Bandari yawafuata wafanyabiashara 100

Bandari yawafuata wafanyabiashara 100

Ogopa mpaka bandari inarusha matangazo kwenye tv stations kuhamasisha watu kutumia bandari ya Dar.
Hayo matangazo wangerushia Kongo. Hapa ndani jamaa liache kuongea shombo na lisambaze pesa linazokusanya. Pesa haijai banaaaa............. ye anainjoi kuona pesa hazina badala ya mzunguko!
 
Dharau ya chama tawala kwa watanzania has run its course. We must do truth.
 
Haya bila shaka wanayaitaka "magwangala"kwa lugha ya huko kwa mkuu wetu. Huu ni uchafu unaotokana na mchanga baada ya kuondoa dhahabu!
JPM na CCM watanyooka tu! Chezea Wapinzani na Wafanyabiashara wewe.Hivi unawezaje kuendesha uchumi kwa ku-harass Wafanyibiashara, Wafanyakazi na Wapinzani?Hawa ni wadau muhimu au Keyplayers kwenye biashara na Uchumi wa nchi! Bado la WATALII kwenye mbuga zetu za Wanyama!
Hivi sasa watalii wengi wamehamia Kenya kwasababu ya Kodi za kijinga! Halafu Rais mzima anasimama anatamba kuwa HAO WATALII NA WASIJE, NI HERI KUWA NA WATALII 500 WANAOLIPA KODI KULIKO MILIONI 2 WASIOLIPA! Haya ni mambo ya hovyo kabisa!!!
Kuna magazeti ya Kenya yaliwekwa hapa yakionyesha watalii wamehamia znz. Kenya kwenyewe wamepungua
 
Juzi kati nilikua namuangalia kupitia tv "Katelephone" akimwangukia Mo Dewji ajaribu kuzungumza na wafanya biashara wenzake warudi na wasikimbie nchini kwenda kufanya biashara nje ya nchi, mpaka huruma.
"... Akiambiwa aangukie anatoa pesa nyingi....... kuliko ile mahari aaliyotoa ..."
 
Uchumi wa soko huo au market economy , hapa mteja ndio mfalme sababu anazo bandari nyingine za kuhamia lakini ingekuwa monopoly kama zamani yaani mteja hana njia nyingine ila kutumia bandari ya Dar hapo ndio mtoa huduma ni mfalme na mteja ana bembeleza !!!
 
Kwenye biashara huwezi kumtukana na kumfukuza mteja wako eti aliibiwa na watumishi wako, ni utoto pasee ktk biashara na kuhitaji mapato yake unaye mtukana. Serikali ilipashwa kuwafukuza na kuwafungulia mashitaka watumishi wake na upande wa pili kuwabembeleza wateja kwa kuwaomba msamaha kwa utumishi mbaya wa ufanyakazi wa vijana wetu. Na kuwaomba wale ambao kweli walikwepa kulipa na kuanza upya. Visasi na ubabe na kuwatishia wafanyabiashara walioibiwa na wafanyakazi wako ni kosa la kiutu uzima.
 
Tatizo lingine wafanyabiashara wanaonekana kuwa maadui wa watawala kwa siku za leo, ambao hasara ktk biashara zao ni furaha kwa baadhi ya viongozi. Na pia hawana wa kuwatetea na matisho kutoka juu yana watisha kufikia kufilisiwa, ni jambo baya na la kutisha kufilisika mali uliyoitafuta kwa taabu dhiki na shida kwa miaka nendarudi. Mkuu awahurumie waanze upya kwa safu ya wafanyakazi wazuri waliopo sasa na awe mkuu wa wote siyo baadhi ya watz tu. Mama yetu alikuwa na baba mwingine aliyetuacha na mama yetu, baba mpya asitufunge kwa kwa makosa ambayo tuliamliwa kuyafanya tukiwa na baba yetu aliyemtangulia bali achambue na kutuona wote ni watoto wa mama mmoja.
 
Ogopa mpaka bandari inarusha matangazo kwenye tv stations kuhamasisha watu kutumia bandari ya Dar.

Hata wangelikuwa wanaweka tangazo kila baada ya dakika 5 bado hatuta tumia ,kodi za kujiamlia sio nzuri na rafiki kwa Wafanya biashara..Tunataka kodi elekezi sio leo unaingiza kontena la kitenge unalimwa kodi inayo tofautiana kabisa na mwenzio alie ingiza kitenge hicho hicho chenye quality sawa na cha kwako..

Tulisha ishauri Serikali ya Jakaya Kikwete kuhusu hilo na walituelewa na kuuweka huo mfumo kwa miezi michache lakini baada ya kuingia huyu bwana Mkubwa akaondoa kila kitu...

Unapoweka kodi elekezi kutokana na bidhaa unatoa fursa kwa wafanya biashara kujua manunuzi /gharama/ na kodi yenyewe ,so ataleta bidhaa huku akijua atapata ngapi na inakuwa ni uhakika zaidi.Sasa hili la kodi la kutegemea Mkadiiaji kaamkaje au anakutizama vipi nalo ni giza ,watu wamepunguza uagizaji wa bidhaa na wengine wamehamisha biashara zao..

Biashara ni kama chain ,ukiondoa kiunganishi kimoja vinaathirika vyote..
 
Wanawafuata "wakwepa kodi"?

Mtu mzima akivuliwa nguo huchutama. Si vibaya kwa serikali kukiri makosa na kujisahihisha. Lakini ingeenda na uwajibikaji ingekuwa bora zaidi.
 
tena ningekuwa mm ni bakhresa ningewaaambia mpige magoti kuniomba radhi kwa kuniita mkwepa kodi alafu niwafotoe foto, hasa YOHANA!
umenichekesha hadi basi mkulu ameamua ageuke nguzo ya chunvi kama mkewe Lutu.hahahaaa bado kuwapigia magoti watalii muda utasema.
 
Back
Top Bottom