Mimi nadhani mleta mada ameleta wazo ambalo lipo ziku zote kuhusu hizi barabara zetu na 10% juu yake.
Mimi ingawa sio mtaalam saana wa kujenga barabara lakini nafikiri kutokana na kujifunza kutoka kwa wenzetu walioendelea, nimeona kuna matatizo kuanzia kwenye wizara husika hadi pale TANROAD.
TANROAD akiwa wakala wa usimamizi wa barabara wana jukuu la kuhakikisha barabara zote hasa za mijini zina hali bora kabisa.
Kabla ya kujengwa barabara mpya inabidi wadau wote wahusishwe wakiwemo wataalam wa upimaji na ramani,wataalam wa mazingira, wale wa uchoraji na hata wataalam wa jiolojia inabidi washirikishwe, inawezekana pia kwamba lami haikai kutokana na wingi wa mchanga na sababu zingine.
Pia kabla barabara haijajengwa hadi itumike kunakuwepo hatua kadhaa ambazo zimechukuliwa ukiwemo upimaji, ubunifu na njia za mifereji ya maji machafu na mvua.
Kwa mfano kwenye uubunifu na uchoraji wa barabara hiyo kuna mambo ya kuzingatia kama vile eneo, ardhi na mteremko, uwezo wa kupitisha maji ya mvua na machafu, wingi wa magari, kiasi cha magari, malori na mabasi yakayopita hapo, uwezekano wa kuendeleza eneo hilo baadae kama vile maduka pembezoni mwa barabara hiyo( na sio kuruka kidaraja cha mbao kwenda dukani kununua mkate) na athari kwa mazingira na wananchi walio karibu na barabara hiyo.
Pia kuna suala la uwiano wa ardhi au Earthwork ambapo kunatafutwa ujazo wa barabara na uwiano wake na mifereji ya maji. Barabara yoyote ile lazima iwe na ujazo wa juu katikati ili kuwezesha maji yatiririkie kwenda kwenye mifereji hasa pale mvua inaponyesha na kuondoa maji hayo yasituame katikati ya barabara hiyo na kusababisha madimbwi na hatimae lami kumomonyoka.
Sasa hii barabara ya mabatini ni moja ya barabara za zamani sana na isingeweza kuwa katika hali hiyo iliyo nayo leo.
Mji wa Dar-es-Salaam bado kuna barabara nyingi tu zinahitaji kujengwa upya na pesa ya kufanya hivyo inaweza kuwepo kwenye makabrasha tu na sio pale hazina.
Lakini lawama inabidi ziende kwa manispaa ya Kinondoni kwani wao ndio wenye kujibu watatafuna vipi pesa za walipa kodi na wanagawana vipi na kwanini Wilaya hiyo yenye biashara lukuki inashindwa kujenga barabara nzuri na zenye hadhi?