara ya ujenzi ni kichaka cha wezi na wapiga bao wa kutafuta fedha ya kampeni ya ccm 2015, huo ndo ukweli!

Arusha wanapaita jiji wakaweka taa za barabarani hazikudumu wiki 2, fedha imeliwa na taa hazifanyi kazi.... ukihoji unavunja na kuvuruga amani.
 
Tatizo ni wakazi wa dar. Wakazi wa dar wao wanaona pesa ndio maendeleo ivyo kujidai kuwa wako bussy kutafuta pesa pasipo kufuatilia miundo mbinu imekaaje. Hakuna asiejua kuwa dar ndio kila uchafu kinapatikana. Maji shida, foleni ndio usiseme, takataka, magereji kukaa ovyo ovyo. Nilitegemea wakazi wa dar ndio wangekuwa kielelezo ya watanzania kwa kuisimamia serikali ifanye kazi za kimaendeleo lakini wao wanasema wanatafuta pesa. Wakazi wa dar wanawaona wenzao wa mikoani wanapoandamana kudai maji, umeme au usafiri kupanda wanawaona wajinga. Katika dunia hii miji mikubwa ndio chachu ya maendeleo halafu mikoa inafuata. Serikali ikileta usanii ni mgomo wa nguvu na huduma itapatikana. Je unafikiri wakazi wa dar wangeungana pamoja wakaandamana kwa amani kudai maji wangeteseka kwa miaka yote hiyo. Acha mle vumbi kwani mnatafuta pesa. Mnafikiti mtazikwa na pesa

jaman mada ni foleni au watu wa dar????hujakatazwa kwenda Kuish dar,ishu ya Miundo mbinu nadhan hujui inamhusu nani,inawahusu watu wa mipango miji,na dunia ya sasa wewe upo busy na nini???maana unawaponda walio busy na kusaka mshiko
 
Suluhisho la Dar ni Reli na flyovers sio huo upuuzi
 
Tatizo lako mleta thread una stress nyingi kichwani mwako,nipe jiji duniani ambalo halina foleni,nipe jiji duniani ambalo miundombinu yake haipanuliwi,mradi wa mabasi yaendayo kasi,ni wa historia ya tangu rais wa kwanza,michoro yake na kila kitu vilikuwepo,serikali ya awamu ya nne imekuja katika utekelezaji tu wa kile ambacho awamu tatu hazikufanya,ni sawa na daraja la kigamboni,michoro yake ipo toka jk.nyerere akiwa rais,kikwete kaja kutekeleza,punguza stress,soma vitu uvijue,na sii thread za kuandika ukiwa kwenye foleni.

Sasa kutekeleza Mipango ya awamu ya I kichwa kichwa bila kuifanyia utafiti na kuiweka katika Mazingira ya sasa sio kukurupuka huko? Huoni ndicho chanzo cha adha tunazopata wakazi wa Dar?

Halafu ni Wapi uliona Mkandarasi akifanya atakavyo na anavyojisikia kama hawa Strabag? Only in Tanzania.

 
Bora hii ya Morogoro wanaweka angalau diversion za kuonekana ungepita Tegeta-Mwenge balaa tupu kila siku mizinga maana wana divert asubuhi ukirudi jioni wameshahamisha diversion wanaweka matofali ya Zege , juzi usiku nimekuba gari ndogo imeingia kwenye jiwe pale Tegeta darajani.
 
Pro-Chadema kupinga kila kitu Strabarg wanafanya kazi mazingira yanawasumbua.

Usitake kuudhi watu bure hapa. Nani kaitaja CHADEMA? Kwani kila aikosoae serikali ni CHADEMA? Kama huna cha kuchangia au kama hii kadhia haikupati kaa kimya!
 
Usitukane wengine kwa kuwa Mungu amekujaalia kupata hicho kijigari chako cha Tshs Milioni 3 si wote wenye uwezo huo! pia Watanzania ndio wanaongoza kuwa na madereva wasio na ujuzi pamoja na Leseni haza wewe Leseni hauna na ndiyo maana ajali nyingi huwa zinatokea Dar kwa kutozingatia sheria za Barabarani kila mtu mwenye kijigali anataka kuwahi tu matokeo ndo hayo. Watanzania wenzangu pia tujifunze kutumia usafiri wa umma wenzetu wazungu wanafanya hivyo baada ya kubaini kuwa ni hasara kubwa kila mtu anaeenda Mjini kutumia usafiri binafsi ila sisu tunasikia fahari kwenda na IST yako Ofisini ili kila mtu akuone kuwa unausafiri wakati unaishi nyumba ya kupanga na kila siku unanyanyasika kwa jambo hili. Pia wakazi wa Dar hawana utaratibu wa maisha kwa utafiti uliofanyika Wakazi wa Dar wanaongoza kwa kuchafua mazingira na mifuko yao ya Rambo kwa kuitupa kila sehemu bila kujali na hasa kwenye mito jambo ambalo si sahihi, pia Wakazo wa Dar wanaongoza kwa kulalamika na kujiona wao ndo Tanzania ila wengine si Tanzania acheni tabia zenu za ajabu ajabu!

