Bandari yawafuata wafanyabiashara 100

Bandari yawafuata wafanyabiashara 100

Teh teh teh.... wanaruhusu kukwepa kodi au wana kodi ambazo ni reasonable!? Punguza jazba na hisia weweee.
Kauli kama hiyo iliwahi kutolewa na Rais, kwa hiyo unamaanisha Rais naye alitakiwa kupunguza jazba na hisia???
 
Sasa Mkulu si alijifanya masikini jeuri kwa kutamba kuwa waliokimbia kutumia bandari ya Dar ni wale wafanyabiashara wakwepa kodi na akawaambia kuwa waende kwenye hizo bandari za nchi nyingine zinazoruhusu mizigo kupita bila kulipiwa kodi?

Sasa baada ya kuona bandari imekauka kabisa ndiyo anakuwa 'mpole' na kutaka kwenda kuwapigia magoti?

Hii nchi haitakiwi kuendeshwa kwa ubabe na matamko ya majukwaani, badala yake inatakiwa kuendeshwa kwa kufuata sheria za nchi na kusikiliza maoni ya wadau mbalimbali namna bora ya kuiendeleza nchi yetu.

Mkulu akiendeleza kuendesha nchi yetu kwa staili yake ya ONE MAN SHOW, hakika nchi yetu itakuwa inaelekea kuwa another Zimbabwe...............
Well, jambo la kutia moyo katika haya yanayotekea ni kwamba maofisa wa Magufuli wameanza kumuelewa ni kiongozi wa aina gani na hawamuogopi tena, sasa wanatoa misimamo na maamuzi ya serikali bila kujali Rais kasema nini.

Wananchi na sisi, kama wanavyofanya wasaidizi wa Magufuli, inabidi tujifunze kum ignore anachokisema. Tumeshajua kwamba huwa Rais anaongea na mihemko zaidi, hakuna mantiki katika mengi anayosema.
 
Me nilisikitika mtu amesitisha ajira stil bado anasema hapa kazi tu Tanzania aliyetuloga alituweza
 
Wafanya biashara ni level nyingine. Sio wa kucheza nao
 
Sasa mbona tunarudi kwa Jakaya kuwapigia Magoti Wakwepa kodi?
tena ningekuwa mm ni bakhresa ningewaaambia mpige magoti kuniomba radhi kwa kuniita mkwepa kodi alafu niwafotoe foto, hasa YOHANA!
 
Serikali imewafuata Wafanyabiashara 100 wapi? Wako Jengo gani kila Udaku unaoenezwa na Wakenya Watanzania wanaujadili kama kweli. Hovyo kabisa..
 
Siyo vizuri kushangilia msichokijua jamani. Hao waliyofuatwa ni wadaiwa sugu wa bandari siyo waleta mizigo. Wao mizigo wataleta na nini wkt meli karibu 7000 duniani zimepaki na zingine zimevunjwa kuwa vyuma chakavu kwa kukosa bidaa? Naona JF siku hizi imekuwa siyo greetthinkers bali imebaki ya wanywa mbege wasiyo na uelewa bali washangiliaji
eti sa hivi mnaanza visingizio eti ukosefu wa mizigo bandarini ni dunia nzima na sio Tanzania..kwa hiyo una manisha uchumi wa dunia unayumba haupo vizuri.na kama ndivyo ni kwa Takwimu zipi na za lini ??? mnavituko nyie lumumba
 
Nilisema mtakuja hadi Durban mnatambaa.Ngoja niandae masharti!
 
No, hujasema ukweli. Gari milioni 5 , kodi milioni 20!
Hapo sasa utakua uleta gari lilichoka hasa hadi utozwe 20 milions. Maana sasa ushazidisha uongo na umeigia kwenye ushabiki sasa. Kodi na vat za magari zinajulikana kama umenunua 5 milions uangalie tathmini ya hilo gari liko kiasi gani. Hata mimi naweza kununua gari la dola 1000 ambalo thamani yake ya sokoni ikawa dola 3000 na ndipo utakapo lipia ushuru kwa dhamani ya dola 3000 na sio hiyo 1000.
Turudi kwenye hoja manao sema hamtumii bandarikwa sababu ya kodi... Lakini kodi iko palepale.Wanao toza kodi sio bandari, ni TRA ndugu. Labda bandari watakusumbua kutoa hilo gari na wakakukamua hela zaidi. Na ndio hilo suala linalo takiwa kuzungumziwa kwa sasa kama Bahresa anavyo sema kwenye hilo gazeti
 
Hapo sasa utakua uleta gari lilichoka hasa hadi utozwe 20 milions. Maana sasa ushazidisha uongo na umeigia kwenye ushabiki sasa. Kodi na vat za magari zinajulikana kama umenunua 5 milions uangalie tathmini ya hilo gari liko kiasi gani. Hata mimi naweza kununua gari la dola 1000 ambalo thamani yake ya sokoni ikawa dola 3000 na ndipo utakapo lipia ushuru kwa dhamani ya dola 3000 na sio hiyo 1000.
Turudi kwenye hoja manao sema hamtumii bandarikwa sababu ya kodi... Lakini kodi iko palepale.Wanao toza kodi sio bandari, ni TRA ndugu. Labda bandari watakusumbua kutoa hilo gari na wakakukamua hela zaidi. Na ndio hilo suala linalo takiwa kuzungumziwa kwa sasa kama Bahresa anavyo sema kwenye hilo gazeti
Kuna thread humu jana alionyesha kodi ya milioni 20, wakati gari amenunua milioni 5!
 
Back
Top Bottom