Bar ya Catalunya yafungwa na TRA muda huu

Bar ya Catalunya yafungwa na TRA muda huu

Maafisa wa TRA muda huu wanaifunga bar ya catalunya iliyoko mwenge jijini DSM kwakutotoa risiti za mamlaka hiyo ( kieletroniki) licha ya Kua Na mashine hizo na wamekua wakitoa risiti za kuandika kwa mkono licha ya maonyo kadhaa

Meneja wa bar hiyo maarufu jijini aljpoulizwa sababu za kufanya hivyo alisema mashine hizo zimekua zikisumbua katika utendaji kazi jibu ambalo haliwakuridhisha maafisa hao nakupiga kufuli kila kona na wameamriwa kutofanya biashara yoyote mpaka watakapo wasiliana na mamlaka hiyo!

Source Mimi mwenyewe Niko eneo la tukio!
Dah.!!,kumbe hata ukipata soda,unatakiwa udai risiti?
 
Wash enzi tu hawa TRA, vituo vyote vya mafuta kupata risiti ya Tra ni vita, wanaangaika na wauza kongoro...p..mbAvu
 
Sioni tatizo kwa hatua TRA walizochukua. Zipo kisheria. Ingawa naona chanzo ni kama afisa mmoja aliagiza bia akaombwa kulipa kwanza kwani sehemu nyingi tunazokunywa hawatoi risiti za TRA!
 
Mmiliki atakuwa kakorofishana na afisa wa tra. Si ajabu wamechuliana wake
 
huu ni uonevu waende huko bandarini na maduka makubwa unanunua mzigo wa laki tano unaandika risti ya elfu hamsini
 
Hao TRA wapuuzi wote,sijui wanawaza nini, inamaana bar zote zinatoa risiti??
 
inabidi hao maafisa wa tra nao wakichukua rushwa watupe risiti za kielectronic au vipi wakuu
 
Back
Top Bottom