Wewe nawe acha mawazo ya kijima ukiwa kwenye nyumba ya kupanga huruhusiwi kununua gari?
 
Ni kielelezo cha ujinga wa Magufulu... sio ujinga wetu.


Mkuu ukiifuata chein ya uongozi utajikuta na sisi wananchi tunahusika kwa kuuchagua mfumo huu wa Serikali ya CCM ulioshindwa kabisa kuleta matokeo yaliokusudiwa kwa wananchi.Hii barabara ya morogoro ki-ukweli inatukera sana hasa sisi wapanda daladala.
 
Barabara za diversion hazitengenezwi vizuri na hivyo ku-cause foleni isiyo kuwa ya lazima, eneo la Kimara bucha kuna mashimo kama mahandaki, viongozi pia wanapita humo na STK zao but hakuna anayejali. Wanajiamulia (Strabag) wenyewe wafungue wapi na wafungue wapi, wachimbe wapi na kuweka madongo hata kama ujenzi haundelei, e.g Kimara mwisho wameweka mdongo na kuacha kinjia chembamba na hakuna kazi inayoendelea, wangetuachia tupite mpaka muda watakao kuwa tayari kufanya kazi, na hiyo diversion road tunayopita haijatengenezwa, ni mashimo matupu, kwa kweli inasikitisha sana. Wananchi nasi tunalalamika tu, hatuelewi la kufanya.
 
Kama ni kulaumiwa washalaumiwa sana. Magufuli anafanya nini sasa kama hata kuwaamrisha tu tanroad waweke vibao na alama hawezi. Mtu unaweza kuingia barabara kuu kutokea feeder road ukatembea hata 3km hujaona kibao cha speed, but ukikutana na trafic wanakupiga fine kwa sababu hukuona kibao kilochopo 5km nyuma!. Hilo nalo Magufuli hana utaalamu nalo?!!!

Hii Nchi wote bure tuu, kuna vibao vya no way vimechongwa na kuwekwa CBD ( central Business District) karibu mwaka sasa, vibao hivyo vikazibwa na magazeti, mvua ikaja magazeti yakaloa, yakatoka kwenye vibao na alama za no way zikaendelea kuwepo. Traffic wanasema hazina kazi yoyote.

Unashangaa kama ni hivyo kwa nini walichora na kwa nini waliweka barabarani
 
Sio Magufuli tu sisi sote ni Wajinga huwezi niaminisha hata kwa mtutu wa Bunduki kuwa Watanzania tuna akili timamu sisi ni Majuha na Mambumbumbu.Samahani lakini ashkumu si matusi


Upo sahihi kabisa mkuu haujakosea kusema hayo uliyoyasema ,hata baba wa taifa hili Mwalimu Jullius Nyerere nae aliutaja"UJINGA" kama adui mmojawapo katika nchi yetu.
 
Acha kutetea upumbavu.... Umeshasikia majiji kama London, New York, Paris na Munich watu wanatumia masaa zaidi ya mawili kufika makazini,,,,, yaan watanzania wengine n makondoo ambayo yanaswagwa hata hayajui yanapelekwa wapi? Hiyo barabara ni kichekesho na hakuna sehem yoyote duniani mabasi hayo eti yaendayo kasi yakatengenezewa barabara yake,,, Hilo bus lililoonyeshwa ni sawa na yanayotumka ulaya na yanatumia barabara moja kama magari mengine.... Ni upuuzi mtupu

Kwani kila kitu lazima tuige Ulaya?

Na sisi hatuwezi kutatua matatizo yetu kwa kutumia solutions zetu wenyewe?
 
Kwani kila kitu lazima tuige Ulaya?

Na sisi hatuwezi kutatua matatizo yetu kwa kutumia solutions zetu wenyewe?

Sio kuiga ulaya ndivyo dunia ilivyo...Kwan haya magari tunayoyatengenezea barabara ni ubunifu wa mwafrika? Elimu na hata hizi herufi unazotumia kuandika ni za kuiga! Kwann kwenye avatar yako umeweka mtu mwenye suti badala ya kumweka mwenye mgolole.... Kuiga sio vibaya ila mbaya pale unapofanya madudu yasiyolingana na unayemwiga....
 
Hii Nchi wote bure tuu, kuna vibao vya no way vimechongwa na kuwekwa CBD ( central Business District) karibu mwaka sasa, vibao hivyo vikazibwa na magazeti, mvua ikaja magazeti yakaloa, yakatoka kwenye vibao na alama za no way zikaendelea kuwepo. Traffic wanasema hazina kazi yoyote.

Unashangaa kama ni hivyo kwa nini walichora na kwa nini waliweka barabarani
Ulizia zilitumika bilioni ngapi kuvitengeneza! You will be very surprised, malafyale! And no one cares. Niliwahi kulihoji jambo hilo. Jasho lilinitoka
 
Kweli kaka mi nlishangaa sana kuona heti hii ndo mbadala wa kupunguza foleni kweli uwezo wetu wa kufikir unapungua kila siku
 
Back
Top Bottom