Barabara ya Mabatini, Kijitonyama: Nani kala 10%?

Barabara ya Mabatini, Kijitonyama: Nani kala 10%?

Mada kama hizi huwa zinaishia kumwaga nyongo yangu tu!!!!

Sababu watu wapo, wanaona na wanasikia, wanaambiwa na kushauriwa ila hawataki tu kufanya kazi, kuoneana aibu, wengi wa wakubwa wamewekeza humo sana tu!!!!

Sasa imefikia wakati kila kitu (almost) kinaenda kwa kujuana hapo ndipo ugumu ulipo!!!!

Wakubwa wakianza biashara nchi lazima itoboke!!!
 
Serikali ya Dar imeamua kumpa tenda zote jamaa wa SKOL na ndiye kwa asilimia kubwa anatengeneza kazi za hovyo ingawaje kuna nyingine kajitahidi...

Hiyo barabara tajwa hapo juu huwa wanajitetea kuwa water table ipo juu hivyo tabaka la changarawe na udongo lililotumika linadidimia na kupelekea lami kudidimia pia...

Hii ndio sababu yao kubwa ya kujitetea

hawo magamba wapuuzi tu, wamezoea kutafuna fedha za umma. water table inahusikaje hapo? wanaongelea surface run off au water table? never heared such a stupid defence!
 
....yaani wahandisi wameshindwa kutoa solution.....unbelievable!............

Kaka mkubwa wahandisi wana nguvu kwenye miradi kama hiyo???!!!
Unajua kwa sasa kampuni nyingi pia wamiliki sio wahandisi na kuna share holders wasio na hata ujuzi wa kufyatua tofali???!!!

Ndiko pesa ilipo huko, 10% yake ni ya kushiba, miradi inayopewa pesa ni ile iliyoko kwa watu "wanaowezekana" ,wagumu na wachapakazi pangu pakavu mwanzo mwisho!!!!

Fuatilia line up ya hiyo wilaya!!!!
 
Ni muhimu kufahamu/kujulishwa facts ulizoulizia........however...mleta mada ambaye pia ni mtumiaji wa barabara hiyo regularly...anasema hata mwaka haujapita......crack za wazi kabisa na potholes zimejitokeza......either material yalikuwa sub-standard au poor workmanship and compaction.......hii ni dhahiri kuwa quality control and assurance.....ilikuwa na walakini.......hebu watupatie test results record za hiyo barabara....ili akina Sikonge na Lole Gwakisa watusaidie na assessment zao.......
Mkuu Ogah huwa napita maeneo yaliyotajwa mara nyingi tu.
Na kama alivvosema mtoa mada, barabara hii bila kuficha iko chini ya viwango vya ujenzi, na ndio maana tunaona matatizo kujitokeza katika kipindi kifupi tu, toka kukamilika kwa ujenzi.

Tatizo linaweza kuwa katika design, workmanship na hata supervision ya mkandarasi.
Kitu kinachoonekana dhahiri ni ile layer the juu ya lami.
Ile layer ya lami ni ndogo mno, kwa macho tu haizidi 15-20mm, wakati standards za urban asphalt concrete roads inatakiwa kuwa 50mm(na definately si chini ya 30mm).

Kwa layer ndogo namna ile sijui wa kulaumu nani, aliye design, aliyejenga au aliye supervise kazi hiyo.
Matokeo ni yale yale-kazi mbaya.

Ni kweli katika hili msema kweli ni Core drilling ili hiyo core ikafanyiwe test na kujua tatizo likowapi.
Najua mkandarasi aliyejenga hapo ni mzawa, lakini ni kazi kama hizi zinazoumiza jina la wkandarasi wazawa, na kuondoa imani ambayo imeanza kujengeka.
 
Hawa ni kuwapeleka CRB na ERB.....wasituletee mchezo....tutaanzia hapo kwanza...halafu wao ndio watatueleza kila kitu.....inabidi wawekwe kwenye list ya INELIGIBLE/DEBARRED firms.......mpaka such time watakapo jirekebisha.......
Mkuu Ogah panatakiwa mlalamikaji katika hili.
Mteja wa kazi hii asipolalamika inabidi pengine serikali kupitia vyombo vyake vifanye uchunguzi wake.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Ogah panatakiwa mlalamikaji katika hili.
Mteja wa kazi hii asipolalamika inabidi pengine serikali kupitia vyombo vyake vifanye uchunguzi wake.


