Bandari yawafuata wafanyabiashara 100

Bandari yawafuata wafanyabiashara 100

Sasa mbona tunarudi kwa Jakaya kuwapigia Magoti Wakwepa kodi?
Ni bora kwa jakaya ajira zlitolewa kwa wakati, nyongeza mishahara ilikuwepo kwa wakati,wanafunz vyuo vikuu walipata boom kwa wakati, n.k huyu wa sasa n matamko tu yasiyo na tija kwa taifa
 
Huwezi kushindana na mfanya biashara!!

Sidhani kama ni hivyo unavyodhani wewe...wewe umesoma kichwa cha habari tu lakini hujasoma stori yenyewe inasemaje...umecomment kishabiki...soma stori ndiyo uje u-comment...
 
Suala la serikali kufuata wafanyabiashara sioni ni tatizo
Kwani serikali aifanya kazi pekee yake nadhani nisahihi ili kujua mtikisiko wa kibiashara wa taifa na dunia kwa ujumla busara itumike.
 
Sasa Mkulu si alijifanya masikini jeuri kwa kutamba kuwa waliokimbia kutumia bandari ya Dar ni wale wafanyabiashara wakwepa kodi na akawaambia kuwa waende kwenye hizo bandari za nchi nyingine zinazoruhusu mizigo kupita bila kulipiwa kodi?

Sasa baada ya kuona bandari imekauka kabisa ndiyo anakuwa 'mpole' na kutaka kwenda kuwapigia magoti?

Hii nchi haitakiwi kuendeshwa kwa ubabe na matamko ya majukwaani, badala yake inatakiwa kuendeshwa kwa kufuata sheria za nchi na kusikiliza maoni ya wadau mbalimbali namna bora ya kuiendeleza nchi yetu.

Mkulu akiendeleza kuendesha nchi yetu kwa staili yake ya ONE MAN SHOW, hakika nchi yetu itakuwa inaelekea kuwa another Zimbabwe...............
Kwani serikali Kali kukaa na wafanyabiashara naona nisawa na utaifa kuweka mbele nadhani nikujua nijinsi gani mtikisiko ulivyo igharimu biashara zao
 
Na bado , baada ya sisi wafanyabiashara kupigiwa goti ( hata hivyo bado hatujakubali ) watafuatwa mamalishe , machinga tayari .
 
wanaruhusu kukwepa kodi au wana kodi ambazo ni reasonable!? Punguza jazba na hisia weweee.
Kwa mujibu wa mkuu wafanyabiashara waliokimbia bandar yetu ni wakwepa kodi.sasa hizi bandari walizokimbilia si ndo wanapokea wakwepa kodi?
 
Chichiem kusema ukweli imeligharimu na inaendelelea kuligharimu sana hili taifa.
Taifa limeoza, na bado hata kwenye hii era ya globalization wao wanaendelea kuliozesha kwasababu ya ubinafsi na upopoma.

Taifa kwa kiasi kikubwa sana linaongozwa na watu wenye uwezo mdogo sana e.g. waangalie wale wabunge wa ndiooo - not so intelligent, trivial, and irresponsible people.
Viongozi wa hili taifa wanafikiri uongozi ni ubabe, kunyeyekewa na kuabudiwa. Wao ni ilimradi tu waitwe waheshimiwa, that's all that matters to them. Na kwasababu hiyo basi, unakuta wote kwenye taifa, i.e. wanaoongoza na wanaoongozwa, wanaendeshwa kwa nguvu za mauongo, maunafiki, kujikweza na kujipaisha kwa kijinga, pamoja na kuishi kwa kutokukubali ukweli (Delutional). Mwisho wa siku matokeo yake ndio haya, siku zinapita, miaka inapita, karne zinayoyoma lakini kama taifa hatuendi popote kimaendeleo.
 
KWA NCHI KAMA YETU ILIYOUZA RASILIMALI ZAKE ZOTE KWA WAZUNGU SI RAHISI KUWANYALI WAFANYABIASHARA.

Bwana King Kong, mimi nashangaa kitu kimoja, tunakosoa kwamba nchi haijali wafanyabiashara, lakini Magufuli akitoa kauli mhemko ya "Mimi ni Rais wa masikini" huwa tunaona poa, tunashangilia, why?

Hakuna hata mtu aliyewahi kumpinga (hata wapinzani) Magufuli kwamba hey, Mr. President, wewe sio Rais wa masikini peke yao, wala hukuchaguliwa na masikini peke yao, kama alivyodai juzi Unguja. Tanzania hakuna "exit poles" za kutathmini nani kamvotia nani.

Wapinzani wanaogopa kupinga kauli ya "Mimi ni Rais wa masikini" wasije wakaonekana ni out of touch, bourgeoisie class wanaoetetea matajiri wenzao.

Lakini hao matajiri ambao Magufuli hawajali ni mimi na wewe tunaomiliki laptop moja, una afford kukaa baa ku order bia tatu, sahani ya nyama na bar maid mmoja, una kiwanja Dar-es-Salaam, una Toyota Carina, una ki agency cha M-Pesa na mitikasi mingine legal lakini isiyoelezeka in 30 seconds, una vitoto viwili una unga unga kuvipeleka English Medium school, kwa Tanzania wewe ni tajiri mchafu! Na haufiti kwenye definition ya kundi la watu ambao Magufuli anawajali.

I wish Watanzania wangelijua hili. Wasingekuwa wanakubali na kushangilia Rais akisema yeye ni Rais wa masikini. Wengi sana, wahangaikaji na wabangaizaji wengi mno tunaachwa nje ya hiyo definition, sembuse li kampuni linalo import makontena ya unga wa ngano? Ndio watalijali?
 
Back
Top Bottom