Barabara ya Mabatini, Kijitonyama: Nani kala 10%?

Barabara ya Mabatini, Kijitonyama: Nani kala 10%?

Watanzania hatutaendelea maisha yetu yote, labda wajukuu wa wajukuu zetu ndio wataanza kuleta maendeleo ya kweli.

Utakuta hapo contractor Mtanzania, client Mtanzania, consultant Mtanzania. Wote wizi, waongo, wazembe, wala na wapokea rushwa.

Kuna kuendelea hapo?

Inashangaza sana, engineer Mtanzania anapima ana design barabara yenye ubora wa hali ya chini, ili iweje? na ma consultant wanakubali na ilhali wanaona, wamesoma na wanajuwa kuwa hii barabara inajengwa chini ya kiwango, wanalishwa kitu kidogo wanapitisha certificates za uongo, na mkaguzi wa mwisho anakuja kuipitisha, utakuta huyu kaajiriwa pale wilayani kama district engineer, anapewa kitu kidogo nae anapitisha.

Hii nchi wanataka Rais aje kuwakagua mpaka chupi wanazovaa, kama wanavaa, kama ziko safi au chafu.

Inaudhi sana.

Nnasema Tanzania ni wakati muafaka kuanzishwa sheria ya kuuwa watoa na wapokea rushwa, bila hivyo tutalalamika usiku na mchana hakuna tija.

Pointi tupu!
 
bbarabara zote ziko ovyo ktk ujenzi, ona barabara ya kinondoni kwenda salenda ona mifereji ilivyojengwa pembeni yaani huyo aliye disign sjui alikuwa anapiga puli wakati huo..ona barabara ya mwai kibaki....mashimo njia mbovu.....tatizo watanzania hatupendi kitengeneza barabara ya kudumu sisi tunatengeneza kitu kinakaa muda mfupi ..wao nia yao wapige hela tu..ubora unaotumika siyo hakuna cha 10% hapo ubora zero
 
Inashangaza sana, engineer Mtanzania anapima ana design barabara yenye ubora wa hali ya chini, ili iweje? na ma consultant wanakubali na ilhali wanaona, wamesoma na wanajuwa kuwa hii barabara inajengwa chini ya kiwango, wanalishwa kitu kidogo wanapitisha certificates za uongo, na mkaguzi wa mwisho anakuja kuipitisha, utakuta huyu kaajiriwa pale wilayani kama district engineer, anapewa kitu kidogo nae anapitisha.

Hii nchi wanataka Rais aje kuwakagua mpaka chupi wanazovaa, kama wanavaa, kama ziko safi au chafu.

Inaudhi sana.

Nnasema Tanzania ni wakati muafaka kuanzishwa sheria ya kuuwa watoa na wapokea rushwa, bila hivyo tutalalamika usiku na mchana hakuna tija.
Ha ha ha !
FF umetoa kali na kweli.
Kazi hii ni WIZI wa mchana.
'i nasema 10% imetawala hapo kwa vile hatujasikia Client ambaye ni Kinondoni zmunicipal akisema fyoko, wakati kala ndoano.
 
Watanzania hatutaendelea maisha yetu yote, labda wajukuu wa wajukuu zetu ndio wataanza kuleta maendeleo ya kweli.

Utakuta hapo contractor Mtanzania, client Mtanzania, consultant Mtanzania. Wote wizi, waongo, wazembe, wala na wapokea rushwa.

Kuna kuendelea hapo?

Yote hayo yanatendeka chini ya uongozi wa Kikwete naona umeona noma kumalizia hilo
 
Tutajiwe huyo contractor
Ni yule yule aliyeboronga barabara ya Tabata.
Kule Ilala Municipal na Jerry Slaa, walikagua barabara na kumwambia airudie yote.
Nimefuatilia , kampuni inaitwa DELI. MONTE, wanaoifahamu tupeni wasifu wakuu.
 
Unafikiri ma engineer wote ni CCM? wakandarasi CCM? Ma consultant CCM?

Punguani wahed.

Na wale wanaowauzia Mafuso chakavu mawili kwa millioni 600 ni CCM?

Kwenye makosa lazima pawekwe wazi na pakemewe, CCM siyo malaika kama aliwahi kusema Nyerere kuwa yeye si malaika na ana makosa yake kama binadam.

CCM ni chama na chama kina binadam hakina malaika. Kumbuka hilo.
Wewe umewahi kuikemea CCM kwenye lipi? Halafu wewe mama una matatizo gani huwezi kujadili bila lugha chafu?! Na usijifanye huelewi hiyo serikali ya CCM imefanya nini kwenye huu uchakachuaji? Kuna hatua zimechukuliwa?
 