Mkuu sasa kama serikali ndio inatoa pesa lakini pesa yake haionekani kuleta thamani tarajiwa na anayetakiwa kutoa lalamiko yuko kimya kweli uchunguzi unahitaji msukumo wa nje???!!!

Hivi madaraka yanayolalamikiwa ya Rais kuwa ni makubwa yana mipaka???!!
 
Last edited by a moderator:
hawo magamba wapuuzi tu, wamezoea kutafuna fedha za watu. water table inahusikaje hapo? wanaongelea surface run off au water table? never heared such a stupid defence!

Mkuu siwatetei ila water table ina athari kubwa kwa properties za soil
 
inachotaka kufanya serikali ni kujisifu 'mwaka 2005 zilijengwa km za lami 1000 na katika awamu yetu hii tumejenga km 2,000' wakati zile 1000km zipo hadi leo na hizo 2,000km walizojenga zimeharibika kabla awamu haijaisha....hio barabara inatia aibu ni kwamba ilipakwa lami!!
 
Mkuu siwatetei ila water table ina athari kubwa kwa properties za soil

lets say ni kweli water table iko juu....je hio barabara ni sehemu pekee yenye water table ya juu kuliko zote ziliwahi kujengwa??
 
lets say ni kweli water table iko juu....je hio barabara ni sehemu pekee yenye water table ya juu kuliko zote ziliwahi kujengwa??

na mbona hiyo water table haikuathiri barabara iliyokuwepo mwanzo? ina maana hiyo water table imejitokeza tangu mwaka jana?
 
Acheni kuwanyanyasa WAZAWA. Mmewashupalia utafikiri wao ndiyo wa kwanza Tanzania kufanya wizi kwa kutumia chama tawala cha CCM? Si mlimsifu Magufuli kuwa Mchapa kazi maridadi? Mkamsifu na Meya sijui wa jiji, sasa mnalialia nini? Tulieni dawa iingie vizuri.

Kwanza namsifu walau imepita miezi kadhaa haijaharibika maana kuna yule Waziri kutoka Kondoa sijui alikuwa akiitwa nani miaka ya 90, alitakiwa kujenga barabara ya Morogoro kuanzia Tanki bovu na hakujenga hata mita moja. Pia huyu aliyetakiwa kujenga hadi Msata kwa Rais wetu, bila aibu yoyote, akazila hela zote na hakujenga hata mita moja.

Acheni ROHO KOROSHO bana. CCM oyeeeeee............. na itatawala milele.

Watanzania hatutaendelea maisha yetu yote, labda wajukuu wa wajukuu zetu ndio wataanza kuleta maendeleo ya kweli.

Utakuta hapo contractor Mtanzania, client Mtanzania, consultant Mtanzania. Wote wizi, waongo, wazembe, wala na wapokea rushwa.

Kuna kuendelea hapo?
 
Mkuu siwatetei ila water table ina athari kubwa kwa properties za soil

ina maana hiyo water table imeanza kujitokeza tangu mwaka wa jana? haikuwepo kabla ya hapo?
 
Mkuu siwatetei ila water table ina athari kubwa kwa properties za soil

We took some guys to school for that purpose, they had to fukcen now this before!!!!!
Hardman why are you becoming soft on firm issues???!!!
 
Last edited by a moderator:
Pole sana ustaadh..wakati iko na mabonde na maji na matope mengi, niliwahi kupita hio njia, nikakuta masela wako pembeni ya barabara wakitega mingo...nikawauliza!! Oya wapi njia? Jamaa akanionyesha pita kule pembeni...

