Bandari yawafuata wafanyabiashara 100

Bandari yawafuata wafanyabiashara 100

tujifunze kufanya utafiti kabla ya kuchukua hatua...tutumie ubabe Wa akili sio Wa vyeo!!!
 
Kufanya hivi ni upuuzi kiwango cha lami ni kutengeneza makundi, hivi hawa washauri wa bob wanatoka sayari gani
Kama ni kweli hili litakuwa kundi untouchables!
Kinachitakiwa ni kuweka mazingira rafiki kwa biashara
Uaminifu
Wepesi wa nyaraka
Uhakika wa kutoa mizigo kwa wakati
Kupunguza mlolongo wa kodi kwa ajili ya kuvutia wateja wengi zaidi
Bandari kufanya kazi 24/7 kwa shift
Nk nk

Well said Kaka.
 
Hakuna nmna nyingine. Solution ni serikali iache kuleta "fyoko fyoko" kwa biashara.
 
Ni bora kwa jakaya ajira zlitolewa kwa wakati, nyongeza mishahara ilikuwepo kwa wakati,wanafunz vyuo vikuu walipata boom kwa wakati, n.k huyu wa sasa n matamko tu yasiyo na tija kwa taifa

Acheni unafiki , eti ajira zilitolewa kwa wakati ,boom lilitolewa kwa wakati wew haujawahi hata pigwa boom na police kwa kugoma kwa sababu ya pesa
 
Sasa Mkulu si alijifanya masikini jeuri kwa kutamba kuwa waliokimbia kutumia bandari ya Dar ni wale wafanyabiashara wakwepa kodi na akawaambia kuwa waende kwenye hizo bandari za nchi nyingine zinazoruhusu mizigo kupita bila kulipiwa kodi?

Sasa baada ya kuona bandari imekauka kabisa ndiyo anakuwa 'mpole' na kutaka kwenda kuwapigia magoti?

Hii nchi haitakiwi kuendeshwa kwa ubabe na matamko ya majukwaani, badala yake inatakiwa kuendeshwa kwa kufuata sheria za nchi na kusikiliza maoni ya wadau mbalimbali namna bora ya kuiendeleza nchi yetu.

Mkulu akiendeleza kuendesha nchi yetu kwa staili yake ya ONE MAN SHOW, hakika nchi yetu itakuwa inaelekea kuwa another Zimbabwe...............
 
Siyo vizuri kushangilia msichokijua jamani. Hao waliyofuatwa ni wadaiwa sugu wa bandari siyo waleta mizigo. Wao mizigo wataleta na nini wkt meli karibu 7000 duniani zimepaki na zingine zimevunjwa kuwa vyuma chakavu kwa kukosa bidaa? Naona JF siku hizi imekuwa siyo greetthinkers bali imebaki ya wanywa mbege wasiyo na uelewa bali washangiliaji
Mimi huwa nakerwa sanaa na watu ambao eti kwa kuwa tuu wabayoyapenda hayajasemwa hapa jamvini basi JF siyo tena jukwaa la great thinkers!! Ningetegemea ungeweka link kuonyesha other ports kama Beira, Mombasa na South Africa hazina mizigo kama yetu, but unakuja tuu na porojo halafu unakandia watu..
 
There's no way tunaweza kuafuata wakwepa kodi... umesikia vibaya mleta mada!! Hao Wakwepa kodi wakubwa, (in Kassim Majaliwa's voice) ndo wameanza kujipendekeza kwetu... nchi zao zimeandika barua wanaomba waje kutumia bandari ya Dar es salaam!! Tumeweka historia Tanzania, wafanyabiashara wa nje kupitia zao wanatuomba watumie bandari yetu!!! Walikimbilia Msumbiji; wakadhani tungewabembeleza... tumewakazia vile vijitalii vizungu vimaskini maskini halafu tuwashobokee hawa Wamatumbi wenzetu??!! Na tushawapelekea ujumbe; barua zao tumezipata lakini wasitushinikize kuwajibu leo wala kesho... wakiona tunachelewa; wakatumie hata bandari ya Angola; hatubabaiki!! Kwanza bandari haikuwa priority yetu; kipaumbele hapa ni viwanda!
Weka attachment ya hiyo barua hapa jukwaani...
 
