Balozi Juma Mwapachu atangaza kurejea CCM...

Balozi Juma Mwapachu atangaza kurejea CCM...

Imekuaje tena huko,wamemuomba hela nini?maana jaama kwa kukaba hawajambo.Kaenda chama cha wanyang'anyi,anategemea nini? Hesabu zimegoma. hahahahha.
na kwa mkubwa km huna mtaji kwel haoni faida yako yy hela kwanza mengine baadae
 
Na sasa nimeamua kulifanya jambo kubwa ili Magufuli ajue sasa niko naye kwasababu sitaki shughuli zangu na za washirika wangu zikwamishwe na Serikali kwa sababu tu huko nyuma niliamua kumsaidia swahiba wangu
E]Hapa Balozi anamaanisha nini?
 
kwahiyo anataka vyeo au? kwa serikali hii ya Magufuri asubiri kuwa mganga wa kienyeji
 
Mimi wa form 2 nitawaza na kuandika nini kama mwenye shahada anatoa upuuzi moyoni mwake..
Kama ndiye mwapachu kuna haja ya kuidelite kazi,kumbukumbu zake zote ktk masjala ya EAC hapa arusha.
 
Hajaandika wakati hapo kuna statement chini ina jina lake?

Ndiyo maana nikauliza hii statement kaandika yeye au anapakaziwa tu?

itakuwa ni yeye, na nilivomsoma inaelekea yupo kimaslahi zaidi, aliondoka kwa ahadi ya madaraka anarudi sababu kubwa washirika wake na biashara zake zisiletewe zengwe akiamini as long CCM ni chama tawala na akiwa CCM itakuwa "business as usual"
 
At this rate sioni tofauti ya the gentry and the social climber Tanzania.

Kina Mwapachu wamemkaribisha na kumtambulisha Nyerere Uingereza alivyoenda kusoma.

Wao ndio walikuwa matawi ya juu tangu enzi za ukoloni.

Sio watu waliokuja mjini juzi.

Wakitoa habari kama hizi wanaaibisha wasomi, wanaojiita wajanja mjini, vipanga wa foreign etc.

I would expect this from the Johnny come lately kina Sumaye, but I guess politics never ceases to surprise.


Talking of Sumaye, sasa naanza kupata picha ugonjwa wake pengine unatokana na 'kamari' kubuma. Mbele giza nyuma kaburi!
 
Duh mbona sisi tusiowahi shika hata cheo cha ukatibu kata hatuhangaiki hivi? Inakuaje wazee wasomi na walioogelea kwenye vyeo miaka nenda rudi wana kuwa waoga wa maisha namna hii?

Aisee Ndio maana nchi hii kupata maendeleo bado sana!!
Hakuna kitu kibaya Mpwa kama kutojiandaa kimaisha, unategemea blaa blaa ndio uishi, ni hatari sana, kwamfano nanihii akiondolewa kwenye Uwaziri leo hii ataishije? au kwa mfano wale Wakuu wa Mikoa na Sefue pia wataishije thereafter? Labda kama walikua na plan B ambao wengi wao kwa kweli hawana. Matokeo yake ndio haya kuwa mropokaji japo kutoka moyoni mwangu kabisa nashindwa kuamini kama ni kweli hii statement ni ya kwake.......huenda pia kuna mchezo wa kutuhamisha toka kwenye ishu ya uchaguzi wa Meya Dar na House Arrest ya Maalim Seif.
 
Haionekani kama lugha ya Balozi Mwapachu but anyway, alihama CCM kwa njaa zake na kama karudi basi ni kwa sababu ya utaratibu uleule wa kwake....KUGANGA njaa! na bila shaka MAERSK wanadaiwa kodi.
Umegonga kwenyewe mkuu...ulijuaje hili sakata!!!?????
 
Mkuu kuna uhakika kuwa ni yeye kaandika? Japo kurudi CCM anaweza kurudi lakini siamini kama anaweza kuwa mbumbumbu namna hii. Watakuwa watu wamemchomekea baada ya kujua karudi CCM
Mkuu nimechangia tu kama tetesi ,Mwapachu hichi siamini kama yeye ndie kaandika
 
Hivi kinawezekana chama mkamkataa mtu akiomba kuwa mwanachama wenu?
 
Tuseme hii habari ni ya kweli....

Kwani hawezi kuishi bila ya kuwa CCM?

Yaani baada ya kuondoka kwa drama vile sasa anaamua kurudi tena?
Kwani kosa lake ni nini si nihaki yake? Lowasa,kingunge sumaye wanaweza rudi si ajabu.
 
Bado siamini kama ni yeye mpaka nione kwenye Tv.
Haiwezekani msomi na mkongwe kama Mwapachu kusema haya maneno ya kitoto kabisa.
Kama kweli nafikiri anazeeka tu vibaya na ana ugonjwa wa akili wa uzeeni.
Haiwezekani. Nimeshtuka sana.
 
Vijana msiwaamini wanasiasa, mtabaki vichaa!

Msikilize hapa Juma Mwapachu anavyosema kuhusu CCM na UKAWA!

Wasikilize na wananchi walichosema baada ya Mwapachu kuongea!

 
Biashara zake na Washirika wake zisikwamishwe na Serikali.......
basi vizuri kajiondoa chama kipate kupumua ila ccm ikimpokea basi tutapigilia msumari wa mwisho ule uchunguzi usemao watanzania ndo wanaongoza kwa unafiki
 
Back
Top Bottom