Nikasanuka baada ya kuona wote wamekunja suruali zao na mashati begani...halafu maji yametuliaaaa. Nikaamua kupita katikati... jamaa wakabaki wanacheka tu mimi nduki!!

hahahaha! mkuu, masela walitaka kukunasisha wapige mingo? uliwatia njaa ile mbaya! kama vile nakuona ulivyokuwa ukichana mawimbi...nimecheka sana i see!!!
 
Acheni kuwanyanyasa WAZAWA. Mmewashupalia utafikiri wao ndiyo wa kwanza Tanzania kufanya wizi kwa kutumia chama tawala cha CCM? Si mlimsifu Magufuli kuwa Mchapa kazi maridadi? Mkamsifu na Meya sijui wa jiji, sasa mnalialia nini? Tulieni dawa iingie vizuri.

Kwanza namsifu walau imepita miezi kadhaa haijaharibika maana kuna yule Waziri kutoka Kondoa sijui alikuwa akiitwa nani miaka ya 90, alitakiwa kujenga barabara ya Morogoro kuanzia Tanki bovu na hakujenga hata mita moja. Pia huyu aliyetakiwa kujenga hadi Msata kwa Rais wetu, bila aibu yoyote, akazila hela zote na hakujenga hata mita moja.

Acheni ROHO KOROSHO bana. CCM oyeeeeee............. na itatawala milele.
Mkuu Sikonge mimi naamini wazawa wanapofanya vizuri basi wapongezwe na kupewa moyo.
Lakini kama huu uozo hata kama unafanywa na mzawa, lazima wawajibishwe kwa makosa ambayo ni dhahiri na wala hayahitaji utaalam kuyaona.
CCM wala haihusiki na hili, mbona Mkurugenzi Mkuu wa TPA kapelekwa mahakamani kwa 10% ya kampuni ya kichina, CCCC, iliyopewa tenda kinyemela katika mradi wa kupanua bandari.
Tatizo hivi vi-10% vinapofusha mtu na haoni kuwa kwa nyuma nguo imepasuka na yuko uchii.

Huu uchi ndo tunaouona katika mradi kama huu wa Mabatini.
 
Apart from design/construction failure barabara zetu nyingi ni za KISIASA. Waweza kuta Consultant aliliona tatizo na remedial but cost ikaonekana iko juu ya bajeti....siasa zikalamisha ifanyike hivyo hivyo.
Hivyo tatizo la barabara hii laweza kuwa zaidi ya moja (10%)
 
Apart from design/construction failure barabara zetu nyingi ni za KISIASA. Waweza kuta Consultant aliliona tatizo na remedial but cost ikaonekana iko juu ya bajeti....siasa zikalamisha ifanyike hivyo hivyo.
Hivyo tatizo la barabara hii laweza kuwa zaidi ya moja (10%)
wakuu OLESAIDIMU RRONDO masopakyindi tpaul pitieni hapa ..mkuu kaweka maelezo ambayo yanashabihiana sana na maelelzo nilotaka kuyatoa
 
Last edited by a moderator:
Faiza ni mnafiki na ndumilakuwili no 1 hapa JF hiki anaponda kule anasifu utawala wa kikwete mwanzo mwisho kutukana ni hulka yake unaweza kujua tu kuwa katoka mazingira gani ! Matusi yake makubwa ni PUNGUANI WAHED NA KUHOROJOKA kwake mtu anayeongea tofauti na mtazamo wake lazima atukanwe
Faiza hupaswi kuchangia chochote hapa kuhusu ubovu wa Barbara ya mabatini huo ni unafiki wa kiwango cha juu kabisa kwakuwa yule unayemtetea mpaka unatoa povu na kuwatusi hata waliokuzidi umri watendaji wake ndio wamefanya haya shame on you little puppet
Tatizo ni lake ni kushikiwa akili na CCM. Watu kama hawa huwa wanatetea ujinga/ubadhirifu mradi tu ni mkono unaowalisha. Eti na yeye anajifanya kulaumu hapa. Yakitokea mazuri wa kwanza kuisifu serikali ya CCM, leo yanazungumzwa mabaya serikali haihusiki. Saa nyingine unaweza kudhani labda mtu hana ubongo kichwani mwake.
 
Back
Top Bottom