There's no way tunaweza kuafuata wakwepa kodi... umesikia vibaya mleta mada!! Hao Wakwepa kodi wakubwa, (in Kassim Majaliwa's voice) ndo wameanza kujipendekeza kwetu... nchi zao zimeandika barua wanaomba waje kutumia bandari ya Dar es salaam!! Tumeweka historia Tanzania, wafanyabiashara wa nje kupitia zao wanatuomba watumie bandari yetu!!! Walikimbilia Msumbiji; wakadhani tungewabembeleza... tumewakazia vile vijitalii vizungu vimaskini maskini halafu tuwashobokee hawa Wamatumbi wenzetu??!! Na tushawapelekea ujumbe; barua zao tumezipata lakini wasitushinikize kuwajibu leo wala kesho... wakiona tunachelewa; wakatumie hata bandari ya Angola; hatubabaiki!! Kwanza bandari haikuwa priority yetu; kipaumbele hapa ni viwanda!
Sereouse[emoji24] ?
Nimechaguliwa na maskini! Siyo matajiri, nitagawa sukari bure zilizofichwa! Mhh leo hii! Mnawafata matajiri kimya kimya! Acheni kucheza na media punguzeni visasi huu mchezo hautaki hasira! Kitaa hamjakaa mtajuaje uchumi? Au uchumi wa kwenye karatas! Ingia kwenye game uone ndo utajua si kila 4+5=9!

[emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji3]
 
Maskini pole sana ndugu yangu....tatizo ni ushabiki umekujaa ika ungejua ungakaa kimya na siku ukilejeshewa akili zako ulizowapa wanasiasa utatamani kulia...
Wewe akili zako ulizomkabidhi yule mbunge Kibajaji ameshakurudushia kwani??
 
Lisu alisema wamewekeza kwenye mitandao ndio najionea kwenye huu uzi!

Siku hizi UKAWA wanapotezea hasira zao kwa vihoja vidogo kweli..
Hivi UKAWA ndio wamefukuza wateja bandarini siyo??
 
yale yale ya Sukari, walipambana na wafanya biashara ya sukari mwishowe wao wenyewe ndio waliosalimu amri, wamepambana na wanaotumia bandari ya Dar sasa wao wenyewe tena ndio wanasalimu amri. Tunasubiri kuchapishwa kwa noti mpya tuone hapa mshindi atakuwa nani.
 
yale yale ya Sukari, walipambana na wafanya biashara ya sukari mwishowe wao wenyewe ndio waliosalimu amri, wamepambana na wanaotumia bandari ya Dar sasa wao wenyewe tena ndio wanasalimu amri. Tunasubiri kuchapishwa kwa noti mpya tuone hapa mshindi atakuwa nani.

Akichapisha noti mpya, uchumi utazidi kudidimia.
 
Naona swala la bandari nimechukuliwa na upinzani kutaka kumkomoa rais.inaonyesha jinsi gani msivyo na uzalendo na hata hamtaki kujua ukwl.maslai mnayo tetea niyawatu wachache mlokuwa mnafaidika na mfumo wa bandari kavu ambao ulikuwa ukitumika kukwepa kodi.sasa imekula kwenu
Rubbish.. Hivi yale makontena kibao ya wakwepa kodi si walitoa orodha? Uliona wapinzani tuu?? Yule jamaa wa TRA mwenye majumba kibao, na yule wa mamilioni kila dakika ni wa upinzani??
 
Tumewafuata huko waliko kuwaambia warudi tuendashe nchi kwa pamoja!. Sio vizuri waondoke bila kujua lengo letu. Tunawapenda sana! Waje walipe kodi tujenge viwanda, tutengeneze ajira!.
 
Back
Top Bottom