Ni yule yule aliyeboronga barabara ya Tabata.
Kule Ilala Municipal na Jerry Slaa, walikagua barabara na kumwambia airudie yote

Mkuu hebu tuwekee jina la kampuni la huyo Mkandarasi......
 
attachment.php
Barabara hii inayopita karibu na kituo cha Polisi Kijitonyama, maarufu kama Mabatini, haina hata mwaka imeanza kumeguka vipande vipande.

Nani kala 10% hapo?
Pole mkuu,hilo eneo lililudiwa hilo syo mara ya kwanza.
 
Nyingi ya barabara zinazolalamikiwa zimejengwa na kampuni iitwayo Delmonte T ltd. Kama kuna mtu ana profile ya hii kampuni aimwage hapa jamvini nafikiri majibu mengi tutayapata hapa
 
DELI MONTE (T)Ltd , sijui ni wa Italiani au vipi, lakini inakuja na kasi ya kuboronga isivyokawaida.

Hawa ni kuwapeleka CRB na ERB.....wasituletee mchezo....tutaanzia hapo kwanza...halafu wao ndio watatueleza kila kitu.....inabidi wawekwe kwenye list ya INELIGIBLE/DEBARRED firms.......mpaka such time watakapo jirekebisha.......
 
Hawa ni kuwapeleka CRB na ERB.....wasituletee mchezo....tutaanzia hapo kwanza...halafu wao ndio watatueleza kila kitu.....inabidi wawekwe kwenye list ya INELIGIBLE/DEBARRED firms.......mpaka such time watakapo jirekebisha.......
Kweli mkuu
Hapa lazima hatua zichukuliwe, lakini nani wa kulalamika wakati hao Kinondoni Municipal wako kimya kwa shibe ya ndoano ya 10%?
Hapa TAKUKURU tu!
 
Nchemba kalamba 10% hapo. Chezea magamba wewe!
 
Wewe umewahi kuikemea CCM kwenye lipi? Halafu wewe mama una matatizo gani huwezi kujadili bila lugha chafu?! Na usijifanye huelewi hiyo serikali ya CCM imefanya nini kwenye huu uchakachuaji? Kuna hatua zimechukuliwa?

Faiza ni mnafiki na ndumilakuwili no 1 hapa JF hiki anaponda kule anasifu utawala wa kikwete mwanzo mwisho kutukana ni hulka yake unaweza kujua tu kuwa katoka mazingira gani ! Matusi yake makubwa ni PUNGUANI WAHED NA KUHOROJOKA kwake mtu anayeongea tofauti na mtazamo wake lazima atukanwe
Faiza hupaswi kuchangia chochote hapa kuhusu ubovu wa Barbara ya mabatini huo ni unafiki wa kiwango cha juu kabisa kwakuwa yule unayemtetea mpaka unatoa povu na kuwatusi hata waliokuzidi umri watendaji wake ndio wamefanya haya shame on you little puppet
 
Kweli mkuu
Hapa lazima hatua zichukuliwe, lakini nani wa kulalamika wakati hao Kinondoni Municipal wako kimya kwa shibe ya ndoano ya 10%?
Hapa TAKUKURU tu!

Nitawatumia ujumbe kote huko i.e. CRB, ERB, TAKUKURU na National Construction Council (ili nao wafuatilie na kushauri).....waufuatilie huu mradi na mingine inayolalamikiwa......ili watueleze what happened.....
 
Serikali ya Dar imeamua kumpa tenda zote jamaa wa SKOL na ndiye kwa asilimia kubwa anatengeneza kazi za hovyo ingawaje kuna nyingine kajitahidi...

Hiyo barabara tajwa hapo juu huwa wanajitetea kuwa water table ipo juu hivyo tabaka la changarawe na udongo lililotumika linadidimia na kupelekea lami kudidimia pia...

Hii ndio sababu yao kubwa ya kujitetea
 
Nitawatumia ujumbe kote huko i.e. CRB, ERB, TAKUKURU na National Construction Council (ili nao wafuatilie na kushauri).....waufuatilie huu mradi na mingine inayolalamikiwa......ili watueleze what happened.....

Trust me hakuna kitakachoendelea chini ya ccm zaidi ya danadana tu
 
Serikali ya Dar imeamua kumpa tenda zote jamaa wa SKOL na ndiye kwa asilimia kubwa anatengeneza kazi za hovyo ingawaje kuna nyingine kajitahidi...

Hiyo barabara tajwa hapo juu huwa wanajitetea kuwa water table ipo juu hivyo tabaka la changarawe na udongo lililotumika linadidimia na kupelekea lami kudidimia pia...

Hii ndio sababu yao kubwa ya kujitetea

....yaani wahandisi wameshindwa kutoa solution.....unbelievable!............
 
Back
Top Bottom